Mama jirani yangu anamfungia ndani mwanaye mwenye ulemavu

Mama jirani yangu anamfungia ndani mwanaye mwenye ulemavu

Fanya mkuu. Mungu atakulipa kwa njia nyingine. Hakuna binadamu anayepaswa kukaa ndani muda wote. Hata kama ni mlemavu ana haki ya kucheza na watoto wengine. Kuna cases nyingi zimeshatokea na watoto walipokuja kugundulika baadae walikuwa wamegeuka na kuwa kama misukule kwa kukaa ndani. Nakumbuka kuona kisa kama hiki. Mtoto alilkuwa anasikika kulia ndani na siku majirani walipovamia wakakuta mtoto amefungwa mnyororo kama mbwa na huwezi kujua tena kama ni binadamu.
Natamani kufanya je atanichukuliaje anaweza kuniroga
 
Kosa liko wapi kama ana umri chini ya miaka mitano hakuna kosa mkuu.kosa ni kutompeleka shule kama ana unri wa kuanza shule
Vp kuhusu kutoliona jua mkuu kwa muda huo wote maana jamaa kapanga hapo hajawah kumuona iwe mchana au usiku

Bado analokosa mtoto anahaki ya kucheza na wenzake pia
 
Vp kuhusu kutoliona jua mkuu kwa muda huo wote maana jamaa kapanga hapo hajawah kumuona iwe mchana au usiku

Bado analokosa mtoto anahaki ya kucheza na wenzake pia
Haki ya kucheza kweli ipo ila haki ya kuliona jua ndio naisikia leo,akifika umri wa kwenda shule atacheza na kuliona jua,huenda changamoto yake kwa umri wake ni hatari kuwa nje
 
Haki ya kucheza kweli ipo ila haki ya kuliona jua ndio naisikia leo,akifika umri wa kwenda shule atacheza na kuliona jua,huenda changamoto yake kwa umri wake ni hatari kuwa nje
Mkuu walau hata kwa siku mtoto apate hewa ya nje hata kwa nusu saa inatosha kumbuka wamepanga chumba kimoja familia yote maana yake vyombo nguo vyote viko humo na ikiwezekana mtoto anajisaidia humo unadhan humo ndan kutakuwa na harufu nzur kwel

Binafs naona atapata na maradh mengne Zaid licha ya ulemavu wake
 
Ni huruma kwa kweli. Ukizaa mtoto mzima ni jambo la kumshukuru sana Mungu. Kuzaa mtot mlemavu na kuikubali hali ni jambo zito kwa baadhi ya wazazi ila kwa wanaokubali na kuwapenda huwatunza vzr na baadae huja kuwa watu wenye maisha mazuri tuu. Labda ungeenda ustawi waje wazungumze nae.
 
Mkuu walau hata kwa siku mtoto apate hewa ya nje hata kwa nusu saa inatosha kumbuka wamepanga chumba kimoja familia yote maana yake vyombo nguo vyote viko humo na ikiwezekana mtoto anajisaidia humo unadhan humo ndan kutakuwa na harufu nzur kwel

Binafs naona atapata na maradh mengne Zaid licha ya ulemavu wake
Kama ni chumba kimoja ni kosa kwa kweli nilidhani ni nyumba kubwa inajitosheleza
 
Haki ya kucheza kweli ipo ila haki ya kuliona jua ndio naisikia leo,akifika umri wa kwenda shule atacheza na kuliona jua,huenda changamoto yake kwa umri wake ni hatari kuwa nje
Kwahyo mkuu hilo la kupata mwanga wa jua huoni kama lina umuhimu?
 
Kwahyo mkuu hilo la kupata mwanga wa jua huoni kama lina umuhimu?
Unaishi upanga au kisutu kwenye apartment ghorofa ya kumi na mbili ,jua utalionea wapi, Ni mfano tu.ila nimeona huyu mama ana room moja hapo ni shida fresh air ni muhimu
 
Natamani kufanya je atanichukuliaje anaweza kuniroga
Weka hapa JF.
Jina la mkoa:
Jina la kata:
Jina la mtaa:
Maelekezo ya jinsi ya kufika kwa urahisi kwa huyo mama kutokea sehemu maarufu mtaani (eg shule/kanisa/hospitali).
Jina (maarufu) la huyo mama. Eg mama Jaki.
Jina na mawasiliano ya balozi wa nyumba kumi au kiongozi yoyote wa mtaa.
Hapo utakua umemaliza kazi yako, wahusika watamfikia kwa uzuri tu.
FK21
 
Sawa mkuu nitafanya ivyo jambo ambalo sio zuri majirani wakimshauri mtoe acheze na wenzake hataki
Nenda kituo Cha polisi,uliza Dawati la jinsia watakupa ushilikiani wa kutosha.

Tena usichelewe.
 
Kosa liko wapi kama ana umri chini ya miaka mitano hakuna kosa mkuu.kosa ni kutompeleka shule kama ana unri wa kuanza shule
Una maana mtoto mwenye umri chini ya mika mitano haruhusiwi kutoka nje? I mean inatakiwa afungiwe ndani tu? I dont think so! Kwa nini wazazi/mzazi asitoke hata kwa matembezi mafupi? Anapokwenda kwa majirani au dukani kwa nini asiende naye ili na yeye a-enjoy mandhari ya nje na kuona ulimwengu ulivyo?
 
Una maana mtoto mwenye umri chini ya mika mitano haruhusiwi kutoka nje? I mean inatakiwa afungiwe ndani tu? I dont think so! Kwa nini wazazi/mzazi asitoke hata kwa matembezi mafupi? Anapokwenda kwa majirani au dukani kwa nini asiende naye ili na yeye a-enjoy mandhari ya nje na kuona ulimwengu ulivyo?
Hakuna hiyo sheria ni uamuzi wa mzazi,kuna watoto kule kitumbini na kusutu hawajawahi kuona mbuzi au ng'ombe,wako ghorofani tu muda wote
 
Vp kuhusu kutoliona jua mkuu kwa muda huo wote maana jamaa kapanga hapo hajawah kumuona iwe mchana au usiku

Bado analokosa mtoto anahaki ya kucheza na wenzake pia
Anatengwa anafungiwa humo mama anaenda mizunguko kiufupi uyo mama anasubiri mtoto afe tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Weka hapa JF.
Jina la mkoa:
Jina la kata:
Jina la mtaa:
Maelekezo ya jinsi ya kufika kwa urahisi kwa huyo mama kutokea sehemu maarufu mtaani (eg shule/kanisa/hospitali).
Jina (maarufu) la huyo mama. Eg mama Jaki.
Jina na mawasiliano ya balozi wa nyumba kumi au kiongozi yoyote wa mtaa.
Hapo utakua umemaliza kazi yako, wahusika watamfikia kwa uzuri tu.
FK21
Nahofia akijua nmemchoma

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Anatengwa anafungiwa humo mama anaenda mizunguko kiufupi uyo mama anasubiri mtoto afe tu

Sent using Jamii Forums mobile app
Weka hapa JF.
Jina la mkoa:
Jina la kata:
Jina la mtaa:
Maelekezo ya jinsi ya kufika kwa urahisi kwa huyo mama kutokea sehemu maarufu mtaani (eg shule/kanisa/hospitali).
Jina (maarufu) la huyo mama. Eg mama Jaki.
Jina na mawasiliano ya balozi wa nyumba kumi au kiongozi yoyote wa mtaa.
Hapo utakua umemaliza kazi yako, wahusika watamfikia kwa uzuri tu.
FK21
 
Jua ni vitamin D.... Hata wafungwa hupewa at least an hour kuwa nje(ndani ya eneo la jela) kupata vitamin na kunyoosha viungo! Sembuse huyo mtoto!
 
Ni katika nyumba ya kupanga moja hapa mjini Dar.

Kuna mama ana watoto wawili mmoja wa kike mzima mmoja ni uyo mlemavu nae ni wa kike anamfungia mwanae ndani kisa hawezi kutembea ni mwaka sasa mtoto hajaliona jua zaidi ya kusikika akilia tu.

Je, hii ni sahihi huwa naumia sana nikisikia sauti ya huyo mtoto akilia ndani.

Nawashilikisha wana Jamiforums wenzangu muweze kuona changamoto wanazopitia walemavu.
Wewe jamaa isije ikawa tunakaa mtaa mmoja maana namimi kwangu kuna hiyo shida mzee.hadi naogopa
 
Back
Top Bottom