MALCOLM X alikuwa hero wangu toka udogoni na nimekisoma kitabu cha maisha yake alichoandika Alex Hailey nikiwa na miaka labda 15/16.
Kitabu hiki kinaitwa, ''The Autobiography of Malcolm X,'' (1965) na kiliandikwa na Alex Hailey na Malcolm X.
Nimekiangalia hapa Maktaba sijakiona lakini kilikuwapo.
Nilitaka nikuwekee uone cover ya 1965 ilivyokuwa.
Kitabu hiki kilichapwa baada ya kufa Malcolm na Alex Hailey akabadilisha mambo mengi katika kitabu.
Alex Hailey alilaumiwa sana kwa kufanya jambo hili.
Movie yake ilitoka mwaka wa 1992 mimi nikiishi mji mdogo Uingereza na nilikweda kuona senema hii kwenye ''premier'' yake muigizaji akiwa Denzel Washington muogozaji na mtengenezaji filamu hii Spike Lee ambae alicheza pia ndani ya hii movie.
Movie hii ilinirudisha utotoni kwani nilisikia nyimbo za nyakati zangu kama, ''Shot Gun ya Junior Walker,'' na ''A Change is Gonna Come,'' ya Sam Cooke.
Nilikuwa sijafika Amerika na nikikuona mbali sana.
Miaka ikapita nikaenda Amerika.
Nilipofika New York nimekuta ndiyo wiki kitabu cha Manning Marable, ''Malcolm X Life of Reinvention,'' ndiyo kimetoka na kwa bahati mbaya mwandishi alikufa wakati anakaribia kufanya uzinduzi wa kitabu hiki.
Nilikinunua kitabu hiki katika duka maarufu la vitabu Marekani, Barnes and Nobles sehemu za Manhattan.
Nilifika Harlem 125 Street mitaa aliyokuwa akivinjari Malcolm X wakati wake katika miaka ya 1950/60.
Nililiona lile jumba Audobon Ballroom ambamo Malcolm X alipigwa risasi.
Jumba hili liko katika njia kuelekea New Jersey kilipo Chuo cha Princeton.
Lakini hii ni stori nyingine siku ikitokea wasaa In Shaa Allah nitaieleza stori hii.
Nimekidhi viwango vya ''uso kwa uso?''
View attachment 2190247