Malumbano ya Hoja ITV: Mfumo wa Muungano wa Serekali tatu

Malumbano ya Hoja ITV: Mfumo wa Muungano wa Serekali tatu

Hata huyu mhadhiri wa chuo kikuu cha bagamoyo anaongea pumba hawa ni ccm hata kibanda mimi sijamuelewa kabisa yuko wp? Leo ccm wamejaa itv wamekinunua kipindi kazi kweli kweli

Nimejiuliza the same na kama mwalimu wa chuo kikuu ni yule mwanangu simpeleki Bagamoyo kwenda kujazwa pumba. Hata kupanga mtiririko wa mawazo hana. Kibanda yy anaumwa na pesa kwa makamishina.
 
hivi kweli ccm ndio mmeamua kuwatuma vijana wenu kumtukana warioba na tume yake. itv watuambie imekuwaje chumba leo kimejaa watu wanaopinga serikali tatu bila kuhusisha upande wa wale wanaounga mkono. Je ccm ndio walioondaa hiyo topic na kujichagua wenyewe kuja kuichangia wenyewe? mtajadilije muungano bila kuhusisha upande wa zanzibar? ITV leo mmetia aibu.

ITV ndio zao hizo kulishiza maswali na kupanga watu wa kujibu.
 
Naona leo wameamua kukusanyana wanaCCM wanaopinga serikali tatu ila kuna jamaa mmoja anasupport serikali tatu (nadhani yuko peke yake) kawagonga kwa data safi sana hata sijui kama watamjibu!!!!

Nimemuona,ni kamishna wa tume ya mabadiiko ya katiba.Jamaa anafafanua mambo vizuri sana.ila leo hawa wachangiaji kama wameandaliwa kwenda kupinga serikali tatu na kumshambulia mzee Warioba.
 
wengine wanasema serikali tatu nikubaguana. sijui nani anambagua nani. hakuna yeyote anayeongelea habari ya zanzibar na madai yao ya mamlaka kamili. wamebaki kumtukana warioba na tume. ila huyu Bw. Pole pole ni kichwa kweli kweli. anaweka data mezani mburuls wa ccm wao ni personal attacks tu.
Kibamba naye haeleweki leo anaipinga rasim jumla. what a u turn! ni mihemko tu hakuna kitu.
 
Wachangiaji karibia wote leo naona walikuwa wamemeza chura rushwa kwa maccm.
 
Kichwa kama cha MSALANI,SIMIYU YETU,LUSUNGO,LUKOSI NA SAMPLE Zingine kama hizo ndiyo unategemea waelewe kweli,Yaani magamba kichwani yamejaa madudu.

Nimempenda sana Humphrey Polepole.Katika mkusanyiko ule nampa maksi nyingi sana.Kwanza anaelewa vizuri sana anachozungumza.Na kwa kweli kawaacha mabali sana kwa kufikiri.Anatumia hoja kujibu hoja.
Mtazame mtu kama,
Monday Likwepa: Hana hoja zaidi ya kumtukana Warioba.Anamjadili Warioba badala ya maoni ya tume.
Godwin Kunambi:Huyu naye ni mwanasheria wa CCM lakini hana kitu kichwani.Hana hoja ya msingi aliyojadili badala ya kutoa povu.
Simon Simalenga:Mwigizaji huyu aliyepewa cheo Clouds Media naye hana uelewa wa masuala ya kijamii.Eti takwimu zile ni chache sana, watanzania hawakuulizwa.Data hizo ni zao kina Warioba.Ina sikitisha sana wachangiaji wa jana waliharibu sana. Simalenga alisema eti watanganyika hawapo kwa hiyo hakuna aliyeulizwa swali hilo.Lakini upande wa pili anasema Wazanzibari na Watanzania bara hawakusema wanataka serikali tatu.Hajui kuwa kafanya tautology.Huwezi kuwa na watanzania halafu humo ndani umewatoa wazanzibari.

Ukweli halisi ni kuwa wenye maslahi tu na mfumo uliopo wanashabika serikali mbili.WEngine walisema eti wazanzibari hawataki serikali tatu.Ni sawa wakisema hivyo kwani wao wana serikali yao.Sisi ndio tunaopaswa kuidai serikali yetu.Tulikubali vipi kuifuta na kutumia jina la Tanzania?Maoni yao ya jana yalikuwa hovyo kabisa na wengi pale waliitwa kichama zaidi. Mchungaji Alphonce naye ni mnafiki sana.Lazima ana agenda ya siri. Kweli haoni matatizo ya Muungano huu?Viongozi wa dini wenye unafiki lazima walaaniwe.
Deus Kibamba nilimwona kama mtu mwenye chuki na tume ya Warioba.Kuna jambo limejificha.Anasema tume haikutembea kila kata na kila kijiji.Hivi kazi hii angepewa yeye angepita kote huko? Tume ngapi zimewahi kuzunguka kila kijiji cha nchi hii?Hata tume ya Jaji Nyalali haikupita kila kijiji.Tujiulize mbona tuna Rais wa nchi lakini hadi anamaliza miaka 10 madarakani hatembelei kila kata ya wilaya?Sembuse tume iliyokuwa inakimbizana na muda?

Mwingine naye akasema eti wao walipewa kazi ya kukusanya maoni tu na kuyapeleka kwa Rais na tume ikafanya kazi ya kuchambua.Hivi ni kweli kuwa Tume ingeleta kila maoni kama yalivyo huyu Kikwete angeweza kweli kuyapitia yote?Ikiwa miswaada tu mingine anasaini bila kuisoma kikamilifu.Kitabu cha biblia pia kimesema na mchungaji Alphonce anajua kuwa si kila alilofanya Yesu limeandikwa kwenye biblia ingekuwa hivyo ulimwengu usingetosha kwa wingi wa vitabu.Tujadili hoja na si kumtukana Warioba.
 
hivi kweli ccm ndio mmeamua kuwatuma vijana wenu kumtukana warioba na tume yake. itv watuambie imekuwaje chumba leo kimejaa watu wanaopinga serikali tatu bila kuhusisha upande wa wale wanaounga mkono. Je ccm ndio walioondaa hiyo topic na kujichagua wenyewe kuja kuichangia wenyewe? mtajadilije muungano bila kuhusisha upande wa zanzibar? ITV leo mmetia aibu.

Mkuu Mcfm40 mimi cpo huko.....nilikuwa nasupport mleta mada kuwa Magambaz wamesponsor show!
 
Back
Top Bottom