Malisa aachiwa kwa dhamana Saa Saba Usiku, moja kwa moja aelekea Hospitali ya KCMC

Malisa aachiwa kwa dhamana Saa Saba Usiku, moja kwa moja aelekea Hospitali ya KCMC

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Jeshi la Polisi Mkoani Arusha limemuachia kwa dhamana Godlisten Malisa majira ya Saa saba Usiku wa kuamkia leo Juni 8, 2024.

Baada ya kuachiwa moja kwa moja yeye na wawakilishi wake wakiongozwa na Wakili Hekima Mwasipu wakaelekea Hospitali ya KCMC kutokana na afya ya Malisa kudaiwa kutokuwa nzuri.

7840c7ee-6619-4ac4-acf5-2f1b0a88bbce.jpeg


Imeelezwa kuanzia jana Malisa amekuwa akilalamika kuwa anaumwa.

Wakili Hekima Mwasipu amesema wamesaini Bondi ya Milioni 10 na anatakiwa kumrejesha kituoni hapo saa tatu Asubuhi ya leo Juni 8, 2024.

============
AWALI ilikuwa hivi:
============

Wakili Kibatala: Malisa hajapewa dhamana, amehojiwa mara mbili, tunasubiri ahojiwe mara ya tatu


Wakili Peter Patience Kibatala amezungumzia suala linalohusu Godlisten Malisa kwa kuchambua kinachoendelea tangu alipokamatwa akiwa Mahakamani Dar es Salaam kisha kusafirishwa hadi Mkoani Kilimanjaro.

Anaelezea alivyokamatwa
Jana (Juni 7, 2024) nikiwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu pamoja na Wakili Hekima Mwasipu tulikuwa katika majukumu ya kusimamia kesi inayowahusu Godlisten Malisa na Boniface Jacob kuhusiana na maandishi fulani yanayowahusu.

Mchakato uliokuwa unafanyika ni “Usikilizaji wa Awali Mahakamani” kwa lengo la kutambua mambo yanayobishaniwa dhidi ya mambo ambayo hayabishawini, kwa sababu kadhaa kesi hiyo ikahirishwa na kupangiwa tarehe nyingine.

Suala lilipomalizika, nikaendelea na majukumu yangu mengine, wakati wateja wangu wanatoka wakiwa ndani ya korido za Mahakama, akajitokeza Askari akajitambulisha na kumuweka chini ya ulinzi Malisa akisema anatuhuma zinazomkabili Mkoani Kilimanjaro na hivyo anatakiwa kuondoka naye.

Alalamika Malisa kukamatwa korido za Mahakamani
Kitendo hicho cha kukamatwa katika korido za Mahakama ni kitu cha kusikitisha, nakumbuka Tundu Lissu alishawahi kukamatwa katika korodo za Mahakama kama hivyo.

Nakumbuka pia kuna muongozo ulitolewa kuwa watu hawatakiwi kukaatwa kwenye korodo ili kuheshimu Mahakama, kaa kuna ulazima wa kuwekwa chini ya ulinzi basi wafanye hivyo nje ya Mahakama kwa maana ya kuheshimu eneo hilo la Mahakama.

Nilipoitwa na kujiridhisha kuwa waliomuweka chini ya ulinzi Malisa ni Askari nikaruhusu aende nao, wakati huohuo Wakili Hekima Mwasipu naye akaanza safari ya kwenda Moshi kwa kuwa walitueleza wanapoelekea.

Hakukuwa na haja ya wao kumfuata Mahakamani, kwani wanajua kabisa lazima aende Mahakamani na wangeweza kumpigia simu aende au kumjulisha mapema.

Malisa kuhojiwa
Usiku huo kuamkia leo (Juni 7, 2024), Malisa amehojiwa chini ya Wakili Hekima Mwasipu, baada ya hapo baadaye mchana akahojiwa tena mara ya pili.

Mahojiano ya mara ya kwanza yanahusu suala lake linalohusu anayedaiwa kuwa ni Mtumishi wa Profesa Adolf Mkenda (Waziri wa Elimu), mara ya pili akahojiwa kuhusu suala linalomhusu Mwalimu anayedaiwa alimuadhibu mtoto hadi akapoteza maisha.

Kuhojiwa mara ya tatu
Kuhusu dhamana hajapewa kwa maelezo kuwa kuna Maafisa wengine wa Usalama wanatarajia kuwasili leo kutoka Makao Makuu, tumeelezwa wanatarajiwa kumuhoji kuhusu suala lingine ambalo hatujaelezwa kuwa linahusu nini.

Pamoja na uwepo wa Wakili Mwasipu pia kuna Wakili mwingine ambaye naye anashiriki kumsimamia Malisa, anaitwa Shecky Mfinanga kutoka Arusha, pia kuna Wakili mwingine wa palepale Moshi.

Afya ya Malisa
Kuhusu afya ya Malisa ipo salama, anaendelea vizuri na mwenyewe anasema tuhuma hizo zimehamishiwa Moshi eneo ambalo anatarajiwa kuwania ubunge.
 
Wakili Peter Patience Kibatala amezungumzia suala linalohusu Godlisten Malisa kwa kuchambua kinachoendelea tangu alipokamatwa akiwa Mahakamani Dar es Salaam kisha kusafirishwa hadi Mkoani Kilimanjaro.

Anaelezea alivyokamatwa
Jana (Juni 7, 2024) nikiwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu pamoja na Wakili Hekima Mwasipu tulikuwa katika majukumu ya kusimamia kesi inayowahusu Godlisten Malisa na Boniface Jacob kuhusiana na maandishi fulani yanayowahusu.

Mchakato uliokuwa unafanyika ni “Usikilizaji wa Awali Mahakamani” kwa lengo la kutambua mambo yanayobishaniwa dhidi ya mambo ambayo hayabishawini, kwa sababu kadhaa kesi hiyo ikahirishwa na kupangiwa tarehe nyingine.

Suala lilipomalizika, nikaendelea na majukumu yangu mengine, wakati wateja wangu wanatoka wakiwa ndani ya korido za Mahakama, akajitokeza Askari akajitambulisha na kumuweka chini ya ulinzi Malisa akisema anatuhuma zinazomkabili Mkoani Kilimanjaro na hivyo anatakiwa kuondoka naye.

Alalamika Malisa kukamatwa korido za Mahakamani
Kitendo hicho cha kukamatwa katika korido za Mahakama ni kitu cha kusikitisha, nakumbuka Tundu Lissu alishawahi kukamatwa katika korodo za Mahakama kama hivyo.

Nakumbuka pia kuna muongozo ulitolewa kuwa watu hawatakiwi kukaatwa kwenye korodo ili kuheshimu Mahakama, kaa kuna ulazima wa kuwekwa chini ya ulinzi basi wafanye hivyo nje ya Mahakama kwa maana ya kuheshimu eneo hilo la Mahakama.

Nilipoitwa na kujiridhisha kuwa waliomuweka chini ya ulinzi Malisa ni Askari nikaruhusu aende nao, wakati huohuo Wakili Hekima Mwasipu naye akaanza safari ya kwenda Moshi kwa kuwa walitueleza wanapoelekea.

Hakukuwa na haja ya wao kumfuata Mahakamani, kwani wanajua kabisa lazima aende Mahakamani na wangeweza kumpigia simu aende au kumjulisha mapema.

Malisa kuhojiwa
Usiku huo kuamkia leo (Juni 7, 2024), Malisa amehojiwa chini ya Wakili Hekima Mwasipu, baada ya hapo baadaye mchana akahojiwa tena mara ya pili.

Mahojiano ya mara ya kwanza yanahusu suala lake linalohusu anayedaiwa kuwa ni Mtumishi wa Profesa Adolf Mkenda (Waziri wa Elimu), mara ya pili akahojiwa kuhusu suala linalomhusu Mwalimu anayedaiwa alimuadhibu mtoto hadi akapoteza maisha.

Kuhojiwa mara ya tatu
Kuhusu dhamana hajapewa kwa maelezo kuwa kuna Maafisa wengine wa Usalama wanatarajia kuwasili leo kutoka Makao Makuu, tumeelezwa wanatarajiwa kumuhoji kuhusu suala lingine ambalo hatujaelezwa kuwa linahusu nini.

Pamoja na uwepo wa Wakili Mwasipu pia kuna Wakili mwingine ambaye naye anashiriki kumsimamia Malisa, anaitwa Shecky Mfinanga kutoka Arusha, pia kuna Wakili mwingine wa palepale Moshi.

Afya ya Malisa
Kuhusu afya ya Malisa ipo salama, anaendelea vizuri na mwenyewe anasema tuhuma hizo zimehamishiwa Moshi eneo ambalo anatarajiwa kuwania ubunge.
Tusubiri tuone itakavyokuwa
 
Huyu dogo inabidi akue kwanza...
 
Huyu dogo inabidi akue kwanza...
Kweli kabisa, anafanya siasa za kitoto, mimi nilimdharau alipokuwa anamuita Nape "bumunda", Nape hajawahi kutoa kauli mbaya kwake, hajamdharau Malisa.

Ila nilijufunza kwamba, kuna uzi mwembamba sana unaotenganisha Malisa halisi, na Malisa ambaye anatumia akili kufikiri, muda wowote anateleza na anaenda kwenye uhalisia wake na kuanza kutoa lugha za kebehi na dharau wakati angeweza kufanya siasa za kisomi
 
Na huko KCMC wasimuachie, alalemo, akitoka jumatatu kwa pilato, analalamo tena Karanga
 
Kuna haja ya ku review mitaala ya chuo Cha CCP na sifa za kuajiri hawa watu pia maana wanaliaibisha taifa mwishowe hiyo kazi itaonekana ni ya vilaza na watu wasiojielewa
Tatizo sio mitaala ya CCP, tatizo ni muundo wa service. Lazima itoke from police force to police service. Muundo wa sasa hata kwa sheria zake ni rahis sana wana siasa ku temper nao, kuwafanya wafanye lolote. Ukiangalia developed country mwanasiasa hana access ya kutemper na police, police ni independent na wanasimamiwa na department maalum

Lakin pia hatuna chombo kinachofuatilia makosa ya police, kama DCI ya kenya, although hawa wana investigate kesi kubwa kubwa, lakini wana uhuru mpaka wa kuchunguza police members haijalish ranks zao. Hiki chombo kina wa keep in check

Hili suala la police kujochunguza wenyewe halaf hawaleti majibu lina ukakasi
 
Malisa anaweza kuozea jela, hizo kesi mbaya sana, mbaya mno, na hivi ana sura laini kama keki ya bezdei
we kijambio mwenye sura ya kijambio.ccm mzuri unajua malisa ni msaada mkubwa wa wagonjwa hapa au unaishia kwenye ujinga
 
Back
Top Bottom