Makonda sasa utujibu kuhusu sakata la Roma Mkatoliki

Makonda sasa utujibu kuhusu sakata la Roma Mkatoliki

Chakaza

JF-Expert Member
Joined
Mar 10, 2007
Posts
40,455
Reaction score
73,145


Tuhuma zako ni nyingi sana kuwa umeshiriki utekaji, mateso na hata uuaji. Pengine hizi tuhuma ni kweli au pia sio kweli. Lakini mwenye majibu kamili ni wewe mwenyewe.

Sasa tuambie ukweli, wakati watu wamejawa na mashaka kuwa Roma Mkatoliki ndio ametoweshwa kabisa kama Ben Saanane ulijitokeza na kusema atarejea Jumapili (kama vile alikuwa nyumbani kwako) na kweli alirudi.

Tuambie tena jee kina Saanane na Azory kwa nini nao hawakurudi "Jumapili" kama mwenzao?
Usione tuko kimya tuna majonzi makubwa mno.

Ili hayo yasiibuke tena kwenye hii mikutano ya kisiasa inayoanza tena nakushauri wahi kujibu tuhuma hizo na kama unasingiziwa lakini unaujua ukweli uweke wazi

Sent from my SM-A125F using JamiiForums mobile app
 
Kwa upande mwingine hata Serikali ilitakiwa itoe taarifa rasmi. Huyu Makonda kuna taarifa iliwahi kutolewa na Serikali ya US kuwa haruhusiwi kuingia nchini Marekani kwa sababu anakiuka haki za binadamu kwa kuwanyima watu haki ya kuishi.

Tuhuma nzito kabisa hizo, Serikali haikustahili kukaa kimya, ilitakiwa itolewe taarifa rasmi kwa umma. Iwaeleze wananchi kuwa tuhuma hizo ni za kweli au uwongo. Kama ni tuhuma za kweli, itamke watu ambao huyu bwana alishiriki kuwaondolea haki ya kuishi. Na pia iseme, imechukua hatua gani dhidi yake maana bado anaranda mitaani.

Kuwaondolea watu haki ya kuishi, japo imetumika lugha yenye mapungufu ya ukali lakini ni tuhuma nzito sana ambazo hazikustahili kuachwa tu!
 
Huo ujasiri nani angekuwa nao wakati mambo yalikuwa dhahir?
Tuhuma nzito kabisa hizo, Serikali haikustahili kukaa kimya, ilitakiwa itolewe taarifa rasmi kwa umma. Iwaeleze wananchi kuwa tuhuma hizo ni za kweli au uwongo. Kama ni tuhuma za kweli, itamke watu ambao huyu bwana alishiriki kuwaondolea haki ya kuishi. Na pia iseme, imechukua hatua gani dhidi yake maana bado anaranda mitaani.
 
Kwa upande mwingine hata Serikali ilitakiwa itoe taarifa rasmi. Huyu Makonda kuna taarifa iliwahi kutolewa na Serikali ya US kuwa haruhusiwi kuingia nchini Marekani kwa sababu anakiuka haki za binadamu kwa kuwanyima watu haki ya kuishi.

Tuhuma nzito kabisa hizo, Serikali haikustahili kukaa kimya, ilitakiwa itolewe taarifa rasmi kwa umma. Iwaeleze wananchi kuwa tuhuma hizo ni za kweli au uwongo. Kama ni tuhuma za kweli, itamke watu ambao huyu bwana alishiriki kuwaondolea haki ya kuishi. Na pia iseme, imechukua hatua gani dhidi yake maana bado anaranda mitaani.

Kuwaondolea watu haki ya kuishi, japo imetumika lugha yenye mapungufu ya ukali lakini ni tuhuma nzito sana ambazo hazikustahili kuachwa tu!

Makonda ashakua pinned na mmarekani hivo kutoboa kwa dunia hii kwake ndio basi tena.
 
Kwa upande mwingine hata Serikali ilitakiwa itoe taarifa rasmi. Huyu Makonda kuna taarifa iliwahi kutolewa na Serikali ya US kuwa haruhusiwi kuingia nchini Marekani kwa sababu anakiuka haki za binadamu kwa kuwanyima watu haki ya kuishi.

Tuhuma nzito kabisa hizo, Serikali haikustahili kukaa kimya, ilitakiwa itolewe taarifa rasmi kwa umma. Iwaeleze wananchi kuwa tuhuma hizo ni za kweli au uwongo. Kama ni tuhuma za kweli, itamke watu ambao huyu bwana alishiriki kuwaondolea haki ya kuishi. Na pia iseme, imechukua hatua gani dhidi yake maana bado anaranda mitaani.

Kuwaondolea watu haki ya kuishi, japo imetumika lugha yenye mapungufu ya ukali lakini ni tuhuma nzito sana ambazo hazikustahili kuachwa tu!
HAKI YA KUISHI WALIYOZUNGUMZIA MAREKANI NI ILE YA WALE JAMAA WA RAINBOW BAADA YA MAKONDA KUWAKAMATA KAMATA

MAKONDA NI NABII😜😜😜
 
Responsibility ni ya serikali na vyombo vya usalama kushughulikia hizo tuhuma, Makonda ni mtu mmoja kama wameshindwa wanajuana wenyewe and maybe hajahusika kama mnavyomshutumu🧐
 
HAKI YA KUISHI WALIYOZUNGUMZIA MAREKANI NI ILE YA WALE JAMAA WA RAINBOW BAADA YA MAKONDA KUWAKAMATA KAMATA

MAKONDA NI NABII😜😜😜
Basi na yeye achukue maji ya upako atembee nayo barabarani na Biblia...😅😅😅
 


Tuhuma zako ni nyingi sana kuwa umeshiriki utekaji, mateso na hata uuaji. Pengine hizi tuhuma ni kweli au pia sio kweli. Lakini mwenye majibu kamili ni wewe mwenyewe.
Sasa tuambie ukweli, wakati watu wamejawa na mashaka kuwa Roma Mkatoliki ndio ametoweshwa kabisa kama Ben Saanane ulijitokeza na kusema atarejea jumapili (kama vile alikuwa nyumbani kwako) na kweli alirudi.
Tuambie tena jee kina Saanane na Azory kwa nini nao hawakurudi "jumapili" kama mwenzao?
Usione tuko kimya tuna majonzi makubwa mno.
Ili hayo yasiibuke tena kwenye hii mikutano ya kisiasa inayoanza tena nakushauri wahi kujibu tuhuma hizo na kama unasingiziwa lakini unaujua ukweli uweke wazi

Sent from my SM-A125F using JamiiForums mobile app
Mwingine anayepaswa kujitokeza kujibu maswali haya ni Lazaro Mambosasa
 
Makonda ashakua pinned na mmarekani hivo kutoboa kwa dunia hii kwake ndio basi tena
Wakimbizi woote duniani huwa wanakimbilia Marekani Nchi ya Wenye Haki.

Ukipigwa pin US umekwisha.

Pamoja na kwamba madikiteta wanapenda Urusi na China na kuiga mambo yao hata siku moja mambi yakiwawia magumu hawakimbiliii huko Urusi wala China wala Korea
 
Back
Top Bottom