Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #21
17.
“Unamfikiriaje?”
“Nani?”
“Rais.”
Joram akatabasamu kidogo kabla hajaongeza, “Sikia Nuru, Rais wa Kiafrika sio mtu wa kujadiliwa na mtu kama mimi na wewe mahala kama hapa. Tunaweza kesho tukajikuta mahabusu, badala ya hotelini, kujibu maswali yasiyoeleweka.”
Nuru naye alicheka. “Usinidanganye Joram,” alisema baada ya kicheko hicho kizuri. “Najua unahitaji muda wa kufikiri. Ameivuruga akili yako. Ulichotegemea sicho ulichokikuta. Akasita tena. Alipomwona Joram yuko kimya akaongeza, “Hata mimi sina budi kusema kuwa amenishangaza. Tulivyopokelewa nyumbani kwake badala ya Ikulu nilidhani ameamua kutusimulia hicho alichotuitia. Sasa utafanyeje, Joram?”
Kama alitegemea jibu, basi alikosea sana. Badala yake Joram alimshika mkono na kumwongoza kwenye lifti ambayo iliwapandisha hadi ghorofani kilikokuwa chumba chao. Chumbani aliendelea kuyakoroga maswali yote ya Nuru juu ya Rais huyo. Ulipofika wakati wa mlo walikuwa wa kwanza kufikia
chumba cha maakuli. Walikula huku wakitazama televisheni ambayo ilikuwa ikionyesha kikundi cha utamaduni kilichokuwa kikiwatumbuiza wageni fulani uwanja wa ndege. Wageni hao walipopita baada ya kuwatazama wachezaji kidogo, kikundi hicho kilisahauliwa na umuhimu kuhamishiwa kwa wageni. Historia zao za nchi zao zilisimuliwa, zikafuatiwa na majibu yao kwa waandishi wa habari. Joram aliyatazama yote hayo ilihali hayaoni. Mara baada ya mlo na bia mbilimbili za kuteremshia aliushika tena mkono wa Nuru na kumwongoza chumbani, ambako sasa alitulia kama awali; akiendelea kutafakari.
Kwa muda aliusahau mkasa huo na kujifikiria mwenyewe. Alikosa nini kwa Mungu hata apewe moyo huu wa kufuatilia mambo yasiyomuhusu ambayo mara zote uifanya roho yake iponee chupuchupu? Kitu gani kilichomwambukiza ugonjwa huu hatari? Tamaa ya kufichua kila siri, kiu ya kumfichua kila mwenye hatia, njaa ya kumpokonya silaha kila mwenye nia mbaya unapochanganyika na uroho wa kushuhudia mibabe iliyokubuhu ikilia hadharani; kama si ugonjwa ni nini?
Joram hakuweza kukumbuka ni lini na nani alimwambukiza maradhi hayo. Yako magonjwa mengine ambayo mwanaume huzaliwa nayo. Pengine Joram ni mmoja wao.
Baba na mama yake wasingesahau jinsi mtoto wao huyu pekee alivyokuwa machachari tangu alipokuwa na umri wa miaka mitatu. Akiwa mtoto aliyepatikana baada ya miaka saba ya kutafutwa kwa namna zote, madaktari na wahenga walishirikishwa, alipopatikana alikuwa kama mboni ya jicho kwa baba na yai la dhahabu kwa mama. Kila mmoja alipenda kumlea kutwa. Lakini iliwashangaza kuona kwamba mtoto huyu hakupenda kabisa kubebwa. Kila aliposhikwa mikononi alisumbua kwa kurusha viteke na vigumi hata akarejeshwa kitandani ambako alitulia.
“Unamfikiriaje?”
“Nani?”
“Rais.”
Joram akatabasamu kidogo kabla hajaongeza, “Sikia Nuru, Rais wa Kiafrika sio mtu wa kujadiliwa na mtu kama mimi na wewe mahala kama hapa. Tunaweza kesho tukajikuta mahabusu, badala ya hotelini, kujibu maswali yasiyoeleweka.”
Nuru naye alicheka. “Usinidanganye Joram,” alisema baada ya kicheko hicho kizuri. “Najua unahitaji muda wa kufikiri. Ameivuruga akili yako. Ulichotegemea sicho ulichokikuta. Akasita tena. Alipomwona Joram yuko kimya akaongeza, “Hata mimi sina budi kusema kuwa amenishangaza. Tulivyopokelewa nyumbani kwake badala ya Ikulu nilidhani ameamua kutusimulia hicho alichotuitia. Sasa utafanyeje, Joram?”
Kama alitegemea jibu, basi alikosea sana. Badala yake Joram alimshika mkono na kumwongoza kwenye lifti ambayo iliwapandisha hadi ghorofani kilikokuwa chumba chao. Chumbani aliendelea kuyakoroga maswali yote ya Nuru juu ya Rais huyo. Ulipofika wakati wa mlo walikuwa wa kwanza kufikia
chumba cha maakuli. Walikula huku wakitazama televisheni ambayo ilikuwa ikionyesha kikundi cha utamaduni kilichokuwa kikiwatumbuiza wageni fulani uwanja wa ndege. Wageni hao walipopita baada ya kuwatazama wachezaji kidogo, kikundi hicho kilisahauliwa na umuhimu kuhamishiwa kwa wageni. Historia zao za nchi zao zilisimuliwa, zikafuatiwa na majibu yao kwa waandishi wa habari. Joram aliyatazama yote hayo ilihali hayaoni. Mara baada ya mlo na bia mbilimbili za kuteremshia aliushika tena mkono wa Nuru na kumwongoza chumbani, ambako sasa alitulia kama awali; akiendelea kutafakari.
Kwa muda aliusahau mkasa huo na kujifikiria mwenyewe. Alikosa nini kwa Mungu hata apewe moyo huu wa kufuatilia mambo yasiyomuhusu ambayo mara zote uifanya roho yake iponee chupuchupu? Kitu gani kilichomwambukiza ugonjwa huu hatari? Tamaa ya kufichua kila siri, kiu ya kumfichua kila mwenye hatia, njaa ya kumpokonya silaha kila mwenye nia mbaya unapochanganyika na uroho wa kushuhudia mibabe iliyokubuhu ikilia hadharani; kama si ugonjwa ni nini?
Joram hakuweza kukumbuka ni lini na nani alimwambukiza maradhi hayo. Yako magonjwa mengine ambayo mwanaume huzaliwa nayo. Pengine Joram ni mmoja wao.
Baba na mama yake wasingesahau jinsi mtoto wao huyu pekee alivyokuwa machachari tangu alipokuwa na umri wa miaka mitatu. Akiwa mtoto aliyepatikana baada ya miaka saba ya kutafutwa kwa namna zote, madaktari na wahenga walishirikishwa, alipopatikana alikuwa kama mboni ya jicho kwa baba na yai la dhahabu kwa mama. Kila mmoja alipenda kumlea kutwa. Lakini iliwashangaza kuona kwamba mtoto huyu hakupenda kabisa kubebwa. Kila aliposhikwa mikononi alisumbua kwa kurusha viteke na vigumi hata akarejeshwa kitandani ambako alitulia.