Makonda: Wanaume wafanyakazi wakatwe asilimia 40 ya mishahara yao wapewe wake zao

Makonda: Wanaume wafanyakazi wakatwe asilimia 40 ya mishahara yao wapewe wake zao

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema anatarajia kupeleka muswada binafsi bungeni, kutaka itungwe sheria ambayo itamka mwanamume ambaye ni mfanyakazi, kukatwa asilimia 40 kwa ajili ya mke wake ambaye ni mama wa nyumbani.

Makonda alisema hayo wakati wa kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, iliyofanyika kimkoa kwenye Viwanja vya Leaders wilayani Kinondoni.

Makonda alisisitiza kuwa hataki kumwona mwanamke yeyote katika Mkoa wa Dar es Salaam akinyanyasika, ndio maana aliamua kuwasaidia wanawake waliotelekezwa na wenza wao na kutoa namba 0682009009 ambayo wanaweza kupiga bure.

Alisema baada ya kuona tatizo lilivyo kubwa la wanawake, ambao wanadhulumiwa mali za wenzao wao baada ya kufariki, kamati iliyokuwa ikisikiliza wajane hao iliandika mapendekezo sheria ya mirathi na imekabidhiwa kwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu.

“Baada ya kamati niliyounda kusikiliza madai ya mirathi tulikuta tatizo ni kubwa, hivyo tuliandika taarifa tukamkabidhi Ummy Mwalimu pia tukaomba sheria ya mirathi itamke kuwa endapo baba atatangulia mbele ya haki basi mama awe ndio msimamizi wa mirathi,” amesema Makonda.

Alisema Sheria ya Ndoa ya Tanzania, imerithiwa kutoka India na ina zaidi ya miaka 120, hivyo sheria ikimpa haki mama lazima atampa mali mwanawe, si kama baba wadogo au shangazi wanavyokuwa wasimamizi wanavyofanya mali hizo kuwanufaisha wao na familia zao na kuwaacha walengwa wakitaabika.

Makonda pia aliwataka wanawake kuwa walezi wazuri wa watoto wao, hata kama wametekelezwa, kuliko kuwajaza maneno yenye uchungu waliokutana nao baada ya kutelekezwa, kwani kufanya hivyo kunasababisha kuwa na kizazi kisichokuwa na maadili.

“Mama unamtolea mtoto wako maneno yenye uchungu baada ya kutelekezwa na baba yake, huyo mtoto haimuhusu kwani kila wakati mnakutana hakuwepo hivyo pambana na hali yako maana tunawafanya watoto waone maisha ndio yalivyo, wengine wanakataa kuolewa wakidhani wanaume wote wako hivyo,” alisema.

“Televisheni zimeleta malezi mengine kwa watoto wetu bila hata kwenda nje ya nchi wameiga tabia ambazo ni kinyume na maadili yetu hivyo wazazi jengeni tabia ya kuzungumza na watoto wenu na kufuatilia mwenendo wake, usingoje kujua tabia za mwanao kutoka kwa dada wa kazi au jirani,” aliongeza.

Alisema wanawake wanatakiwa kupambana na utamaduni wa makabila unaokataza wanawake kurithi mali, mfumo dume na kuishi kwa kusubiri kuambiwa unaweza bali mwanamke ajikubali kuwa anaweza bila kuambiwa na mtu.

Aliwataka wanawake kujiimarisha kiuchumi kwani akiwa na kipato hatonyanyasika, na kueleza kuwa katika kila halmashauri kuna mikopo isiyo na riba wanayoweza kukopa na kwa mwaka jana hadi sasa zaidi ya Sh bilioni 40 vimekopeshwa.

Kila mwaka Machi 8 ni Siku ya Wanawake Duniani na ilianza kutokana na jitihada za wanawake 15,000 mwaka 1908 walipoandamana jijini New York nchini Marekani, wakidai kupunguziwa muda wa kufanya kazi, ujira wa kuridhisha na haki ya kupiga kura.

Mwaka 1910 katika mkutano wa kimataifa wa wafanyakazi wanawake jijini Copenhagen nchini Denmark walikubaliana kwa pamoja na mara ya kwanza ilisherekewa mwaka 1911, Austria, Denmark, Ujerumani na Uswisi. Sherehe ya 100 ilifanyika mwaka 2011, hivyo mwaka huu ni sherehe ya 107 ya wanawake duniani na kitaifa imefanyika mkoani Simiyu ambako mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan.
View attachment 1381780
Chanzo: HabariLeo
Kwa sisi wengine ambao hatuja ajiriwa inakuaje tukiwa na wake zetu mswada wetu utakuaje maana kuna kaubaguzi hapa vile yaani
 
Wakifanya hivi Dkt Mwaka atabaki na asilimia ngapi maana bado ataongeza tena mke😂😂😂
 
He is dangerously stupid...
Ningemuona wa maana sana kama angeweza kusaidia kuongeza ajira za kinamama na wao wajiinue kiuchumi.

Hapa si tu kafanya kosa la kutoongeza uzalishaji (anataka kilichopo kigawanywe badala ya kuongeza uzalishaji), bali pia amewadhalilisha wanawake kuwa ni watu wasioweza kujitafutia wenyewe, mpaka wapewe kilichotafutwa na wanaume.
 
LEO TULIKUWA NA KIKAO KIZITO KWELI KWELI.
SISI TUKIWA MABAHARIA, TUMEFIKIA MAKUBALIANO KWAMBA KIONGOZ WETU ANAUONA MZURI SANA NA TUNAOMBA FIKIRA ZA KIONGOZI ZIDUMU(TUSEME WOTE JAMANI).
KWA HIVYO TUNAKUBALI 40% IKATWE, KAMA ITAMPENDEZA AKATE HATA 60%(MAANA ANAWEZA KWANI YEYE NDIYE MWAJIRI).
Lakini sasa:1.HATA TUKIMGONGA BARMAID MAGETONI TUSISEMWE MAANA 40% TUSHATOA,
2.TUSIULIZWE JUU YA ADABU ZA WATOTO KWANI 40% IPOO
3.TUSIULIZWE AKIPATWA NA MSIBA, MAGONJWA KWANI SI BADO 40% IPO MZEEBABA.
4.WAKWE,NDUGU N.K WASITUJUE KWANI 40% BADO IPOO.
zidumu fikra za kiongizi mtukufu!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukiweka hiyo 40%,bima ,heslb plus kodi unarudi na mbupu home mwisho wa mwezi
 
Ningemuona wa maana sana kama angeweza kusaidia kuongeza ajira za kinamama na wao wajiinue kiuchumi.

Hapa si tu kafanya kosa la kutoongeza uzalishaji (anataka kilichopo kigawanywe badala ya kuongeza uzalishaji), bali pia amewadhalilisha wanawake kuwa ni watu wasioweza kujitafutia wenyewe, mpaka wapewe kilichotafutwa na wanaume.

The guy is not that bright.

I mean, how does that empower women?

Badala ya kuja na mipango ya kuwainua wanawake, yeye anakuja na upuuzi wa kumfanya mwanamke aendelee kuwa duni na tegemezi kwa mwanaume!

Mwanamke kuendelea kuwa tegemezi kwa mwanaume, hakumuinui hata kidogo.

Aje na mpango wa kutoa mikopo midogo midogo yenye unafuu kwenye riba. Mikopo inayoweza kumsaidia mwanamke kuanzisha walau ka-biashara kake kadogo.

Aje na mipango ya kuwafunza wanawake kazi na kuwafunza biashara zenye manufaa kwao ili wawe na uhuru wa kifedha [financial independence].

Aje na mpango wa kuwafunza wanawake namna ya kuongeza vipato vyao na kuongeza akiba ya fedha.

Aje na mpango wa kuwajengea wanawake self-esteem na kuwafanya wajiamini [confidence].

Katika kufanya hayo, kwa kujua au hata kutojua, atakuwa anatengeneza viongozi katika jamii.

Wasichana wadogo wakikua huku wanaona wanawake wakijifanyia mambo wao wenyewe bila kutegemea wanaume, watakua wakijua kuwa hata wao wanaweza kufanya jambo lolote lile na jinsia yao si kikwazo.

Ila, mambo kama haya kwa mtu kama Makonda, ni mambo makubwa sana yaliyomzidi kimo.

Ndo maana anaona kumkata mwanaume asilimia 40 ya kipato chake kama ndo suluhisho 🤣.

The guy is dangerously stupid.

Picture him being president in an imperial presidency like the one we have now...

He could rule by diktat on a whim almost every single day.
 
The guy is not that bright.

I mean, how does that empower women?

Badala ya kuja na mipango ya kuwainua wanawake, yeye anakuja na upuuzi wa Kim fanya mwanamke aendelee kuwa duni na tegemezi kwa mwanaume!

Mwanamke kuendelea kuwa tegemezi kwa mwanaume, hakumuinui hata kidogo.

Aje na mpango wa kutoa mikopo midogo midogo yenye unafuu kwenye riba. Mikopo inayoweza kumsaidia mwanamke kuanzisha walau ka-biashara kake kadogo.

Aje na mipango ya kuwafunza wanawake kazi na kuwafunza biashara zenye manufaa kwao ili wawe na uhuru wa kifedha [financial independence].

Aje na mpango wa kuwafunza wanawake namna ya kuongeza vipato vyao na kuongeza akiba ya fedha.

Aje na mpango wa kuwajengea wanawake self-esteem na kuwafanya wajiamini [confidence].

Katika kufanya hayo, kwa kujua au hata kutojua, atakuwa anatengeneza viongozi katika jamii.

Wasichana wadogo wakikua huku wanaona wanawake wakijifanyia mambo wao wenyewe bila kutegemea wanaume, watakua wakijua kuwa hata wao wanaweza kufanya jambo lolote lile na jinsia yao si kikwazo.

Ila, mambo kama haya kwa mtu kama Makonda, ni mambo makubwa sana yaliyomzidi kimo.

Ndo maana anaona kumkata mwanaume asilimia 40 ya kipato chake kama ndo suluhisho 🤣.

The guy is dangerously stupid.

Picture him being president in an imperial presidency like the one we have now...

He could rule by diktat on a whim almost every single day.
Lawama kwa Kikwete na Magufuli aliyemteua na anayeendelea kumuacha.

Lakini naona Magufuli naye haoni tatizo, kwa sababu wote hawajapishana kitu.
 
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema anatarajia kupeleka muswada binafsi bungeni, kutaka itungwe sheria ambayo itamka mwanamume ambaye ni mfanyakazi, kukatwa asilimia 40 kwa ajili ya mke wake ambaye ni mama wa nyumbani.

Makonda alisema hayo wakati wa kilele cha maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani, iliyofanyika kimkoa kwenye Viwanja vya Leaders wilayani Kinondoni.

Makonda alisisitiza kuwa hataki kumwona mwanamke yeyote katika Mkoa wa Dar es Salaam akinyanyasika, ndio maana aliamua kuwasaidia wanawake waliotelekezwa na wenza wao na kutoa namba 0682009009 ambayo wanaweza kupiga bure.

Alisema baada ya kuona tatizo lilivyo kubwa la wanawake, ambao wanadhulumiwa mali za wenzao wao baada ya kufariki, kamati iliyokuwa ikisikiliza wajane hao iliandika mapendekezo sheria ya mirathi na imekabidhiwa kwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu.

“Baada ya kamati niliyounda kusikiliza madai ya mirathi tulikuta tatizo ni kubwa, hivyo tuliandika taarifa tukamkabidhi Ummy Mwalimu pia tukaomba sheria ya mirathi itamke kuwa endapo baba atatangulia mbele ya haki basi mama awe ndio msimamizi wa mirathi,” amesema Makonda.

Alisema Sheria ya Ndoa ya Tanzania, imerithiwa kutoka India na ina zaidi ya miaka 120, hivyo sheria ikimpa haki mama lazima atampa mali mwanawe, si kama baba wadogo au shangazi wanavyokuwa wasimamizi wanavyofanya mali hizo kuwanufaisha wao na familia zao na kuwaacha walengwa wakitaabika.

Makonda pia aliwataka wanawake kuwa walezi wazuri wa watoto wao, hata kama wametekelezwa, kuliko kuwajaza maneno yenye uchungu waliokutana nao baada ya kutelekezwa, kwani kufanya hivyo kunasababisha kuwa na kizazi kisichokuwa na maadili.

“Mama unamtolea mtoto wako maneno yenye uchungu baada ya kutelekezwa na baba yake, huyo mtoto haimuhusu kwani kila wakati mnakutana hakuwepo hivyo pambana na hali yako maana tunawafanya watoto waone maisha ndio yalivyo, wengine wanakataa kuolewa wakidhani wanaume wote wako hivyo,” alisema.

“Televisheni zimeleta malezi mengine kwa watoto wetu bila hata kwenda nje ya nchi wameiga tabia ambazo ni kinyume na maadili yetu hivyo wazazi jengeni tabia ya kuzungumza na watoto wenu na kufuatilia mwenendo wake, usingoje kujua tabia za mwanao kutoka kwa dada wa kazi au jirani,” aliongeza.

Alisema wanawake wanatakiwa kupambana na utamaduni wa makabila unaokataza wanawake kurithi mali, mfumo dume na kuishi kwa kusubiri kuambiwa unaweza bali mwanamke ajikubali kuwa anaweza bila kuambiwa na mtu.

Aliwataka wanawake kujiimarisha kiuchumi kwani akiwa na kipato hatonyanyasika, na kueleza kuwa katika kila halmashauri kuna mikopo isiyo na riba wanayoweza kukopa na kwa mwaka jana hadi sasa zaidi ya Sh bilioni 40 vimekopeshwa.

Kila mwaka Machi 8 ni Siku ya Wanawake Duniani na ilianza kutokana na jitihada za wanawake 15,000 mwaka 1908 walipoandamana jijini New York nchini Marekani, wakidai kupunguziwa muda wa kufanya kazi, ujira wa kuridhisha na haki ya kupiga kura.

Mwaka 1910 katika mkutano wa kimataifa wa wafanyakazi wanawake jijini Copenhagen nchini Denmark walikubaliana kwa pamoja na mara ya kwanza ilisherekewa mwaka 1911, Austria, Denmark, Ujerumani na Uswisi. Sherehe ya 100 ilifanyika mwaka 2011, hivyo mwaka huu ni sherehe ya 107 ya wanawake duniani na kitaifa imefanyika mkoani Simiyu ambako mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan.
View attachment 1381780
Chanzo: HabariLeo
Aibu ya kung'azishwa na bawacha... Anataka ajisafishe aonekane alikuwa na nia nzuri.
 
Nimekutana na bango kwenye hizi skrini zenu za matangazo barabarani [ADN], muda huo linasomeka “TANZANIA NI TAJIRI”.... kwa hayo machache naunga mkono hoja yako.

Nchi iuzwe tugawane kila mtu afe na chake, maisha yenyewe yako wapi.... mara Corona hii hapa.
Niliiona hii kwenye kituo cha mwendokasi.
 
Huyu Makonda ana ajenda gani na wanawake? kila siku wanawake wanawake kama anawahurumia na anatakakuwasaidia kweli,siaitake serekali yake iwalipe wanawake hizo asilimia 40 kupitia kwenye mshahara wa waume zao kuliko kutoa matamko ambayo hayawezekani wakati mshahara wenyewe hata nusu mwezi hautoshi.
 
Amekuwa bunge kupitisha hiyo sheria au anabwabwaja ovyo kama kawaida yake. This man ooh, tuzidi kumhurumia tu!!!
 
Hivi anaijua mentality ya mwanamke? akipewa hiyo 40% bado ataikodolea macho ile uliyobaki nayo ifanye matumizi yote ya nyumbani pamoja na nywele zake na kucha, hiyo 40% inakoishia haijulikani..
 
Hili jamii daima huwa linaibua vitu minor, na vyote halivikamilishi.Kwa kufikiria kipuuzi,linadhalilisha u RC!Kwa kukirupuka hv,inafaa litumbuliwe, cjui uncle huwa analilea kwa nn yan!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom