Mama kapata mafao, afanye biashara gani?

Sinto shangaa vijana wenye adabu ndogo wakikuomba namba ya bimkubwa...teh[emoji28]
 
Akili ishachoka kuna mtu ametoa wazo zuri kama anaeneo na mafao mazuri bora ajenge tu mana akili yake ilishaisha ofisi akisema apambane na biashara stress atakufa mapema bure ujana wake alikuwa wp mshauri ale hela yake taratibu
 
biashara itakayo mfaa kwa umri wake afungue duka vyombo ikae kama part time tu uku akianza kujenga nyumba ili apangashine ila hizo biashara ya usafiri ni pasua kichwa iwe pikipiki au gari asisubutu
 
Atafute location nzuri ya watu afungue duka la makolokolo yaan mahitaji ya kila siku. Au kama hapo mtaani watu wanaonunua mtaani ni wengi aweke duka. Dukani aweke huduma za kifedha kama M-Pesa, TigoPesa n.k
 
Atafute sehemu nzuri penye watu na eneo lenye hatimiliki na vipimo vya ardhi vinavyotambulika, alafu anunue hilo eneo ajenge nyumba either ya kupangisha kwa mtu mmoja mmoja au ajenge guest house. Pesa itayobaki atulie tu atumie kwa matumizi yake binafsi, amshukuru mungu kumpa uhai mrefu. Msimshauri afanye biashara huu ni muda wake wa kupumzika.
 
Mkuu anasema anaona usumbufu wa kusimamia ujenzi
 
ni nini maana ya kuita JF ni jukwaa la GREAT THINKERS mkuu? mtendee haki muomba ushauri, hayo mengine baki nayo mwenyewe.....
 
watoto wake hamuwezi kumsaidia kusimamia ujenzi?

kama ujenzi hataki aweke fixed deposit 90% ya mafao awe anakula riba tu
Anaweza pia kupata ushauri kwa wajuzi wa mambo ya dhamana za Serikali kwani nimeliona tangazo kwenye social media likinadi juu ya mambo ya dhamana za serikali Benki Kuu.
 
Mshauri Mama ajenge nyumba za kupanga Dodoma
dom sahvi nyumba zinshuka thaman watumish walishahamia wote wameenea
Nyumba sahv zinashushwa bei ili waliojenga mpya nao wawavutie wateja (ni bora kupata mpangaj wa lak1 kulko kukosa kabsa) we kama umejoanga kupga hela dom sahau nakushauri bora ujenge dar
 
Hakuna mstaafu aliyetajirika kwa kuwekeza pension. Hiyo hela mwambie ale pole pole asogeze miaka mingine mitano ya maisha yake. Asisahau kununua ka Vitz ili naye atembee akiwa amekaa.
 
Ajenge nyumbani zingine apangishe aachane na biashara ya pikipiki, hiyo ni biashara kichaa vijana ni wahuni sana.
Kiufupi mafao ya kustaafu sio ya kuanzisha biashara au hata kusomesha watoto /ujenzi Wa nyumba ya kuishi sasa kwa vile alishaanza kuwa na wanafunzi wapangaji ni bora kuimarisha na kujiwekea akiba apate matumizi na matibabu yake
 
Mkuu anasema anaona usumbufu wa kusimamia ujenzi
Duuuh anataka anunue pikipiki maana amna usumbufu wa kununua vile ana hela ni sawa pia boss maana mambo yasiwe mengi na mengi yasiwe mambo
 
Kiufupi mafao ya kustaafu sio ya kuanzisha biashara au hata kusomesha watoto /ujenzi Wa nyumba ya kuishi sasa kwa vile alishaanza kuwa na wanafunzi wapangaji ni bora kuimarisha na kujiwekea akiba apate matumizi na matibabu yake
Kwahiyo unataka aweke chini ya mto awe anajichukulia kidogo kidogo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…