Ali Nassor Px
JF-Expert Member
- May 6, 2022
- 2,384
- 3,926
Imechambuliwa na kuandikwa na Ally Nassor Px .
Tarehe 5 February 2023.
Sehemu ya kwanza kuipost ni hapa JF sehemu ya pili itakuwa ni Facebook na mwisho kabisa nitamalizia Twitter.
...........................................................
Video imetoka juzi Tarehe 3 mwezi wa pili mwaka 2023.
Saa 4 kamili asubuhi.
ikiwa imeongozwa na director ivan.
mpaka sasa tarehe 5 mwezi wa pili 2023 video hii ina jumla ya watazamaji
Milioni 2.4
nilichopenda kwenye video ya zuwena ni video ambayo inaonesha uhalisia wa kinachoimbwa na ningependa kuoana zaidi na zaidi video zenye uhalisia na kile kinachoimbwa inawezekana kikatutambulisha jamii ya watanzania kirahisi kwa jamii nyingine.
Twende moja kwa moja kwenye uchambuzi wa video yenyewe.
video ni kali sana kwa upande wangu naipa rate ya 8 / 10. kuna baadhi ya makosa ya ufundi yalionekana kwenye video lakini hauwezi kuyaona mpaka utulie ila mimi nataka nikuoneshe.
..........................................................
1. MMASAI WA BANDIA
Mwanzo wa video sekunde ya 33 ( 00:33).
anaonekana jamaa wenye asili ya kimasai akikimbiza punda wawili.
ila kama utakuwa makini utangundua kuwa yule sio Mmasai halisi. wakati mmasai halisi alikuwepo kwenye video alionekana alipiga gitaa mwanzo kabisa Sekunde ya 3 ( 00: 03).
mmasai aliyekuwa akikimbiza punda alionekana wa kutengeneza ukitazama alikuwa kavaa soksi chini na buti la Timberland (rangi ya bagia ).
...............................................................
2. MUHUSIKA MMOJA KUOENEKANA SEHEMU MBILI TOFAUTI.
Ukitazama video sekunde ya 46 ( 00: 46).
kuna mzee utamuona alikuwa anasoma urithi. na inajulikana siku zote mtu ambaye anapewa jukumu la kusoma urithi ni mtu wenye heshima zake na anaaminiwa sana.
Sasa ukitazama video ya zuwena utamuona yule mzee aliyekuwa anasoma hosia wa urithi.
aonekana akiwa bar anamtunza zuwena alivyokuwa anacheza juu ya meza dakika ya (1 : 40).
...............................................................
3. TATOO ZA DIAMOND NA KIPINI PUANI.
Inawezekana ni ngumu sana kumpiga diamond make up ambayo itaficha tattoo zake. ila inaonesha director alisahau pia ata kumwambia diamond atoe japo kile kipini chake pale puani mwanzo mpaka mwisho wa video diamond anaonekana na kipini puani.
kumbuka video imebeba uhalisia wa maisha ya watu wa kipato cha chini ni ngumu sana kumkuta mtu wa kipato cha chini ana tatoo mwilini na kipini puani.
............................................................
4. MTU KUCHEKA KWENYE TUKIO LA KUSHTUA.
Ukitazama vizuri dakika ya ( 2: 14).
kipande ambacho diamond anaenda kumuokoa zuwena alivyokuwa anataka kubakwa.
kuna jamaa mmoja kati ya wale wabakaji wanne kuna jamaa kavaa koti jeusi na suruali nyeupe. wakati wenzake wameshituka mmoja anapandisha suruali fasta fasta yeye alikuwa anamtazama mwenzake anayepandisha suruali huku akicheka.
..............................................................
5. MATANGAZO YA MAKAMPUNI MBALIMBALI .
Mwaka 2012 Ronaldinho Gaucho alifutiwa mkataba na company ya Cocacola baada ya kuonekana chupa za Pepsi kwenye mkutano wake na waandishi wa habari.
kuonekana chupa ya soda ya Pepsi. ila habari za Ronaldinho tuachane nazo.
Kila mtu anajua kuwa Diamond ukiachana na kujishusisha na sekta ya muziki lakini pia ni Company ambassador wa company mbalimbali.
sasa sijajua kuwa diamond ana mkataba na kampuni mbalimbali zilizoonekana kwenye video yake.
Dakika ya (1:00) Yanaonekana madish mawili ya Azam Tv juu ya mabanda yanayouza nguo.
Dakika ya ( 2: 06) linaonekana tangazo la TTCL na DOUBLEMINT
Dakika ya ( 2: 10 ) Diamond anaonekana anandesha pikipiki ya kutoka company ya TOYO.
Dakika ya ( 2: 12) hadi dakika ya 2: 22) akiwa kaingia kumuokoa zuwena na anatoka pia yanaoenaka maboksi ya company ya MSAFI, KASUKU na JUMBO
Dakika ya ( 3: 33) akiwa bar anaimba kwa mbali yanaonekana mafriji ya Coca-cola wakati kila mtu anajua diamond ni Ambassador wa Pepsi.
....................................
6. KUONEKANA KWA NEMBO YA SERENGETI LAGER.
Uwenda point hii isiwe na nguvu sana ila point hii ndio inaweza ukaipa nguvu zaidi point namba 5 kuonekana kwa matangazo mbalimbali ya makampuni mbalimbali.
ukitazama bar watu wote walikuwa wanakunywa bia ambazo zilikuwa hazina utambulisho wa nembo kuwa ni bia za aina gani na zinatokea kampuni gani.
hii yote ilikuwa kutoonesha nembo ya kampuni ambayo diamond ana ubalozi nayo.
ila dakika ya ( 3:50) kuna kosa lilifanyika kuna muhudumu anatembea na chupa za bia. kuna chupa mmoja inaaonekana na nembo la SERENGETI LAGER.
_____________________________________
Lengo la kuandika uzi huu sio kukosoa na kuishusha hadhi video ya msanii husika ila ni kukumbusha uwepo umakini zaidi kwa waongozi ( Madirector).
Nadhani Msanii husika hana kosa katimiza wajibu wake kwa asilimia kubwa sana kaimba nyimbo kali lakini pia ka act vizuri sana kwenye video kwa maelekezo ya director.
Tarehe 5 February 2023.
Sehemu ya kwanza kuipost ni hapa JF sehemu ya pili itakuwa ni Facebook na mwisho kabisa nitamalizia Twitter.
...........................................................
Video imetoka juzi Tarehe 3 mwezi wa pili mwaka 2023.
Saa 4 kamili asubuhi.
ikiwa imeongozwa na director ivan.
mpaka sasa tarehe 5 mwezi wa pili 2023 video hii ina jumla ya watazamaji
Milioni 2.4
nilichopenda kwenye video ya zuwena ni video ambayo inaonesha uhalisia wa kinachoimbwa na ningependa kuoana zaidi na zaidi video zenye uhalisia na kile kinachoimbwa inawezekana kikatutambulisha jamii ya watanzania kirahisi kwa jamii nyingine.
Twende moja kwa moja kwenye uchambuzi wa video yenyewe.
video ni kali sana kwa upande wangu naipa rate ya 8 / 10. kuna baadhi ya makosa ya ufundi yalionekana kwenye video lakini hauwezi kuyaona mpaka utulie ila mimi nataka nikuoneshe.
..........................................................
1. MMASAI WA BANDIA
Mwanzo wa video sekunde ya 33 ( 00:33).
anaonekana jamaa wenye asili ya kimasai akikimbiza punda wawili.
ila kama utakuwa makini utangundua kuwa yule sio Mmasai halisi. wakati mmasai halisi alikuwepo kwenye video alionekana alipiga gitaa mwanzo kabisa Sekunde ya 3 ( 00: 03).
mmasai aliyekuwa akikimbiza punda alionekana wa kutengeneza ukitazama alikuwa kavaa soksi chini na buti la Timberland (rangi ya bagia ).
...............................................................
2. MUHUSIKA MMOJA KUOENEKANA SEHEMU MBILI TOFAUTI.
Ukitazama video sekunde ya 46 ( 00: 46).
kuna mzee utamuona alikuwa anasoma urithi. na inajulikana siku zote mtu ambaye anapewa jukumu la kusoma urithi ni mtu wenye heshima zake na anaaminiwa sana.
Sasa ukitazama video ya zuwena utamuona yule mzee aliyekuwa anasoma hosia wa urithi.
aonekana akiwa bar anamtunza zuwena alivyokuwa anacheza juu ya meza dakika ya (1 : 40).
...............................................................
3. TATOO ZA DIAMOND NA KIPINI PUANI.
Inawezekana ni ngumu sana kumpiga diamond make up ambayo itaficha tattoo zake. ila inaonesha director alisahau pia ata kumwambia diamond atoe japo kile kipini chake pale puani mwanzo mpaka mwisho wa video diamond anaonekana na kipini puani.
kumbuka video imebeba uhalisia wa maisha ya watu wa kipato cha chini ni ngumu sana kumkuta mtu wa kipato cha chini ana tatoo mwilini na kipini puani.
............................................................
4. MTU KUCHEKA KWENYE TUKIO LA KUSHTUA.
Ukitazama vizuri dakika ya ( 2: 14).
kipande ambacho diamond anaenda kumuokoa zuwena alivyokuwa anataka kubakwa.
kuna jamaa mmoja kati ya wale wabakaji wanne kuna jamaa kavaa koti jeusi na suruali nyeupe. wakati wenzake wameshituka mmoja anapandisha suruali fasta fasta yeye alikuwa anamtazama mwenzake anayepandisha suruali huku akicheka.
..............................................................
5. MATANGAZO YA MAKAMPUNI MBALIMBALI .
Mwaka 2012 Ronaldinho Gaucho alifutiwa mkataba na company ya Cocacola baada ya kuonekana chupa za Pepsi kwenye mkutano wake na waandishi wa habari.
kuonekana chupa ya soda ya Pepsi. ila habari za Ronaldinho tuachane nazo.
Kila mtu anajua kuwa Diamond ukiachana na kujishusisha na sekta ya muziki lakini pia ni Company ambassador wa company mbalimbali.
sasa sijajua kuwa diamond ana mkataba na kampuni mbalimbali zilizoonekana kwenye video yake.
Dakika ya (1:00) Yanaonekana madish mawili ya Azam Tv juu ya mabanda yanayouza nguo.
Dakika ya ( 2: 06) linaonekana tangazo la TTCL na DOUBLEMINT
Dakika ya ( 2: 10 ) Diamond anaonekana anandesha pikipiki ya kutoka company ya TOYO.
Dakika ya ( 2: 12) hadi dakika ya 2: 22) akiwa kaingia kumuokoa zuwena na anatoka pia yanaoenaka maboksi ya company ya MSAFI, KASUKU na JUMBO
Dakika ya ( 3: 33) akiwa bar anaimba kwa mbali yanaonekana mafriji ya Coca-cola wakati kila mtu anajua diamond ni Ambassador wa Pepsi.
....................................
6. KUONEKANA KWA NEMBO YA SERENGETI LAGER.
Uwenda point hii isiwe na nguvu sana ila point hii ndio inaweza ukaipa nguvu zaidi point namba 5 kuonekana kwa matangazo mbalimbali ya makampuni mbalimbali.
ukitazama bar watu wote walikuwa wanakunywa bia ambazo zilikuwa hazina utambulisho wa nembo kuwa ni bia za aina gani na zinatokea kampuni gani.
hii yote ilikuwa kutoonesha nembo ya kampuni ambayo diamond ana ubalozi nayo.
ila dakika ya ( 3:50) kuna kosa lilifanyika kuna muhudumu anatembea na chupa za bia. kuna chupa mmoja inaaonekana na nembo la SERENGETI LAGER.
_____________________________________
Lengo la kuandika uzi huu sio kukosoa na kuishusha hadhi video ya msanii husika ila ni kukumbusha uwepo umakini zaidi kwa waongozi ( Madirector).
Nadhani Msanii husika hana kosa katimiza wajibu wake kwa asilimia kubwa sana kaimba nyimbo kali lakini pia ka act vizuri sana kwenye video kwa maelekezo ya director.