Makosa ya Upinzani

Makosa ya Upinzani

Lakini tuna kina Raila Tanzania? Mazingira ya kisiasa yanatoa fursa ya kujenga kina Raila?
Unawezaje kupewa dola ilhali vyombo vya dola havikuamini? Maana taifa haliongozwi na siasa tu. Idara za usalama na majeshi zina nafasi kubwa sana katika kuamua mustakabali wa nchi. Wanasiasa wa Tanzania ni mara ngapi tunajenga rappour na watu wa usalama ili angalau kujua wanawaza nini. Hakuna.

Hatuna akina Raila na tunaweza tusipate. Lakini tunashindwa kumpata Svangirai? mtu ambaye maisha yake, hamu yake, historia yake ni kupigania haki za wanyonge kikweli kweli bila woga? come on guys! Robert Mugabe alikuwa anaungwa mkono na waZimbabwe kuliko Kikwete, jamaa ni mbabe kuliko yeyote yule Tanzania. ZANU-PF ilikuwa inaungwa mkono kuliko CCM inavyoungwa mkono.

Lakini tumeshuhudia wananchi wa Zimbabwe wakichagua wabunge wa upinzani na Svangirai akipata zaidi ya 47% licha ya Mugabe kuiba na kutishia maafisa wa kura. Mkuu wa majeshi wa Zimbabwe alishasema hawezi kumpigia saluti kiongozi wa upinzani hata akishinda Urais. Lakini wananchi bado walimchagua Svangirai. Wananchi walipiteswa na wengine wakauawa lakini bado tu.

Upinzani wa Tz umejifunza nini toka MDC?

Mkuu Zitto, muda huu ndo ulikuwa wa kujenga chama na kuhamasisha wananchi kwa ajili ya uchaguzi. Lakini kimyaaaa hakuna operation sangara wala zinduka. Viongozi wetu mnasubiri muda wa kampeni. Hakuna ushindi hapo. Ninawasiwasi sana na ninyi viongozi wetu, kama kweli mnania thabiti ya kushika dola.
 
Mwanakijiji,

Thanks for this thread, nilikuwa na raise swali hili hili earlier today.

Katika attachment yako Professor Solinger amesema

"These opposition victories should be regarded not simply as the
product of a finally freed-up, democratically expressed public will, but
as the outcome of a lengthy process of unraveling of single-party domination,
first unleashed long before by the decision to allow "limited elections"
and then given a critical boost by the perhaps necessary result of
those elections, a split in the ruling party."

Sasa mimi naona kama sisi ndio kwanza tunaelekea katika hiyo "critical boost" aliyoisema ya "split in the ruling party".

Sasa opposition yetu inaweza kuitumia hii nafasi vizuri au kui squander.

Mimi naamini sana katika voter education, hivi opposition wana mkakati gani na voter education?

Kuna mkuu kaja hapa over the weekend na report za kutoka vijijini huko watu wanafikiri J.S Malecela bado ni Prime Minister (mpaka nikawa siamini nikamuuliza kama anatania) utawaeleza vipi watu hawa wasipigie kura CCM?

Mimi naamini watu wakijulishwa hali vyama vya upinzani vinaweza kupata si tu wanachama wengi wapya, bali hata na viongozi wengi wenye talent na kuweza kutupa chama mbadala tunachokitaka.

Lakini upinzani priority zao ziko wapi? Program zao za voter education ziko wapi? Network zao ziko extensive kiasi gani? Policies zao ziko intuitive kiasi gani? Wanaonyeshaje tofauti za dhahiri kati yao na CCM? Wanaonyeshaje kwamba wamekomaa na wanaweza kuendesha nchi vyema zaidi ya CCM? Watatuhakikishiaje kwamba CCM hawawezi kutumia machinery ya dola kuiba kura hata kama tukiwapigia upinzani, tume ya uchaguzi ni ya CCM!

Samahani kwa kuuliza maswali mengi kuliko majibu kwa sababu na mimi sijaona majibu ya maswali haya, majibu ambayo yanaweza kuwafanya watu waweke imani katika upinzani na kuamua kuwatoa CCM.
 
Lakini upinzani priority zao ziko wapi? Program zao za voter education ziko wapi? Network zao ziko extensive kiasi gani? Policies zao ziko intuitive kiasi gani? Wanaonyeshaje tofauti za dhahiri kati yao na CCM? Wanaonyeshaje kwamba wamekomaa na wanaweza kuendesha nchi vyema zaidi ya CCM? Watatuhakikishiaje kwamba CCM hawawezi kutumia machinery ya dola kuiba kura hata kama tukiwapigia upinzani, tume ya uchaguzi ni ya CCM!

Samahani kwa kuuliza maswali mengi kuliko majibu kwa sababu na mimi sijaona majibu ya maswali haya, majibu ambayo yanaweza kuwafanya watu waweke imani katika upinzani na kuamua kuwatoa CCM.

CCM wanayo yote hayo uliyoyauliza?
 
CCM wanayo yote hayo uliyoyauliza?

Forget about CCM, CCM ndiyo tatizo, na CCM ndiyo incumbent, na CCM ndiyo ina electorate ya watu wanaofikiri Malecela ni PM mpaka leo. Kwa hiyo CCM wao wanachotaka ni ku maintain the status quo, kwa hiyo hawana haja ya kuleta voter education kwa sababu voter education is to their disadvantage.they would rather have an uneducated electorate in order to stay inpower.Chiligati kasema wazi juzi kwamba priority ya CCM ni ku stay in power, kwishne.

On top of that CCM wana a nationwide network, kwa hiyo at least in the network aspect jibu la swali lako ni Yes, CCM wana extensive network, je upinzani una a matching network? Tunajua upinzani ni mchanga ukilinganishwa na CCM, lakini huu ndio wakati wa kuonyesha ukomavu na kujitutumua kushindana nao, after all miaka 17 si midogo hivyo.

Ni kazi ya wapinzani na wataka mabadiliko kuleta haya mambo.Huwezi kutegemea CCM ilete voter education itakayo wa expose kwamba wao wako incompetent, it will be counterproductive to them.

Ndiyo maana nauliza ili kuwafunga magoli CCM, wapinzani wana mikakati gani kuhusu haya mambo.

Wengi tunajua historia ya upinzani Tanzania, na mheshimiwa Zitto katika post yake ya mwanzo anakuwa overly defensive unnecessarily to an extent (preaching to the choir as some would say).Yaani tunavyowasema wapinzani hapa si kwa sababu hatuwapendi, ni kwa sababu tunapenda mabadiliko, ila, pamoja na yote waliyofanya obviously it is not enough na ndiyo maana bado wao ni wapinzani.

Ndiyo maana nauliza, ili kuelevate upinzani hawa watu wana mikakati gani mipya? What are they doing differently? maana tunaweza kuwa tunazunguka katika merry go round kila miaka mitano hapa, tunapiga kelele CCM hivi, CCM vile kwa sababu tunarudia vitu vilevile kwa jinsi ile ile tukitegemea matokeo tofauti.
 
duh, umetupiga sana. Hata hivyo unfairly. Unapoangalia makosa ya kambi ya upinzani ni vema uangalie 'factors' za ndani na za nje. Katika swot analysis hizi ni fursa na vitisho. Hapo utaweza kutoa hukumu sahihi kabisa.

Vilevile ni muhimu sana kuangalia historia ya vyama hivi katika muktadha wa historia ya tanzania na utamaduni wa kisiasa wa watanzania. Vyama katika nyakati tofauti - kuanzia kina marando na bagenda, mtei na makani, fundikira na kasanga tumbo na mapalala na seif walipoamua kujitoa mhanga na kuanzisha vyama - kumekuwa na hatu kadhaa zimepigwa katika kujenga dmeokrasia ya kweli katika nchi yetu.

Watu wanaiweka tanzania katika mizania ya nchi nyingine jambo ambalo ni kosa kubwa maana tanzania inapaswa kupimwa kutokana na historia yake. Zoezi la ujenzi wa taifa na kuwa na taifa moja chini ya uongozi mahiri wa mwalimu lilifanywa katika misingi ya udikteta mkubwa sana na chini ya amri moja ya 'zidumu fikra za mwenyekiti'. Tanzania ikajenga jamii ya watu wanaoheshimu mamlaka bila kuhoji na hata vyama vingi vilipoanzishwa vilionekana ni vya wasaliti. Ni mtu mmoja tu mpaka sasa ambaye alikonga nyoyo za watanzania na kuaminiwa - augustino lyatonga mrema - lakini naye akavurugwa sana na dola, kuitwa pandikizi na kuondoa kabisa credibility yake katika jamii. Jamii imefanywa kuamini kuwa mrema ni 'kichaa' na hana sifa ya uongozi. Hii ni kazi iliyopangwa na kutekelezwa kwa ustadi mkubwa kiasi kwamba leo ni watanzania wachache sana ambao wanakumbuka sacrifice ya mrema katika ujenzi wa demokrasia nchini.

Tusipojifunza na kuelewa historia hii ya vuguvugu la demokrasia tanzania tutaishia kulaumu watu kila kukicha bila kwenda mbele. Ccm itaendelea kutawala na kila baada ya miaka mitano kutakuwa kinatokea chama kina nguvu na baadae kuangushwa, wabunge wenye nguvu na baadae kuangushwa na hata wanasiasa wenye mvuto na baadae kupakwa matope na kunuka.

Demokrasia hulindwa. Viongozi hulindwa zaidi ili kubakia kama alama ya harakati. Raila odinga aliongoza harakati za mapinduzi kenya mwaka 1982, akaswekwa lupango kwa miaka zaidi ya tisa na kuishi uhamishoni nchini norway kwa miaka mingi. Akajiunga na chama cha baba yake mwaka 1992 ford, kikavunjika na kuwa na ford-k na ford-a. Baba yake mzee jaramogi alipokufa raila akataka kunyakua uongozi wa chama, akashindwa na michael kijana wamalwa na raila akaenda kuanzisha chama chake ndp. Akaivunja ndp na kuingia kanu kuwa katibu mkuu na akaipasua kanu vipande 2 na kuanzisha ldp. Akaingiza ldp katika muungano wa narc na kumpa kibaki urais (literally alimpa urais maana kibaki alikuwa armchair leader of opposition). Akatoka narc na kuanzisha odm-k, akagombana na kalonzo na kuanzisha odm na leo ni waziri mkuu mwenye nguvu kenya.
Mchakato wote huu raila alionekana msaliti, mpenda vyeo na mtu wa vita. Lakini leo huna tena kanu na raila alipata kuniambia, demokrasia afrika itaimarika tu iwapo vyama vilivyoleta uhuru vitapasukapasuka na kuondoa ile claim yao ya sisi tulileta uhuru - hii ni claim ya ccm na hata kumkumbatia mwalimu kama wao.

Lakini tuna kina raila tanzania? Mazingira ya kisiasa yanatoa fursa ya kujenga kina raila?
Unawezaje kupewa dola ilhali vyombo vya dola havikuamini? Maana taifa haliongozwi na siasa tu. Idara za usalama na majeshi zina nafasi kubwa sana katika kuamua mustakabali wa nchi. Wanasiasa wa tanzania ni mara ngapi tunajenga rappour na watu wa usalama ili angalau kujua wanawaza nini. Hakuna.

Mwanakijiji utaandika mpaka utachoka na kutulaumu mpaka utakasirika. Demokrasia ya tanzania itajengwa kwa sober approach ya kutazama historia yetu na kujua 'political culture' ya watanzania. Unatutaka tuchukue fursa inapotokea. Wazo murua kabisa. Lakini capacity ipo wapi? Wapo wap wanaofikiri na kuziona fursa? Wapo wapi watu wanaojenga scenerios na kujiuliza what if?

Tulianza vizuri zoezi la kujenga imani kwa wananchi kupitia bunge. Tulifanikiwa kupata sizable number ya wabunge wa ccm na kujenga coalition nzuri na kupashana habari. Tukamezwa. Tukajikuta tumewauzia ajenda tukijua kabisa hawatafika nayo mbali.

Ndani ya ccm hivi sana wanachowaza ni nani atakuwa rais ajaye kati ya membe na lowasa. Hakuna ajenda ya taifa, hakuna vision pale. Lakini wanasiasa wa upinzani tunaimba nyimbo zao hawa mabwana na hata 'opinion makers' kama wewe mwanakijiji mnaimba nyimbo zao.

Juzi nilisema hapa jf, lets be sober and scan the political situation objectively. Kinachoniumiza kichwa ni kwamba, kuna vijana wachache katika vyombo vyetu vya ulinzi na usalama wamechoka na bickerings za wanasiasa. Watataka ku restore order! Mzee sarakikya aliiwahi kuniasa kuwa tusiruhusu hali hiyo itokee kwani ikitokea hawatarudi makambini! Ili isitokee kuna haja ya kufikiri vizuri - ignore ccm

kama ambavyo wewe mheshimiwa zito ambavyo umekuwa ukitungiwa uongo,fitna na majungu na wapambe wa mbowe wanaohisi amani ya wao kutawala inahatarishwa na wewe.

Nimesikitika sana kusikia kuwa mbowe bado ana bifu la uchaguzi.umemuachia nafasi na kashinda kwa asilimia 96 bado analia kuwa anawafukuza wanachama wengine. Kweli tuna safari ndefu sana.kwenye demokrasia ya vyama mimi naona cuf wako juu kuliko utumbo anaoufanya mbowe na wenzake.
 
Upinzani Tanzania uko hivi:-
a) Sehemu ya kutokea kama ni vijana..yaani kupata vyeo, jina na hatimaye kwenda kusoma au kurudi CCM mifano mnayo wenyewe
b) Kwa watu wazima kutengeneza network na kufanya biashara na CCM kila baada ya uchaguzi (simply) kuhadaa wananchi..
c) NGO za kuchota pesa kutoka kwa wafadhili na namna nzuri ya kuongea na Rais wa Tanzania siku ya uhuru na mialiko Ikulu.
Tufanyaje??..movement within (CCM) and outside CCM iandaliwe, movement ndani ya serikali
Kivipi?...(Ndani ya CCM wapo vijana waliochoka wanaweza kuanzisha movement
Nje....(wapo vijana hususan hapa JF, Chadema and CUF ambao wananweza kuanzisha movements vuguvugu
Vijana wengi wako serikalini (walimu, civil servants, jeshini wameshachoka na haya mambo) wanaweza kuanzisha movement..
results: Not very soon it can also be painfull...
When and who: Nani aanze. mtafuteni AbdulSykes knows how to start succesfully movements..
 
kama ambavyo wewe mheshimiwa zito ambavyo umekuwa ukitungiwa uongo,fitna na majungu na wapambe wa mbowe wanaohisi amani ya wao kutawala inahatarishwa na wewe.

Nimesikitika sana kusikia kuwa mbowe bado ana bifu la uchaguzi.umemuachia nafasi na kashinda kwa asilimia 96 bado analia kuwa anawafukuza wanachama wengine. Kweli tuna safari ndefu sana.kwenye demokrasia ya vyama mimi naona cuf wako juu kuliko utumbo anaoufanya mbowe na wenzake.

Umezisikia wapi hizi habari?
 
Na ndio maana niliwahi kutoa maoni yangu humu kwamba kuna makundi mawili hapa nchini hatujayatumia vizuri.

Moja ni wafanyakazi wa Nchi hii. Tangu walipoondoka CCM ambako ilikuwa ni Jumuia kama UWT wamebaki yatima. Matokeo yake kila mfanyakazi na lwake. Baadhi wamejiunga na mafisadi wa CCM kuambulia angalau makombo.

Kundi la pili ni wanafunzi na wanavyuo mbalimbali. Nadhani wewe Zitto ulijiunga na CHADEMA ungali chuoni. Sasa hivi tumewakatisha tamaa wanavyuo wetu. CCM bado wana CHIPUKIZI wao. Watoto wadogo kabisa wanaiimbia CCM, wanazima Mwenge, wanacheza halaiki. Upinzani hamlikemei hili. Watoto wetu wanazaliwa na vyama kama wanavyozaliwa na KABILA na DINI za wazazi wao.
WildCard,
Zingatia maneno ya Zitto Udikteta wa Nyerere chini ya chama Kimoja.
Kilikuepo chama cha Wafanyakazi NUTA kilikuwa na nguvu na kilikuwa tishio kwa serskali na Waajiri. Nyerere akakigeuza kuwa Bawa la TANU/CCM na kukiita JUWATA. Nao wakaanza kuhubiri Fikra za Mwenyekiti.Kuhusu Wanavyuo tumeona humu Walidiriki kuchapwa Viboko hadharani.
Vyama vya Upinzani kosa lao kubwa ambalo Mzee Mwanakijiji hakulitaja ni ukosefu wa PESA za kujiendesha na kuendeshea Kampeni za Uchaguzi wakati Unapowada. Hivyo ni sahihi pengine kwa Watanzania kujaribu kuokoa Merrikebu yenye Vinoo vya Dhahabu, na kuuacha Mtumbwi uliobeba Makopa na Unga wa Muhogo.
 
Sidhani kama hii issue ni vema tuwashushie wapinzani pekee. Hata sisi watanzania tunahusika kwa njia moja au nyingine. Kama sisi watanzania wenyewe tunaona ubabaishaji wa serikali na watendaji wake kwa nini tuendelee kuwapa dhamana ya kutuongoza??????? Silaha yetu KURA TU.

Kuna wabunge wengi wanajua uchafu wa serikali lakini wametulia tu badala ya kuiwajibisha. Na hii si wabunge wa upinzani tu bali hata CCM lakini sisi wananchi tunashindwa kuelewa kuwa hao wabunge wako pale kwa niaba ya nani. Mfano, Mh. Mwakyembe na wengineo ambao walikuwa kwenye ile kamati yake wakidai kuwa kama wabunge pamoja na Lowassa watajaribu kujitetea bungeni na kuiponda kamati ya Mwakyembe, basi Mwakyembe na wenzake wataeleza yote ambayo hawakueleza au kuweka ndani ya ripoti. Kwa misingi au sababu hiyo utaona kuwa ile ripoti haikukamilika kwa sababu kuna maneno au ukweli mwingine ulifichwa. Sasa huo ukweli ulifichwa kwa manufaa ya nani?

Mh. Zitto naye amejaribu ku-relate mabadiliko katika demokrasia pamoja na historia ya nchi. Ninakubaliana na hoja yake lakini linapokuja suala la kuwatumikia wananchi kwa uadilifu halina suala la historia ya nchi. MPs need to be responsible to the people and not their parties. Kuna thread moja Mh. Zitto aligusia mambo ya double posho kwa wabunge na vilevile alisema kuwa kuna wabunge wengine wanachukuwa pesa nyingi zilizotengwa kwa ajili ya Transportation na matengenezo ya magari yao lakini wanasafiri kwa mabasi wakiacha magari yao bila kutumia. Alisema kuwa anawafahamu hao wabunge, sasa kama unawafahamu kwa nini aendelee kukaa kimya wakati watanzania wanapoteza kodi zao kulipia HUDUMA HEWA? Suala ni uwajibikaji, it doesn't matter unawakilisha jimbo gani. Hii pesa inayochukuliwa kwa huduma hewa ingeweza kutengeneza madawati au kununua vitabu kwa ajili ya watoto wetu mashuleni.

Nimegusia pande zote, chama tawala na upinzani. Utaona kuwa kuna siri nyingi za maovu ya serikali wabunge wetu hawataki kuiwajibisha serikali. Ninaamini mtu kama Mh. Zitto atakuwa anajua kashfa nyingi kuhusu nishati na madini. Lakini anaweza kuuchubuwa na asiseme chochote akiwa na moja yake kichwani. Wabunge kazi yenu mojawapo ni kuisimamia serikali, inapokosea lazima iwajibishwe. Say all what you know, na serikali lazima tu itakuja na majibu.
 
Umezisikia wapi hizi habari?
You are the living proof,kama sample wamekuchukua wewe, median,standard variation n.k zimeangukia kwenye point inayoitwa Mwafrika.

Hakuna asiyejua jinsi unavyomchukia Zitto na upande uliokuwa kwenye uchaguzi, ulionywa hapa na watu kibao kuwa usichukue upande, nyie ndio mmenilazimisha kutuma post humu kwa lengo la kutovumilia tena upumbavu wenu, mnajuana mko wangapi humu

ila wenye kutaka facts na truth wanaongalia mstakabali wa taifa hili, wanaojadili ideas, wewe haumo humo, kama msafara wewe ni mjusi kaitika msafara wa Kenge

huu ni ukweli kataa kubali, pinga
 
Back
Top Bottom