Mama kapata mafao, afanye biashara gani?

Genta
 
Kweli kuanza biashara mpya uzeeni sio tombola la uhakika. Uwezekano wa kuua mtaji kabisa ni mkubwa sana.

Kuna wadau wametoa wazo la fixed deposit. Badala ya fixed deposit anaweza kuwekeza kwenye mojawapo ya mifuko ya UTT (hasa Jikimu, Ukwasi) ambapo atakula faida yake 9-10% polepole huku mtaji ukibaki.
 
Especially nyumba za kupanga maeneo ya chuo au karibu na town
Mnaropoka tu karibu na town na maeneo ya chuo bila kujua thaman ya viwanja maeeneo hayo....hiyo thaman ya viwanja inaweza wagharimu mafao yao yote
 
Ndugu ngoja nikwambie ukweli bila kuficha.
Kwa umri wake biashara inayofaa ni kujenga nyumba za kupangisha tu labda na fremu mbele ya nyumba tu.
Sasa hapo inategemea na mtaji wake ni kiasi gani.
Kwa mfano Kama pesa yake ni Zaid ya milioni 50 ajenge apartments ndogo ndogo Kama nne hivi,yaani chumba sebule mara 4 na kila moja atapangisha kwa laki 1 kwa hyo kila mwezi anapokea laki 4 ita saidia sana.
Kuna biashara zingine hazimfai kwa umri wake bali zinawafaa vijana kwa sababu wakifilisika Wana nguvu za kutafuta pesa tena na kuanza upya.
 
Ushauri huu utamsaidia hata mjukuu wake. B blessed bro.
 
Mtu anaomba ushauri unatoa wosia. Mwaga ushauri mkuu
 
Kama mafao yanamtosha na anapata pension yake kila mwezi huu ni muda wa kupumzika sio kukimbizana na kupeana stress hususan na wapigaji wa kibongo...

Amefanya kazi miaka yake yote.., huu ni muda wa ku-retire, kama yupo bored afanye kitu alichokizoea ili tu asibweteke sio kuanza biashara ambayo hajawahi kuifanya maisha yake yote..., biashara nayo ina skills zake and as they say you can not teach an old dog new tricks....
 
Ajenge hostel nzr kwa ajili ya wanafunzi wa Chuo hapo iringa. I’m very sure hyo itamlipa
 
Pana nyumba Frelimo zinauzwa bei ya kawaida utaiboresha na uhakika wa wapangaji upo pia,na pia kuna nyumba zinauzwa zipo mbili kwenye uwanja mmoja m/40 zina wapangaji tayari wana lipa laki mbili kila mmoja
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…