Mali za umma zinapouzwa, watumishi wa Serikali wasiruhusiwe kununua sababu si walipa kodi

Mali za umma zinapouzwa, watumishi wa Serikali wasiruhusiwe kununua sababu si walipa kodi

What is PAYE, PAY AS YOU EARN?
Ambapo watumishi wa serikali hawakatwi hata hiyo PAYE kiuhalisia.

OC inakatwa?
Allowances?
OT?

Ninasikia kule binafsi, ni lazima vyote vipitishwe kwenye mkeka na kupigwa kodi.

Basic - 100,000
Paye - 9%*100,000
NHIF - 5%
Tucta - 2%
N.K

Allowances - FoC
 
Unajua kwamba mtumishi kuna kitu anaiuzia serikali ndiyo maana inamlipa ?
Nafahamu. Anatoa huduma na anapata mapato kutokana na huduma aliyotoa. Lakini halipi kodi. Watu wa sekta binafsi ndiyo wanazalisha na kulipa kodi. Kodi hiyo inaenda kulipa watumishi wa umma, kujenga barabara, kujenga nyumba nk nk. Sasa inakuingia akilini mtu ambaye mshahara wake umetoka kwenye kodi achukue atoe sehemu fulani na kusema analipa kodi? Ni haki mtu huyu kupewa kipaumbele au hata kuruhusiwa kununua mali zilizotokana na walipa kodi?
 
Utalipaje kodi kwa kutumia pesa ya kodi. Watumishi mishahara yao inategemea watu wengine walipe kodi. Kwa hiyo yale makato yao hayaongezi chochote kwenye kodi ya nchi.
Unapendelea walipe kiasi gani ili iitwe kodi?Kwa sababu "umeeleza" wanacholipa kwa nyakati hizi si "kodi"!
 
Mishahara yao inatokana na kodi. Sasa atatumiaje pesa ya kodi kulipa kodi? Ataongeza chochote kwa kulipa kodi kwa kutumia kodi? Watumishi wote kuanzia Rais, hawatakiwi kupewa nafasi ya kununua mali za umma zilizopatikana kwa kutumia kodi.
Kwa hoja hiyo mfano mtu anapewa tenda ya Serikali.mfano kujenga barabara analipwa na Serikali pesa inayotokana na kodi na yeye pia akipokea hela analipa kodi kwa hiyo huyo naye sio mlipa kodi ?
 
Nafahamu. Anatoa huduma na anapata mapato kutokana na huduma aliyotoa. Lakini halipi kodi. Watu wa sekta binafsi ndiyo wanazalisha na kulipa kodi. Kodi hiyo inaenda kulipa watumishi wa umma, kujenga barabara, kujenga nyumba nk nk. Sasa inakuingia akilini mtu ambaye mshahara wake umetoka kwenye kodi achukue atoe sehemu fulani na kusema analipa kodi? Ni haki mtu huyu kupewa kipaumbele au hata kuruhusiwa kununua mali zilizotokana na walipa kodi?
Sekta binafsi wanaopata tenda mbali mbali mbali serikalini na kulipwa na serikali na wao kulipa kodi je hao nao ni.walipa kodi au la? Maana wanalipa kodi kwa pesa za kodi walizolipwa kwa tenda zao serikalini
 
Unapendelea walipe kiasi gani ili iitwe kodi?Kwa sababu "umeeleza" wanacholipa kwa nyakati hizi si "kodi"!
Hawawezi kulipa kodi kwa kutumia mishahara iliyotokana na kodi. Labda kama wana shughuli mbali na kazi ya serikali.
 
Habari wakuu. Wakati wa Mkapa ulitokea uuzaji wa nyumba za serikali. Na kigezo cha kuweza kununua nyumba hizo ilikuwa uwe mtumishi wa serikali. Jamii iliona ni sawa na haki. Lakini kumbe jambo sawa na la haki ilikuwa kwa watumishi hao kutoruhusiwa kabisa kununua nyumba zile.

Wanazuoni wanasema kuwa mali za serikali zinapatikana kwa kupitia kodi. Kwahiyo hata hata wakati zinapouzwa ni haki wale walipa kodi ndiyo wakapewa nafasi ya kununua. Watumishi wa serikali, kuanzia Rais, mawaziri, wabunge na watumishi wengine wote wanaolipwa na serikali si walipa kodi bali ni watu wanaotumia kodi.
Si haki kumuuzia mtu ambaye hakuhusika kuchangia kupatikana mali hiyo huku ukimuondoa kabisa yule aliyehusika kuinunua.


Kwa mantiki hiyo. Mali yoyote ya serikali inapouzwa, iwe nyumba, magari, viwanja, mashamba nk nk. Watumishi wa serikali hawapaswi kuruhusiwa kununua.

Nawasilisha
Mkuu, kwa nini umeamua kuyasema yote haya bila kuwa na uhakika wa point unayoitetea?

Kifupi wafanyakazi wa serikali ni walipa kodi wazuri wasioweza kukwepa, tena kodi kubwa kubwa.

Ningelikuelewa kama ungelisema kuwa, wasipewe nafasi ya kununua mali hizo kwa sababu, wanaghushi ubovu wa vifaa na kujiuzia bei ya kutupwa, hapo ningeielewa context.

Nyumba, sijui magari nk nk vingi vizima hughushiwa ubovu ili waweze kujiuzia kwa bei ndogo.

Jambo jingine wanufaika katika minada hiyo ni wakubwa wenye vyeo huko makazini, lakini mtumishi wa chini mpaka akauziwe, jua kazunguka mbuyu!

Wangelipigwa marufuku kujiuzia mali hizo wao, basi minada hiyo ingelikuwa ya haki na manufaa, si kwa serikali tu bali kwa umma.
 
Kwa hoja hiyo mfano mtu anapewa tenda ya Serikali.mfano kujenga barabara analipwa na Serikali pesa inayotokana na kodi na yeye pia akipokea hela analipa kodi kwa hiyo huyo naye sio mlipa kodi ?
Yah, huyu ni kama mtumishi wa serikali. Haongezi hata mia kwenye jumla ya kodi iliyokusanywa na nchi. Kuna watu wamelipa kodi ndiyo pesa ya kujenga barabara ikapatikana. Sasa hiyo pesa iliyotoka kwenye kodi itatoaje kodi tena?
 
Hawawezi kulipa kodi kwa kutumia mishahara iliyotokana na kodi. Labda kama wana shughuli mbali na kazi ya serikali.
Sasa,umewezaje kuwaweka katika kundi la wasiolipa "kodi" ilhali haujui na hauna takwimu za "shughuli zoo" nyingine zaidi ya ajira zao?No research,no data,no right to speak!Huoni kama unabahatisha,unaongopa na kuwadhalilisha watumishi wa serikali?
 
Sasa,umewezaje kuwaweka katika kundi la wasiolipa "kodi" ilhali haujui na hauna takwimu za "shughuli zoo" nyingine zaidi ya ajira zao?No research,no data,no right to speak!Huoni kama unabahatisha,unaongopa na kuwadhalilisha watumishi wa serikali?
Mtu anaweza kuwa vitu vingi kwa wakati mmoja. Mtumishi wa serikali na mkulima au mfanyabiashara kwa wakati mmoja. Mi nazungumzia mtumishi wa serikali. Mtumishi wa serikali halipi kodi.
 
Mtu anaweza kuwa vitu vingi kwa wakati mmoja. Mtumishi wa serikali na mkulima au mfanyabiashara kwa wakati mmoja. Mi nazungumzia mtumishi wa serikali. Mtumishi wa serikali halipi kodi.
Umeelewa nilichouliza?Tafadhali,rudia tena kuelewa nilichokuuliza.
 
Tuwe tunajielimisha. PAYE siyo kodi. Haiongezi chochote kwenye kodi ya nchi iliyokusanywa. Watumishi waumma ni watumia/wala kodi. Si walipa kodi.
Haiongezi chochote hiyo hela ikikatwa inaenda wapi??

#MaendeleoHayanaChama
 
Yah, huyu ni kama mtumishi wa serikali. Haongezi hata mia kwenye jumla ya kodi iliyokusanywa na nchi. Kuna watu wamelipa kodi ndiyo pesa ya kujenga barabara ikapatikana. Sasa hiyo pesa iliyotoka kwenye kodi itatoaje kodi tena?
Haya mfanyakazi wa Serikali kapata mshahara ambao unatokana na kodi

Anaenda kununua bidhaa dukani kwa mfanyabiashara baada ya kupata mshahara halafu huyo mfanyabiashara analipa kodi kwa hicho alichonunua mfanyakazi

Je huyo mfanyabiashara ni mlipa kodi kwa tafsiri yako? Sababu hela ya kodi ndio kapokea iliyoletwa na mfanyakazi wa serikalini anayelipwa kupitia kodi
 
Mkuu, kwa nini umeamua kuyasema yote haya bila kuwa na uhakika wa point unayoitetea?

Kifupi wafanyakazi wa serikali ni walipa kodi wazuri wasioweza kukwepa, tena kodi kubwa kubwa.

Ningelikuelewa kama ungelisema kuwa, wasipewe nafasi ya kununua mali hizo kwa sababu, wanaghushi ubovu wa vifaa na kujiuzia bei ya kutupwa, hapo ningeielewa context.

Nyumba, sijui magari nk nk vingi vizima hughushiwa ubovu ili waweze kujiuzia kwa bei ndogo.

Jambo jingine wanufaika katika minada hiyo ni wakubwa wenye vyeo huko makazini, lakini mtumishi wa chini mpaka akauziwe, jua kazunguka mbuyu!

Wangelipigwa marufuku kujiuzia mali hizo wao, basi minada hiyo ingelikuwa ya haki na manufaa, si kwa serikali tu bali kwa umma.
Unapoint nzuri. Watumishi kuruhusiwa kununua mali za serikali kunaleta mgongano wa kimaslahi. Lakini pia hawalipi kodi. Wao ni watumiaji wa kodi. Hili lipo toka enzi za wafalme na machifu. Kodi/hongo ilitolewa na raia kugharamia maisha ya chifu na maofisa wao. Kusema leo 'machifu' na 'maofisa' wao wanalipa kodi ni kutupiga kiini macho.
 
Haiongezi chochote hiyo hela ikikatwa inaenda wapi??

#MaendeleoHayanaChama
Nafikiri inarudi kwenye kodi ilikotoka. Ipo hivi. Mfano serikali imekusanya kodi Milioni mia tano. Ikatumia milioni mia moja kulipa mishahara watumishi wake. Milioni tisa wakakatwa kama PAYE. Je unafikiri jumla ya kodi ya serikali inakuwa imeongezeka kuwa milioni mia tano na tisa? Hapana.
Badala yake kodi Tsh milioni 91 imetumika kulipa mishahara na serikali imebakiwa na milioni 409. Kwahiyo, watumishi wa umma ni wala kodi, si walipa kodi.
 
Back
Top Bottom