Mali za umma zinapouzwa, watumishi wa Serikali wasiruhusiwe kununua sababu si walipa kodi

Mali za umma zinapouzwa, watumishi wa Serikali wasiruhusiwe kununua sababu si walipa kodi

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
Habari wakuu,

Wakati wa Mkapa ulitokea uuzaji wa nyumba za serikali, na kigezo cha kuweza kununua nyumba hizo ilikuwa uwe mtumishi wa serikali. Jamii iliona ni sawa na haki, lakini kumbe jambo sawa na la haki ilikuwa kwa watumishi hao kutoruhusiwa kabisa kununua nyumba zile.

Wanazuoni wanasema kuwa mali za Serikali zinapatikana kwa kupitia kodi, kwa hiyo hata wakati zinapouzwa ni haki wale walipa kodi ndiyo wakapewa nafasi ya kununua. Watumishi wa serikali, kuanzia Rais, mawaziri, wabunge na watumishi wengine wote wanaolipwa na serikali si walipa kodi bali ni watu wanaotumia kodi.

Si haki kumuuzia mtu ambaye hakuhusika kuchangia kupatikana mali hiyo huku ukimuondoa kabisa yule aliyehusika kuinunua. Kwa mantiki hiyo, mali yoyote ya Serikali inapouzwa, iwe nyumba, magari, viwanja, mashamba n.k, watumishi wa serikali hawapaswi kuruhusiwa kununua.

Nawasilisha.
 
Askari analipwa kwa huduma yake ya rushwa na ubabe wa uniform
Mwalimu analipwa kwa kudumaza akili za watu
Daktari, nesi, famasia, n.k wanalipwa kwa kuuza kemikali hatarishi
Waandisi wanalipwa kwa kuzibua mifereji, kukodisha mavyombo ya ujenzi, kuongeza bando, n.k

Ninachojaribu kusema ni kuwa, watumishi wa umma wanalipwa kwa huduma wanazotoa, na wao wanalipa kodi
 
Askari analipwa kwa huduma yake ya rushwa na ubabe wa uniform
Mwalimu analipwa kwa kudumaza akili za watu
Daktari, nesi, famasia, n.k wanalipwa kwa kuuza kemikali hatarishi
Waandisi wanalipwa kwa kuzibua mifereji, kukodisha mavyombo ya ujenzi, kuongeza bando, n.k

Ninachojaribu kusema ni kuwa, watumishi wa umma wanalipwa kwa huduma wanazotoa, na wao wanalipa kodi
Hiki ndo kiwango cha uelewa wa Watanzania walio wengi! Upeo mdooooogo na unaweza kukuta aliyeandika Uzi huu ni graduate!
Watumishi wa Umma ndo walipa Kodi wa uhakika kuliko wewe unayeropoka hovyo huku hujui kitu!
Sidhani hata kama ulishawahi kusikia kitu kinaitwa PAYE!
 
Askari analipwa kwa huduma yake ya rushwa na ubabe wa uniform
Mwalimu analipwa kwa kudumaza akili za watu
Daktari, nesi, famasia, n.k wanalipwa kwa kuuza kemikali hatarishi
Waandisi wanalipwa kwa kuzibua mifereji, kukodisha mavyombo ya ujenzi, kuongeza bando, n.k

Ninachojaribu kusema ni kuwa, watumishi wa umma wanalipwa kwa huduma wanazotoa, na wao wanalipa kodi
Na inawezekana mwalimu wako alikidumaza maana akili si zako hizo ulizotumia kuandika hapa
 
Haujui kwamba watumishi wa umma ndiyo wanaoongoza kwa kulipa kodi nchi hii, tena kiulazima kodi inakatwa juu juu bila kona kona.

Bora wafanyabiashara wanaweza wakakwepakwepa, hawa watumishi hawana hiyo option.
Ile siyo kodi. Haiongezi chochote kwenye kodi ya nchi.
 
Habari wakuu. Wakati wa Mkapa ulitokea uuzaji wa nyumba za serikali. Na kigezo cha kuweza kununua nyumba hizo ilikuwa uwe mtumishi wa serikali. Jamii iliona ni sawa na haki. Lakini kumbe jambo sawa na la haki ilikuwa kwa watumishi hao kutoruhusiwa kabisa kununua nyumba zile.

Wanazuoni wanasema kuwa mali za serikali zinapatikana kwa kupitia kodi. Kwahiyo hata hata wakati zinapouzwa ni haki wale walipa kodi ndiyo wakapewa nafasi ya kununua. Watumishi wa serikali, kuanzia Rais, mawaziri, wabunge na watumishi wengine wote wanaolipwa na serikali si walipa kodi bali ni watu wanaotumia kodi.
Si haki kumuuzia mtu ambaye hakuhusika kuchangia kupatikana mali hiyo huku ukimuondoa kabisa yule aliyehusika kuinunua.


Kwa mantiki hiyo. Mali yote ya serikali inapouzwa, iwe nyumba, magari, viwanja, mashamba nk nk. Watumishi wa serikali hawapaswi kuruhusiwa kununua.

Nawasilisha
unajua maana ya kodi mkuu?
unajua kitu kinaitwa PE kwenye mshahara?
watumishi wa umma wanalipa kodi kwa uhakika kuliko kundi lingine lolote
 
Hiki ndo kiwango cha uelewa wa Watanzania walio wengi! Upeo mdooooogo na unaweza kukuta aliyeandika Uzi huu ni graduate!
Watumishi wa Umma ndo walipa Kodi wa uhakika kuliko wewe unayeropoka hovyo huku hujui kitu!
Sidhani hata kama ulishawahi kusikia kitu kinaitwa PAYE!
Utalipaje kodi kwa kutumia pesa ya kodi. Watumishi mishahara yao inategemea watu wengine walipe kodi. Kwa hiyo yale makato yao hayaongezi chochote kwenye kodi ya nchi.
 
unajua maana ya kodi mkuu?
unajua kitu kinaitwa PE kwenye mshahara?
watumishi wa umma wanalipa kodi kwa uhakika kuliko kundi lingine lolote
Assume nchi nzima ina watumishi wa umma tu. Unafikiri kuna kodi hata buku itapatikana? Maana mtumishi wa umma pesa yake anategemea watu wa sekta binafsi walipe kodi ndiyo apate mshahara. Mtumishi wa umma haongezi hata Tsh mia kwenye kodi ya nchi. Ukisikia wabunge na watumishi wanajisifu kulipa kodi jua ni upotoshaji.
 
Nadhani mleta mada tumsamehe tu tatizo ni exposure..hajui kuna kitu kinaitwa PAYE.

Watumishi wa umma wanafyekwa pesa kulipia kodi kila mwisho wa mwezi.

#MaendeleoHayanaChama
Tuwe tunajielimisha. PAYE siyo kodi. Haiongezi chochote kwenye kodi ya nchi iliyokusanywa. Watumishi waumma ni watumia/wala kodi. Si walipa kodi.
 
Na inawezekana mwalimu wako alikidumaza maana akili si zako hizo ulizotumia kuandika hapa
Ahahahaha
Nimekuelewa mkuu, jitahidi uwe mtumishi mwema unayezingatia maadili na weledi, mbona mafisadi tunawataja tu na hawana NYONGO kama hii!
 
Habari wakuu. Wakati wa Mkapa ulitokea uuzaji wa nyumba za serikali. Na kigezo cha kuweza kununua nyumba hizo ilikuwa uwe mtumishi wa serikali. Jamii iliona ni sawa na haki. Lakini kumbe jambo sawa na la haki ilikuwa kwa watumishi hao kutoruhusiwa kabisa kununua nyumba zile.

Wanazuoni wanasema kuwa mali za serikali zinapatikana kwa kupitia kodi. Kwahiyo hata hata wakati zinapouzwa ni haki wale walipa kodi ndiyo wakapewa nafasi ya kununua. Watumishi wa serikali, kuanzia Rais, mawaziri, wabunge na watumishi wengine wote wanaolipwa na serikali si walipa kodi bali ni watu wanaotumia kodi.
Si haki kumuuzia mtu ambaye hakuhusika kuchangia kupatikana mali hiyo huku ukimuondoa kabisa yule aliyehusika kuinunua.


Kwa mantiki hiyo. Mali yote ya serikali inapouzwa, iwe nyumba, magari, viwanja, mashamba nk nk. Watumishi wa serikali hawapaswi kuruhusiwa kununua.

Nawasilisha
What is PAYE, PAY AS YOU EARN?
 
Naomba aliyemuelewa huyu mleta mada anieleweshe nimesoma mara 3 simuelewi _kuhusu mtumishi wa serikali halipi kodi.
 
Watumishi wa umma ni walipa kodi
Mishahara yao hukatwa kodi

Revise your head
Mishahara yao inatokana na kodi. Sasa atatumiaje pesa ya kodi kulipa kodi? Ataongeza chochote kwa kulipa kodi kwa kutumia kodi? Watumishi wote kuanzia Rais, hawatakiwi kupewa nafasi ya kununua mali za umma zilizopatikana kwa kutumia kodi.
 
Back
Top Bottom