Mkalukungone mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 862
- 1,755
Mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge,uwekezaji wa Umma PIC, Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Paul Christian Makonda leo Jumatatu Februari 17, 2025 amewakaribisha wajumbe wa kamati hiyo ambao ni wabunge wa Bunge la Tanzania kutumia mafao yao kwenda kuwekeza Jijini humo, badala ya kutumia Mafao hayo ya Ubunge kwenda kuwapatia wajumbe, ili kuwapitisha kwenye uchaguzi.
Soma Pia: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Akihimiza umuhimu kuwapatia wajumbe wa mikutano ya vyama vya siasa ndoto za kule nchi inapoelekea, maono ya wagombea na mipango ya kuwaondoa wapigakura kwenye mikwamo mbalimbali ikiwemo umaskini, Mhe. Makonda amesema Arusha inazo fursa mbalimbali za kiuwekezaji na ni muhimu kwa Wabunge hao kuweka alama ya utumishi wao wa kibunge kupitia uwekezaji wa maeneo mbalimbali mkoani Arusha ikiwemo sekta ya migahawa na hoteli kutokana na mahitaji makubwa ya huduma hizo.
Soma Pia: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Akihimiza umuhimu kuwapatia wajumbe wa mikutano ya vyama vya siasa ndoto za kule nchi inapoelekea, maono ya wagombea na mipango ya kuwaondoa wapigakura kwenye mikwamo mbalimbali ikiwemo umaskini, Mhe. Makonda amesema Arusha inazo fursa mbalimbali za kiuwekezaji na ni muhimu kwa Wabunge hao kuweka alama ya utumishi wao wa kibunge kupitia uwekezaji wa maeneo mbalimbali mkoani Arusha ikiwemo sekta ya migahawa na hoteli kutokana na mahitaji makubwa ya huduma hizo.