Makonda kamtaja Chid Mapenzi, huyu ni nani? Tupeni file!

Nawafamu zaidi ya watu watano personally waliotajwa na makonda especialy wale wa international.huyu jamaa wala sio mtu mkubwa kwenye biashara ya unga.ni punda tu na mpambe wa kina omary sanga tena hana hata hela ya maaana,huyo omary sanga mwenyewe kashafilisika ndo wanamtaja.
Chidi mapenzi ni mshenzi mmoja ivi anapenda kuvaa kuliko kula.labda akatumike kusaidia polisi kuwataja maboss wake.kiboko last time nimemuona Sham shui po HK mwaka 2014 kama skosei.na ukikutana naye wala huwezi kudhani ni mafia.
 
Ongezea asali kwenye huu uzi wako...dizaini km uko full nondo ila mvivu kuandika! Utadhan mtu wa masomo ya sayansi bwana
 
Ongezea asali kwenye huu uzi wako...dizaini km uko full nondo ila mvivu kuandika! Utadhan mtu wa masomo ya sayansi bwana
Kwa kifupi makonda anadili na wauza unga wadogo na wale waliofilisika kama kina omary sanga na kina kanyau.Omary Sanga alikuwa ndo mpokeaji wa mizigo yote inayoingizwa china na mapunda na muuzaji kwa wanaijeria ambo ndio masaplaya wa unga rejareja china na nchi jirani.hivi sasa ameshafulia na sio major tena kama zamani.Huyu chidi mapenzi ni mishentauni mmoja ivi blazameni na mdananda kama kina petit.na hata petit akija china huwa pamoja naye.

China mainland na hong kong ndio soko kubwa la unga unaotoka bongo kwa miaka mingi hivyo hata mabosi wa unga huwa wanakuwa huku mara kwa mara .na uzuri wa huku unaweza ukawa hata mkuu wa nchi na ukaja ukakaa huku hata mwaka bila kujulika.kina chonji,shkuba,kiboko na kingpins wengine nimewajulia huku,uzuri wa huku hata akija waziri ama tajiri mkubwa mnakaa naye maskani mnapiga story,so unakutana na watu wengi wakubwa wa hadhi tafauti tafauti ambao usingeweza kukutana ama kukaa nao pamoja bongo.nitaendela.
 
Nilijua tu mkuu una nondo za hatari... ni wachache wanaotambuaga watu wenye madini! Wazee wetu walitumia akili za kipelelezi na kiuchunguzi ili kujua mtoto yupi yuko smart na mwisho wa siki walipewa taarifa nyeti sana...
Kama hutojali endelea kumimina hii asali juu ya mkate tumalizie kiporo.
 
Una vingi ila u mvivu kusema.... Jazia jazia
 
Shkuba ndo aliimbwa na FA ( hustler kama Ali Shkuba natimba kila kiwanja)
 
Huyu chidi mapenzi kaja china 2012 kama skosei,alikuwaga shanta wa nguo kkoo na kinondoni,anafahamiana na watoto wamjini na wauza unga wengi wakibongo walioko guangzhou na hong kong,zaidi ya upunda na upambe hana ukubwa wowote kwenye biashara ya unga ni kama kina petit tu.
 
Inaendela.kusema kweli Tanzaia tuko vizuri kwenye biashara ya madawa.na kama ingekuwa ni sekta inayotambuliwa na halali basi tungeongoza afrika nzima na tungekuwa na dangote wetu.Kwanza tanzania ni corridor/highway/njia panda ya mizigo ya unga wa aina zote kuanzia heroin(musharaf)kutoka pakistan,cocaine(pele)kutokea brazil,mandrax na meth.zile precursor chemicals alizotaja sianga kuwa zimeingizwa nchini ndizo hutumika kutengenezea meth.Sasa basi hii ni biashara kubwa sana.sisi tunapokea mizigo kutoka kila kona inakotengenezewa alafu sisi ndo tunaexport kuwapelekea consumers duniani kote.bei ya mfuko mmoja wa heroin (1kg)hapo bongo mpaka mwisho wa mwaka 2016 ilkuwa dola 9000 ila ukienda UK 0.1g inauzwa euro 10 kwahyo ukifanikiwa kupeleka mfuko mmoja unaweza kupata hadi dola 40000 kwa bei ya jumla. ni biashara yenye faida kubwa sana na wenye biashara hii wanapesa mingi na wengi hawafahamiki kabisa.
 
Chid Benzi na Chid Mapenzi ni watu wawili tofauti!!!!
Ila wana common factors nyingi tu!wote ni watanzania ,wanaishi dar, mmoja ni msanii na mwingine ana mahusiano na msanii,majina yao ya kupanga yanashabihiana,wote wanajihusisha na unga ilihali mmoja anatuhumiwa kuutumia na mwingine kuusambaza.
Conclusion !hawa watu wana mahusiano ya karibu bila wenyewe kujijua!
 
Titimunda kwa nn huko china mnachangamana na kila mtu yan mkubwa, kibosile, choka mbaya nk.
Je ni kwa vile mpo wachache hivyo mtu.akijitenga anabak mwenyewe ama? Na kwa nn china ndio penye sheria ngumu dunian lakin still kila anaechipukia hizi dawa rpute zake zinakuwa za china....au huo userious wao wa kuwa smart ni ktk news tu za vyombo vya hbr
 
Una vingi ila u mvivu kusema.... Jazia jazia
Ukijaziajazia sana unaweza jikuta umesema yasiyotakiwa kusemwa hadharani au ukaji expose identity yako.
Tanzania tukitaka tuidihibiti biashara ya unga kuna vitu viwili vya kufanya.
1.kuongeza ulinzi kwenye mipaka yetu na njia zote zinazotumika kuingiza na kutoa hii midude kwenda nje.imagine dar es salaam pekee ina bandari bubu 50,border za Tanzania ziko loose kuliko viungo vya siri vya kahaba,achana na bandari bubu tunayo hadi mipaka bubu.Mashine za kukagulia mizigo nazo mbovu sasa unategemea utadhibitije hii biashara.ndani ya wiki hizi mbili ambazo makonda kaunguruma unajua zishaingizwa kilo ngapi za unga na punda wangapi wamepakia ndege ktk airport zetu?.customs nako kumejaa rushwa.unaweza pitisha hata fuvu la binaadamu ukiwa na hongo stahili.

2.Kudhibiti pesa ya unga.Hakuna jambo gumu kwa drug dealers wa nchi zilizoendelea kama kutakatisha pesa zao za faida ya unga na kuziingiza kwenye system.lakini kibongobongo ni rahisi mno.kwa makadirio yangu kila siku guanghzou pekee inatakatisha si chini ya dola 50,000-100,000 za unga na kuziingiza kwenye system ya pesa bongo kiurahisi kabisa.kwa wale wakazi wa diaspora kuna kitu kinaitwa remittance huduma kama inayotolewa na western union na moneygram,.sasa huku kuna western union za kienyeji.GSM wanahusika kiasi kikubwa na hili tena walivyomabaradhuli wanatuchaji sisi wafanyabiashara katika kutakatisha fedha zao,wakati wengine wanafanya bure.
Bongo ni kawaida ya mtu kuwa na pesa isiyo na maelezo yaani mtu anabiashara ya milioni kumi lakini ana mali za milioni 500.na huwa hakuna maswali.kwa wenzetu mali zako zinatakiwa kuendana na kipato chako kinachotambuliwa na serikali.
Kwahyo cha msingi ni kudhibiti tu pesa ya unga isiwe inamove freely kama ilivyo hivi sasa.kwa mfano ni ngumu kwa drug dealer wa colombia kuhamisha dola laki moja ya unga kutoka marekani kurudi nchini kwake kuliko dealer wa tanzania kuhamisha faida yake ya dola milioni kutoka china kuja dar es salaam.
 
Mkuu kwanini usimsaidie kamishna siang'a!?
 
Hatuko wengi kivile alafu wengi ni watu wa mishemishe zinazofanana wengi tunakaa miji ileile na vitongoji vilevile wanafunzi ndio wametawanyika.unajua ukiwa nje unakuwa na hamu ya kujichanganya na watu wa kwenu so wengi unakuta tunakutana kwenye migahawa ya kibongo,na mishe nazo zinafanana hata viongozi wakija nao hujichanganya nasisi kwanza hakuna choka mbaya kiivyo huku.maana maisha yenyewe yalivyo expensive ukiwa huna pesa unajirudia zako bongo tu maaana huku hakunaga kuzamia ama kuoverstay.

Kuhusu unga na sheria kali ni kwamba skuzote supply ikibanwa ilhali demand ipo basi price inakuwa kubwa sana.huku hela ipo hususani hongkong.nawafahamu small time dealers wakiuza vipinchi tu lakini wanapiga hela nzuri.Hong kong nimji wa tatu duniani kwa ukali wa gharama za maisha baada ya singapore na zurich,huku maisha yako juuu kuliko maelezo,kwahyo gharama ya unga nayo ni kubwaa.na kihistoria china imeanza matumizi ya madawa since 1800s mpaka kuja kutokea opium wars.kwakifupi demand ya unga ni kubwa kuliko supply.bangi tu inauzwa RMB 200 kwa kete sawa na alfu sabini ya kibongo sasa inagine heroin na coke zinauzwa bei gan
 
Mkuu kwanini usimsaidie kamishna siang'a!?
Kwani unadhani nayoyazungumza ni mapya wanayafahamu vizuri tena wanajua zaidi ya nisiyoyajua mimi.kwamfano mimi Ayubu kiboko sikuwa nikifahamu kuwa ni major drug dealer,nlikuwa napishana naye tu mitaani,wengi naowajua nimewajua sababu tu ya harakati za maisha sio kwamba ni rafiki zangu au na mimi na deal na hizo mambo,nakumbuka mara ya kwanza kuuona unga nlikuwa form 1 jamaa alinionyesha kakifuko kadogo kanailoni akanambia unaona hii,hii nizaidi ya milioni mbili nkabaki kushangaa vipi ungaunga kiasi kidogo namna ile una bei kubwa namna ile.
Sio china tu brazil,iran,pakistani mpaka kolombia na peru kuna wabongo wanaliendeleza libeneke la unga.Mie mwenyewe hata nkitaka leo niingie naweza tena sio kwenye upunda,kwenye supply chain yenyewe na money laundering lakini bdo ninaimani na kimwogopa mnyaazmungu.
 
Na kuna huyu mwingene aliyetajwa na Makonda kuacha ChidinMapenzi,huyu jamaa hela za Unga kanunulia daladala nyingi za Mwananyamala -Buguruni,wakimkuta na hatia hizo gari wazitaifishe
 
Na kuna huyu mwingene aliyetajwa na Makonda kuacha ChidinMapenzi,huyu jamaa hela za Unga kanunulia daladala nyingi za Mwananyamala -Buguruni,wakimkuta na hatia hizo gari wazitaifishe
Huyo jamaa unaambiwa ana nyumba mpaka india na ulaya seuze daladala
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…