Mama mkwe hataki niolewe na mwanaye kisa mimi ni Mchaga

Mama mkwe hataki niolewe na mwanaye kisa mimi ni Mchaga

Halafu utakuta watu weusi wanamlalamikia malkia wa uingereza kwamba ana ubaguzi dhidi ya Meghan wakati sisi huku ndo taabu
 
Ngoja kwaresma iishe, turudi kutrend.
Ni hivyo tyu sipendi kutrend huko miandaoni[emoji28][emoji28] ningemchukua gara b piaaa... kwanini uutese moyo wako kisa kabilaaa...


Halafu tunajuaga kuwaka balaa. Kama si mchagga basi nyaki beibe[emoji28][emoji28][emoji91][emoji91]

Kwaresma malizika tuunganishe familia.
 
Usibebe mimba kwani hicho siyo kigezo, huyo jamaa ana nia njema kwa dalili za awali shida yangu ni kwamba mama mkwe asipokupenda huwa ni ngumu Sana kukukubali hata umlambe mwisho ninyi wachaga huwa hamjui African chemistry sasa take care ukiolewa na huyu jamaa unaweza pigwa fenesi siyo kipapai ukajikuta kwenye shida.
Yaweza kuwa Mungu kakuonesha uhalisia wa upande wa pili kwamba they don't want you ingekuwa Mimi ningechunguza hatma ya kuolewa na huyo jamaa na ningetoka na jibu tena nikiwa confident.
 
Habari zenu wapendwa?

Mwenzenu na matatizo sielewi nichukue uamuzi gani naombeni mnishauri wapendwa, nilianza mahusiano na mkaka wa kimakuwa toka 2016 kiukweli ananipenda sana na Mimi nampenda na Mungu ametujalia mwaka Jana mwezi wa 12 kapeleka mahari kwetu akanivalisha na Pete ya uchumba.

Baada ya hapo wakualiana na wazazi harusi iwe mwezi wa 4 mwaka huu Ila baada ya muda mama yake akamwambia naomba harusi mfanye mwezi wa 7 nataka nijipange sherehe iwe kubwa tukamkubalia kupeleka hadi wa 7 Ila Cha kushangaza juzi kipindi wamekaa kwenye kikao Cha kuandaa kamati ya harusi mama mtu akasema harusi isogezwe tena iwe mwezi wa 10

Baada ya mwanae kumbana mama yake kuwa kwanini kila cku unapeleka mbele akamwambia sitaki uowe mwanamke wa kichaga ndomana nafanya hivi, kiukweli mwanae alichukia sana kuskia hiyo kauli akanipa mrejesho kuwa mama yake hataki anioe kisa mimi mchaga Ila kwakuwa nakupenda tumeshirikiana mambo mengi siwezi kukuacha tutafunga ndoa mwezi wa 8 bila hata ndugu zake kuwepo atasimamia shoo mwenyewe bila msaada wa ndugu zake nikamwitikia sawa

Ila hapa nawaza usikute huu uamuzi ameuchukua sababu ya hasira nahisi Kama akitulia atanibadilikia asikilize ndugu zake aniache na kinachoniumiza zaidi ni kwamba nimetoka naye mbali kanipotezea muda na hivi kapeleka hadi mahari kwetu watu wanasubiri harusi.

Kama akinibadilikia sijui hii aibu tutaibebaje na familia yangu, nimechanganyikiwa mpaka nawaza sijui nimbebe tu mimba ili azidi kuwa na msimamo aogope kupoteza mke na mtoto!,

Ila nakosa jibu huyu mama simuelewi kwanini ananifanyia hivi Kama alikuwa hataki niolewe na mwanae kwanini hakumzuia kipindi anapeleka mahari wakamsapoti apeleke, kinachoniumiza ni aibu kwetu mahari imeenda alafu ikitokea tukiachana kisa mama yake aibu itakuwa kubwa Bora hata angekuwa hajapeleka mahari.

Ndugu zangu naombeni ushauri wenu nifanyaje kulishinda hili jaribu lililopo mbele yangu, Ndugu zangu Bado sijawambia Kama Kuna huu mgogoro maana hata sijui watalipokeaje nachanganyikiwa Mimi jamani
Sisi wengine tuna bahati unapata mchumba unawajulisha nyumbani baba & mama wanakwambia tunakuombea mwanangu hadi mnazaa mtoto ndo wanauliza kabila gani vile mkwe wetu? Pole sana piga moyo konde
 
Sawa naona sa hivi kuna Chaggaphobia inaendelea ila yote yaliozungumzwa nimejaribu kurelate katika Familia yetu na wake ndugu zangu waliowaoa ambao kimsingi wala siyo wachaga

1.Mnyakyusa huyu aliolewa na kwa sasa ndoa ina kama miaka minne changamoto ya hyu dada alikua mkorofi na mwenye dharau sana siyo tu kwenye familia yake tofauti na tulivyodhani bali hata kwetu sisi binafsi nakumbuka nlipita kwao Arusha kipnd hicho naelekea chuo nilichoshangaa chakula kikipikwa mezani dada wa kazi alikua akila mlo tofauti na watu wengine mfano sku ya kwanza kufika ilipikwa kuku na kitimoto nkashangaa dada yeye anakula majani ya kunde nlihuzunika mno na kumpa chakula changu nlichokua nimeongeza.

2.Mgogo Huyu nae kaolewa na ndgu yangu hana muda sana kwenye ndoa hyu nlisikia taarifa kutoka kwa watu kuwa ana Choyo,Dharau na muigizaji hatar nkashangaa hadi siku nlipothibitisha baada ya siku kupita kwao nkiwa kikazi Dom baada ya kukuta kwenye chumba chao cha dharura yan Store kukiwa na Masanduku makubwa ya nguo kama wote nlipouliza kwa beki 3 mbona nguo akasema nguo ni za mama nkamuliza zinavaliwa mbona ziko hovyo?akajibu hazivaliwi tena zimetupwa tu hko nkajiuliza si bora angewapa YATIMA au watu wasojiweza
Tukio lingine na dharau alilolifanya yule shemeji yangu nkiwa bado nipo hapo najiandaa kuondoka ni pale aliponiambia "NIMUOSHEE GARI LAKE tena alilohongwa na Bro. huku akijua mm na yeye tumelingana kiumri japo kanipita mwaka bila kusahau wadhifa wangu mm ni nani mpka anambie vile nkajikuta nimeshamjibu kwa dharau huku bwana ake yan Bro akiwa pale bila kuongea chochote

3.Mkinga,shemeji yangu yeye alikua na chuki binafsi sna juu ya ndugu na baadhi hta marafiki wa ndgu yangu na pia chao kilikua ni chao tu ilifikia kipind mdogo wetu wa kike alikua akifunga shule anapitia kwao kisha kurudi home Moshi sbbu wao wanaishi Moro na dogo alikua akisoma Moro.

Sasa shida ikaja kuna siku dogo alikua akisumbuliwa na tumbo la P akawa anaomba hawezi hta kutoka chumban kwake na hvyo akamwagiza beki tatu kilichofuata yule huyo mwanamke akamwambia beki tatu amwambie aache kujilegeza matokeo yake dogo mpka akapoteza damu nyingi na kulazwa hospitalin huku uhai wake ukiwekwa rehani. Hapo bado visa vingine kama vile kusoma text za dogo kwa lazima kwenye simu zake na kumwambia bro na mimi kuwa dogo ni mhuni

4. Mjita huyu nlipewa story yake by the way alieoa alikua ni ndugu yangu mtoto wa mjomba hyu mwanamke alikua ni Bahili to the extent hata ukifika kwake hta maji ya kunywa hupati licha ya kufunguliwa mabiashara chungu nzima na mumewe lakini hela yake kubwa ilikua haijulikan inaenda wapi yan hta chumvi hawez nunua atapigiwa mme simu
Siku mtoto kaumwa kampgia mme simu hajapokea kapigia ndgu wa mme simu haijapokelewa mtoto kazidiwa mpka kashikwa na degedege matokeo mtoto kaparalyse

#YOTE HAYA YANAAKISI NINI HASA KATIKA HUU UZI NA NYUZI NYINGINEZO KUWA WANAWAKE AU WATU KUTOKA MAKABILA MENGINE WANAONEKANA THEY ARE SO PERFECT YAN HAWANA HATA CHEMBE YA UBAYA NDANI YAO ILA KWA WACHAGA NDO WAHUNI,WAKOROFI,WAUAJI YAN KILA SIFA MBAYA NI WAO

Lakini ikumbukwe kuwa anayesisitiza UKABILA ndio mkabila Na pia kikubwa Huku JF watu wengi mnainekana kuwa na chuki binafsi tu juu ya WACHAGA au watu kutoka Kask sababu kuna kitu either wamewazidi hamna au mnataka mkiige kwao mwishowe Hamuwezi



Asaalam Aleykum
Kunywa soda hapo kwa mangi nitalipa kaka
 
HIYO IKO WAZI .....SIKU MOJA NILIKUWA NA MJOKE MAZA ........KWAMBA MAZA EEEEH""""NTAOA MCHAGA [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]. Ile sijamalizia kauli yangu aiseeeeeh ......nilikwepa mwiko wa kusongea ugali ...[emoji28][emoji28][emoji28] ....Ata sijui kwan huku nyanda za juu kusin wachaga wanaogopwa sana
 
Dah pole sana, ila mimi ni mtu wa maono naona kabisa mtaoana na maisha yatakuwa fresh tu na furaha kwaiyo acha mawazo pika chakula kizur mle na mumeo .LAZIMA MUOANE LABDA JAMAA NDIO AWE HATAKI LAKINI SIO HUYO MAMA.
KISHA MSAMEHE HUYO MAMA KAMA HAKIJATOKEA KITU
Maono Tena?[emoji119]
 
Kwako kimeumana ulazimishe ndoa au auchane nayo?

kwa mwanaume wako kimeumana, huku mchumba huku mwanamke?

Mama mkwe kimeumana, amekuonyesha anakupenda ila anashindwa kukubali kumtoa mtoto wake kuja kwa mchaga

Pasua kichwa[emoji119][emoji119][emoji119][emoji119][emoji119][emoji119]
 
Wazazi wangu waliniambia siyo vizuri kwenda ukweni kabla hujaolewa siyo heshima na ukiangalia ni kweli pia mchumba angu nilimuuliza akanambia ni kweli inabidi Mimi mwenyewe nitafute siku special nikupeleke kukutambulisha rasmi Ila siyo Mimi kujipeleka mwenyewe inakuwa siyo heshima
Hapo ndipo ulijimaliza! Ujanja ni kuwawin mfano kujua lugha ya kwao. Naamini hujui hata kusalimia kimakua. Angalia una bahati maana kimakua mtoto ni wa mjomba. Ukiolewa mume wako anahamia kwenu. Jiongeze ili wakupokee, ukikaa na uchaga wa kuamini wazazi wako umekwisha.
 
Mie mbona girlfriend wangu huwa naenda nae kwetu, anamsaidia na maza kuangua machungwa... Nyie washamba wa wapi aisee?? Amkeni
kujipeleka peleka kwa wazazi wa a mere boyfriend ndiyo ujanja wa wapi? Mkarudie kufundishwa heshima,
 
Jamani eeh you are asking for too much. Mtu akiwa interested kujifunza lugha ya mwenzi wake ni sawa, na sio kufanya kila kitu ili tu kuwaimpress wakwe. Anatakiwa awapende tu na sio kuwa-impress. Asije akaishia kuspend maisha yake yote kuwaimpress watu ambao wanaweza wakagoma vilevile kumpenda. Awapende tu na kuwatreat vizuri, hiyo inatosha kabisa.
Hapo ndipo ulijimaliza! Ujanja ni kuwawin mfano kujua lugha ya kwao. Naamini hujui hata kusalimia kimakua. Angalia una bahati maana kimakua mtoto ni wa mjomba. Ukiolewa mume wako anahamia kwenu. Jiongeze ili wakupokee, ukikaa na uchaga wa kuamini wazazi wako umekwisha.
 
Hapo ndipo ulijimaliza! Ujanja ni kuwawin mfano kujua lugha ya kwao. Naamini hujui hata kusalimia kimakua. Angalia una bahati maana kimakua mtoto ni wa mjomba. Ukiolewa mume wako anahamia kwenu. Jiongeze ili wakupokee, ukikaa na uchaga wa kuamini wazazi wako umekwisha.
Ila watu jamani[emoji119][emoji119]yaani akajipe na kazi ya kujifunza lugha za watu kisa ndoa?
Sindo maana mtaendelea kusema tuna ego?[emoji28][emoji23][emoji23]

Acha tuonekane viburi. Hiyo ndoa ama utopolo? Ajifunze akitaka mwenyewe. English yenyewe inatushinda. Hapo ukute hata kichagga chake hakijui ndo akahangaike na lugha za watu?

Hivi haya yotemumejoweka katika nafasi kama kala zake? Mungejisikiaje?

@miss_chagga... ndoa si utumwa. Ukishaona mambo yanakuzidia kama ub quit haraka sana. Ndoa si kupelekeshana. Khaaa..... kila mtu abaki na asili yake
 
Jamani eeh you are asking for too much. Mtu akiwa interested kujifunza lugha ya mwenzi wake ni sawa, na sio kufanya kila kitu ili tu kuwaimpress wakwe. Anatakiwa awapende tu na sio kuwa-impress. Asije akaishia kuspend maisha yake yote kuwaimpress watu ambao wanaweza wakagoma vilevile kumpenda. Awapende tu na kuwatreat vizuri, hiyo inatosha kabisa.
Yaani mimi nisivyojua kuvungaa[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Naanza kujifunza kimakua wkati kichagga sikiwezi vizuri kisa kumfurahisha mama mkwe. Kwanza naenda kuishi nao? Mimi napenda mapenzi bana siyo lugha. Nideekeeeee... akijua kimakua ndo atakua approved ama[emoji23]
 
Mtazamie kwanza uache kumpa hiyo Nyapu yako uone msimamo wake maana ukiendelea kumwacha akanyage nyapu daily mwana anaweza kujisahau
 
Em wasituchoshe jamani. Wakwe ndiyo tuwageuze Mungu wetu sasa khaaa
Yaani mimi nisivyojua kuvungaa[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Naanza kujifunza kimakua wkati kichagga sikiwezi vizuri kisa kumfurahisha mama mkwe. Kwanza naenda kuishi nao? Mimi napenda mapenzi bana siyo lugha. Nideekeeeee... akijua kimakua ndo atakua approved ama[emoji23]
 
Nazidi kuchanganyikiwa sijui hata nisimamie upande gani yani ubongo umechoka Kuna kitu kinanisukuma nipige tu mayowe sijui kwanini nahisi ni dalili za kuchanganyikiwa hivi mnajua haya mambo ni magumu sana jamani uwiiiiiiiii!!!! Jana Kuna mtu alishauri huku kuwa ukikubali mfunge ndoa bila ndugu zake watasema umemloga nikaona kweli nikamshauri mchumba angu amuombe mchungaji akaongee na mama yake ili akubali nikamwambia Mimi nataka amani sitaki vita akanijibu nimechoka kuwabembeleza tena usiwaze hilo nmeshasema tunafunga ndoa kuhusu kwetu achana napo uko nshamaliza hakutaka hata niendelee kuongelea hili swala hivi ningefanyaje jamani haya mambo ni mazito jamani acheni usiombe yakukute peke yangu bila Mungu sitoweza yani Kama Jana usiku sijalala hapa naskia tu Kuna sauti inanisukuma nipige mayowe na ninahisi siku ya leo haitopita bila kupiga mayowe ubongo ushastack natamani hata atokee mtu aniteke kupoteza ushahidi maana ujasiri wa kuwaambia kwetu sina kabisa wazazi wangu watakufa na presha wakisikia Jana tu nmemgusia dada yangu juu juu naye presha ikampanda ikabidi tu nimwambie nilikuwa nakutania mambo yako sawa maana alianza hadi kulia sembuse wazazi Ee Mungu naomba nitetee
Dah miss chuga umeongea kwa hisia sana mamie yaani mpaka umenigusa ndani ndani kabisa ya moyo,i can feel you my dear,ninaumia pamoja na wewe,kwa kweli una wakati mgumu sana mpenzi,ushauri humu ni mwing sana umetolewa,la msingi mwombe Mungu akuongoze ufanye maamuzi sahihi ambayo hayatakuwa na madhara kwenu nyote lakini pia take your time usiharakishe kuchukua maamuzi nina amini muda unaweza kutoa majibu mujarabu,time tells mamie,kila la kheri my dear na upone upesi hayo maumivu yako ya kihisia .
 
Habari zenu wapendwa?

Mwenzenu na matatizo sielewi nichukue uamuzi gani naombeni mnishauri wapendwa, nilianza mahusiano na mkaka wa kimakuwa toka 2016 kiukweli ananipenda sana na Mimi nampenda na Mungu ametujalia mwaka Jana mwezi wa 12 kapeleka mahari kwetu akanivalisha na Pete ya uchumba.

Baada ya hapo wakualiana na wazazi harusi iwe mwezi wa 4 mwaka huu Ila baada ya muda mama yake akamwambia naomba harusi mfanye mwezi wa 7 nataka nijipange sherehe iwe kubwa tukamkubalia kupeleka hadi wa 7 Ila Cha kushangaza juzi kipindi wamekaa kwenye kikao Cha kuandaa kamati ya harusi mama mtu akasema harusi isogezwe tena iwe mwezi wa 10

Baada ya mwanae kumbana mama yake kuwa kwanini kila cku unapeleka mbele akamwambia sitaki uowe mwanamke wa kichaga ndomana nafanya hivi, kiukweli mwanae alichukia sana kuskia hiyo kauli akanipa mrejesho kuwa mama yake hataki anioe kisa mimi mchaga Ila kwakuwa nakupenda tumeshirikiana mambo mengi siwezi kukuacha tutafunga ndoa mwezi wa 8 bila hata ndugu zake kuwepo atasimamia shoo mwenyewe bila msaada wa ndugu zake nikamwitikia sawa

Ila hapa nawaza usikute huu uamuzi ameuchukua sababu ya hasira nahisi Kama akitulia atanibadilikia asikilize ndugu zake aniache na kinachoniumiza zaidi ni kwamba nimetoka naye mbali kanipotezea muda na hivi kapeleka hadi mahari kwetu watu wanasubiri harusi.

Kama akinibadilikia sijui hii aibu tutaibebaje na familia yangu, nimechanganyikiwa mpaka nawaza sijui nimbebe tu mimba ili azidi kuwa na msimamo aogope kupoteza mke na mtoto!,

Ila nakosa jibu huyu mama simuelewi kwanini ananifanyia hivi Kama alikuwa hataki niolewe na mwanae kwanini hakumzuia kipindi anapeleka mahari wakamsapoti apeleke, kinachoniumiza ni aibu kwetu mahari imeenda alafu ikitokea tukiachana kisa mama yake aibu itakuwa kubwa Bora hata angekuwa hajapeleka mahari.

Ndugu zangu naombeni ushauri wenu nifanyaje kulishinda hili jaribu lililopo mbele yangu, Ndugu zangu Bado sijawambia Kama Kuna huu mgogoro maana hata sijui watalipokeaje nachanganyikiwa Mimi jamani
Mkuu pole sana kwa hayo yote unayopitia kwa sasa kwani ni kipindi kigumu sana kimaisha na ni Mungu tu anaweza kukuvusha salama katika kipindi hiki hivyo nakushauri pamoja na ushauri mwingi ambao watu wameutoa humu Piga Magoti mlilie Mwenyezi Mungu hakika yeye hufanya njia pasipo na njia.

Pili nakushauri usijaribu kubeba mimba kama ulivyoeleza hapo kwenye uzi ili kushinikiza ndoa hii ni hatari sana kwa muskabali mzima wa maisha yako ya kesho, pia muombe Mungu akuondolee wazo la kutaka kujiua hii ni roho chafu naomba isipate nafasi.

Tatu ongea na huyo mume mtarajiwa umjue mtu mwenye maamuzi katika familia yao kwa sasa ni nani kutokana na kwamba baba yake hayupo, ukimpata huyo mwambie mtarajiwa amfuate aongee nae na pale inapowezekana wahusishwe viongozi wa dini ili huyo mtu aende akaongee na mama na kumueleza madhara atakayoyasababisha kwa uamuzi wake wa kutokutaka ndoa ifungwe na aelezwe haya yote yanayokuumiza ikiwa ni pamoja na yeye kukubali kuja kutoa mahari na kuvalishwa pete ili hali akijua kuwa hataki mwanae akuoe.

Ikiwa namba tatu hapo juu itafanikiwa basi nakutakia kila la kheri kwenye maisha mapya utakayoanza,ikiwa haitafanikiwa mim kwa nafasi yangu nakushauri usifunge ndoa bila wazazi wa mume kuwepo nina kesi nyingi za hivi maisha yenu yatakuwa magumu sana na hutayafurahia; kumbuka huyo ndio mtu ambaye mtaishi wote kwa kipindi chote cha maisha yako kilicho baki.

Mwisho kabisa ushauri wangu kwa wakuu wote hapa wachaga kama yalivyo makabila mengine wana mazuri yao na mapungufu yao ila kwenye kutoa maoni tuwe makini na kauli zetu tunaweza kulaani vizazi vyetu bila kujua. Mama na baba wakwe mliopo hapa na wale watarajiwa tujifunze jambo hapa sio vizuri kuumiza mtoto wa mwenzio kiasi hiki "what goes around comes around".
 
Back
Top Bottom