Malalamiko mbalimbali kuhusu mabadiliko ya vifurushi yaliyofanywa na mtandao wa Tigo kwa mwaka 2020

Ttcl ipo juu, kwa buku unapewa GB 4 asubuhi mpaka SAA mbili usiku unapewa 500 alafu unamalizia GB 3.5 kuanzia saa mbili usiku mpaka kukuche, na speed ni 4G

Kwa wengine wenye connections wanaungwagwa data lisilo na kikomo Voda kwa 35,000 kwa mwezi, naskia hili lipo kwa wafanyakazi wa Voda ila limevujishwa, kuna mshkaji wangu hata mwezi haujaisha kashusha gb mia nane hadi sasa maana anashushia wenzake movie na series
 
Mimi sielewi! Voda nimeshafungiwa simu hazitoki ila mnara unasoma na simu zinaingia naperuzi kama kawaida sasa ndio wamefunga nini hawa mafi?
 
Chakaza,
Kama line milioni 20 zinafungiwa unadhani haya makampuni ya simu yatajiendeshaje?Kumbuka fixed costs zao ziko pale pale!
Akumbuke pia TCRA nao wanatakiwa kupeleka gawio serikalini, hivyo asifikiri kampeni za simu zimejiamulia wenyewe kuongeza gharama
 
Kupunguza Vifurushi na jambo moja
Jambo Baya sana
Umejikongoja kupata hako ka GB
Yaani Kanavyo isha !!
Kiukweli Mitandao imekuwa Majanga kwa sasa
Mie napata Data safi shida GB 5
Zinapita kwa Muda mfupi sana tofauti na Zaman
Kumbe hata wanaccm mmeguswa ! basi mimi nikajua kwa vile simu zenu mmepewa na Pole pole basi labda kutakuwa na nafuu
 
Ama kweli mtandao wa Tigo ni mtandao wanafunzi. Inawezekana vipi waseme kifurushi cha week ni 2500/- unapata dk 250 kisha ukisha ukishajiunga wanakwambia dk 90 upige kuanzia saa 4 ucku mpka 11 alfajiri.

Sasa hawa jamaa wanadhani sisi tunakesha kwa kuongea badala ya kudumisha ndoa zetu. Ukisikia dhulma ndo hii kutoka Tigo.

Kwanini wasifafanue kabla mtu hujajiunga ili ukubali kujiunga au ukatae. TIGO TIGO TIGO MUNGU ANAWAONA NA MTALIPWA KWA HILI
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…