Malecela avunja ukimya!

Malecela avunja ukimya!

inaonekana kikwete anawasiwasi sana ndio maana ametuma watu wake, mtu ambaye anamuogopa ni MWANDOSYA na ndio maana amempa wizara ya Umwagiliaji ili asisikike lakini mpaka sasa hivi watu wake wapya ni ovyo(masha, ngeleja, mkullo, membe labda pinda) na hamna hata mmoja ambaye anakubalika zaidi ya mwandosya. kuna taarifa kwamba "rebels are backing mwandosya" na kikwete ajui afanye nini maana yake akimfukuza kazi ndio chati inapanda. Only time will tell

Prof katulia tuli kama wizara sio nyeti ila tusubiri.... will see
 
1. inaonekana kikwete anawasiwasi sana ndio maana ametuma watu wake, mtu ambaye anamuogopa ni MWANDOSYA na ndio maana amempa wizara ya Umwagiliaji ili asisikike

2. lakini mpaka sasa hivi watu wake wapya ni ovyo(masha, ngeleja, mkullo, membe labda pinda) na hamna hata mmoja ambaye anakubalika zaidi ya mwandosya.

3. kuna taarifa kwamba "rebels are backing mwandosya" na kikwete ajui afanye nini maana yake akimfukuza kazi ndio chati inapanda. Only time will tell

Mawazo yako yanajichanganya, hivi Wizara gani ukipewa ndio unasikika?. Na kusikika sio sababu ya kupata umaarufu, unaweza kusikika kwa mabaya. Nadhani jitihada kwa ile nafasi uliyopewa ndio zinakufanya wananchi wajue kuwa unatenda kazi ipasavyo. Hivyo kusema alimpa Wizara eti ya Umwagiliaji ili asisikike ni mwisho wa kufikiri, asingepewa kabisa ungesema nini?.

Mimi nidhani kupingana ndani ya CCM si "uadui", ile ni demokrasia, kama kuna wanamuunga mkono Mwandosya, hiyo ni demokrasia nzuri sana ndani ya Chama chao, inaonekana wako huru, manake haiwezekani wanachama wote wawe na mawazo na mapenzi sawa kwa mtu mmoja.

Upinzani TZ uko mbali sana kushinda, manake badala ya kuangalia yapi yataweza kuing'oa CCM, inaangaliwa jinsi CCM itakavyobomoka kupitia wafuasi wake. Kazi ipo.
 
Kama CCM wataamua kutompinga JK 2010 ni haki yao kama chama - huu hauna mjadala. Hata kama inatukera vipi. Kilichobaki ni KUTOPIGIA KURA CCM!!! Mi nasema tuache kuingilia masuala ya CCM, nakubaliana na FMES katika hilo. Let them hang themselves with a long rope called JK!
Sisi tukiona tu JK kapitishwa basi tujue hatuwapi kura CCM. hata mbunge mmoja wa CCM asipewe hata awe Mwandosya etc. na wapiga kura wawaeleze waheshimiwa. Huwezi kuwa CCM ukasapoti ufisadi na utenadji mbovu wa JK alafu ukajinadi eti we ni tofauti. No sir! Na kama wananchi wataweza kuweka msimamo wao wazi basi watawalazimu akina Mwandosya etc tu-reassess na finally to quit hicho chama kisicho na maana na malengo - CCM
Hivyo wana JF, wacha JK apendekezwe 2010, lakini tuwe stari wa mbele kuelimisha wananchi kwa nini wasiwape kura CCM.... because of JK!!!
 
Wakuu,
Mtanisamehe sana katika hili lakini Ukweli ni kwamba hakuna mtu CCM anayeweza kuongoza nchi zaidi ya Kikwete....Hakuna mtu hata mmoja ndani ya CCM mwenye ubavu anayeweza kupingana na Mtandao wa Mafisadi - HAKUNA..Na kwa mabaya yake yote na mapungufu yake yote Kikwete bado ni rais bora kuliko yoyote katika fikra zangu ndani ya CCM...

Hivyo tunachotakiwa sisi wananchi kama tunapigana na chaguo la Malecela au Chiligati basi bila shaka sisi wenyewe ndio wenye Upofu, kwani yaonyesha wazi bado tuna tumaini kuwa yupo mtu ndani ya CCM anaweza kufanya kazi nzuri kuliko Kikwete badala ya kutazama nje ya CCM...

Jamani viongoizi wengi ndani ya CCM wamepandikizwa iwe na Kikwete au Lowassa, sasa sielewi nani mbora kati yao. Hakuna mbunge hata mmoja aliyepita Ubunge kwa haki lilaah wote wamepandikizwa hivyo CCM tunavuna walichokipanda.. Sii Mwandosya wala Kinana wote ni mapandikizi, mbegu zilizopandwa na msitegemee hata siku moja kuvua mazao tofauti..

Chaguo letu pekee ni rais toka Upinzani..
 
kama huo ndio utaratibu na utamaduni wa chama
ni bora wauingize kwenye katiba ili hii kitu ifanyike "automatic"
bila gharama kubwa ya kipesa. vinginevyo itakuwa ni ufujaji wa pesa
ambazo naamini kiasi kikubwa kinatokana na ruzuku ambazo nazo
hutokana na kodi ya wananchi na si wanachama tu.

Naam, Chiligati na Malecela wanataka kupindisha katiba ya CCM kwa manufaa ya kudumisha 'utamaduni wao ndani ya chama' wa kuachiana kukaa madarakani. Ni bora watwambie katiba ya CCM ipo kama usanii tu na inaweza kupindishwa wakati wowote ule bila kujali athari za kufanya hivyo ambazo haziathiri CCM pekee yake bali nchi nzima ya Watanzania.
 
Naam, Chiligati na Malecela wanataka kupindisha katiba ya CCM kwa manufaa ya kudumisha 'utamaduni wao ndani ya chama' wa kuachiana kukaa madarakani. Ni bora watwambie katiba ya CCM ipo kama usanii tu na inaweza kupindishwa wakati wowote ule bila kujali athari za kufanya hivyo ambazo haziathiri CCM pekee yake bali nchi nzima ya Watanzania.

- CCM ina utamaduni wake kama wa Democrats kule US wa kuwapitisha kwa nguvu zote marais wa taifa kutoka chama chao, Malecela na Chiligati hawana ubavu wa kubadili katiba ya CCM, lakini one thing wana ubavu wa kusema hadharani maoni yao binafsi kama nani wanamtaka kuongoza taifa kutokea CCM,

- Matatzio ya fear na inferior ya wananchi wa vyama vingine hayawezi kuwa matatizo ya taifa wala CCM, malalmiko mengi hapa bila hoja ya msingi ya kulisaidia taifa ni waste of time ya wananchi wa Tanzania na ni kuwapotosha kwa makusudi. CCM tuna utamaduni wetu hopefully na huko upnade wa pili mano pia utamaduni wenu, na sitaki kuamini kuwa ni utamaduni wa kulia lia bila sababu ya msingi.

CCM Juu Zaidi! Kidumu.

FMES!

 
FMES,

..kama Kikwete angekuwa ame-deliver hakuna mwana CCM angekuwa na mshawasha wa kum-challenge for the second term.

..Mzee Malecela, na Cpt.Mkuchika hawana hoja za kutetea rekodi ya utendaji kazi ya Raisi Kikwete. hiyo ndiyo sababu ya msingi ya wao kubakikia wakisisitiza "utamaduni wa CCM" uheshimiwe.
 
Kama u mpinzani wa kweli na unaamini kuwa Kikwete hajafanya chochote basi unapaswa uchekelee wazo la yeye kupitishwa na CCM tena.
 
- CCM ina utamaduni wake kama wa Democrats kule US wa kuwapitisha kwa nguvu zote marais wa taifa kutoka chama chao, Malecela na Chiligati hawana ubavu wa kubadili katiba ya CCM, lakini one thing wana ubavu wa kusema hadharani maoni yao binafsi kama nani wanamtaka kuongoza taifa kutokea CCM,


Kama utakavyokumbukua Vingunge wengi walitaka na walidhani kwamba Hillary ndiye aliyestahili kuwa Rais na wengi walimuunga mkono, lakini wakaacha demokrasi ndani ya chama ifanye vitu vyake na hatimaye tunajua nani aliyebuka kidedea. Hata political analysts hawakumpa nafasi kabisa Obama kutokana na jina kubwa lakina Clinton, uwezo wao wa kuchangisha pesa na walivyo na umaarufu mkubwa siyo tu ndani ya chama chao, bali Marekani na dunia nzima. Utamaduni wa kutuwekea Rais ambaye hana uwezo wa kuongoza nchi Watanzania hatuutaki maana hauna maslahi yoyote kwa nchi yetu. Hivyo hivyo ndani ya CCM hawa akina Chiligati na Malecela waache unafiki wa kuwatisha wagombea ambao wanataka kumchallange Kikwete kwamba kufanya hivyo ni kupoteza muda wao. Hawa wote wanaupigia debe utendaji finyu ulionyeshwa na serikali ya Kikwete na wanafanya hivyo si kwa maslahi ya nchi yetu bali kwa maslahi yao wao wenyewe.

- - Matatzio ya fear na inferior ya wananchi wa vyama vingine hayawezi kuwa matatizo ya taifa wala CCM, malalmiko mengi hapa bila hoja ya msingi ya kulisaidia taifa ni waste of time ya wananchi wa Tanzania na ni kuwapotosha kwa makusudi. CCM tuna utamaduni wetu hopefully na huko upnade wa pili mano pia utamaduni wenu, na sitaki kuamini kuwa ni utamaduni wa kulia lia bila sababu ya msingi.
CCM Juu Zaidi! Kidumu.


FMES!

[/QUOTE]

Naam hayo ni matatizo ya Taifa. Tumapokuwa na Rais anayeogopa kuwashughulikia mafisadi pamoja na kuwa kuna ushahidi wa kutosha dhidi yao basi ni lazima tuwe na wasiwasi. Tunapokuwa na Rais ambaye anashindwa kutimiza hata moja ya ahadi zake wakati wa akampeni zake, inabidi tuwe na wasi wasi kwamba kiongozi tuliyekuwa naye hatufai. Tunapokuwa na Rais ambaye anaamua kunyamaza kimya katika issue mbali mbali zenye uziti mkubwa katika maslahi ya nchi kama gharama za vitambulisho ambayo ni shilingi bilioni 200 na Dowans 60 bilioni na kisha kuambiwa na mwandishi wake kwamba hahusiki basi ni ushahidi tosha kwamba Raid huyo hatufai maana katika kila issues ambazo zinakuwa na mjadala mzito nchini yeye hahusiki na huamua kukaa kimya kama haelewi kinachoendelea ndani ya nchi anayoingoza. Wananchi ni lazima wawe na wasi wasi kuwa na Rais ambaye hataki kujihusisha kabisa na mijadala ambayo inagusa maisha ya kila siku ya wale anayewaongoza. Hakuna chochote alichofanya Kikwete katika muda aliokaa madarakani ambacho kimeleta maendeleo yoyote kwa Watanzania.
Kikwete kama katika nchi nyingine ambazo wana katiba zenye nguvu na kujali maslahi ya nchi zao basi angeshapigiwa kura ya kutokuwa na imani naye kwa utendaji hafifu tangu alipoingia madarakani, lakini kwa nchi yetu bado tunaendeleza "utamaduni wa kuachiana" Rais akae madarakani kwa miaka 10bila kutathmini kufanya hivyo kutakuwa na athari zipi kwa Watanzania.

Kigumu chama cha mafisadi...kigumu
 
ni haki kwa mwananchi yeyote kuwa concerned pale anapoona
viongozi wa chama tawala na wabunge wanapoanza kushabikia
ukiukwaji wa katiba ya chama kwa kusisitiza utamaduni na jadi.
ccm wanafahamu fika kwamba angalau mwanachama mmoja aliishatangaza
nia yake ya kuchukua fomu za kugombea kuteuliwa na chama chake
kugombea urais sasa wanamwambia nini huyu mwanachama?

kama mtu haoni umuhimu wa kuzingatia katiba ya chama je itashangaza
akipuuza katiba ya nchi?

watu wanatetea ukiukwaji wa katiba katika kupata mchanganuo wa
ugombea urais kwa tiketi ya ccm. Je watasema nini "mteuliwa" huyo
akishinda urais wa nchi na atakapoanza kupuuza katiba ya nchi kwa
kisingizio cha utamaduni au uzoefu?

ndio maana ni vyema kuingiza kipengele cha "utamaduni" kwenye katiba
ya chama ili akiteuliwa mtu kwa misingi ya mazoea ieleweke angalau
katiba ya chama haijavunjwa.
 
- Maneno mazito sana mkuu haya na ubarikiwe.

Idumu CCM.

FMEs!

Kale kalikizo kameisha ghafla,uzuri wako huwa unaaga lakini huwa unarudi kimya kimya... hii ndiyo JF utaandika tuu...karibu jukwaa la SIASA wazee wa sauti za ........tuendelee kumkoma nyani hata kimya kimya.

Idume JF.
 
Kale kalikizo kameisha ghafla,uzuri wako huwa unaaga lakini huwa unarudi kimya kimya... hii ndiyo JF utaandika tuu...karibu jukwaa la SIASA wazee wa sauti za ........tuendelee kumkoma nyani hata kimya kimya.

Idume JF.

- Mkuu hii ni demokrasia unaweza hata kutangaza kufa halafu ukasema hukufa na ukarudi hapa, ndio maana ninaweza kutoka kurudi kulia kucheka, lakini one thing sivunji sheria, Mwinyi alitoka uwaziri akarudi kama waziri tena Sokoine alijiuzulu baadaye akarudi tena, pole sana kama ninakukwaza lakini hoja hujibiwa kwa hoja na kwa sasa nipo, naona unahngaika sana mkuu uliwekeza kwa Mwandosya nini? Pole sana imetoka hiyo!

Haya sasa tumkome nyani mkuu, Bwa! ha! ha! ah!

FMEs!
 
Kama CCM wataamua kutompinga JK 2010 ni haki yao kama chama - huu hauna mjadala. Hata kama inatukera vipi. Kilichobaki ni KUTOPIGIA KURA CCM!!! Mi nasema tuache kuingilia masuala ya CCM, nakubaliana na FMES katika hilo. Let them hang themselves with a long rope called JK!

Susuviri,
Malecela na Chiligati wao sio CCM? Hiki ni chama ambacho hata wapinzani wana hisa. Tulishaambiwa hapa kuwa kuna zaidi ya 4milioni kwa hiyo Malecela hawezi kuwa msemaji wa wote hao 4 milioni? Wanajua kuwa upinzani wako weak kwenye uraisi kwa hiyo wanataka kumuendeleza Kikwete kwa maslahi yao binafsi. Kwa nini wawanyimwe wengine nafasi ya kuchagua kwa vile tu Malecela kateua?


Wakuu,
Mtanisamehe sana katika hili lakini Ukweli ni kwamba hakuna mtu CCM anayeweza kuongoza nchi zaidi ya Kikwete....Hakuna mtu hata mmoja ndani ya CCM mwenye ubavu anayeweza kupingana na Mtandao wa Mafisadi - HAKUNA..Na kwa mabaya yake yote na mapungufu yake yote Kikwete bado ni rais bora kuliko yoyote katika fikra zangu ndani ya CCM...

Mkandara,
Are you serious or you were joking? Kama ingekuwa ni kweli kuwa Kikwete ni bora kuliko wengine, kwa nini anaogopa ushindani? How about Mwandosya, Mwakyembe, Reginald Mengi n.k. Hao wote si ni CCM?


Hivyo tunachotakiwa sisi wananchi kama tunapigana na chaguo la Malecela au Chiligati basi bila shaka sisi wenyewe ndio wenye Upofu, kwani yaonyesha wazi bado tuna tumaini kuwa yupo mtu ndani ya CCM anaweza kufanya kazi nzuri kuliko Kikwete badala ya kutazama nje ya CCM...

Mkandara,
Hapa naona kipofu ni wewe. Chaguo la Malecela na Chiligati litakuwa linaendelea kumsaidia Mzee Malecela, na wanae ili waendelee na utumishi balozini n.k., Chiligati -uwaziri. Tuliobaki uKikwete hautusaidii, unatumalizia tu nchi. Ndio maana tuna machaguo tofauti.
 
naomba nitajiwe competent candidates wa urais kwa sasa tanzania

That's a weak question. najua unataka utajiwe kati ya mawaziri unaowajua wewe ili ubenchmark mapungufu yao na JK. We are 41 mil by now we have several CEO's and several Managers these also stands a good chance to rule Tanzania.
 
watu wako tiyari kumng'oa kikwete ndio maana wanataka isiende kamati kuu
wajumbe wa nec wakipewa nafasi ya kupiga kura watampa mtu mwingine tu na ndio maana wapambe wa JK (malecela na chilagati) wanawakatisha watu tamaa na wanajua ni wakina nani kwa ajili kampeni zi shaanza

Hakuna hata mmoja aliekuwa tayari kumng;oa Kikwete zaidi ya vyama vya upinzani kwa CCM hilo halipo ni propaganda tu za kisiasa ili kutufanya wengine tuache shughuli za kuwapinga na kusikiliza longolongo zao.
 
1.
Makaayamawe;

Malecela na Chiligati wao sio CCM? Hiki ni chama ambacho hata wapinzani wana hisa. Kwa nini wawanyimwe wengine nafasi ya kuchagua kwa vile tu Malecela kateua?


- Now I see, kumbe wapinzani mna hisa ndani ya CCM, no wonder ni upinzani weak, Malecela hasikilizwi ndani ya CCM, sasa anawezaje kuteua nani awe rais?


2.
Are you serious or you were joking? Kama ingekuwa ni kweli kuwa Kikwete ni bora kuliko wengine, kwa nini anaogopa ushindani? How about Mwandosya, Mwakyembe, Reginald Mengi n.k. Hao wote si ni CCM?

- Si nilisema mkuu kwamba una tatizo moja linakusumbua kwa sababu umewekeza kwa somebody ndio maana maneno ya Malecela yameharibu mlo, si hapa unajisema mwenyewe ulikowekeza, i mean now it makes a sense umewekeza wapi!

3.
Hapa naona kipofu ni wewe.

- Acha matusi weka hoja sio viroja.

4.
Chaguo la Malecela na Chiligati litakuwa linaendelea kumsaidia Mzee Malecela, na wanae ili waendelee na utumishi balozini n.k., Chiligati -uwaziri. Tuliobaki uKikwete hautusaidii, unatumalizia tu nchi.

- Huo utumishi wa ubalozini ambao watoto wote wa Malecela mpaka kumfanya mzee kmtaka Kikwete waliajiriwa na Rais? Na wapi ubalozi wa huo?


5.
Ndio maana tuna machaguo tofauti.

- Sawa sawa, basi heshimu machagu ya wenzako kama tunavyoheshimu machaguo yako ya Mwakembe, Mwandosya na Mengi.

Respect.

Wazee wa sauti ya umeme FMES!
 
ni haki kwa mwananchi yeyote kuwa concerned pale anapoona
viongozi wa chama tawala na wabunge wanapoanza kushabikia
ukiukwaji wa katiba ya chama kwa kusisitiza utamaduni na jadi.
ccm wanafahamu fika kwamba angalau mwanachama mmoja aliishatangaza
nia yake ya kuchukua fomu za kugombea kuteuliwa na chama chake
kugombea urais sasa wanamwambia nini huyu mwanachama?

kama mtu haoni umuhimu wa kuzingatia katiba ya chama je itashangaza
akipuuza katiba ya nchi?

watu wanatetea ukiukwaji wa katiba katika kupata mchanganuo wa
ugombea urais kwa tiketi ya ccm. Je watasema nini "mteuliwa" huyo
akishinda urais wa nchi na atakapoanza kupuuza katiba ya nchi kwa
kisingizio cha utamaduni au uzoefu?

ndio maana ni vyema kuingiza kipengele cha "utamaduni" kwenye katiba
ya chama ili akiteuliwa mtu kwa misingi ya mazoea ieleweke angalau
katiba ya chama haijavunjwa.

Kafara, hawa Chama Cha Mafisadi wako tayari kupindisha katiba yao ili kuundekeza uzembe na utendaji dhaifu. Hii ndiyo imesababisha nchi yetu kubaki nyumba kimaendeleo miaka nenda miaka rudi.

Baada ya kukimbia nchi Ballali, Kikwete angeweza kutumia urafiki wake aliokuwa nao na Kichaka na kuhakikisha anarudishwa nchini ili kusaidia uchunguzi wa ufisadi wa EPA. Hata pale ambapo aliyekuwa balozi wa Marekani alipotamka hadharani kwamba nchi yake ilikuwa tayari kuisaidia Tanzania ili kumrudisha Ballali nchini, Kikwete hakuichangamki offer hiyo sijui ni kwa sababu zipi hasa zilizomfanya aamue hivyo. Huu ulikuwa na uzembe wa hali ya juu ambao haukuweka mbele maslahi ya nchi.

Ilipoundwa tume ya kuchunguza Richmond walitoa mapendekezo ya kuondoloewa madarakani Mkuu wa PCCB Edwards Hosea na Mwanasheria Mkuu hadi hii leo mapendekezo hayo hayajafanyiwa kazi na Kikwete hajasema lolote pamoja na tume ile kutumia mabilioni ya pesa. Huu ni uzembe mwingine.

Swala la mikataba ya madini. Tume ya Bomani ambayo iliundwa na Rais ilikabidhi ripoti yake mwaka mmoja uliopita na kutoa mapendekezo mbali mbali ili kuhakikisha Watanzania tunanufaika na rasilimali zetu. Ni mwaka mmoja sasa hakuna chochote kilichofanyika katika mapendekezo yale.

Chenge kakutwa na mabilioni ya pesa aliyoyapata kwa njia za kifisadi katika ununuzi wa Rada, hadi hii leo bado anapeta uraiani na Kikwete anayetaka tumuamini kwamba anapambana na mafisadi hajachukua hatua yoyote dhidi ya Kikwete kama vile kumtia ndani na kuhakikisha mapesa kwenye account za akina Idrissa Rashid na Chenge waliyoyapata kiharamu yanarudishwa hazina. Njemba imeendelea kunyamaza kimya.

Kiwira kaamua kukaa kimya hajatia neno kuhusu Mkapa kujiuzia mgodi ule kwa njia za kifisadi. Mgodi sasa unakufa na wafanyakazi hawajalipwa mishahara zaidi ya miezi sita sasa, jamaa bado yuko kimya tu.

Kesi za EPA na akina Mramba kama kweli alikuwa anataka kuonyesha kwamba amedhamiria kupambana na mafisadi, basi angeamuru kesi zile ziendeshwe siku tano au sita kwa wiki ili zimlizike haraka, lakini hakufanya hivyo. Zitapigwa kalenda na hatimaye tutaambiwa hakuna ushahidi wa kutosha na hii itakuwa ni baada ya uchaguzi wa 2010. Watanzania tutakuwa tumepigwa na changa la macho.

Idrissa Rashid, Mattaka, Ndullu pamoja na kuvurunda TANESCO, ATCL na BoT bado wanapeta tu, huu ni uzembe mwingine.

Ule mjadala wa kununua/kutonunua mitambo ya Dowans hakutoa hata kauli hata mwandishi waka Comical Salva alitamka hadharani Rais hahusiki na Dowans!!!! Hebu tufananishe na jinsi Obama alivyojikita katika issue za AIG na kashfa nyingine mbali mbali, utaona ni jinsi gani Kikwete alivyokuwa pale kama picha tu.

Walifanya usanii kwenye mapesa ya EPA na kutwambia zilirudishwa bilioni 69, walipoombwa waweke majina ya waliorudisha mapesa hayo hadharani na kiasi kilichorudishwa na kila mmoja na yamewekwa katika bank ipi wakashindwa kufanya hivyo.

Hawana lolote zuri la kusema katika kipindi ambacho Kikwete amekuwa madarakani linalomfanya Kikwete astahili kupewa awamu nyingine, bali ni huu utamaduni wao ndani ya chama cha mafisadi na watetezi wa utendaji mbovu kwamba wanaachiana kukaa madarakani kwa miaka 10 hata kama huyo wanayemuachia ameonyesha hana uwezo wowote wa kuiongoza nchi.

Ndiyo maana hili la mgombea binafsi wa Urais wanalipiga vita sana maana wanajua baadhi ya wanaccm wanaweza kabisa kuchukua form kama wagombea binafsi na hatimaye kumbwaga mgombea wa CCM.

I hope ndani ya CCM wale ambao wanajiona wana qualifications za kuwa Rais watayadharau na kuyapuuza maneno ya Chiligati na Malecela na hatimaye kuamua kuingia kwenye kinyang'anyiro ndani ya CCM dhidi ya Kikwete.

Chiligati na Malecela kama wanataka kuendeleza usanii wao wa kuendekeza viongozi wazembe basi katiba ibadilishwe ili kuruhusu wagombea binafsi ambao wanajiona wana sifa ya kuwania Urais Tanzania wafanye hivyo. Hili litasaidia katika kukimaliza chama cha mafisadi.
 
Je mhe zito kabwe amevuta kutoka dowans ili awatetee

1. Pepo baya la kisiasa laanza kuinyemelea Chadema,mambo si shwari
Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema ambacho kinadaiwa kuingiliwa na pepo baya la kisiasa.

Na Ramadhan Semtawa

2. UPEPO wa kisiasa katika kambi ya upinzani unavuma vibaya, kufuatia hali ya mambo ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kuwa tete. Hali tete ya kisiasa ndani ya Chadema imekuja wakati viongozi wa Chama cha Tanzania Labour (TLP), wakiwa katika hali ya malumbano makali kuelekea kwenye uchaguzi. Nacho chama cha CUF kiliingia kwenye hali ya wasiwasi kisiasa kipindi cha uchaguzi wa viongozi wake hivi karibuni.


3. Wakati upepo huo mbaya ukizidi kuvuma kwa kambi hiyo, Chadema moja ya vyama makini chenye historia ya kutatua mambo yake kimyakimya na kuwa na misingi imara ya uongozi kutoka kwa waasisi akina mzee Edwin Mtei na Bob Nyanga Makani, sasa nacho mambo si shwari. Tathimini ya kichambuzi na duru za kiuchunguzi juu ya mwelekeo wa mambo kwa kuangalia mtiririko wa matukio, mpasuko huo ndani ya Chadema unatokana na suala la ununuzi wa mitambo ya Dowans.


4. Kutofautiana kwa mawazo na misimamo kwa viongozi wa juu ndani ya Chadema kuhusu Dowans, ni jambo ambalo limesababisha mgawanyiko ndani ya chama. Msuguano huo wa fikra na misimamo, ambao umeonekana katika kipindi cha muda wa wiki takriban tatu sasa, ukiwahusisha zaidi Naibu Katibu Mkuu ambaye pia ni mwanasiasa mwenye nguvu, Zitto Kabwe na viongozi wenzake kama akina Dk Wilbrod Slaa, unaonyesha chama hicho sasa kinapita katika wakati mgumu kisiasa.


5. Chadema tayari, kilipita katika wakati mgumu kisiasa baada ya kuondokewa na akina Dk Amaan Kabour, aliporejea Chama Cha Mapinduzi( CCM) na wakati kifo cha Makamu Mwenyekiti marehemu Chacha Wangwe. Wakati wa kuondoka kwa Dk Kabour, Chadema ilipigwa na mawimbi mazito kisiasa kisha ikaweza kuvuka, ndipo mwaka jana ukatokea mvutano mwingine kati ya Wangwe na viongozi wa juu hasa Mwenyekiti Freeman Mbowe katika kutaka kuchukua nafasi ya Mwenyekiti taifa.


6. Hata hivyo, joto hilo la kisiasa la sasa ambalo linatokana na ununuzi wa mitambo ya Dowans ambao umekuja katika kipindi kigumu cha kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu na mkuu hapo mwakani, unaweza kuisumbua Chadema. Tayari, nyufa ndani ya Chadema zinazotokana na ununuzi wa mitambo ya Dowans, zimeanza kujitokeza kufuatia viongozi hao kutoa kauli zinazoonyesha misimamo tofauti kuhusu ununuzi wa mitambo ya Dowans.


7. Wakati Zitto ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma, akisimamia kidete ununuzi wa mitambo hiyo, viongozi wengine wa Chadema wakiongozwa na Dk Slaa pamoja na Mwenyekiti Mbowe, wanapinga.
Katika kudhihirisha ufa huo, wakati Zitto alimtaka mbunge wa Kyela Dk Harrison Mwakyembe, atangaze maslahi yake katika Kampuni ya Power Pool East Africa, Dk Slaa alinukuliwa na gazeti la Mwanachi Jumapili akisema hakupaswa kutangaza maslahi.


8. Dk Slaa katika kauli hiyo, anaonekana kupingana na msaidizi wake wa karibu ambaye ni Zitto katika msimamo kuanzia Dowans na hata uanahisa wa Dk Mwakyembe katika Power Pool. Msuguano huo unaangaliwa kama moja ya chanzo, kinachoweza kuleta mpasuko ndani ya Chadema.


9. Tayari, msimamo huo wa Zitto kuhusu ununuzi wa mitambo ya Dowans na kurusha makombora kwa Dk Mwakyembe, umekuwa ukimfanya ahusishwe na harufu ya ushawishi wa nguvu ya fedha za watuhumiwa wa ufisadi. Hivyo, kauli za vigogo hao wa Chadema kupinga ununuzi wa mitambo ya Dowans, ni sawa na msimamo wa chama kukana kauli ya Naibu Katibu Mkuu wake.

10. Kauli hiyo ya Mbowe ambaye ni Mwenyekiti, ilikuja mahususi kujibu swali kuhusu vipi Zitto aunge mkono ununuzi wa mitambo ya Dowans na msimamo wa chama ni upi. Hata hivyo, kauli hiyo bado inaonekana kushindwa kuondoa wingu zito ndani ya Chadema, kwani Mbowe alimtaka Dk Mwakyembe ahamie chama hicho kwa maelezo kwamba hawezi kupambana na ufisadi ndani ya CCM.


11. Mbowe katika kauli hiyo, alisema mfumo ambao Dk Mwakyembe anautumikia hauwezi kupambana na ufisadi, kauli ambayo ilikuwa ni pigo jingine kwa Zitto kwani tayari amekuwa katika malumbano ya kisiasa na mbunge huyo wa Kyela hadi kurushiana makombora akimtaka ajiuzulu nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Madini.


12. Pia, tangu mjadala wa Dowans, Zitto hajawahi kushiriki vema katika mikutano ya operesheni Sangara mkoani Kilimanjaro, huku mara nyingi akiwa Dar es Salaam.
 
Back
Top Bottom