Mama mkwe hataki niolewe na mwanaye kisa mimi ni Mchaga

Mama mkwe hataki niolewe na mwanaye kisa mimi ni Mchaga

Ushauri wangu ni hivi olewa kwingine maisha ndio haya mbona wanawake wachuga wanaolewa na wazungu umetoka wapi na vibudu ,?? Wamekomaa kama Nini
The more modern a girl, the less her value as a wife.

What does a man want?

Love, appreciation, children,and hot dinner after work made by his smiling wife.

Not someone who is tired from her own job, doesn't want kids, and can't cook.
 
Mama mkwe yuko sawa. Mpare na Mchaga umuozeshe mwanao! Nani anataka kahaba nyumbani. Heri ya Mhaya hata Mnyaturu kuliko mchaga tena mmachame. Yethu! Wanajamiiana kama inzi, kaka dada, mjomba shemeji baba mkubwa na mdogo mradi kila ajaye anapewa tu
Acha ujinga. Unakuwa kama haukatwi.
 
Ndoa ni yenunna siyo ya mama mkwe So as long as mnapendana fanyeni hta kimyakimya ,kuna wazee bado wana viji elements vya kipumbavu vya kizamani kbsa.
 
Miss Chuga mdogo angu;
1. Ni wanaume wachache sana ambao wanaweza wakaamua kwenda kinyume na wazazi wao, especially mama zao. Wanawake tukipenda huwa tunaforce kivyovyote huko nyumbani hadi mchumba atakubaliwa, wakibisha sana tunabeba mimba au tunahamia kwa mwanaume bila ndoa, maisha yanasonga. Ila hawa wenzetu, atakaloliamua mama mkwe mara nyingi ndiyo linakuwa final say. Usijiaminishe sana kwamba mchumba wako ana msimamo sana na hautobadilika. Nina rafiki angu Mmachame yalimkuta kama yako, mwisho wa siku mchumba akamwambia mimi siwezi kuendelea na mipango ya ndoa bila wazazi wangu. Ila Mungu sio wakwe, alikuja akaolewa zake na mtu mwingine na yupo anadunda na ndoa yake. (Hopefully wa kwako atapambana hadi mwisho)

2. Kamwe usije ukaungana na mtoto wa mama mkwe kwenda kinyume na mama mkwe; huo utakuwa ni ugomvi wa maisha, na ikiwezekana ugomvi utaendelea hadi kwa watoto wako (ya Hamissa na Mama Diamond). Yes kuna muda wazazi wanazingua, but still tunahitaji baraka zao, hata kama watazitoa kinafki na kuja kujumuika nanyi kwenye sherehe yenu. Usikubali kufunga ndoa na huyo mchumba wako kama wazazi wake hawajaridhia. Yeye anachotakiwa kufanya ni kuwalainisha na kuwaelewesha huko nyumbani kwao hadi waje wakubali. Usishindane na mama mkwe; kesho watapatana na kijana wake ila wewe ndiyo utabaki kuwa adui yake.

Naweza kukuelewa unajisikiaje, aibu unayoiwazia, kuchekwa na kuchambwa na wananzengo, bado muda wako na upendo ulioinvest kwenye hayo mahusiano, labda unaona na umri umeshaenda aisee inaumiza sana. Lakini pamoja na yote hayo, ikitokea imeshindikana kufunga hiyo ndoa; lia mshukuru Mungu kwa yote. Na usije ukakaa unajilaumu sijui ukaharibu maisha yako kisa umeachwa; hujafanya kosa lolote la kukufanya uachike: wewe kuzaliwa mchaga sio kosa wala sio dhambi na huwezi kubadili kabila lako ili kuwaridhisha wakwe. Kuvunjika kwa uchumba sio mwisho wa maisha

Imagine ukiforce hiyo ndoa, utaishi maisha ya aina gani na wakwe zako? Usije ukajidanganya kwamba labda mtaishi mbali na wakwe zako so ni sawa tu; mdogo angu hao ndugu mtawahitaji tu, na watoto wako watawahitaji hao ndugu wa baba zao pia.

Na usijidanganye kubeba mimba, kwa sababu unaweza kubaki single mom, ndoa isifungwe na hata huyo mtoto wako wasiwe na habari naye. Acha mambo yaende naturally, muache mchumba wako apambane hadi kieleweke. Ikishindikana basi mama, wewe sio wa kwanza wala wa mwisho kuvunja uchumba, na wakati mwingine ni bora kuvunja uchumba kuliko kuvunja ndoa. Familia nyingine unaenda kujipa mateso tu.

Muombe Mungu, mapenzi yake yatimizwe kwenye huo uchumba wenu. Litakalotokea lolote, kubaliana nalo then mshukuru Mungu. Yeye anakuwazia mema siku zote, na anaijua kesho yako.

Na nyie wanaume muulizage mapema kwa mama zenu, wawaambie hawataki muoe kabila gani: sio unakaa na mtoto wa mtu miaka 5 afu ndiyo mama mkwe anakuja "sitaki mchaga sijui mnani". Afu alivyokosa huruma eti aliruhusu kabisa utolewe mahari. Mungu amsamehe, hiyo mbegu isije ikamea kwa mabinti zake.

Ukiona linakuchanganya sana, washirikishe ndugu zako. Usije ukadondoka kwa presha bure. Mungu na akutetee
Huu ndio ulikuwa uahauri bora zaid kwa huyo miss chugga
 
Habari zenu wapendwa?

Mwenzenu na matatizo sielewi nichukue uamuzi gani naombeni mnishauri wapendwa, nilianza mahusiano na mkaka wa kimakuwa toka 2016 kiukweli ananipenda sana na Mimi nampenda na Mungu ametujalia mwaka Jana mwezi wa 12 kapeleka mahari kwetu akanivalisha na Pete ya uchumba.

Baada ya hapo wakualiana na wazazi harusi iwe mwezi wa 4 mwaka huu Ila baada ya muda mama yake akamwambia naomba harusi mfanye mwezi wa 7 nataka nijipange sherehe iwe kubwa tukamkubalia kupeleka hadi wa 7 Ila Cha kushangaza juzi kipindi wamekaa kwenye kikao Cha kuandaa kamati ya harusi mama mtu akasema harusi isogezwe tena iwe mwezi wa 10

Baada ya mwanae kumbana mama yake kuwa kwanini kila cku unapeleka mbele akamwambia sitaki uowe mwanamke wa kichaga ndomana nafanya hivi, kiukweli mwanae alichukia sana kuskia hiyo kauli akanipa mrejesho kuwa mama yake hataki anioe kisa mimi mchaga Ila kwakuwa nakupenda tumeshirikiana mambo mengi siwezi kukuacha tutafunga ndoa mwezi wa 8 bila hata ndugu zake kuwepo atasimamia shoo mwenyewe bila msaada wa ndugu zake nikamwitikia sawa.

Ila hapa nawaza usikute huu uamuzi ameuchukua sababu ya hasira nahisi Kama akitulia atanibadilikia asikilize ndugu zake aniache na kinachoniumiza zaidi ni kwamba nimetoka naye mbali kanipotezea muda na hivi kapeleka hadi mahari kwetu watu wanasubiri harusi.

Kama akinibadilikia sijui hii aibu tutaibebaje na familia yangu, nimechanganyikiwa mpaka nawaza sijui nimbebe tu mimba ili azidi kuwa na msimamo aogope kupoteza mke na mtoto!

Ila nakosa jibu huyu mama simuelewi kwanini ananifanyia hivi Kama alikuwa hataki niolewe na mwanae kwanini hakumzuia kipindi anapeleka mahari wakamsapoti apeleke, kinachoniumiza ni aibu kwetu mahari imeenda alafu ikitokea tukiachana kisa mama yake aibu itakuwa kubwa Bora hata angekuwa hajapeleka mahari.

Ndugu zangu naombeni ushauri wenu nifanyaje kulishinda hili jaribu lililopo mbele yangu, Ndugu zangu Bado sijawambia Kama Kuna huu mgogoro maana hata sijui watalipokeaje nachanganyikiwa Mimi jamani
jitafakari sana, si ajabu ukiolewa huyo jamaa atakuja kugeuza hilo sakata kuwa fimbo kwako. Mtakapohitilafiana kidogo hata kama yeye ndiye amekosea, badala ya kuzungumza na kutengeneza si ajabu atakuwa anakwambia anajuta laiti angemsikiliza mama yake.......
 
Miss Chuga mdogo angu;
1. Ni wanaume wachache sana ambao wanaweza wakaamua kwenda kinyume na wazazi wao, especially mama zao. Wanawake tukipenda huwa tunaforce kivyovyote huko nyumbani hadi mchumba atakubaliwa, wakibisha sana tunabeba mimba au tunahamia kwa mwanaume bila ndoa, maisha yanasonga. Ila hawa wenzetu, atakaloliamua mama mkwe mara nyingi ndiyo linakuwa final say. Usijiaminishe sana kwamba mchumba wako ana msimamo sana na hautobadilika. Nina rafiki angu Mmachame yalimkuta kama yako, mwisho wa siku mchumba akamwambia mimi siwezi kuendelea na mipango ya ndoa bila wazazi wangu. Ila Mungu sio wakwe, alikuja akaolewa zake na mtu mwingine na yupo anadunda na ndoa yake. (Hopefully wa kwako atapambana hadi mwisho)

2. Kamwe usije ukaungana na mtoto wa mama mkwe kwenda kinyume na mama mkwe; huo utakuwa ni ugomvi wa maisha, na ikiwezekana ugomvi utaendelea hadi kwa watoto wako (ya Hamissa na Mama Diamond). Yes kuna muda wazazi wanazingua, but still tunahitaji baraka zao, hata kama watazitoa kinafki na kuja kujumuika nanyi kwenye sherehe yenu. Usikubali kufunga ndoa na huyo mchumba wako kama wazazi wake hawajaridhia. Yeye anachotakiwa kufanya ni kuwalainisha na kuwaelewesha huko nyumbani kwao hadi waje wakubali. Usishindane na mama mkwe; kesho watapatana na kijana wake ila wewe ndiyo utabaki kuwa adui yake.

Naweza kukuelewa unajisikiaje, aibu unayoiwazia, kuchekwa na kuchambwa na wananzengo, bado muda wako na upendo ulioinvest kwenye hayo mahusiano, labda unaona na umri umeshaenda aisee inaumiza sana. Lakini pamoja na yote hayo, ikitokea imeshindikana kufunga hiyo ndoa; lia mshukuru Mungu kwa yote. Na usije ukakaa unajilaumu sijui ukaharibu maisha yako kisa umeachwa; hujafanya kosa lolote la kukufanya uachike: wewe kuzaliwa mchaga sio kosa wala sio dhambi na huwezi kubadili kabila lako ili kuwaridhisha wakwe. Kuvunjika kwa uchumba sio mwisho wa maisha

Imagine ukiforce hiyo ndoa, utaishi maisha ya aina gani na wakwe zako? Usije ukajidanganya kwamba labda mtaishi mbali na wakwe zako so ni sawa tu; mdogo angu hao ndugu mtawahitaji tu, na watoto wako watawahitaji hao ndugu wa baba zao pia.

Na usijidanganye kubeba mimba, kwa sababu unaweza kubaki single mom, ndoa isifungwe na hata huyo mtoto wako wasiwe na habari naye. Acha mambo yaende naturally, muache mchumba wako apambane hadi kieleweke. Ikishindikana basi mama, wewe sio wa kwanza wala wa mwisho kuvunja uchumba, na wakati mwingine ni bora kuvunja uchumba kuliko kuvunja ndoa. Familia nyingine unaenda kujipa mateso tu.

Muombe Mungu, mapenzi yake yatimizwe kwenye huo uchumba wenu. Litakalotokea lolote, kubaliana nalo then mshukuru Mungu. Yeye anakuwazia mema siku zote, na anaijua kesho yako.

Na nyie wanaume muulizage mapema kwa mama zenu, wawaambie hawataki muoe kabila gani: sio unakaa na mtoto wa mtu miaka 5 afu ndiyo mama mkwe anakuja "sitaki mchaga sijui mnani". Afu alivyokosa huruma eti aliruhusu kabisa utolewe mahari. Mungu amsamehe, hiyo mbegu isije ikamea kwa mabinti zake.

Ukiona linakuchanganya sana, washirikishe ndugu zako. Usije ukadondoka kwa presha bure. Mungu na akutetee
Kwa hamisa na mondi kulitokea nn kwani?

Sent from my Nokia C1 using JamiiForums mobile app
 
Wewe na huyo mchumba wako nyie ndo wenye mamuzi, kwanza wewe ni mchaga wa wapi?

Mimi nimeoa mchaga wa Mwika maeneo ya Lole marela, kipindi tunachumbiana wazazi wangu na wazazi wake pia hawakupenda.

Wazazi wangu walikuwa wanaogopa wachaga kwamba hawadumu na wanaume na wako after money, lakini pia na yeye wazazi wake walikuwa wanaogopa kabila langu kwamba ni wakorofi wanapiga wanawake.

Lakini kwa msimamo wetu, nilitoa mbuzi wawili, moja wa baba na moja wa mama, mbege zilinyweka mbona, still now nampenda mke wangu sana naye ananipenda balaa.

Kuweni na msimamo vijana!!
 
Mama dangote, hampend mobeto, na mond anamsikiliza mama yake, na ndio mana hawako poa Sana hata na yule mtoto waliozaa na hamisa.
Imeshathibitika kuwa yule mtoto si wa DIAMOND au hujui hilo?
 
kwa sasa tupe mrejesho nini kilijiri????? kama mlioana ndao inaendeleaje??
 
Back
Top Bottom