Malezi Duni na Utandawazi ndio Chanzo cha ongezeko la mijadala ya kupinga na kukosoa ndoa na maisha ya ndoa

Malezi Duni na Utandawazi ndio Chanzo cha ongezeko la mijadala ya kupinga na kukosoa ndoa na maisha ya ndoa

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
301,577
Reaction score
754,412
Good morning Tanganyika!

Nimeshindwa kuvumilia baada ya kuona ongezeko la mada za kupinga kuoa, ndoa na maisha ya ndoa! Jamii Forums ni kama kioo cha Taifa kwasasa. Think tank kubwa ya nchi nathubutu kusema iko humu JF, sasa kitu kinapotrend sana Jamii forums ni lazima upate picha ya kinachoendelea nchini.

Hili ongezeko la mada za kupinga, kukosoa, kukejeli ndoa na maisha ya ndoa si jambo zuri hata kidogo bali ni msiba kwa taifa zima! Kuna sumu mbaya wamelishwa vijana wetu na imewaingia barabara!

~ Kukataa ndoa ni kukataa kujikubali.
~ Ni kukataa kujitambua.
~ Ni kukataa majukumu.
~ Ni kukosa malezi sahihi.
~ Ni kukosa akili.
~ Ni kukosa hekima.
~ Ni kwenda kinyume na maagizo ya Mwenyezi Mungu (kwa waamini).
~ Ni kukosa upendo upeo na maono!

Tunataka kuunda Taifa gani bila ndoa?
~ Ndoa ndio chanzo cha familia.
~ Ndoa ni dalili njema ya ukomavu wa akili.
~ Ndoa ni msingi wa uwajibikaji kujali, amani, furaha na upendo.
~ Ndoa ni future, bila ndoa future haina maana sana.

~ Makuzi yasiyo sahihi.
~ Wazazi wasiojitambua.
~ Wazazi wasio na muda wala ukaribu na familia zao.
~ Utandawazi.
~ Elimu potofu mitandaoni juu ya dhana nzima ya ndoa na maisha yake ni visababishi vikubwa mno vya matokeo hasi wanayopata vijana kuhusu ndoa na wao bila kujitambua huyafanya hayo kama ndio uhalisia na kuja na mada za kila aina.

Kama maandiko ya misahafu ya kiimani yanawaasa wanaume waishi na wanawake kwa akili, tafsiri yake ni kwamba mkataa ndoa hana akili ndio maana hawezi kuishi maisha ya ndoa.

Ukomavu wa kiakili, maono na hekima hukufanya uitamani ndoa ili kujipima. Uwezo wako wa kumudu maisha ya ndoa. Utayari wako wa kuhudumia ndoa. Ujasiri wako wa kuyakabili magumu ya ndoa nk, nk.

Ndoa ni kwa ajili ya wanaume kamili. Ndoa si kwa ajili ya wavulana!

Mjadala utaendelea.
 
Mkuu Mimi naona Maisha ya Mtu kukaa single bila Attachment na Mwanamke ni mazuri Sana

Kula vizuri
Lala vizuri
Sali Sana
Kataa ndoa
Tafuta pesa kwa ajili yako na wazazi na wasiojiweza huu mradi wa Ndoa unawafaidisha wanawake tu.
 
Wengi hawajitambui Wana stress za maisha instead ya kutafuta wanawake wenye heshima wanagombana haww wavaa nusu uchi ..Nina rafiki zangu wengi wameoa wale wanawake wa dini haswa wako kweny ndoa zaidi ya miaka 5 wanafurahi .

Sio unaona mwanamke alishawahi kuwa na majamaa kibao huko nyuma unafikria atatulia kwani we ni Nan? ..wenzenu wanaoa wanawake wanajielewa wao ni hao wanapokutana nao bar sijui coco beach wakidanga
 
Mkuu Mimi naona Maisha ya Mtu kukaa single bila Attachment na Mwanamke ni mazuri Sana

Kula vizuri
Lala vizuri
Sali Sana
Kataa ndoa
Tafuta pesa kwa ajili yako na wazazi na wasiojiweza huu mradi wa Ndoa unawafaidisha wanawake tu.
Kwa hyo hao wazazi wako walishushwa mbiguni ..Haukuzaliwa kuja kumtumikia mzazi wako inawezekana hata wazazi wako hawajwahi kusaidia wazazi wao.

Tengeneza familia yako na mwanamke mweny heshima wako kibao we endelea kufauta hawa sijui mmekutana chuo ,sijui mweupe
 
Kwa hyo hao wazazi wako walishushwa mbiguni ..Haukuzaliwa kuja kumtumikia mzazi wako inawezekana hata wazazi wako hawajwahi kusaidia wazazi wao.

Tengeneza familia yako na mwanamke mweny heshima wako kibao we endelea kufauta hawa sijui mmekutana chuo ,sijui mweupe
Mkuu Maisha ni vipaumbele Mimi lazima nisapoti wazazi kwanza na wasiojiweza
 
Mkuu Maisha ni vipaumbele Mimi lazima nisapoti wazazi kwanza na wasiojiweza
Hata wwe unaelekea kuwa mzazi amini ..Tafuta familia ,tabia usizozipenda usivumilie kabisa kwa mkeo mtarajiwa Bora ukachukue kijijini.

Angalia tabia za mama ako na jinsi alivyokulea basi nawe tafuta mwanamke mwenye tabia izo ikiwezekana muombe mama ako akutafutie mchumba kutoka jamii yake.
 
mshana Umelaumu sana upande mmoja bila kutuwekea sababu zao, ingependeza utuwekee sababu zao tuzipime, ili tujue, vipi hao unaotaka waolewe, wao wanajitambua? wana malezi bora toka kwa wazazi wao? wana akili? wana hekima? wana upendo, upeo, na maono?
 
mshana umelaumu sana upande mmoja bila kutuwekea sababu zao, ingependeza utuwekee sababu zao tuzipime, ili tujue, vipi hao unaotaka waolewe, wao wanajitambua? wana malezi bora toka kwa wazazi wao?
Mshana Jr na Robert Heriel
Robert anaunga mkono kataa ndoa campaign akiwakilisha vijana wa kiume
Na Jr anakataa hoja akiwatetea dada zetu ambao kila siku Wanazidi kupoteza potential
 
Good morning Tanganyika!

Nimeshindwa kuvumilia baada ya kuona ongezeko la mada za kupinga kuoa, ndoa na maisha ya ndoa! Jamii Forum ni kama kioo cha Taifa kwasasa....
Kelele za usawa zimeondoa maana ya ndoa, ndoa imekuwa jukwaa la kushindana na kuonyeshaNA umwamba
hiyo ndo sababu watu wanaona bora wakae single.

Baba ukirudi tu nyumbani unaombwa kukaguliwa simu. tumepoteza nafasi ya utawala.

Baba lazima uhofiwe
 
Hata wwe unaelekea kuwa mzazi amini ..Tafuta familia ,tabia usizozipenda usivumilie kabisa kwa mkeo mtarajiwa Bora ukachukue kijijini ..Angalia tabia za mama ako na jinsi alivyokulea basi nawe tafuta mwanamke mwenye tabia izo ikiwezekana muombe mama ako akutafutie mchumba kutoka jamii yake.
Kwanini niende umbali wote huu kisa tuu ndoa wakati naweza tuu nikapata mtoto na nikamlea vizuri bila hata hayo maisha ya ndoa.
 
Nilichogundua, migogoro ya ndoa siku hizi haihitaji ushauri wa wazee, kwani wazee wetu waliishi maisha yao tofauti na vijana wa sasa, wanatofautiana upendo, malezi, na vingine vingi.

Hivyo watu hao kuwapelekea migogoro ya ndoa leo, ni sawa na kutumia njia zilizopitwa na wakati kutibu tatizo jipya, muhimu vijana hawa hawa wa sasa ndio washauriane namna ya kumaliza matatizo yao ya ndoa, kwasababu wao ndio wanayaishi matatizo ya sasa.
 
Mkuu Mimi naona Maisha ya Mtu kukaa single bila Attachment na Mwanamke ni mazuri Sana

Kula vizuri
Lala vizuri
Sali Sana
Kataa ndoa
Tafuta pesa kwa ajili yako na wazazi na wasiojiweza huu mradi wa Ndoa unawafaidisha wanawake tu.
Haya ni maneno alitakiwa ayaandike mdada aisee mwanaume unatakiwa uoe, uwe kichwa na uongoze familia
vinginevyo una fail ile mbaya
 
Usipooa utaolewa.
Unawezaje kufuga ng'ombe wakati maziwa yapo mengi tena mengine unapewa bure kabisa.
Watu walioa au kuolewa wanaishi kama hawako kwenye ndoa.
Nina ushahidi

1. Wanawake waliolewa wanazaa nje. Kuna mwanamke kazaa na mchepuko watoto 2 na mwanaume hajui. Watu wanalea watoto wa nje bila kujua

2. Nilishawahi kutembea na wanawake za watu. Mwingine nilimjaribu anizalie mtoto akakubali.
Kama hawa wanafanya hivi, kuna haja gani ya kuoa? Wake za watu wanaliwa sana mpk unapata hofu ya kuoa
 
Back
Top Bottom