EINSTEIN112
JF-Expert Member
- Oct 26, 2018
- 21,711
- 35,644
Winnie Achieng (33) amefariki dunia baada ya gari alilokuwa akiendesha kutumbukia katika bahari ya Hindi mjini Mombasa, Kenya huku mwanaye wa miaka 12 akiogelea hadi ufukweni.
Taarifa iliyotolewa na jeshi la polisi inaeleza kuwa Winnie alifariki wakati akipatiwa matibabu hospitali muda mfupi baada ya kuokolewa.
Inaeleza kuwa alikuwa akiendesha gari aina ya Toyota Vitz akitokea eneo la Changamwe kwenda mjini Mombasa akiwa na mwanaye wa kiume mwenye umri wa miaka 12 ambaye alifanikiwa kuogelea na kutoka ndani ya maji.
“Mtoto alifanikiwa kuogelea kabla maji hayajamzidi nguvu lakini mama yake alishindwa kutoka ndani ya gari kutokana na mkanda kumbana hadi pale alipokuja kuokolewa na wasamaria wema huku akiwa ameshakunywa maji mengi.”
“Baada ya kufanikiwa kujiokoa kutoka kwenye maji mtoto alikuwa na majeraha kadhaa
katika mwili wake ambayo alitibiwa hospitalini kabla kuondoka na baba yake kwenda nyumbani,” inaeleza taarifa hiyo.
Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo, Omar Chigamba, amesema kuwa aliona gari hilo likiendeshwa kwa kasi kabla ya kuingia baharini na alikimbia kwenda kuwaokoa waliokuwa kwenye gari lakini alimkuta mama huyo akiwa katika hali mbaya.
Chanzo: Mwananchi
Taarifa iliyotolewa na jeshi la polisi inaeleza kuwa Winnie alifariki wakati akipatiwa matibabu hospitali muda mfupi baada ya kuokolewa.
Inaeleza kuwa alikuwa akiendesha gari aina ya Toyota Vitz akitokea eneo la Changamwe kwenda mjini Mombasa akiwa na mwanaye wa kiume mwenye umri wa miaka 12 ambaye alifanikiwa kuogelea na kutoka ndani ya maji.
“Mtoto alifanikiwa kuogelea kabla maji hayajamzidi nguvu lakini mama yake alishindwa kutoka ndani ya gari kutokana na mkanda kumbana hadi pale alipokuja kuokolewa na wasamaria wema huku akiwa ameshakunywa maji mengi.”
“Baada ya kufanikiwa kujiokoa kutoka kwenye maji mtoto alikuwa na majeraha kadhaa
katika mwili wake ambayo alitibiwa hospitalini kabla kuondoka na baba yake kwenda nyumbani,” inaeleza taarifa hiyo.
Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo, Omar Chigamba, amesema kuwa aliona gari hilo likiendeshwa kwa kasi kabla ya kuingia baharini na alikimbia kwenda kuwaokoa waliokuwa kwenye gari lakini alimkuta mama huyo akiwa katika hali mbaya.
Chanzo: Mwananchi