Malumbano ya Hoja ITV: Mfumo wa Muungano wa Serekali tatu

Malumbano ya Hoja ITV: Mfumo wa Muungano wa Serekali tatu

lumumba wamejaza mamluki buku 7 wote wanamtukana warioba kweli njaa mbaya sana washiriki wa leo wote ------------ nimeamua kuzima tv nilale tu

Nakushauri uvunje tv ndugu yangu.
 
Kuna mzee hapo sijui Likwepa au Likweka atajua mwenyewe anaongea kama yuko kwenye Sports starehe!!!!
 
Hata huyu mhadhiri wa chuo kikuu cha bagamoyo anaongea pumba hawa ni ccm hata kibanda mimi sijamuelewa kabisa yuko wp? Leo ccm wamejaa itv wamekinunua kipindi kazi kweli kweli
 
Naangalia ITV Kipindi ni Live.Wanajadiliana juu Muungano wa Serikali.

Nadhani wachangiaji wa maada husika iwe kwa makusudi ama kwa kutokuelewa wameamua kuonyesha umbumbu juu ya masuala ya Muungano.

kwa ujumla waliohudhuria asilimia kubwa ni waoga na wamechanganyikana na wana CCM na waliotumwa na CCM KUSEMA YALE WALIOYASEMA ITV.

Ikiwa tunajua wazi kuwa Wakati Muungano unaanzishwa kulikuwa na pande mbili yaani Nchi ya Tanganyika na Nchi ya Zanzibar ili kupata Tanzania yenye Muungano wa serikali mbili inakuwaje leo Tuisahau na kuitupilia mbali Nchi ya Tanganyika kana kwamba haijawahi kuwepo???

Hapa tulipofikia tayari Zanzibar imepewa mamlaka kamili wana Bendera yao,Wimbo wao wa Taifa,Rais wao,Jeshi lao na Katiba Yao.

Kwanini Kuinyima haki stahili Nchi ya Tanganyika kwa hofu za kupandikizia kwa makusudi?

Njia mbadala iliyopo ili kuimarisha Muungano iliyobakia ni Kuirejesha Tanganyika na Tanganyika ikirejea Lazima pawepo na Muungano wa Serikali tatu.Zaidi ya hapo matatizo ya Muungano hayata koma daima na hayana suluhu maana bado yatakuwa na mapungufu mengi yenye kuibua hisia na mitazamo yenye kuleta dharau ama kutoheshimiana kwa pande zote mbili.

Kamwe Muungano huwezi kuvunjika kwa sababu ya kuwepo kwa Serikali Tatu.

CCM acheni hofu za kuondolewa madarakani,ni vema mkajiamini hata katika mabadiliko yoyote,Acheni kupandikiza chuki,hofu na Migawanyiko ili Kubakia Muungano wa serikali mbili kwa Lengo la CCM Kubakia Madarakani.
 
mimi naona ccm wamechanganyikiwa,nimesikitika kuona viti vyote vimejaa maccm,wakiongea pumba tupu na kumkebei warioba,nimeshangaa sana kumsikia,deosi kibamba,nikajiuliza huyu nae,ni kinyonga???? wote wameacha kujadili hoja wana,mjadili mtu ambae ni warioba,
 
Kwa mara ya kwanza nimekichukia kipindi,lumumba wameletwa na malori? Kitufe cha like kimerudi,nigongeeni basi

Kuna MPUUZI mmoja,kadai Jaji Warioba,lengo lake ni kumuangusha Kikwete. Na hakuwa akimuunga mkono,kwani alikuwa na mtu wake!
 
mimi naona ccm wamechanganyikiwa,nimesikitika kuona viti vyote vimejaa maccm,wakiongea pumba tupu na kumkebei warioba,nimeshangaa sana kumsikia,deosi kibamba,nikajiuliza huyu nae,ni kinyonga???? wote wameacha kujadili hoja wana,mjadili mtu ambae ni warioba,

well said
 
Leo itv mmefanya kitu ambacho ni kibaya sana kwa sababu mnawajua wachangiaji wazuri na wenye uwelewa mkubwa kwa nini amkupendekeza majina yao ili leo wawepo?
matokeo yake mmewachagua wana ccm wa lumumba pekee na wengine wamewatia aibu sana kwa sababu wameshindwa kujitetea na kuitetea hoja.
 
Wachangiaji wenyewe hawasomi, walikuwa wanaongea pumba tu
 
Deaus kibamba anasema rasim zote mbili hazizungumzii rasilimali za taifa

Taratibu kweli inadhihiri. Kumbe ana kinyongo cha kukosa kuchaguliwa kwenye tume. Ameanza kuhisabu hela walizopewa makamishina.
 
Deaus kibamba anasema rasim zote mbili hazizungumzii rasilimali za taifa

ktk siku ambazo kibamba amechemsha nadhan ni leo, sio yule niliyemzoea akiongea kitu kweli unakubali, leo ziro
 
Naomba kufahamishwa leo ITV wametumia kigezo gani kuchagua wachangiaji wa kipindi au ndio kampeni zimeanza?

Nafikiri ni kadi ya CCM, na hata Kibanda nae ni wakala leo. Eti leo rasimu haina maana yoyote!
 
well said

hivi kweli ccm ndio mmeamua kuwatuma vijana wenu kumtukana warioba na tume yake. itv watuambie imekuwaje chumba leo kimejaa watu wanaopinga serikali tatu bila kuhusisha upande wa wale wanaounga mkono. Je ccm ndio walioondaa hiyo topic na kujichagua wenyewe kuja kuichangia wenyewe? mtajadilije muungano bila kuhusisha upande wa zanzibar? ITV leo mmetia aibu.
 
kama kweli ccm wanataka kuimarisha muungano wa tanzania....kwa nini wasidai tuwe na serikali moja tuuu badala ya tatu???

​Serikali hiyo iitwe serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
 
dah naona jamaa walijipanga mapema kwenda kuvamia kipindi maana haiwezekani wote wakawa wanamshambulia warioba kwa kuleta wazo la serikali tatu. yaani ni aibu ukisikiliza maana jamaa wanaonekana wamepanga cha kuongea kabisa

Lakini hawajaongea kitu kwani hawana data wala facts zozote, hawana hata solutions za matatizo ya huo muundo wao.
 
Wamejaa vijana wa lumumba wanazungumza upuuzi na wengine awana uwezo wa kuzungumza

jamani km kuna mtu anaweza kuweka hapa jamvini clip ya hiki kipindi ili watu wawasikie hawa watu wa lumumba walivyokuwa wanachangia pasi kuwa na hoja kiasi cha mtu mmoja kuwashinda kwa HOJA, nimeamini ''UKWELI mdogo unagaragaza UONGO mwingi''
 
Back
Top Bottom