Malezi ya wazazi wa siku hizi na dosari zake!

Malezi ya wazazi wa siku hizi na dosari zake!

Bilashaka huyo mtoto hakua mtoto mchanga. Na huyo mama anaechezewa kalio anaona kawaida tu! Pengine kamzowesha hivyo siku nyingi sasa mama mtu haoni aibu kuchezewa kalio hadharani
Nakubali maneno ya yule mzee kwenye msiba kwamba vizazi vinavyokuja huko baadae yawezekana mtoto "akaonjeshwa" ili apajue alipo tokea eti ikiwa ni ishara ya mapenzi ya mama kwa mtoto! Dunia inakwenda kasi sana
yule mtoto ni kati ya miaka 5-7 hivi yaani nilihisi aibu mimi
 
Mm mwanangu wa kiume sijawah kumchapa wala kumgombeza ila ananiogopa kuliko anavyomwogopa mama yake anaemchapa mara kwa mara akikosea, kauli yangu anaiheshimu hata iweje kama hajaridhika ataishia kutoa machozi kimya kimya sio kwa makelele atakunja sura tu kuanza kulia kumkimblia mama yake, ila ajabu ananipenda kuliko maelezo nikiwa nae hataki niende popote anataka nikae nae tu, mke wangu anasema namdekeza ila in reality i just have strong bond na yeye down in my heart ila anaheshimu kauli yangu namuombea Mungu anipende na kuniheshimu hvyo milele
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Msamehe bure amesahau Ile kauli ya "asiyefunzwa na mamaye hufunzwa na ulimwengu"
hajui hata ni kwanini huwa tunasema "lugha mama" na sio "lugha baba'
 
Jumapili iliyopita nilihudhuria kwenye msiba wa ndugu wa rafiki yangu, Miongoni mwa waombolezaji alikua dada mmoja mwenye miaka kama 26-30, alikuwa na mwanae wa kama miaka minne hivi

Sijui ilikuaje lakini mara yule dogo akaanza kulia na kisha kumvurumishia ngumi na mateke mama yake. Mama mtu akabakia kusema tu " Brian stooop banaa". Mpaka mama mmoja alipokuja akamwambia hiyo ni aibu mwanao hata kama ni mdogo unamuachia akupige hivyo hebu ingieni kule chumbani mkabembelezane

Watoto wote wadogo sio ajabu kuwa na utundu lakini utundu mwingine nahisi kama ni wa kukosa adabu na unaendekezwa na wazazi hasa wakike.

Nimewahi kushuhudia mtoto wa chini ya miaka mitano akiipasua simu ya mama yake kwa makusudi kwa kuibamiza chini na mama mtu anasema "mmmh leo sijui kakasirika nini huyu!" halafu akaanza kumbembeleza!

Kuna mtoto wa shangazi yangu aliwahi kumtupia usoni mfuko wa chips mama yake baada ya kugundua alicholetewa sio alichomuagiza wakati anaenda kazini!

Hapo kwenye msiba baada ya tukio la huyo mama na mtoto watu walisema mengi sana kuhusu dosari za kimalezi za wazazi wa kike wa siku hizi. Kuna mzee mmoja akawa anasema dunia inavokwenda huko baadae hayo mapenzi ya mama na mwana yanaweza kufikia hatua ya aibu zaidi hata mama "kumuonjesha" mwanae atakapo balehe

Sina hakika kama haya mambo ya kudekeza watoto kiasi hiki yalikuwepo zamani ila nahisi mengine ni kuwapotosha watoto kwa kuwapa malezi yasiyofaa.
Mlee mtoto katika njia ipasayo naye hataiacha hata atakapokuwa mzee.

Mtoto usimnyime mapigo,ukimpiga kwa fimbo hatokufa,bali utakuwa umemuweka katika njia sahihi.

Mungu nisaidie siku nikipata mwanangu nimlee katika njia sahihi,
Sitaki kuwa too harsh,pia sitaki kuwa too kind.
 
Nikikumbuka kipigo alichokuwa ananipa mama yangu mpaka leo nacheka na kumshukuru sana kama kaka mkubwa kipigo kile kilinisaidia kufuata njia inayofaa na wadogo zangu wakaniiga. Kosa lolote liwe dogo au kubwa nilitandikwa sana na mama, kuchapwa malapa ya usoni kama yote, baba yeye alikuwa hapigi mara kwa mara ila akifikishiwa kesi na mama jiandae kufa. Alikuwa na waya huo wa umeme acha kabisa.
Aisee..acha kabisa na mtoto wa kwanza inakuwa kama wewe ndo zana, mama alikuwa anapiga mpaka anang'ata....kifupi yeye alikuwa ndo uncharge...! Baba hakuwa mpigaji kiviile lakini akiunguruma huko asiye na kosa mwenye kosa wte ni kutetemeka tu...
 
nakumbuka kuna mama mmoja alinipa mtoto wake nimpakate yeye akawa amesimama mbele yetu mtoto akaanza kumshika kalio mi nikamtoa mkono wake haraka kakaniangalia kwa hasira akarudisha mkono pale huku anapapasa kabisa yule mama akageuka akamuangalia mtoto wake halafu akageuka mbele huku mtoto akiendelea kuchezea tako la mama yake mmama wa pembeni yangu ndo akaanza kujibizana na yule mmama ikawa gumzo kwenye gari watu wote kimya kusikiliza ugomvi
Mi nikamuweka mtoto kwenye siti niliyokaa nikashuka tu kituo kilichofuata
Mh, hii ni hatari sana mkuu
 
Hahahahahaha hongera kwa maza ako

Nakumbuka bi mkubwa ilikuwa akipika kitu sikipendi nikisusa tu kosaaa nachezea kipigo nakalishwa kwenye sahani na lazima Nile,,,,, ila Nampa pongezi sababu mpaka sasa hakuna mwenye jeuri ya kuinua bakuli lake kumjibu bi mkubwa akiongea na tena tukimvuruga kama tupo karibu nae vibao tunachapwa
Halafu we Nyambonde hebu nitafute
 
Back
Top Bottom