Makosa ndani ya Makala ya Mama Maria Nyerere Kutimiza Miaka 93

Makosa ndani ya Makala ya Mama Maria Nyerere Kutimiza Miaka 93

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
MAKALA YA MAMA MARIA NYERERE KUTIMIZA MIAKA 93 NA MAKOSA NDANI YA MAKALA

Kuna makala imewekwa mtandaoni kuhusu Mama Maria Nyerere kutimiza miaka 93 hii leo.

Makala hii imesheheni mengi katika maisha ya Mama Maria.

Nimeisoma na imenifurahisha na kunielimisha katika mengi ambayo sikuwa nayajua vyema.

Juu ya hayo yote makala hii imeruka sehemu muhimu sana katika maisha yake na kwa kweli si yake tu bali na ya mumewe Mwalimu Nyerere na historia ya TANU na pia kuandika mengine ambayo si ya kweli.

Makala hii inazungumza duka alilofungua Mama Maria Magomeni.

Mwandishi anaeleza duka hili kuwa duka lililokuwa linauza bidha kadhaa.

Hii si kweli Mama Maria alikuwa na duka dogo la kuuza mafuta ya taa.

Yako makosa mengi lakini hapa sitayazungumza tutizame hili hapo chini:

‘’In the mid 1950s, Mwalimu & his family were living at Magomeni Mapipa where they rented a small house.

This was after they had stayed in John Rupia's house at Mission Quarter, Kariakoo for one year.

This followed Mwalimu Nyerere's abrupt resignation as a teacher at St. Francis Pugu on March 22, 1955.

Mama Maria, to make ends meet, opened a small shop in their small house at Magomeni to sell sugar, soaps, salt, cooking oil etc.

She believed in living within her means and working hard for everything.

She was a rock to Mwalimu Nyerere's family.’’

Nimerekebisha machache katika historia ya Mama Maria Nyerere kwa kueleza historia yake kwa kutumia maelezo ya wale waliompokea Mwalimu alipofika Dar es Salaam mwaka wa 1952 ili historia muhimu ifahamike vizuri kwa faida ya kizazi hiki na kizazi kijacho:

"Napenda kueleza kitu kidogo katika historia ya Mama Maria Nyerere.

Katika akina mama wa mwanzo kufahamiana na Mama Maria Nyerere alikuwa Bi. Mwamvua bint Mrisho maarufu kwa jina la Mama Daisy.

Walifahamiana kwa kuwa Mama Daisy alikuwa mke wa Abdul Sykes na kama tujuavyo Mwalimu Nyerere baada ya kuacha kazi ya ualimu alikwenda kuishi nyumbani kwa Abdul Sykes Mtaa wa Stanley na Sikukuu.

Hapa ndipo Mama Maria na Mama Daisy walipounga udugu.

Hii ilikuwa mwaka wa 1955.

Mama Daisy amenihadithia anasema baada ya miaka mingi kupita alikutana na Mama Maria Ukumbi wa Diamond Jubilee Mwalimu alipotoa hotuba kuwaaga Wazee wa Dar es Salaam.

Mama Maria alichukua fursa hii kuonana na kuzungumza na akina mama wa Dar-es-Salaam.

Mama Maria na Mama Daisy walikumbatiana kwa mapenzi Mama Maria akaieleza hadhira ile kuwa Mama Daisy na mumewe ndiyo waliowapokea yeye na mumewe Dar es Salaam.

Duka la mafuta ya taa la Mama Maria alilifungua Mtaa wa Mchikichi na Livingstone wakati wanaishi nyumbani kwa Abdul Sykes.

Akina mama ambao walikuwa jirani na duka hili walikuwa Bi. Chiku bint Said Kisusa ambae alikuwa anaishi mtaa huo wa Mchikichi kona na New Street (sasa Lumumba Avenue).

Duka la mafuta ya taa la Magomeni Mapipa Mama Maria alilifungua nyumbani kwa Ali Msham Mtaa wa Jaribu.

Ali Msham alikuwa amefungua tawi la TANU nyumbani kwake na Mwalimu alipohamia Maduka Sita Magomeni ikabidi Mama Maria awe anakwenda Kariakoo kila siku.

Ali Msham ndipo alipotoa nafasi nyumbani kwake duka lihamishiwe hapo ili kumpumzisha Mama Maria na shida ya kuparamia mabasi na watoto asubuhi kwenda Kariakoo.

Duka la mafuta ya taa la Mama Maria la hapo Maduka Sita lilikuja baadae.

Tunamtakia Mama Maria umri tawil na afya njema."

Picha hiyo hapo chini ni nyumba ya Mwalimu Maduka Sita Magomeni na huyo anaeingia ndani ya nyumba hiyo ni yeye mwenyewe.

Angalia bango juu ya nyumba linalotangaza duka la mafuta ya taa.

323194726_553729993036637_5201274679647759998_n.jpg
 
Always historia kama hii iwe na ukweli, welldone mtoa mada na kuelezea ukweli, sasa mwenye ukweli zaidi au bora wa huu pls ulete hapa na sio kejeli
Nkanini,
Naamini kabisa mwandishi hakuwa na nia ya kupotosha historia yeye kaandika kama alivyopokea historia hiyo kutoka vyanzo.

Tofauti iliyopo kutoka vyanzo hivyo na historia niliyoandika mimi baada ya kuona makosa ya historia iliyokuwako ni kuwa mimi nimeiandika historia upya kutokana na kwanza Nyaraka za Sykes.

Hawa ndiyo waliokuwa na yote kuanzia mwanzo African Association ilipoundwa na baba yao 1929.

Watoto na wao wakawa ndani ya uongozi wa siasa za Tanganyika kuanzia 1947 baada ya WW II.

Na hawa watoto ndiyo wakaja kumpokea Julius Nyerere 1952 na wakawa nae Mwalimu akiwa Pugu anasomesha kisha wakaishi nae nyumbani kwao 1955 alipoacha kazi na kuwa mtumishi wa TANU.

Ilipoandikwa historia ya TANU na Chuo Kikuu Cha CCM Kivukoni akina Sykes hawakuhojiwa.

Huu ndiyo ukawa mwanzo wa kuwa na historia iliyokuwa haina ukweli.

Ally Sykes akanipa nyaraka alizokuwanazo kuhusu historia hii nami nikaandika kitabu ambacho wengi sasa mnakifahamu.
 
Bado kipo hiki mkuu?
Uzuri umeweka picha ambayo ina bango la kuwa ni mawakala wa mafuta ya taa ya Shell Crown. Lakini pia kuna bango la Cocacola na pembeni kuna lingine ambalo bidhaa zake hazionekani vizuri. Kwa picha hiyo ni dhahiri kuwa alikuwa anauza bidhaa zaidi ya mafuta ya taa. Sasa kama kwenye hili unasema uongo kwa nini tukuamini kwenye mengine?

Amandla.....
Nguruvi3 JokaKuu
 
Uzuri umeweka picha ambayo ina bango la kuwa ni mawakala wa mafuta ya taa ya Shell Crown. Lakini pia kuna bango la Cocacola na pembeni lingine ambalo bidhaa zake hazionekani vizuri. Kwa picha hiyo ni dhahiri kuwa alikuwa anauza bidhaa zaidi ya mafuta ya taa. Sasa kama kwenye hili unasema uongo kwa nini tukuamini kwenye mengine?

Amandla.....
Nguruvi3 JokaKuu
Fundi...
Sikutegemea kuaminiwa na kila mtu.
Unasoma na ikiwa unaona ni uongo basi.

Hatuwezi kugombana.

Lakini kuna watu wajuzi wa African History mimi wananiamini wananipa kazi na wananialika kwenye vyuo vyao kuzungumza na wananialika kwenye mikutano.

Nilitiwa katika mradi wa Oxforfd University Press, Nairobi wa kuandika historia kwa shule za msingi na wamechapa kitabu changu, ''The Torch on Kilimanjaro,'' (2007) na kunishirikisha katika kingine kilichojumuisha waandishi wa nchi tofauti za Afrika, ''The Mermaid of Msambweni,'' (African Anthology) (2008).

Vitabu vyangu vingine vipya ni ''The School Trip to Zanzibar,'' (2020) na ''Rajabu Ibrahim Kirama Jemadari wa Vita Kuwa Jemadari wa Uislam,'' (2021).

Nimeshirikishwa pia katika mradi wa Harvard na Oxford University Press, New York kuandika Dictionary of African Biography (DAB) (2011) na niliombwa kuandika historia ya Kleist Sykes (1894 - 1949).

Wewe kughitilafiana na mimi na kuniona muongo ni jambo la kawaida sana wala hufanyi hivyo kwa kuwa unanichukia.

Hii ni silka ya sisi sote binadamu kuona kitu kwa sura tofauti.
Ingekuwa sote tunakubaliana kila kitu dunia ingechusha.

Hii ndiyo sababu sijajitetea na kulazimisha niaminike ila nimesema lile ninalolijua kuwa Mama Maria biashara yake ilikuwa ni kuuza mafuta ya taa.

Hata katika Nyerere Biography (2020) imeandikwa hivyo.

Historia hii ya duka la mafuta ya taa si wengi walikuwa wanaijua hadi pale mimi nilipoiandika na mimi nimeijua kwa kuwa wanunuzi wake wake walikuwa shangazi zangu akina Mwalimu Sakina na Mwalimu Fatna wakiishi Mtaa wa Mchikichi na wakijuana na Nyerere na Mama Maria.

1672547267652.jpeg
1672547340768.png
1672547761564.jpeg
1672548892490.jpeg




 
Fundi...
Sikutegemea kuaminiwa na kila mtu.
Unasoma na ikiwa unaona ni uongo basi.

Hatuwezi kugombana.

Lakini kuna watu wajuzi wa African History mimi wananiamini wananipa kazi na wananialika kwenye vyuo vyao kuzungumza na wananialika kwenye mikutano.

Nilitiwa katika mradi wa Oxforfd University Press, Nairobi wa kuandika historia kwa shule za msingi na wamechapa kitabu changu, ''The Torch on Kilimanjaro,'' (2007) na kunishirikisha katika kingine kilichojumuisha waandishi wa nchi tofauti za Afrika, ''The Mermaid of Msambweni,'' (African Anthology) (2008).

Vitabu vyangu vingine vipya ni ''The School Trip to Zanzibar,'' (2020) na ''Rajabu Ibrahim Kirama Jemadari wa Vita Kuwa Jemadari wa Uislam,'' (2021).

Nimeshirikishwa pia katika mradi wa Harvard na Oxford University Press, New York kuandika Dictionary of African Biography (DAB) (2011) na niliombwa kuandika historia ya Kleist Sykes (1894 - 1949).

Wewe kughitilafiana na mimi na kuniona muongo ni jambo la kawaida sana wala hufanyi hivyo kwa kuwa unanichukia.

Hii ni silka ya sisi sote binadamu kuona kitu kwa sura tofauti.
Ingekuwa sote tunakubaliana kila kitu dunia ingechusha.

Hii ndiyo sababu sijajitetea na kulazimisha niaminike ila nimesema lile ninalolijua kuwa Mama Maria biashara yake ilikuwa ni kuuza mafuta ya taa.

Hata katika Nyerere Biography (2020) imeandikwa hivyo.

Historia hii ya duka la mafuta ya taa si wengi walikuwa wanaijua hadi pale mimi nilipoiandika na mimi nimeijua kwa kuwa wanunuzi wake wake walikuwa shangazi zangu akina Mwalimu Sakina na Mwalimu Fatna wakiishi Mtaa wa Mchikichi na wakijuana na Nyerere na Mama Maria.

View attachment 2465067View attachment 2465069View attachment 2465075View attachment 2465083



Mohammed, una kawaida ya kutaka kuaminiwa hata kama ulichokiandika kina mashaka. Kwa vile unaamini kuwa hamna mtu mwingine anayeijua historia ya Nyerere kuliko wewe basi tu akikataa kukubaliana na kila unachosema unaona ana kuchukia. Mimi nimekupinga kutokana na kile ambacho wewe mwenyewe umekiweka kama ushahidi kuwa Mama Maria alikuwa anafanya biashara ya mafuta ya taa. Mimi sipingi kuwa alikuwa anafanya biashara hiyo la hasha. Ninachopinga ni wewe kumpinga muandishi mwenzako ambae alisema alikuwa anauza vitu vingi kidogo, ukikazania kuwa alikuwa anauza mafuta peke yake. Lakini ukiangalia poster zilizo nje ya hilo duka tunaona zinatangaza Coca-Cola na vitu vingine. Na hii ilikuwa ni kawaida na inaendelea mpaka sasa. Ni wafanyabiashara wachache sana wanaoweza kuspecialise kwenye kitu kimoja.

Umepinga pia kuwa hakuishi kwenye nyumba ya Rupia bali aliishi kwa wakina Sykes. Hili nalo unali complicate bila sababu. Inawezekana kabisa kuwa Mwalimu alipoacha kazi alihamia kwa Sykes. Lakini vile vile kuna uwezekano kuwa baada ya hapo alihamia kwenye mojawapo ya nyumba za Rupia ambae inajulikana kuwa alikuwa ana nyumba nyingi tu.

Unatuelezea urafiki wa mke wake Sykes na mama Maria kana kwamba alikuwa rafiki yake pekee. Mama Maria ni mkatoliki na bila shaka alikuwa na marafiki wengi zaidi ya mama Daisy.

Mimi siku zote nakuambia kuwa nafurahia simulizi zako za wazee wako wa Gerezani na ninaamini ni mchango mzuri katika historia yako. Ninachokupinga ni pale unapotaka kuifanya hiyo ndio historia pekee inayotakiwa kupewa uzito.

Amandla...
 
Mohammed, una kawaida ya kutaka kuaminiwa hata kama ulichokiandika kina mashaka. Kwa vile unaamini kuwa hamna mtu mwingine anayeijua historia ya Nyerere kuliko wewe basi tu akikataa kukubaliana na kila unachosema unaona ana kuchukia. Mimi nimekupinga kutokana na kile ambacho wewe mwenyewe umekiweka kama ushahidi kuwa Mama Maria alikuwa anafanya biashara ya mafuta ya taa. Mimi sipingi kuwa alikuwa anafanya biashara hiyo la hasha. Ninachopinga ni wewe kumpinga muandishi mwenzako ambae alisema alikuwa anauza vitu vingi kidogo, ukikazania kuwa alikuwa anauza mafuta peke yake. Lakini ukiangalia poster zilizo nje ya hilo duka tunaona zinatangaza Coca-Cola na vitu vingine. Na hii ilikuwa ni kawaida na inaendelea mpaka sasa. Ni wafanyabiashara wachache sana wanaoweza kuspecialise kwenye kitu kimoja.

Umepinga pia kuwa hakuishi kwenye nyumba ya Rupia bali aliishi kwa wakina Sykes. Hili nalo unali complicate bila sababu. Inawezekana kabisa kuwa Mwalimu alipoacha kazi alihamia kwa Sykes. Lakini vile vile kuna uwezekano kuwa baada ya hapo alihamia kwenye mojawapo ya nyumba za Rupia ambae inajulikana kuwa alikuwa ana nyumba nyingi tu.

Unatuelezea urafiki wa mke wake Sykes na mama Maria kana kwamba alikuwa rafiki yake pekee. Mama Maria ni mkatoliki na bila shaka alikuwa na marafiki wengi zaidi ya mama Daisy.

Mimi siku zote nakuambia kuwa nafurahia simulizi zako za wazee wako wa Gerezani na ninaamini ni mchango mzuri katika historia yako. Ninachokupinga ni pale unapotaka kuifanya hiyo ndio historia pekee inayotakiwa kupewa uzito.

Amandla...
Fundi...
Unanitilia maneno yako kinywani mwangu.

Sijasema popote unanichukia.

Sijapata kusema nataka niaminiwe kwa haya niyajuayo.

Hiyo ni khiyari ya mtu sina uwezo wa kulazimisha.

Hilo la kuwa hakuna mtu ajuaye historia ya Nyerere kunishinda maneno hayo kasema Prof. Shivji baada ya kufanya mahojiano na mimi wakati wanatafiti Nyerere Biography.

Hakuishia hapo katika Nyerere Biography wameandika kuwa Maktaba yangu ni kati ya maktaba 3 kubwa katika historia ya Nyerere.

Maktaba zingine 2 ni ya Dr. Salim Ahmed Salim na ya Brig. General Hashim Mbita.

Historia inasema Mama Maria biashara yake ilikuwa mafuta ya taa sikupata kusikia popote kuwa alikuwa anauza na bidhaa zingine.

Hata Nyerere Biography inasema hivyo.

Kuhusu nyumba aliyoishi Mwalimu baada ya kuacha kazi Nyerere Biography inasema alikaa kwa Ally Sykes na chanzo cha taarifa hii ni Abbas Sykes.

Abbas Sykes ndiye aliyehamishwa nyumba ili Nyerere aingie.

Abbas huyo huyo Nyerere Biography inasema Mwalimu aliishi nyumbani kwa Ally Sykes Mtaa wa Kipata.

Hapa ndipo ilipo starehe na raha ya historia ya Mwalimu Nyerere.

Kuhusu marafiki wa Kikatoliki wa Mama Maria siwezi kukataa kuwa alikuwanao lakini historia ya Mama Maria inaeleza marafiki wake wanaofahamika walikuwa jamaa zake Abdul Sykes - Bi. Chiku bint Said Kisusa mke wa Sharif Abdallah Attas, na watoto wao Sakina na Fatna.

Ukipenda wajumuishe Bi. Titi Mohamed, Tatu bint Mzee, Hawa bint Maftah na Halima bint Khamis akina mama mstari wa mbele TANU.

Unasema unapinga historia ya Abdul Sykes kupewa uzito.

Sawa una haki ya kufanya hivyo.
Lakini kitabu cha Abdul Sykes kinakwenda sasa toleo la 5 na kipo sasa robo karne na kinasomwa na kujadiliwa kila siku.

Hapa leo mwaka mpya tumeamka na Abdul Sykes.
 
Fundi...
Unanitilia maneno yako kinywani mwangu.

Sijasema popote unanichukia.

Sijapata kusema nataka niaminiwe kwa haya niyajuayo.

Hiyo ni khiyari ya mtu sina uwezo wa kulazimisha.

Hilo la kuwa hakuna mtu ajuaye historia ya Nyerere kunishinda maneno hayo kasema Prof. Shivji baada ya kufanya mahojiano na mimi wakati wanatafiti Nyerere Biography.

Hakuishia hapo katika Nyerere Biography wameandika kuwa Maktaba yangu ni kati ya maktaba 3 kubwa katika historia ya Nyerere.

Maktaba zingine 2 ni ya Dr. Salim Ahmed Salim na ya Brig. General Hashim Mbita.

Historia inasema Mama Maria biashara yake ilikuwa mafuta ya taa sikupata kusikia popote kuwa alikuwa anauza na bidhaa zingine.

Hata Nyerere Biography inasema hivyo.

Kuhusu nyumba aliyoishi Mwalimu baada ya kuacha kazi Nyerere Biography inasema alikaa kwa Ally Sykes na chanzo cha taarifa hii ni Abbas Sykes.

Abbas Sykes ndiye aliyehamishwa nyumba ili Nyerere aingie.

Abbas huyo huyo Nyerere Biography inasema Mwalimu aliishi nyumbani kwa Ally Sykes Mtaa wa Kipata.

Hapa ndipo ilipo starehe na raha ya historia ya Mwalimu Nyerere.

Kuhusu marafiki wa Kikatoliki wa Mama Maria siwezi kukataa kuwa alikuwanao lakini historia ya Mama Maria inaeleza marafiki wake wanaofahamika walikuwa jamaa zake Abdul Sykes - Bi. Chiku bint Said Kisusa mke wa Sharif Abdallah Attas, na watoto wao Sakina na Fatna.

Ukipenda wajumuishe Bi. Titi Mohamed, Tatu bint Mzee, Hawa bint Maftah na Halima bint Khamis akina mama mstari wa mbele TANU.

Unasema unapinga historia ya Abdul Sykes kupewa uzito.

Sawa una haki ya kufanya hivyo.
Lakini kitabu cha Abdul Sykes kinakwenda sasa toleo la 5 na kipo sasa robo karne na kinasomwa na kujadiliwa kila siku.

Hapa leo mwaka mpya tumeamka na Abdul Sykes.
Na wewe vile vile unaniwekea maneno kinywani. Hakuna mahali nilipopinga historia ya Abdul Sykes au Sykes mwingine yeyote kupewa uzito. Ninachopinga ni wewe kufanya hao ndio historia nzima ya mapambano yetu ya uhuru. Hawakuwa peke yao kama vile Nyerere hakuwa peke yake.

Historia ipi hiyo ya Mama Maria inayosema marafiki zake walikuwa ni hao wakina mama wa kiislamu peke yake. Kwa akili za kawaida tu zingesema kuwa huyu mama ni lazima alikuwa na marafiki zake ambao walikuwa ni wakristo wenzake na sio waislamu peke yao.

Sikupingi kuwa Nyerere alikaa katika nyumba ya wakina Sykes. Lakini kwa vile haujasema alikaa kwa muda gani, kuna uwezekano kuwa baada ya hapo alihamia kwenye mojawapo ya nyumba za John Rupia.

Hilo la wakina Issa Shivji, Dr. Salim Ahmed na Hashim Mbita ni la kwako. Lakini kwa vile najua Mwalimu mwenyewe alikuwa na vitabu mpaka nyumba yake ilikuwa haitoshi nasita kuamini kuwa ulikuwa na kumbukumbu za historia yake kuliko yeye mwenyewe.

Kwa vile wewe binafsi haujawahi kusikia kuwa mama Maria alikuwa anauza soda pamoja na mafuta ya taa hakumfanyi aliyesema hivyo kuwa muongo. Picha uliyoweka inaonyesha kuwa kuna uwezekano kuwa ni kweli. Kwa vile haujaweka chanzo ya hayo madai, ni vigumu kujua kama mwandishi aliambiwa hivyo na mama Maria mwenyewe.

Amandla...
 
Na wewe vile vile unaniwekea maneno kinywani. Hakuna mahali nilipopinga historia ya Abdul Sykes au Sykes mwingine yeyote kupewa uzito. Ninachopinga ni wewe kufanya hao ndio nzima ya mapambano yetu ya uhuru. Hawakuwa peke yao kama vile Nyerere hakuwa peke yake.

Historia ipi hiyo ya Mama Maria inayosema marafiki zake walikuwa ni hao wakina mama wa kiislamu peke yake. Kwa akili za kawaida tu zingesema kuwa huyu mama ni lazima alikuwa na marafiki zake ambao walikuwa ni wakristo wenzake na sio waislamu peke yao.

Sikupingi kuwa Nyerere alikaa katika nyumba ya wakina Sykes. Lakini kwa vile haujasema alikaa kwa muda gani, kuna uwezekano kuwa baada ya hapo alihamia kwenye mojawapo ya nyumba za John Rupia.

Hilo la wakina Issa Shivji, Dr. Salim Ahmed na Hashim Mbita ni la kwako. Lakini kwa vile najua Mwalimu mwenyewe alikuwa na vitabu mpaka nyumba yake ilikuwa haitoshi nasita kuamini kuwa ulikuwa na kumbukumbu za historia yake kuliko yeye mwenyewe.

Kwa vile wewe binafsi haujawahi kusikia kuwa mama Maria alikuwa anauza soda pamoja na mafuta ya taa hakumfanyi aliyesema hivyo kuwa muongo. Picha uliyoweka inaonyesha kuwa kuna uwezekano kuwa ni kweli. Kwa vile haujaweka chanzo ya hayo madai, ni vigumu kujua kama mwandishi aliambiwa hivyo na mama Maria mwenyewe.

Amandla...
Fundi...
Nimepokea taarifa kuwa Mama Maria pamoja na mafuta ya taa alikuwa akiuza Coca-Cola:

"SALESMAN ALIEKUWA ANAMPELEKEA SODA ZA COCA-COLA NI MAREHEMU AMAL BAFADHIL. NI SHEMEJI YAO KINA MOHAMED BAHADORY WA MKUNGUNI STREET."

Ukoo wa Bahadory ni maarufu Dar es Salaam ya miaka ile.

Hapana sababu ya sisi kuvutana na historia ya Abdul Sykes kama unaikubali au la.

Kuwa kulikuwa na wengine ni kweli lakini hawakutajwa popote hadi pale mimi nilipowataja ndani ya kitabu cha Abdul Sykes.

Watu hushangaa ninaandika TANU kadi no. 5 ni ya Denis Phombeah Mnyasa wa Nyasaland, no. 6 Dome Okochi Budohi Mluya kutoka Kenya kisha nikaweka na picha nimepiga na yeye Nairobi 1972 nikiwa na umri wa miaka 20.

Naona hukupenda mimi kujumuishwa na Dr. Salim Ahmed Salim na Brig. Hashim Mbita kuwa ni wenye maktaba kubwa iliyosheheni taarifa za Mwalimu.

Mimi hili pia limenishtusha sana.
Unasema ni la kwangu.

Hapana hili si la kwangu hili ni la taifa lililopoteza historia yake sasa wanaikusanyq upya.

Prof. Shivji anatoka Kigoda Cha Mwalimu Nyerere.

CCM wameniomba niwapatie baadhi ya Nyaraka za Sykes.

Mwakilishi wa Ford Foundation aliwasilana na mimi ili nitoe msaada kwa Nyerere Foundation.

Kuna mambo hujuzuia kusema.

Nina nyaraka za Mwalimu yeye hana na alipata miaka mingi iliyopita kuziomba kwa Ally Sykes.

Baadhi ya nyaraka hizi nimewapa watafiti waliozihitaji na baadhi zipo Library of Congress, Washington DC na vyuo vingi Marekani.

Unajua katika miaka ya 1980 Mwakilishi wa Library of Congress Tanzania alikuwa Ahmed Rashaad Ali.

Mimi huyu ni baba yangu.
Nadhani umenielewa.

Mimi sina kawaida ya kumuita mtu muongo wala kumtukana mtu au kumkejeli mtu katika mnakasha.

Humchukulia kuwa hajui na wajibu wangu ni kumfunza na ikiwa hataki hapana ugomvi.

Nakuwekea picha ya mmoja wa watoto wa Mzee Bahdoury - Ismail ''Gigi'' Bahdoury.

Hili jina la Gigi ni kwa ajili alikuwa na kipaji kikubwa sana cha kucheza mpira katika vijana wa Dar es Salaam.

Gigi lilikuwa jina la mchezaji wa Italy Luigi ''Gigi' Riva katika miaka ya 1960s.

1672583220756.jpeg

Ismail ''Gigi' Bahdoury Muscat 1999.

1672583380604.jpeg

Kushoto: Ahmed Rashaad Ali, Dr. Harith Ghassany na Mwandishi

1672583486837.jpeg

Library of Congress, Washington DC
 
Back
Top Bottom