SAKATA LA MAKONTEÑA YA MAKONDA KUPIGWA MNADA LITIZAMWE UPYA
Na: Mtetezi wa Wanyonge.
Nimemsikia Waziri Mipango akisema kuwa Lazima Makontena hayo Yalipiwe Kodi ama yapigwe Mnada ili serikali ipate Kodi yake...
My Take
Tukumbuke kuwa Makontena hayo ya Vifaa ni Watanzania wenzetu wamejitolea na ndiyo maana hakuna kiwanda kilichopewa tenda hiyo na huo ni msaada kama alivyopata misaada ya Miguu Bandia, Ujenzi wa Hospital, Viwanja vya Mpira, magari ya Police , Pikipiki, Computer [emoji335] na vingine vingi alivyowai kufanya.
Makonda aliomba Samani si kwa faida yake bali kwa faida ya Watanzania na Kuipunguzia Serikali mzigo wa Manunuzi ya Vifaa hivyo.
Leo Kigezo Kimekuwa SHERIA! Sawa lakini Sheria zinatungwa, kusomwa na kutafsiriwa na wanadamu na bado huacha mwanya wa busara kutumika na kila kesi huamliwa kulingana na mazingira na ushahidi wake. (Ndio maana kuna Dissenting decision/Opinion and or Consential/Concurring Opinion)
Na Ikumbukwe Kuwa Sheria ya kodi inaruhusu busara kutumika pale inapoonesha kuwa vitu au mali zitatumika kwa manufaa ya jamii ya wanyonge na sio mtu binafsi.
Ikiwa Makanisa, NGOs nk. Kila kukicha yanapewa misamaha ya kodi kwa idhini ya MaRC na MaDC kulikoni hasa haya Makontena ya Viti vya Walimu? Computer za Shule? Meza na nk...?
Nikweli Yalitumwa kwa Jina la Paul Makonda Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Lakini kampeni yake Iko wazi tangu awali na si ya kificho, Walioyatoa walitamka wazi ni ya nini na hayana faida kwa Makonda bali kwa Taifa na Watu wake hasa Wanyonge walio wengi.
Sasa Msuguwano Huu unatoka wapi?
Hiyo Kodi Ni Bei gani?
Kodi inadaiwa hapo inathamani Kubwa kuliko Samani ya hivyo Vifaa?
Hiyo Kodi Inaweza kununua vifaa vyote hivyo?
Haya Vikipigwa Mnada Serikali itapata Bei Gani? Hiyo Bei Inaweza kununua Samani zote hizo?
Tusing'ang'ane na Sheria inayotupotezea kingi zaidi kwa Kukomalia Kodi nakupoteza Mali Kubwa zaidi ya Kodi, Hekima na Busara zinaweza Tatua hili kwa Kukaa nakujadili Faida na Hasara za Kodi, Faida na Hasara zakuendelea kuwa na Vifaa hivyo, Faida na Hasara za Vifaa hivyo Kuingia kwenye Majengo yanayongoja Vifaa na Wanyonge kuvitumia.
RC Makonda Ameomba Misaada Majengo yamejengwa yanahitaji Samani, Serikali Imesaidiwa na Wazalendo wa Taifa hili waishio ughaibuni kwanini Tuwafanye wajione hawana Thamani kwa Kujitoa kwao kusaidia Nchi yao?
Mh Waziri Mipango na Wasaidizi wako na Watu wa TRA mlitizame Upya Jambo hili.
Mlio Karibu na Mh Rais Fikisheni Kilio cha Wanyonge wakatumie Vifaa hivi.
Iko Misamaha Mingi sana ya Kodi Kupitia Vifaa hivyo kuwa Vinaenda kuhudumia Jamii basi Dhamila Kuu ikatimie kwa Vifaa hivyo Kusamehewa Kodi na Vikatumike Mashuleni.
Mnyonge Mnyongeni haki yake Mpeni!
Hapa Hatumkomoi Makonda ila Tunataka Kuwakomoa Walimu na Watoto wa Shule wenye uhitaji wa Vifaa hivyo.
Sakata la Makontena Liangaliwe upya kwa Maslahi Mapana ya Taifa Hili na Wanyonge wenye Uhitaji wa Vifaa hivyo.
Waziri Mipango Fanya Mipango Vifaa viwafikie Wanyonge bila Kodi, Manake hata Mkisema Kodi ilipwe analipa nani?
Makonda aloomba kwa Niaba ya serikali?
Au Tuwaombe Pesa Walotupa Msaada tena wao Ndo walipe Kodi tena?
Kwani Tunataka Kumfurahisha nani katika hili? Au Kumkomoa Nani katika Hili?
Wanaoteseka ni Walimu na Watoto wa shule, Misuli tunayotunishiana Viongozi Haitusaidii sisi watanzania kwa ujumla.
Kodi na Mnada kwa Vifaa hivyo Vyote vinatuumiza kwani Vinapelekea Kupoteza Vifaa vyenye uhitaji kwa wanyonge.
Kodi tunazikusanya ili Tununue Vifaa vya Shule, Leo Hii Vifaa Vimekuja Buree na Vingi vyenye ubora zaidi sisi hatuvitaki kisa Kodi.
Inasikitisha sana hii Hali....
Tunaomba Viongozi walitizame upya jambo huli.
Makontena haya Faida kwa Mkonda zaidi ya Faida kwa Wanyonge na Serikaki yao ambao wanahitajika Kuhenyeka kwa Mika kadhaa huku wakilipa kodi ndo waweze kununua Vifaa vyote hivyo.
Sent using Jamii Forums mobile app
SAKATA LA MAKONTEÑA YA MAKONDA KUPIGWA MNADA LITIZAMWE UPYA
Na: Mtetezi wa Wanyonge.
Nimemsikia Waziri Mipango akisema kuwa Lazima Makontena hayo Yalipiwe Kodi ama yapigwe Mnada ili serikali ipate Kodi yake...
My Take
Tukumbuke kuwa Makontena hayo ya Vifaa ni Watanzania wenzetu wamejitolea na ndiyo maana hakuna kiwanda kilichopewa tenda hiyo na huo ni msaada kama alivyopata misaada ya Miguu Bandia, Ujenzi wa Hospital, Viwanja vya Mpira, magari ya Police , Pikipiki, Computer [emoji335] na vingine vingi alivyowai kufanya.
Makonda aliomba Samani si kwa faida yake bali kwa faida ya Watanzania na Kuipunguzia Serikali mzigo wa Manunuzi ya Vifaa hivyo.
Leo Kigezo Kimekuwa SHERIA! Sawa lakini Sheria zinatungwa, kusomwa na kutafsiriwa na wanadamu na bado huacha mwanya wa busara kutumika na kila kesi huamliwa kulingana na mazingira na ushahidi wake. (Ndio maana kuna Dissenting decision/Opinion and or Consential/Concurring Opinion)
Na Ikumbukwe Kuwa Sheria ya kodi inaruhusu busara kutumika pale inapoonesha kuwa vitu au mali zitatumika kwa manufaa ya jamii ya wanyonge na sio mtu binafsi.
Ikiwa Makanisa, NGOs nk. Kila kukicha yanapewa misamaha ya kodi kwa idhini ya MaRC na MaDC kulikoni hasa haya Makontena ya Viti vya Walimu? Computer za Shule? Meza na nk...?
Nikweli Yalitumwa kwa Jina la Paul Makonda Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Lakini kampeni yake Iko wazi tangu awali na si ya kificho, Walioyatoa walitamka wazi ni ya nini na hayana faida kwa Makonda bali kwa Taifa na Watu wake hasa Wanyonge walio wengi.
Sasa Msuguwano Huu unatoka wapi?
Hiyo Kodi Ni Bei gani?
Kodi inadaiwa hapo inathamani Kubwa kuliko Samani ya hivyo Vifaa?
Hiyo Kodi Inaweza kununua vifaa vyote hivyo?
Haya Vikipigwa Mnada Serikali itapata Bei Gani? Hiyo Bei Inaweza kununua Samani zote hizo?
Tusing'ang'ane na Sheria inayotupotezea kingi zaidi kwa Kukomalia Kodi nakupoteza Mali Kubwa zaidi ya Kodi, Hekima na Busara zinaweza Tatua hili kwa Kukaa nakujadili Faida na Hasara za Kodi, Faida na Hasara zakuendelea kuwa na Vifaa hivyo, Faida na Hasara za Vifaa hivyo Kuingia kwenye Majengo yanayongoja Vifaa na Wanyonge kuvitumia.
RC Makonda Ameomba Misaada Majengo yamejengwa yanahitaji Samani, Serikali Imesaidiwa na Wazalendo wa Taifa hili waishio ughaibuni kwanini Tuwafanye wajione hawana Thamani kwa Kujitoa kwao kusaidia Nchi yao?
Mh Waziri Mipango na Wasaidizi wako na Watu wa TRA mlitizame Upya Jambo hili.
Mlio Karibu na Mh Rais Fikisheni Kilio cha Wanyonge wakatumie Vifaa hivi.
Iko Misamaha Mingi sana ya Kodi Kupitia Vifaa hivyo kuwa Vinaenda kuhudumia Jamii basi Dhamila Kuu ikatimie kwa Vifaa hivyo Kusamehewa Kodi na Vikatumike Mashuleni.
Mnyonge Mnyongeni haki yake Mpeni!
Hapa Hatumkomoi Makonda ila Tunataka Kuwakomoa Walimu na Watoto wa Shule wenye uhitaji wa Vifaa hivyo.
Sakata la Makontena Liangaliwe upya kwa Maslahi Mapana ya Taifa Hili na Wanyonge wenye Uhitaji wa Vifaa hivyo.
Waziri Mipango Fanya Mipango Vifaa viwafikie Wanyonge bila Kodi, Manake hata Mkisema Kodi ilipwe analipa nani?
Makonda aloomba kwa Niaba ya serikali?
Au Tuwaombe Pesa Walotupa Msaada tena wao Ndo walipe Kodi tena?
Kwani Tunataka Kumfurahisha nani katika hili? Au Kumkomoa Nani katika Hili?
Wanaoteseka ni Walimu na Watoto wa shule, Misuli tunayotunishiana Viongozi Haitusaidii sisi watanzania kwa ujumla.
Kodi na Mnada kwa Vifaa hivyo Vyote vinatuumiza kwani Vinapelekea Kupoteza Vifaa vyenye uhitaji kwa wanyonge.
Kodi tunazikusanya ili Tununue Vifaa vya Shule, Leo Hii Vifaa Vimekuja Buree na Vingi vyenye ubora zaidi sisi hatuvitaki kisa Kodi.
Inasikitisha sana hii Hali....
Tunaomba Viongozi walitizame upya jambo huli.
Makontena haya Faida kwa Mkonda zaidi ya Faida kwa Wanyonge na Serikaki yao ambao wanahitajika Kuhenyeka kwa Mika kadhaa huku wakilipa kodi ndo waweze kununua Vifaa vyote hivyo.
Sent using Jamii Forums mobile app
Maswali mawili unayopaswa kujiuliza. SWALI NO 1 inakuingia akilini kuwa diaspora waishio marekani wakakuchangia vifaa vya elimu kontena ishirini? SWALI NO 2 unao uhakika kuwa kwenye hayo makontena ishirini kuna hizo samani za shule peke yake? NOTE, TRA na waziri hawajakurupuka
Sent using Jamii Forums mobile app
Hiv chadema ndo wamemtuma waziri mpango amwambie bashite alipe kodi? Hebu tuondoleeni wendawazimu hapa nyie vichaa nini?Chadema wana wivu sana na Makonda lakini mkae mkijua amewaacha mbali sana na saco cos yenu
Sent using Jamii Forums mobile app
HAHAAAA SAWASAWA MKUUNilimaanisha kwa hoja zako umemaliza kabisa mjadala, ndio ukweli kabisa
Hatua ya kupiga mnada pia ni busara, tena iliyotukuka...Busara inayotumika kusamehe wakwepa kodi ,itumike pia kwenye makontena haya ili walimu wasiendelee kukaa chini na kukalia viti vichafu.
Kama tatizo ni sheria hata mikutano ya vyama vya siasa ipo kikatiba lakini imepigwa marufuku na watu wameelewa
Sent using Jamii Forums mobile app
Hahhaha...mimi naona mbali kwa darubini kaliBashite lipa kodi unalialia nini huu muda unaohangaika kuwatuma Hawa mambumbumbu waje kukutetea huku kwenye mtandao ungeutumia kutafuta hiyo kodi. Kama kweli hivyo vifaa ni Mali ya mkoa unashindwa nini kutoa amri kila manispaa ichangie hiyo kodi ilipwe? Au umeingiza vifaa vya hoteli yako ya mwanza mzee baba?
We Jamaa siku hizi umekuwa Mjinga!!Kwanza kwa mlio walimu mtanielewa ninaposema waziri kakurupuka wala hazijui changamoto za elimu
ukisikiliza kwa umakini kwenye hotuba yake ya juzi utagundua kabisa aelewi anachokiongea...
Anaongelea maswala ya elimu bure kitu ambacho ni nje kabisa ya mada ya makontena
swala hapa ni vifaa kwa ajiri ya kusaidia elimu ya dsm ambayo ina changamoto nyingi ikiwa na mrundikano wa wanafunzi na mambo kibao
Makonda inawezekana kuna sehemu alikosea katika mchakato huo lakini serikali walitakiwa kuwa wajanja wangeruhusu kwanza vitu viingie ndio waanze kuvimonitor wapate ushahidi wa kutosha ndio waje kumtuhumu.
matokeo yake wananchi nao wameyabeba na kusahau watoto wao ndio wanakaa chini milele
mimi niko na ushahidi kabisa nilienda shule moja na taasisi fulani kutoa msaada wa computer lakini unakuta walimu stafu viti tu vya kukalia haviwatoshi hii ni aibu kama mwalimu hana kiti stafu mwanafunzi je darasani itakuwaje?
tukiweka siasa pembeni Makonda yupo sahihi kabisa na ana nia njema ingawa anaweza kuwa kafanya makosa kutumia jina lake kwa ushauri mbovu wa watendaji waliopo chini yake lakini naamini tatizo letu la elimu ni kubwa mno kuliko jina la makonda kuwa kwenye makontenana hili swala tunalibabe kishabiki sana kama kawaida yetu...
kwamba mimi ni chadema Gambo akifiwa na mzazi wake nashangilia, mimi ni ccm Sugu akipata msiba nashangilia upuuzi mtupu.
Hivi waziri anavipiga mnada vitu vya shule za dsm watu tunashangilia leo halafu kesho jangwani secondary inakuwa ya mwisho tunaanza kumponda makonda ...
Hivi vitu vikinunuliwa na wafanya biashara sisi wananchi wa kawaida tutafaidika vipi direct kama ambavyo tungeviona kwenye shule zetu? namimi naongeza na alaaniwe kabisa atakae vinunua.
"Form four wanakaribia pia kuanza mtihani msisahau kuleta mrejesho hapa wa shule za umma"
Haahhha...JF wakati mwingine ni kiwa cha burudaniYani hapa ndo Wana ccm wameshindwa wawe wapi either kwa RC or Waziri.
Mana unaweza ukawa kwa Wazira yakamkuta ya Nape wakashindwa kula matapishi yao, wakawa kwa RC ukasikia amepangiwa majukumu mengine? Niwashauri tu Wana ccm mlivyokua ni wafuata upepo kuweni tu katikati uku mkisubri Baba yenu ataamua nini, ili atakako favor ndo muende uko.
Sent using Jamii Forums mobile app
MimiMkuu Kimla, kwanza asante kuniheshimu, heshima is earmned, na ikipotea, its gone!. Siku zote mimi ni mkweli na very transparent, nikiamini transparency ndio the only way ya ku resolve hii issue. Containers zile 20 zimefunguliwa, ni samani new and used.
Hoja yangu ni ndogo sana, maadam, samani hazina msamaha wa kodi, kiwango cha kodi ni bilioni 1.2, itaigharimu serikali yetu, kutumia bilioni 20 kununulia the same amount of samani zenye the same quality and finishing kutoka Keko.
Hiyo kodi serikali inadai, kodi ya 1.2 bilions kwenye samani za shule, halafu inakuja kulipa bilioni 20, kununua the same samani toka Keko!. Hii ni akili au matope?!.
Hii sii mara ya kwanza kwa serikali yetu kufanya maamuzi ya ajabu. Ni sakata la Richmond.
P.
- Tume ya Mwakyembe imesema Richmond ni kampuni hewa, wanatuibia kupia capacity charges za milioni 152 kwa siku, hivyo wakashauri tuvunje mkataba, na hatutashitakiwa, popote kwa sababu kampuni hewa, haiwezi kushitaki popote, hivyo tukavunja mkataba.
- Tukawasha mitambo ya IPTL kwa inayofua umeme mdogo kwa gharama kubwa mara 2 ya Richmond, huku ikitumia mitambo chakavu mara 10 ya Richmond, na kuchafua mazingira mara 100 ya Richmond. Na malipo haya ndio yamezalisha escrow.
- Tukashitakiwa kwa kuvunja mkataba, tukalipishwa tozo ya Dowans, waliotushauri tuvunje, wakajiapiza hatulipi "over my dead body"
- Msingi wa kulipishwa ni japo Richmond ni kampuni hewa, mitambo ya Richmond sio mitambo hewa, na umeme unaofuliwa na mitambo hiyo, ni umeme kweli sio umeme hewa, hivyo malipo ya Richmond, ni malipo ya capacity chargers za mitambo kweli na malipo ya umeme unaofuliwa.
- Kiukweli hiyo tozo tulilipa kimya kimya ambapo gharama yake ni mara 10 ya malipo ya halali kama tusingevunja mkataba!.
- Mitambo ile ikanunuliwa na Simbion, mitambo ile ile, capacity charges zile zile na tukalipa na kuendelea kulipia hadi Magufuli ameingia.
- Waliotushauri kuvunja mkataba na kujiapiza, ndio wale wale waliokuwa wakicheza ngoma na mama Clinton siku Simbion inazaliwa.
- Tumevunja mkataba wa Richmond wa capacity charges ya milioni 152 kwa siku, tukalipishwa faini ya mara kumi zaidi, kisha tukasaini mkataba wa Simbion wa capacity charges ya milioni 152 kwa siku!.
- Hii ni akili au matope?!.
- Sasa tunauza samani za shule kwa mnada kutafuta bilioni 1.2 ya kodi za serikali. Halafu serikali hiyo hiyo inatoa bilioni 20, ya kodi kununulia samani za waalimu kutoka Keko. Hii ni akili au matope?.
Ahsante mkuu
Tangu lini Mpango akawa Chadema, kwanza vile sio vifaa vya shule ni fenicha za hotel.Chadema wana wivu sana na Makonda lakini mkae mkijua amewaacha mbali sana na saco cos yenu
Sent using Jamii Forums mobile app