A
Anonymous
Guest
Eneo Mbutu limekuwa sehemu kuu ya kuchimbwa vifusi kwa ajili ya ujenzi mbalimbali.
Hatari kuu kwa watumiaji wa barabara ni haya malori kujaza vifusi kupita kiasi kinachotakiwa na hakuna hatua inayochukuliwa na mamlaka husika.
Moja ya madhara ambayo yamekuwa yakitokea ni kumwagika kwa vifusi barabarani hali ambayo inahatarisha usalama kwa watumiaji wengine wa barabara.
Askari wa usalama barabarani tunawaona wapo ila hawachukui hatua za kukomesha hii hali.
Ukichanganya na ubovu wa barabara kwa sasa tunaomba mamlaka husika ikiwemo TARURA, TANROAD na vikosi vya usalama barabarani kiuchukua hatua haraka kabla madhara zaidi hayajatokea
Hatari kuu kwa watumiaji wa barabara ni haya malori kujaza vifusi kupita kiasi kinachotakiwa na hakuna hatua inayochukuliwa na mamlaka husika.
Moja ya madhara ambayo yamekuwa yakitokea ni kumwagika kwa vifusi barabarani hali ambayo inahatarisha usalama kwa watumiaji wengine wa barabara.
Askari wa usalama barabarani tunawaona wapo ila hawachukui hatua za kukomesha hii hali.
Ukichanganya na ubovu wa barabara kwa sasa tunaomba mamlaka husika ikiwemo TARURA, TANROAD na vikosi vya usalama barabarani kiuchukua hatua haraka kabla madhara zaidi hayajatokea