Mama Mongella - Aghushi na Kutafuna Mamillioni Ya Pesa!

Mama Mongella - Aghushi na Kutafuna Mamillioni Ya Pesa!

Alishayazoea ya CCM, Viongozi wengi wa CCM ni wachafu sio watakatifu hata kidogo hivyo kuwa hivi wala tusishangae kabisa maana ufisadi kila sehemu labda wa kijibu ni Spika na, Mafisadi wapo watu wengi wa kila namna, Kuanzia Tanzania mpaka Bunge la Africa
 
Na Aristariko Konga
BALOZI Getrude Mongella, Rais wa kwanza wa Bunge la Afrika (PAP) amelazimika kujiuzulu kutokana na tuhuma za matumizi mabaya ya fedha na ajira za upendeleo katika ofisi hiyo.
Hatua ya kulazimishwa kuachia ngazi imekuja baada ya mlolongo wa malalamiko kutoka kwa wabunge wa PAP kutokuridhika na mwenendo wa matumizi ya fedha na uendeshaji wa ofisi hizo.
Nafasi yake imechukuliwa na Dk. Idriss Ndele Moussa, Mbunge kutoka Chad, katika uchaguzi uliofanywa na bunge hilo 28 Mei mwaka huu. PAP ina makao makuu katika mji wa Midrand, nchini Afrika Kusini.
Dk. Ndele aliibuka mshindi baada ya kuwashinda wagombea wenzake wawili; Lassane Sawadogo, mbunge kutoka Burkina Faso na Mustafa El Gendy, kutoka Misri.
Dk. Ndele aliapishwa na Dk. Mongella kuchukua wadhifa huo mpya, akiwa na kazi ya kufanya mabadiliko makubwa ya uongozi na utendaji wa PAP, kutokana na maagizo ya wabunge ya 19 Mei, mwaka huu huko Midrand.
Bunge la Afrika pia lilichagua makamu wanne wa rais ambao ni Bethel Amadi (Nigeria), anayewakilisha Kanda ya Afrika Magharibi na Mary Mugyenyi (Uganda) anayewakilisha Afrika Mashariki.
Wengine ni Laroussi Hammi (Algeria) anayewakilisha kanda ya Kaskazini, na Joram Gumbo (Zimbabwe) anayewakilisha kanda ya Kusini mwa Afrika.
Mabadiliko yanatokana na kuwapo tuhuma dhidi ya Mongella kuwa chini ya uongozi wake, ajira zilipatikana kwa misingi ya upendeleo na bila kufuata taratibu za ajira wala sifa za watumishi.
Habari zinasema kuwa katika siku za karibuni, kabla ya mabadiliko hayo, Mongella alijaribu kung’ang’ania ili aendelee na wadhifa huo, lakini alishinikizwa kuachia ngazi, jambo ambalo lilikamilika 28 Mei mwaka huu.
Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Dk. Thomas Kashilila, alipoulizwa juzi Jumatatu, alikiri kuwa na taarifa za Mongella kuacha wadhifa huo, ingawa ofisi yake haikuwa na taarifa rasmi kutoka PAP.
“Tumepata taarifa kupitia njia nyingine, lakini hatuna taarifa rasmi kuwa kaacha wadhifa huo,” alisema Dk. Kashilila.
Mwenendo wa Mongella uliishakuwa hoja hadi wakuu wa nchi za Afrika kuunda kamati maalum ya kufanya uchunguzi wa usimamizi na uendeshaji wa PAP.
Taarifa zinasema bunge lilijadili kwa kina taarifa ya kamati hiyo na kujiridhisha kuwa kulikuwa na matumizi mabaya ya fedha.
Katika hatua ambayo haikutarajiwa, inaelezwa kuwa serikali ya Tanzania imekubali kubeba mzigo wa kulipa fedha zote ambazo Mongella alituhumiwa kuzitumia vibaya.
Taarifa zinasema awali, hata baada ya serikali ya Tanzania kuchukua mzigo huo, Mongella alishauriwa ajiuzulu ili kulinda heshima ya Tanzania, lakini aligoma kufanya hivyo.
Wabunge wa Bunge walilalamika kwa viongozi wakuu wa nchi za Afrika juu ya uongozi wake kwa ujumla, ambao wanadai haukuwa na dira wala tija.
“Kuna madai pia kwamba aling’ang’ania kubaki katika nyumba ya Bunge na alipolazimishwa kuondoka akaamua kuhama na fenicha zote za ndani akidai ni zake, jambo ambalo si la kweli,” alisema mbunge mmoja wa Bunge la Afrika kutoka Tanzania ambaye hakupenda kutajwa jina.

Aidha, uongozi wa Mongella umelalamikiwa kwa kushindwa kufanya jambo la maana wakati uliendelea kugharimu rasilimali za nchi za Afrika.
Mjadala wote wa kumuondoa Mongella ulikuwa unaripotiwa moja kwa moja kwenye vyombo vya habari vya Afrika Kusini na Namibia. Kuna wakati Mongella alilazimika kukatisha kikao cha Bunge hilo na kufanya mazungumzo ya faragha na makamu wake wawili.
Baada ya kikao hicho cha siri, Mongella aliamuru waandishi wa habari waliokuwa wakifuatilia kikao waondoke, jambo ambalo lilifanyika.
Naye mbunge mpya wa Tanzania katika PAP, John Cheyo amesema Mongella atakumbukwa kwa kuwa rais wa kwanza wa PAP.
Ni MwanaHALISI iliyowahi kuandika katika toleo Na. 73 la Novemba 28 hadi 4 Desemba 2008, kwamba Mongella alikuwa anatuhumiwa kutenda makosa ya kukosa uaminifu, wizi na utoaji ajira kinyume cha taratibu.
Kuhusu wizi, Mongella anatuhumiwa kutafuna dola za Kimarekani 138,000 sawa na Sh. 180 milioni za Tanzania, mali ya PAP.
Katika tuhuma za utoaji ajira, Mongella anatuhumiwa kuajiri jamaa zake ndani ya Sekretarieti ya Bunge hilo, kinyume cha taratibu. Tayari Bunge limeagiza kufuta ajira zilizofanywa na Mongella.


Kwenye moja ya magazeti ya Tanzania leo tarehe 15.06.2009 limeongelea suala la Dkt Slaa kukusudia kuhoji Bungeni kuhusu matumizi ya TZS milioni 180 kumlipia Dkt. Mongella huko Bunge la Afrika kama fedha zilizopotea chini ya utawala wake.

SWALI:NINI KIMEMSIBU HUYU MAMA ALIYEKUWA KATIBU WA ULE MKUTANO WA DUNIA WA AKINA MAMA WA BEIJING?
MAMA ALIYEKUWA ANATAZAMWA KAMA "MODEL" KWA VIONGOZI VIJANA WANAWAKE WA KITANZANIA?

........yaani kusurvive kwa huyu mama........miye nilikuwa napigia mstari tu ule usemi wa Nyani Ngabu............this thing came too late......and clearly its a bad image to our nation............
 
Kumbe acha Karamage amfaidi mke wa Mongella. Mongela na Karamage ni Dugu moja. Wanabebana Kifisadi na wanasaidiana kifisadi.

Hivi huyu mama si ndiyo inasemekana alipotoka Beijing yeye na kundi lake walikuwa wamejaza kwenye vijaluba semCondoms??!!!
 
Ila ni aibu kubwa sana kwa Tanzania jamani kama hayo yaliyosemwa ni ukweli.
 
MMh kama hizo tuhuma ni kweli atakuwa ametuangusha sana,na nchi yetu kwa ujumla kweli fedha fedheha
haya mambo ni ya kweli kabisa na nilikuwa south africa wakati yanatokea na it was higherly covered negatively in her regard. nimemwona anajitetea kwenye vyombo vya habari watu wanamchafulia jina....hana pa kutokea
 
Folks hii habari imejulikana kitambo sana. Ambao hawafuatilii mambo ndo wanashangaa. Ukweli ni kwamba hii kashfa ya huyu mama ni ya siku nyingi..infact JK na Membe walijaribu kulimaliza kikubwa na wakubwa wenzao kwenye mkutano wa wakubwa wa Africa lakini pressure ilikuwa kubwa sana. Ndo maana TZ ilikubali kulipa gharama za upotevu wa pesa. Ilibidi huyu mama afukuzwe kwenye kikao cha AU kule Accra juzi juzi..lakini nadhani JK alitumia diplomasia kuogopa damage kwa nchi yetu.

In all, this is not new. FMES na wengine kibao humu nadhani waliweka details nyingi humu JF na tuhuma zake kuchambuliwa. na huu wizi uliripotiwa na international auditors..nadhani KPMG au Coopers kama sikosei.

Ni kama leo tukisikia Tibaijuka ameondolewa..wengine hatutashangaa maana dossier ipo siku kibao kuonyesha jinsi mama alivyovuruga..

Let her go..its a disgrace..Sema tuu wanaharibia wengine wenye moyo wa kuhangaika na kusonga mbele banking on diplomatic image of our country.

Hii ishu kama ulivyosema mkuu ni ya siku nyingi sana hadi ilishasahaulika hadi ilivyoibuka tena juzi juzi na wabunge wa Bunge la Afrika kuishikia bango hadi kieleweke.
Ninachojiuliza:
1. Hivi Tanzania kuamua kulipa/kufidia upotevu huo inatafsirika vipi? Does it mean kuwa serikali inawajibika kwa makosa ya huyu mama?

2. The fact kwamba kalazimika kuwajibika, uwajibikaji huo wa kuachia ngazi tu hautoshi. Hata kama alipata nafasi hiyo kwa jitihada binafsi bado alikuwa na dhamana na hivyo anapaswa kuwajibishwa zaidi baada ya kuliingizia serikali hasara.

Sitaki kuamini hiki ndicho kilichotokea maana I have lot of respect for this Lady.
GOD FORBID!
 
........yaani kusurvive kwa huyu mama........miye nilikuwa napigia mstari tu ule usemi wa Nyani Ngabu............this thing came too late......and clearly its a bad image to our nation............

Heheheheheheheee....

Limama hili lina sura mbaya inayoendana na tabia yake ya ufisadi.
 
naona wengine hamna uhakika kama hili ni kweli...kwa taarifa ni kweli na huyu mama amejizalilisha sana na pia kuiletea aibu nchi yake, wakati wa bunge la PAP habari zake ziliandikwa sana kwenye magazeti ya south na kuna watu walishangaa sana kule kama kweli huyu mama anaweza kufanya vile...ni aibu na sijui kwa nini anakuwa mbishi maana alikuwa hataki hata kuwajibika..

lakini pia serikali kuingilia kati na kutaka kulipa hasara aliyosababisha ni unacceptable..why?? je serikali imeridhia kama aliyoyafanya si sahihi?
kama serikali imeona si sahihi, anachukuliwa hatua gani???
na je mpaka sasa serikali ya TZ imefanya uchunguzi gani, na taarifa imetolewa wapi??? intakuwa inafanya kosa kubwa sana....
 
Kama Slaa anavyo taka kulivalia hili suala serikali inabidi kumkata kwenye mafao yake na ikibidi kuuza Mali zake , na adhabu zingine zinazo stahili.
 
Hii ishu kama ulivyosema mkuu ni ya siku nyingi sana hadi ilishasahaulika hadi ilivyoibuka tena juzi juzi na wabunge wa Bunge la Afrika kuishikia bango hadi kieleweke.
Ninachojiuliza:
1. Hivi Tanzania kuamua kulipa/kufidia upotevu huo inatafsirika vipi? Does it mean kuwa serikali inawajibika kwa makosa ya huyu mama?
2. The fact kwamba kalazimika kuwajibika, uwajibikaji huo wa kuachia ngazi tu hautoshi. kwa jitihada binafsi kugombea bado alikuwa na dhamana na hivyo anapaswa kuwajibishwa zaidi baada ya kuliingizia serikali hasara.
Sitaki kuamini hiki ndicho kilichoteka maana I have lot of respect for this Lady.
GOD FORBID!


WoS na mimi naungana na wewe hapa.

Kuhusu TZ kulipa hizi pesa haiwajibiki. LAKINI nadhani Membe na JK waliamua kufanya hivi kama damage control dhidi ya taifa letu. Maana report ya auditors ilikuwa so scathing against matumizi mabaya ya pesa na madaraka ya huyu mama. Na ukichukulia hizi ni nafasi za ku-lobby..kama issue inge escalate mama akafukuzwa at the level kama Accra na wakuu wa nchi za Africa..Tanzania ingekuwa in the hole..next time tukitaka kupendekeza wagombea kwenye nafasi kubwa kama hizi. So basically it was a diplomatic game kulipa hizi pesa.

Labda cha kujiuliza..will this issue be swept under the carpet? huyu mama atawajibishwa kwa namna yoyote ile? Kwa kuijua nchi yangu ilivyo..hii imetoka..na hata kama juzi uliangalia Press conference ya huyu mama wakati anakuja..alisema"she has done proud all Africa women"..well you can see..matapeli tunawapokea kwa ushujaa.

What Iam sure of, huyu mama kazi hii ameondolewa kwa nguvu. Na South Africa na nchi nyingine hii issue ilikuwa well covered-only in Bongo!
 
Kumbe acha Karamage amfaidi mke wa Mongella. Mongela na Karamage ni Dugu moja. Wanabebana Kifisadi na wanasaidiana kifisadi.

Hivi huyu mama si ndiyo inasemekana alipotoka Beijing yeye na kundi lake walikuwa wamejaza kwenye vijaluba semCondoms??!!!
Mkulu naomba ufafanue kidogo.
 
hiyo yote haisaiidii labda hao PAP wamchukulie shelia wenyewe lakini sisi kama watanzania hatuwezi kufanya chochote juu yake, tutabaki kuumia tu.

nadhani itakuwa ngumu hawa PAP kuchukua hatua nyingine zaidi ya kumfukuza[kumlazimisha ajiuzulu]wao wanauhakika chao kitarudi,si serikali yetu italipa kwa mapene yetu walipa kodi?kazi kwetu sisi wavuja jasho wa nchi hii
KWELI NCHI HII INAJENGWA NA WENYE MOYO NA KULIWA NA WENYE CHOYO
 
mimi ningependa kujua kama hizo hela za "damage control" zimetoka mifuko binafsi na sio za kwetu walala hoi, Jk na Membe naomba watueleze zimetoka wapi hizo hela? kama ni damage control basi wangetoa na kumlazimisha azirudishe kama walivyomfanyia yule mbunge wa zamani alitumia pesa zetu kumpeleka mkewe matibabu nje.
 
nadhani itakuwa ngumu hawa PAP kuchukua hatua nyingine zaidi ya kumfukuza[kumlazimisha ajiuzulu]wao wanauhakika chao kitarudi,si serikali yetu italipa kwa mapene yetu walipa kodi?kazi kwetu sisi wavuja jasho wa nchi hii
KWELI NCHI HII INAJENGWA NA WENYE MOYO NA KULIWA NA WENYE CHOYO
Tatizo langu lipo kwenye maeneo mawili:

1.Je ni kiasi gani cha Fedha Serikali yetu imeahidi kulipa kutokana na mismanagement ya Dkt. Mongella?

2.Kuanguka kwa huyu mama ni KUANGUKA KWA "KIPIMO" ambacho Watanzania hususani akina mama wenye matarajio ya kufanikiwa kisiasa WALIKUWA WANAKITUMIA "KIPIMO" HICHO(yaani Dkt Mongella) kijipima walipofikia.
 
Mwalimu akifufuka leo akazisikia habari hizi.....Huyu mama alikuwa ni mmoja wa watu walooaminiwa sana na Mwalimu.
Yes.
Na hicho ndicho kilichonisukuma kuuliza swali la msingi,NINI KIMESIBU HUYU MAMA????????!!!!!!
 
Na Aristariko Konga
BALOZI Getrude Mongella, Rais wa kwanza wa Bunge la Afrika (PAP) amelazimika kujiuzulu kutokana na tuhuma za matumizi mabaya ya fedha na ajira za upendeleo katika ofisi hiyo.
Hatua ya kulazimishwa kuachia ngazi imekuja baada ya mlolongo wa malalamiko kutoka kwa wabunge wa PAP kutokuridhika na mwenendo wa matumizi ya fedha na uendeshaji wa ofisi hizo.
Nafasi yake imechukuliwa na Dk. Idriss Ndele Moussa, Mbunge kutoka Chad, katika uchaguzi uliofanywa na bunge hilo 28 Mei mwaka huu. PAP ina makao makuu katika mji wa Midrand, nchini Afrika Kusini.
Dk. Ndele aliibuka mshindi baada ya kuwashinda wagombea wenzake wawili; Lassane Sawadogo, mbunge kutoka Burkina Faso na Mustafa El Gendy, kutoka Misri.
Dk. Ndele aliapishwa na Dk. Mongella kuchukua wadhifa huo mpya, akiwa na kazi ya kufanya mabadiliko makubwa ya uongozi na utendaji wa PAP, kutokana na maagizo ya wabunge ya 19 Mei, mwaka huu huko Midrand.
Bunge la Afrika pia lilichagua makamu wanne wa rais ambao ni Bethel Amadi (Nigeria), anayewakilisha Kanda ya Afrika Magharibi na Mary Mugyenyi (Uganda) anayewakilisha Afrika Mashariki.
Wengine ni Laroussi Hammi (Algeria) anayewakilisha kanda ya Kaskazini, na Joram Gumbo (Zimbabwe) anayewakilisha kanda ya Kusini mwa Afrika.
Mabadiliko yanatokana na kuwapo tuhuma dhidi ya Mongella kuwa chini ya uongozi wake, ajira zilipatikana kwa misingi ya upendeleo na bila kufuata taratibu za ajira wala sifa za watumishi.
Habari zinasema kuwa katika siku za karibuni, kabla ya mabadiliko hayo, Mongella alijaribu kungangania ili aendelee na wadhifa huo, lakini alishinikizwa kuachia ngazi, jambo ambalo lilikamilika 28 Mei mwaka huu.
Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Dk. Thomas Kashilila, alipoulizwa juzi Jumatatu, alikiri kuwa na taarifa za Mongella kuacha wadhifa huo, ingawa ofisi yake haikuwa na taarifa rasmi kutoka PAP.
Tumepata taarifa kupitia njia nyingine, lakini hatuna taarifa rasmi kuwa kaacha wadhifa huo, alisema Dk. Kashilila.
Mwenendo wa Mongella uliishakuwa hoja hadi wakuu wa nchi za Afrika kuunda kamati maalum ya kufanya uchunguzi wa usimamizi na uendeshaji wa PAP.
Taarifa zinasema bunge lilijadili kwa kina taarifa ya kamati hiyo na kujiridhisha kuwa kulikuwa na matumizi mabaya ya fedha.
Katika hatua ambayo haikutarajiwa, inaelezwa kuwa serikali ya Tanzania imekubali kubeba mzigo wa kulipa fedha zote ambazo Mongella alituhumiwa kuzitumia vibaya.
Taarifa zinasema awali, hata baada ya serikali ya Tanzania kuchukua mzigo huo, Mongella alishauriwa ajiuzulu ili kulinda heshima ya Tanzania, lakini aligoma kufanya hivyo.
Wabunge wa Bunge walilalamika kwa viongozi wakuu wa nchi za Afrika juu ya uongozi wake kwa ujumla, ambao wanadai haukuwa na dira wala tija.
Kuna madai pia kwamba alingangania kubaki katika nyumba ya Bunge na alipolazimishwa kuondoka akaamua kuhama na fenicha zote za ndani akidai ni zake, jambo ambalo si la kweli, alisema mbunge mmoja wa Bunge la Afrika kutoka Tanzania ambaye hakupenda kutajwa jina.

Aidha, uongozi wa Mongella umelalamikiwa kwa kushindwa kufanya jambo la maana wakati uliendelea kugharimu rasilimali za nchi za Afrika.
Mjadala wote wa kumuondoa Mongella ulikuwa unaripotiwa moja kwa moja kwenye vyombo vya habari vya Afrika Kusini na Namibia. Kuna wakati Mongella alilazimika kukatisha kikao cha Bunge hilo na kufanya mazungumzo ya faragha na makamu wake wawili.
Baada ya kikao hicho cha siri, Mongella aliamuru waandishi wa habari waliokuwa wakifuatilia kikao waondoke, jambo ambalo lilifanyika.
Naye mbunge mpya wa Tanzania katika PAP, John Cheyo amesema Mongella atakumbukwa kwa kuwa rais wa kwanza wa PAP.
Ni MwanaHALISI iliyowahi kuandika katika toleo Na. 73 la Novemba 28 hadi 4 Desemba 2008, kwamba Mongella alikuwa anatuhumiwa kutenda makosa ya kukosa uaminifu, wizi na utoaji ajira kinyume cha taratibu.
Kuhusu wizi, Mongella anatuhumiwa kutafuna dola za Kimarekani 138,000 sawa na Sh. 180 milioni za Tanzania, mali ya PAP.
Katika tuhuma za utoaji ajira, Mongella anatuhumiwa kuajiri jamaa zake ndani ya Sekretarieti ya Bunge hilo, kinyume cha taratibu. Tayari Bunge limeagiza kufuta ajira zilizofanywa na Mongella.


Kwenye moja ya magazeti ya Tanzania leo tarehe 15.06.2009 limeongelea suala la Dkt Slaa kukusudia kuhoji Bungeni kuhusu matumizi ya TZS milioni 180 kumlipia Dkt. Mongella huko Bunge la Afrika kama fedha zilizopotea chini ya utawala wake.

SWALI:NINI KIMEMSIBU HUYU MAMA ALIYEKUWA KATIBU WA ULE MKUTANO WA DUNIA WA AKINA MAMA WA BEIJING?
MAMA ALIYEKUWA ANATAZAMWA KAMA "MODEL" KWA VIONGOZI VIJANA WANAWAKE WA KITANZANIA?


Kama itakuwa ni kweli mama Mongella amefanyika haya, itakuwa ni aibu kubwa sana kwa nchi yetu ya TANZANIA (Kisiwa cha AMANI)

Ni ufisadi uliovuka mipaka kwa kweli. Jina la Tanzania linaanza kusifika kwa mambo mabaya sasa...... MIMI BINAFSI NILIKUWA NAMCHUKULIA HUYU MAMA KAMA MFANO WA KUIGWA KWA MAMA ZETU KATIKA FANI HII YA UONGOZI. Naamini atakuwa hata pia amewavunja moyo wanawake wenzake katika hili.....

Kelele za EPA ya ndani ya nchi zimedhibitiwa, na sasa ...."Hiyo ni international EPA".

MAMA MONGELA UMETUTIA AIBU KWA KWELI SISI KAMA WATANZANIA...
 
Kama kuna mfuko wa "damage control" basi akina Jeetu Patel, Chenge, Liyumba, Yona, Mramba na watuhumiwa wote nao walipiwe hasara waliyoisababishia serikali. Kwa nini ni Mongella tu ndiyo analipiwa ?? Naona serikali yetu labda ina makundi ya mafisadi wazuri na mafisadi wabaya, mafisadi wazuri wanalipiwa hasara zote walizosababisha.

Sijui ni nani anaamua huyu alipiwe na huyu asilipiwe. Pia wale wote walio jela kwa kuiba benki, kuku, nguo, magari, nao serikali iwalipie watoke jela!!!! Kaazi kweli.....
 
mimi ningependa kujua kama hizo hela za "damage control" zimetoka mifuko binafsi na sio za kwetu walala hoi, Jk na Membe naomba watueleze zimetoka wapi hizo hela? kama ni damage control basi wangetoa na kumlazimisha azirudishe kama walivyomfanyia yule mbunge wa zamani alitumia pesa zetu kumpeleka mkewe matibabu nje.

Mzee mzima

Bila shaka hela iliyolipwa huko PAP itakuwa ni jasho letu. JK na Membe wamlipie Mongela damage control kwa fedha za mifukoni mwao kwa kuogopa kitu gani?si wanajua tu fungu lipo la kodi za wadanganyika zitachotwa na kulipia madeni ya kishenzi kama hilo la mongela.

Na hapo ndio ujue kwamba sasahivi Tanzania uadilifu kwa viongozi ni sifuri. Wamezoea kula pesa zetu na kisha kutupigisha siasa za maji taka lakini safari hii mongela kakutana na wajanja wamemnasa.Kazi iliyobaki ni moja tu; kwa wana ukerewe wamuwajibishe huyu mama pamoja na kulitia aibu taifa lakini pia amewaaibisha sana wana ukerewe ambao ni watu waadilifu na wachapa kazi.
 
MMh kama hizo tuhuma ni kweli atakuwa ametuangusha sana,na nchi yetu kwa ujumla kweli fedha fedheha
KAMA NI KWELI

Kabla ya kufikiria kuniangusha cha kwanza naongelea kuhusu hela ambazo serikali imejicommit kuzilipa,

  • je zinatoka fungu gani la bajeti
  • na kama serikali imekubakli kubeba mzigo basi inamaana matumizi yake yalikuwa halali kama haikuwa halali kwann wakubali kulia kwamaana nyingine serikali yetu ni ya wezi
  • kama ikiwa fedha zimetumika isivyo halali basi huyu mama hatakiwi kunyamaziwa apelekwe mahakamani maramoja kujibu tuhuma maana ni kilekile alicofanya Mahalu hapa
Mwisho kabisa huyu mama ameonyesha mbegu ya ccm, kama kawaida yao hawajui maisha mengine zaidi ya wizi, amevunja heshima yake na yanchi alishindwa nn kusubiri muda mfupi uliobaki wauonguzi wake anondoke kwa sifa na mfano mzuri

WHAT A SHAME!!!
 
Back
Top Bottom