Makonda na mind games: Ukubali usikubali, Rais Samia anasahihisha madudu ya Hayati Magufuli!

Makonda amerudia aliyowahi kuyasema Ndugu pole pole, hii bado ni awamu ya tano, ni wahuni wachache tu ndio wanajifanya hawatambui hilo na kuiita awamu ya sita.
 

Kunywa bilauri ya maji, kisha tulia. Halafu anza kuweka mawazo yako hatua kwa hatua. Utafanikiwa kuleta hoja inayoeleweka yenye majibu mengi kuliko maswali.
Ulichofanya hapo, ni haraka haraka kama unaoga nje.
 
Kweli pesa imepotea, matumaini yangu kipato kitaongezeka, ajira zimeonhezekap, wawekezaji wanarudi, hali ya hofu haipo tena.
 
Huyu Makonda apewe ubalozi hukoo UKRAINE...
Kama polepole alipigwa Cuba .then huyu huko kutamfaa..

Moyo wake umejaa chuki .visasi na gubu..

Hovyoo..
Ukraine hatuna uhusiano nao! Pale tuna uhusiano na Poland na Urusi
 
Yako mengi sana ,saizi wale jobless wa kuznia 2016-2021 wengi wao wamepata kazi.

Wengine Hawa hapa [emoji116]View attachment 2945673

Hao unaowaita cheti fake Samia kawalipa mafao , Magufuli alishindwa [emoji16][emoji16]
Kulipwa haihusiani na taaluma!
Samia kawalipa kama Rushwa ya kura za Urais 2025.
Lakini bado hawajawa na vyeti halali.
Ni vyeti fake mpaka wanaondoka Duniani.
 
Kulipwa haihusiani na taaluma!
Samia kawalipa kama Rushwa ya kura za Urais 2025.
Lakini bado hawajawa na vyeti halali.
Ni vyeti fake mpaka wanaondoka Duniani.
Kwani kawalipa jasho lako au lao? Rushwa gani hapo kwani watapigiwa simu na kukaguliwa upande waliopigiwa kura?

Mwendazake hakuwa na pesa akatafuta weak areas na kufukuza Wafanyakazi,wanafunzi na blaa blaa zingine.

Mbona Vyombo vya usalama na Wana siasa hakuwagukuza Kwa visingizio vya vyeti fake?
 
Hata kama katumwa , kwani kuna mtu anaweza kuhodhi ukweli kuwa Magufuli alikuwa dikteta ambaye kwa vitendo vyake kuna watu walipoteza maisha?
Ukweli huo hsutofutika.
Wale wafanya biashara wa Singida waliopotea kawapoteza Samia sio? Wale wanaodaiwa kupotea saizi nani anawapoteza? Kwa vile walipotea kipindi cha Magufuli mnasema kawapoteza Magufuli ila waliopotea kipindi hiki cha Samia mnasema Samia hahusiki!
 
Wale wafanya biashara wa Singida waliopotea kawapoteza Samia sio? Wale wanaodaiwa kupotea saizi nani anawapoteza? Kwa vile walipotea kipindi cha Magufuli mnasema kawapoteza Magufuli ila waliopotea kipindi hiki cha Samia mnasema Samia hahusiki!
Flawed logic.
Arguments na logic kama hizi ni sawasawa na kusema punda ana masikio mawili, binadamu ana masikio mawili.
Kwa hiyo punda ni binadamu!!!
 
Flawed logic.
Arguments na logic kama hizi ni sawasawa na kusema punda ana masikio mawili, binadamu ana masikio mawili.
Kwa hiyo punda ni binadamu!!!
Wewe naomba uniambie wale vijana wa Kariakoo watano wako wapi? Yule mfanyabiashara aliyekuwa anaidai TRA milion 900 kafariki mazingira ya kutatanisha hamsemi! Nyinyi nyumbu akili hamna ni wapumbavu wa kuokoteza maneo! Hata sasa watu wanapotea vile vile kipindi cha Kikwete Chacha Wangwe alifariki kiutata,Dr Mvungi wa katiba mpya aliuliwa,Mtikila pia alifariki kiutata,Dr Ulimboka alitekwa na watu kibao walipata matatizo ila ulivyo ndezi unaona ya Magufuli tu Mpumbavu wewe!
 
Acha uongo wote ni wale wale, wizi wa kura umeendelea kuwepo Magu akiwa kaburini,

Usijitoe ufahamu.
Inawezekana lakini toa ushahidi.
Magufuli alikufa lakini mafisadi wa kisiasa bado wapo, hawakufa naye.
 
Mkuu unaharisha historia.
Ila kiujumla wewe ridhika na ukweli kuwa sasa hivi hofu ya kubzmbikwa kesi, kuwekwa ndani, kesi za kupika uhujumu uchumi, na hata Task Force za kuwsibia safznyabiashara, vyote hivyo hakuna tena.
Mama Samia hoyee!
 
Inawezekana lakini toa ushahidi.
Magufuli alikufa lakini mafisadi wa kisiasa bado wapo, hawakufa naye.
Ndo nasema acheni unafiki,

Sa100 Si msafi maana ameendeleza wizi wa kura,

Yeye na Magu ni wamoja katika angle hiyo.

Hivyo mako, is right.
 
Samia atavuna alichopanda kwa kuteua Mamluki mwenye kashfa , unachagua mtu mchafu ili uwawin Wasukuma , ni msukuma yupi wa kushawishika na Makonda ?

kazi mnayo .
Kwanini Makonda aliposimama umati ulimshangilia kuliko wote pale
Kwa hiyo wale waliolikwa pale walikuwa wasukuma.
Mbona mnachuki na wasukuma sana.
 
Ndo nasema acheni unafiki,

Sa100 Si msafi maana ameendeleza wizi wa kura,

Yeye na Magu ni wamoja katika angle hiyo.

Hivyo mako, is right.
Na tetesi za uhusika wa Makonda kumpiga risasi Tundu Lissu unalizungumziaje?
 
Mkuu unaharisha historia.
Ila kiujumla wewe ridhika na ukweli kuwa sasa hivi hofu ya kubzmbikwa kesi, kuwekwa ndani, kesi za kupika uhujumu uchumi, na hata Task Force za kuwsibia safznyabiashara, vyote hivyo hakuna tena.
Mama Samia hoyee!
Wewe Samia unamuona wa maana kawahamisha Wamasai kwa nguvu kutoka Ngorongoro huku akiumiza na kuua watu! Wewe ulivyo mpuuuzi unamuona wa maana sana!
Hakuna uongozi ulio msafi ni wewe ndezi tu ndo unaamini huo uijinga! Huyu huyu Samia Kanajisi NHIF na kusabibisha wagonjwa hasa watoto na akina mama kutopata matibabu! Unajua wangapi wanapoteza maisha kutokana na maamzi ya serakali yake!
Uzembe wa watendaji wa serkali unaumiza watu kiasi gani unaliujua hilo? Wangapi wamefariki mahospitalini kwa ujinga na uzembe wa serkali yake! Kichwa lako hilo haliwezi kuona hili! Hakika wewe ni Bogus na mbinafsi sana usiyeangalia maisha wa wenzako!
 
Na tetesi za uhusika wa Makonda kumpiga risasi Tundu Lissu unalizungumziaje?
Ni zile zile sawa na za wale vijana wa CAG kufariki Kwa Sumu 2022,

Pesa za umma zimeendelea kupotea zaidi sana chini ya sa100, kada wa CCM amepigwa Sumu na kufariki hivi majuzi Yule Mushi,

Mako, Magu na sa100 ni wamoja Hasa katika wizi wa kura.

Mwenezi Yuko sawa, sa100 Si msafi ni wale wale.
 
Tujaalie..
Umri,
Jinsia na
Itikadi zako tafadhali.
 
Na tetesi za uhusika wa Makonda kumpiga risasi Tundu Lissu unalizungumziaje?
Tetesi ndo nini? Kama ushahidi unao nenda Mahakamani acha kubwabwaja! Said kubenea alisema kama unataka kujua Ben Saanane alipo muulize Mbowe! Hata Dr Slaa alisema mnatabia ya kutekana ili kusingizia serkali!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…