Makonda: Wageni kutoka nchi zilizoathirika na Corona wanapowasili tu huwekwa karantini katika Hotel maalum kwa siku 14

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Mkuu wa mkoa wa Dsm mh Makonda amesema wageni wote wanaoingia jijini wakitokea nchi zilizoathirika zaidi na corona watawekwa karantini ya siku 14 katika hoteli maalum kwa gharama zao wenyewe.

Makonda amesema Hotel hizo hazitatangazwa kwa sababu za kiusalama na kuepusha unyanyapaaji kwa wageni.

Kadhalika mh Makonda amewataka wananchi wa jiji la Dsm kuendelea kuzingatia usafi katika maeneo yao ikiwemo kunawa mikono kwa sabuni.

Source Channel ten tv!
 
Hivi bado kuna wageni wanaingia humu nchini?

Watu ambao katika nchi zao kutembea tu mitaani wanazuiwa,ndio kweli watakuja Bongo?

Alafu hii issue si tumeambiwa ina wasemaji maalumu?

Au restriction iko tu katika kutangaza idadi ya wagonjwa?
 
Kwa hiyo mgeni akitoka nje ya nchi akashukia mikoa mingine kisha kuingia DSM hausiki na karantini?! What is so special in DSM and not deserve to be cared to the rest of regions serious towards the campaign against this deadly disease?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Atashughulikiwa huko huko alikoingilia utaratibu uko wazi.
 
Gharama za kukaa karantini ni bei gani kwa siku?
 
Na yeye ameruhusiwa kuongelea hili suala? Au ni vile hawezagi kunyamaza?
 
Mkuu wangu wa mkoa nahisi kama angewaachia designated personnel wa kusemea hili janga waseme peke yao.
 
We ujui nguvu ya Naibu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…