Malcom X akipunga upepo Dar es Salaam

Malcom X akipunga upepo Dar es Salaam

..tunaweza kusema Sheikh Ali Muhsin ana bahati hakuuwawa.

..labda kwasababu alifungwa ktk magereza[ Dsm, Dom, Mwanza, Bukoba] ya Tanganyika.

..angeachwa Zanzibar huenda angeuawa kama wakina Hanga, Twala, Mdungu Usi, Majura, na wengine.

..naomba isieleweke kwamba hakupitia mateso, kwani kukaa kifungoni toka 1964 mpaka 1974 ni mateso makubwa.

.. Mohamed Said unaweza kunielekeza wapi naweza kununua tafsiri ya Koran iliyoandikwa na Sheikh Ali Muhsin?
Hivi mpaka anafungwa, aliwahi kufikishwa mahakamani kweli ?..

...Na kama wamgemfikisha mahakamani unadhani wangemshitaki kwa kosa gani ?
 
MALCOLM X alikuwa hero wangu toka udogoni na nimekisoma kitabu cha maisha yake alichoandika Alex Hailey nikiwa na miaka labda 15/16.

Kitabu hiki kinaitwa, ''The Autobiography of Malcolm X,'' (1965) na kiliandikwa na Alex Hailey na Malcolm X.

Nimekiangalia hapa Maktaba sijakiona lakini kilikuwapo.
Nilitaka nikuwekee uone cover ya 1965 ilivyokuwa.

Kitabu hiki kilichapwa baada ya kufa Malcolm na Alex Hailey akabadilisha mambo mengi katika kitabu.

Alex Hailey alilaumiwa sana kwa kufanya jambo hili.

Movie yake ilitoka mwaka wa 1992 mimi nikiishi mji mdogo Uingereza na nilikweda kuona senema hii kwenye ''premier'' yake muigizaji akiwa Denzel Washington muogozaji na mtengenezaji filamu hii Spike Lee ambae alicheza pia ndani ya hii movie.

Movie hii ilinirudisha utotoni kwani nilisikia nyimbo za nyakati zangu kama, ''Shot Gun ya Junior Walker,'' na ''A Change is Gonna Come,'' ya Sam Cooke.

Nilikuwa sijafika Amerika na nikikuona mbali sana.
Miaka ikapita nikaenda Amerika.

Nilipofika New York nimekuta ndiyo wiki kitabu cha Manning Marable, ''Malcolm X Life of Reinvention,'' ndiyo kimetoka na kwa bahati mbaya mwandishi alikufa wakati anakaribia kufanya uzinduzi wa kitabu hiki.

Nilikinunua kitabu hiki katika duka maarufu la vitabu Marekani, Barnes and Nobles sehemu za Manhattan.

Nilifika Harlem 125 Street mitaa aliyokuwa akivinjari Malcolm X wakati wake katika miaka ya 1950/60.

Nililiona lile jumba Audobon Ballroom ambamo Malcolm X alipigwa risasi.
Jumba hili liko katika njia kuelekea New Jersey kilipo Chuo cha Princeton.

Lakini hii ni stori nyingine siku ikitokea wasaa In Shaa Allah nitaieleza stori hii.
Nimekidhi viwango vya ''uso kwa uso?''

View attachment 2190247
Nianze na maelezo ya picha "Wengi hawajui hili lakini alikuwa akifikia mitaa Gerezani".
Mohamed Said unaweza kunisaidia uelewa kutoka Maktaba yako endapo kuna uhusiano wowote uliopo katika Safari za Malcolm X mitaa ya Gerezani na Gerezani na harakati za uhuru wa Tanganyika/ Siasa za mji wa Dar es Salaam katika miaka ya 1950. Pamoja na kuwa picha haijataja ni ya mwaka gani, lakini maandiko yanaeleza kuwa baada ya kuhitilafiana na mwenzake Elijah Poole a.k.a Elijah Muhammad kuhusu muelekeo na mtizamo wa kisiasa wa Nation of Islam (NoI), Malcolm X aliachia ngazi katika uongozi wa harakati za NoI mwaka 1964 na ni katika kipindi hicho ndipo aliposafiri sana barani Afrika na hata Mashariki ya Kati ambako alienda Hijja na kuitwa el-Hajj Malik el Shabazz.
1. Inawezekana alikuwa akifika Gerezani miaka ya 1950s?,
2. Je, hapo Gerezani alikuwa akipenda kufikia mitaa ipi kati ya Kipata, Kitchwele (Uhuru), Kirk (Lindi), Somali au Kiungani?
3. Nation of Islam ilianzishwa mwaka 1931, Je?, Kuna mahusiano yeyoye kati ya Nation of Islam ya Waamerika Weusi na Chama cha Waislamu wa Tanganyika (Al Jamiatul Islamiyya Fi Tanganyika) kilichoanzishwa Gerezani mwaka 1933?

Natanguliza shukrani zangu za dhati.
 
Nianze na maelezo ya picha "Wengi hawajui hili lakini alikuwa akifikia mitaa Gerezani".
Mohamed Said unaweza kunisaidia uelewa kutoka Maktaba yako endapo kuna uhusiano wowote uliopo katika Safari za Malcolm X mitaa ya Gerezani na Gerezani na harakati za uhuru wa Tanganyika/ Siasa za mji wa Dar es Salaam katika miaka ya 1950. Pamoja na kuwa picha haijataja ni ya mwaka gani, lakini maandiko yanaeleza kuwa baada ya kuhitilafiana na mwenzake Elijah Poole a.k.a Elijah Muhammad kuhusu muelekeo na mtizamo wa kisiasa wa Nation of Islam (NoI), Malcolm X aliachia ngazi katika uongozi wa harakati za NoI mwaka 1964 na ni katika kipindi hicho ndipo aliposafiri sana barani Afrika na hata Mashariki ya Kati ambako alienda Hijja na kuitwa el-Hajj Malik el Shabazz.
1. Inawezekana alikuwa akifika Gerezani miaka ya 1950s?,
2. Je, hapo Gerezani alikuwa akipenda kufikia mitaa ipi kati ya Kipata, Kitchwele (Uhuru), Kirk (Lindi), Somali au Kiungani?
3. Nation of Islam ilianzishwa mwaka 1931, Je?, Kuna mahusiano yeyoye kati ya Nation of Islam ya Waamerika Weusi na Chama cha Waislamu wa Tanganyika (Al Jamiatul Islamiyya Fi Tanganyika) kilichoanzishwa Gerezani mwaka 1933?

Natanguliza shukrani zangu za dhati.
Changa...
Ndugu yetu aliandika akiwa na nia ya kunifedhehesha kwa kuwa mimi nimeeleza mengi kuhusu Gerezani katika harakati za TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika.

Nami kwa kuwa aliitaja Gerezani yangu nami nikaona nimlipe "in his own coin," ndipo nikamtajia na kumwekea picha nikiwa Harlem, New York mitaa ya Malcolm X kumfanya afikiri.

Na mwengine aliyenipiga kijembe kuwa mie limbukeni wa New York nikamwekea picha niko Paris kumdhihirishia kuwa mbona nimefika kwingi?
 
Wengi hawajui hili lakini alikuwa akifikia mitaa Gerezani.

View attachment 2187679
Kweli Malcom X aliwahi kufika Tz , ila bado nina mashaka kama hapo ni Tu kweli isije ikawa picha ya uwongo kuzushiwa hapo ni Gerezani Tz kama ya Puttin ile yupo Tz hivyo nataka kujua uhakika kama hapo Gerezani inatokea wapi ?
 
MALCOLM X alikuwa hero wangu toka udogoni na nimekisoma kitabu cha maisha yake alichoandika Alex Hailey nikiwa na miaka labda 15/16.

Kitabu hiki kinaitwa, ''The Autobiography of Malcolm X,'' (1965) na kiliandikwa na Alex Hailey na Malcolm X.

Nimekiangalia hapa Maktaba sijakiona lakini kilikuwapo.
Nilitaka nikuwekee uone cover ya 1965 ilivyokuwa.

Kitabu hiki kilichapwa baada ya kufa Malcolm na Alex Hailey akabadilisha mambo mengi katika kitabu.

Alex Hailey alilaumiwa sana kwa kufanya jambo hili.

Movie yake ilitoka mwaka wa 1992 mimi nikiishi mji mdogo Uingereza na nilikweda kuona senema hii kwenye ''premier'' yake muigizaji akiwa Denzel Washington muogozaji na mtengenezaji filamu hii Spike Lee ambae alicheza pia ndani ya hii movie.

Movie hii ilinirudisha utotoni kwani nilisikia nyimbo za nyakati zangu kama, ''Shot Gun ya Junior Walker,'' na ''A Change is Gonna Come,'' ya Sam Cooke.

Nilikuwa sijafika Amerika na nikikuona mbali sana.
Miaka ikapita nikaenda Amerika.

Nilipofika New York nimekuta ndiyo wiki kitabu cha Manning Marable, ''Malcolm X Life of Reinvention,'' ndiyo kimetoka na kwa bahati mbaya mwandishi alikufa wakati anakaribia kufanya uzinduzi wa kitabu hiki.

Nilikinunua kitabu hiki katika duka maarufu la vitabu Marekani, Barnes and Nobles sehemu za Manhattan.

Nilifika Harlem 125 Street mitaa aliyokuwa akivinjari Malcolm X wakati wake katika miaka ya 1950/60.

Nililiona lile jumba Audobon Ballroom ambamo Malcolm X alipigwa risasi.
Jumba hili liko katika njia kuelekea New Jersey kilipo Chuo cha Princeton.

Lakini hii ni stori nyingine siku ikitokea wasaa In Shaa Allah nitaieleza stori hii.
Nimekidhi viwango vya ''uso kwa uso?''

View attachment 2190247
Nataka kujua mambo gani mtunzi(Alex Haley) aliyobadilisha kwenye kitabu ?
 
Wajinga...
Msome katikati ya mistari utamuelewa.
Ukimuelewa hutasema, ''Utajuaje...''

Nawe kwa kauli hiyo na neno ''nu yoku.''
Umekuwa kama yeye.

Nami nitakupa jibu kama nililompa yeye.

Hii utajuaje yako ya ''nu yoku'' ingekuwa na maana kama ningekuwa nimefika New York peke yake.

Vipi kuhusu hiyo hapo chini?

View attachment 2190165
Paris
Hongera mzee wetu
One day ntakua hapo
 
Hivi mpaka anafungwa, aliwahi kufikishwa mahakamani kweli ?..

...Na kama wamgemfikisha mahakamani unadhani wangemshitaki kwa kosa gani ?
Proved,
Swali lako Waingereza wangesema ni "tricky," yaani linatatanisha.

Ali Muhsin hakufikishwa mbele ya vyombo vya sheria.

Serikali halali imepinduliwa.

Viongozi wa serikali halali iliyopinduliwa washitakiwe mahakamani.

Kisha unauliza, "hypothetical question," endapo angeshitakiwa kosa lake lingekuwa lipi?
 
Adrian,
Sijui Alex Hailey alibadilisha kitu gani.
Mimi nimekisoma mwaka huu nimeona mtunzi amekitendea haki kuna vitu sikutarajia kabisa kuvikuta(kama kuficha hivyo vingekuwa vya kwanza) katika kitabu chake mfano Malcom X anapoelezea uislamu kwa mazuri na kuupampa nk ila kwenye vitu alivyofuta nahisi itakuwa sehemu za kuzungumzia vibaya mahayudi .
 
Back
Top Bottom