Mama Mongella - Aghushi na Kutafuna Mamillioni Ya Pesa!

Mama Mongella - Aghushi na Kutafuna Mamillioni Ya Pesa!

Ni mama yangu wa ubatizo,hence in my eyes she can do no WRONG.

So she can do no wrong in your eyes simply because ni mama yako wa ubatizo? Kwani wengine wenyewe maozu hawana utoto wa ubatizo? You can't be seriious man. Lakini hamna neno at least kuna other eyes which can see the other side you choose to cover your eyes from.
 
Folks hii habari imejulikana kitambo sana. Ambao hawafuatilii mambo ndo wanashangaa. Ukweli ni kwamba hii kashfa ya huyu mama ni ya siku nyingi..infact JK na Membe walijaribu kulimaliza kikubwa na wakubwa wenzao kwenye mkutano wa wakubwa wa Africa lakini pressure ilikuwa kubwa sana. Ndo maana TZ ilikubali kulipa gharama za upotevu wa pesa. Ilibidi huyu mama afukuzwe kwenye kikao cha AU kule Accra juzi juzi..lakini nadhani JK alitumia diplomasia kuogopa damage kwa nchi yetu.

In all, this is not new. FMES na wengine kibao humu nadhani waliweka details nyingi humu JF na tuhuma zake kuchambuliwa. na huu wizi uliripotiwa na international auditors..nadhani KPMG au Coopers kama sikosei.

Ni kama leo tukisikia Tibaijuka ameondolewa..wengine hatutashangaa maana dossier ipo siku kibao kuonyesha jinsi mama alivyovuruga..

Let her go..its a disgrace..Sema tuu wanaharibia wengine wenye moyo wa kuhangaika na kusonga mbele banking on diplomatic image of our country.


We need to be honesty with ourselves. Tunajitia aibu nyumbani na sasa tumetia aibu nje. Kama akitokea mtu akianza ku-question ni kwanini watanzania hawapati nafasi kwenye jumuiya za kimataifa nitashangaa sana. Ajabu sana nitashangaa kama akija nyumbani hajachukuliwa hatua, kama serikali imetumia pesa kwa kulinda heshima yetu, na sijui kama kweli imelindwa, huyu mama akirudi anatakiwa aadhibiwe.

She is such a disgrace. Jamani nchi yetu inanuka ufisadi, na watanzania sasa tumeanza kunuka ufisadi. Aibu tupu.
 
We need to be honesty with ourselves. Tunajitia aibu nyumbani na sasa tumetia aibu nje. Kama akitokea mtu akianza ku-question ni kwanini watanzania hawapati nafasi kwenye jumuiya za kimataifa nitashangaa sana. Ajabu sana nitashangaa kama akija nyumbani hajachukuliwa hatua, kama serikali imetumia pesa kwa kulinda heshima yetu, na sijui kama kweli imelindwa, huyu mama akirudi anatakiwa aadhibiwe. She is such a disgrace. Jamani nchi yetu inanuka ufisadi, na watanzania sasa tumeanza kunuka ufisadi. Aibu tupu.
Ataadhibiwa na nani? Wote mbona watanyoosheana vidole? Ndiyo bongo yetu ya leo, nasikitika kusema. It is very sad indeed.
 
Nadhani mama alikuwa anavuta muda kwa kuwa mbishi kuachia ngazi akitarajia wamatumbi wengine ni wepesi wa kusahau kama wadanganyika. Lakini hatimaye baada ya takribani miaka miwili amekubali kung'oka.Hiyo ndio aina ya viongozi tulio nao Tanzania, hata kama mtu ameboronga kiasi gani ataendelea kung'ang'ania madarakani tuuuuuuuuuu!

Shame on you Mama Mongela huo ufisadi uufanyie shamba la bibi Tanzania sio bunge la afrika.Kule kuna watun wanaona vizuri na wanaozungumza bila kupepesa macho,wanakuangalia usoni moja kwa moja.

Kazi kwenu wana-Ukerewe mtuondolee aibu hii tuliyoipata kama taifa.
 
Hawa ni sehemu ya hiki kizazi cha wala rushwa wa ccm. Yeye alifkiria huko nje kwa wenzetu wanalidana kama ccm wanavyolindana hapa. Anatakiwa awajibike kwa madhambiyake.
 
Kweli

Ukistaajabu ya Musa....................., Mwalimu Nyerere huko aliko naona anasikitika sana.

Mungu Tusaidie kwani hatujui tutendalo
 
Huyu mama ndo alivyo alishawahi kumleta mkono kwa mkono ndugu yake aliyekuwa na Division four pale Bodi ya Mikopo kwa ajiri ya kupewa mkopo wa elimu ya juu huku akitambua fika kwamba hana vigezo!! Mkopo alipewa na huyo kijana bado anasoma China mpaka hivi sasa!!

Za mwizi arobaini!!

Wadau hivi kwa nini hajamfungulia kesi kabisa, wamtupe keko kama kina Liyumba kwa matumizi mabaya ya ofisi???
 
Kweli

Ukistaajabu ya Musa....................., Mwalimu Nyerere huko aliko naona anasikitika sana.

Mungu Tusaidie kwani hatujui tutendalo


Kazi tunayo sisi tulio bado hai maana wafu hawajui lolote....Nyerere alishafanya kazi yake hapa duniani..akaondoka kwenda kupumzika kwa amani.
 
Nimesoma kwenye gazeti moja maarufu hapa bongo wiki hii ati fedha hizo alizotafuna serikali yetu itazilipa.Jamani hii ni sawa?....na baada ya hapo itakuwaje?...sheria itachukua mkondo wake?
 
Wakati fulani, Mh Msekwa angali bado Spika alisema Bungeni kuwa huyu mama muda wake wa kuwa Rais wa PAP ulikuwa umemalizika kwa kuwa Bunge letu lilikuwa linakaribia kumaliza muda wake. Mama Mongela alikasirika huyo. Kumbe alishaanza kufisadi huko.

Halafu kama haya yanayosemwa na kuandikwa humu ni kweli, huyu mama atakuwa smart kwelikweli! Anaendesha maisha ya kawaida sana pale nyumbani kwake Makongo.
 
Ukipewa kazi ya kurina asali, mikono yako ikatapakaa asali, je utaisugua mikono kwenye vumbi ili kujisafisha au utailamba?
 
Yaani nimesikitishwa sana na habari hii. Mama yetu wewe tulitegemea ungetusaidia kulisafisha taifa letu linalonuka rushwa, wizi na ubadhilifu wa mali za uma machoni mwa mataifa ya nje kumbe imekuwa kinyume. Kw amatendo yako umeudhihirishia ulimwengu kuwa Waafrika ndivyo tulivyo wote ndugu moja. Umeudhihirishia ulimwengu kuwa Tanzania na Wanigeria hatuna tofauti yoyote zaidi ya lafudhi kwani hata rangi za bendera one can mistaken the two!!

Mama mbona umetuweka pahala pagumuu kiasi hiki? Unataka Africa ituangalieje Watanzania waliobahatika kushika nyadhifa za juu duniani? Mama Asha Rose Migizo kazi unayo, Prof. Tibaijuka (ingawa nawe nilisikia umekumbwa na kashfa) sina uhakika na hili- pole kwa aibu mliyopatiwa na Mama yetu.

Mama tulitegemea uwe mfano mzuri kwetu mambo uliyoyafanya unanifanya nifikirie aina ya uchafu na uozo uliopo katika Bunge letu tukufu maana kama wewe uliyeaminika kuwa msafi kati ya wote umeweza kuyafanya hayo huko juu, ni mangapi yanawezakufanyika na wabunge wetu huku chini?

Naililia Tanzania.
 
Kama ni za kweli..ni aibu, tena si ndogo. Jamani mwenye habari za ndani za huyu mama aziaanike hapa, maana tunaweza jua ni kwanini kafanya hivyo. Au ndo kaanza tu na kudakwa..mmh lakini hizi ni za mwizi ni arobaini. JF intelligence we need more data about this beijing icon.

CCM Chama Cha Makomunisti.Unaona hilo jembe na nyundo vilivyokuwa positioned? Wameondoa sickle wakaweka jembe.


su.gif


tz%7Dccm.gif

Kidumu Chama Cha Mapinduzi

...halafu alikuwa anautaka urais wa nchi!

Sasa pale Ikulu sijui ndio ingekuwaje kama angeupata,i'm sure yule mtoto wake ambaye ni DC Kigoma huko labda angempa ubosi wa PCB!

Jamani,hao ndio viongozi wetu...always drooling where there's $$$
Mh,

Hii imeibuka tena! Since 2007 ilikaa kimya tu...

Mnamharibia mama wakati uchaguzi umekaribia wakati yeye majuzi kasema "As PAP President, I made Tanzanian women proud"
 
Mwenyewe Agoma Kuzungumza!

Rais wa Bunge la Afrika, Mama Getrude Mongella, anatuhumiwa kutenda makosa ya kukosa uaminifu, Wizi na utoaji ajira kinyume na taratibu za kazi yake:-

1. WIZI:- anatuhumiwa kutafuna Dola za US, 138,000 ambazo ni sawa na shillingi 180Millioni za Tanzania.

2. UAJIRI:- anatuhumiwa kuajiri ndugu zake kinyume na sheria za kazi yake, akiwemo mkwe wake, yaani mke wa mtoto wake.

Katika kikao cha AU kilichopita nchini Ghana, nchi za Afrika zilimuamuru mama huyo kurudisha hela hizo mara moja huku uchunguzi ukiwa unaendelea, kikao hicho pia kilihudhuriwa na Rais Kikwete.

Mama Mongella, anatuhumiwa kujilipa US/Dola 800, kwa siku akilifanyia kazi bunge hilo la Afrika, na huku akiwalipa US/Dola 400 kwa siku ndugu zake aliowaajiri huko AU, wakati pia akilipwa na bunge la Tanzania kwa kazi hiyo hiyo. Mkwe wake mama huyu tayari ameshaachishwa kazi na bunge hilo na wengine wako njiani kurudishwa tayari Tanzania.

Katibu wa Bunge la Tanzania, ndugu Foka, alithibitisha kupata habari hizo za tuhuma dhidi ya Mama Mongella, na amekiri kwamba ni kweli Bunge letu la Tanzania limekuwa likimlipa mama huyo fedha zote anazostahili akiwa analifanyia kazi bunge la Afrika, kwa mujibu wa makubaliano na bunge hilo la Afrika, ambalo liliwaomba mwanzoni wakati anaanza kuwa liwe linamlipa ili asilipwe na bunge hilo la AU.

Taarifa za uchunguzi tayari zimefanyika na SADC, ikishirikiana na kampuni ya KP GM ya Kenya, ambazo izmeshauri mama huyo kufukuzwa kazi na kurudisha mapesa hayo kwa AU, mara moja. Mbunge mmoja wa bunge hilo la AU, Ndugu Wanyancha,(Serengeti-CCM) amekubali kuwa kweli Mama anakabiliwa nashutuma nzito sana ambazo zitatukosesha urais huo kwa muda mrefu sana ujao, juhudi zote za kuzungumza naye kuhusu hiii sualazimakwama kutokana na kukataa kwake, mama huyo.



Source: Mwana-Halisi.

Huyu mama atakuwa alijaribu kuleta kale ka mtindo ka wakina jk ( tabia za baadhi ya viongozi wa kitanzania ) ndani ya Umoja wa nchi za Kiafrika ( AU). kwa kutegemea kuna kulindana. sio kosa lake , Natumia usemi usemao....ASIYEFUNZWA NA ***** HUFUNZWA NA ULIMWENGU..

Hapa ni fundisho tosha kwa Kundi zima la kina JK kwani mtoto kaiga tabia za wazazi nyumbani. Aibu kwa taifa.tena aibu sana..

Watu wa jinsi hii huwa na wafananisha na wanafunzi wa sekondari ama vyuoni wenye tabia za kuiba nguo za ndani ( chupi ) za wanafunzi wenzao. How does it feels 😕!!!!


wizi , undugunazation, ufisadi mpaka kwenye nchi za watu ? Mwataka kwenda kula jasho la waafrika wengine pia, Hamjatosheka na jasho la watanzania tu ?

Huyu mama alitakiwa akitua tu bongo moja kwa moja na hao aliowashirikisha kwenye ulaji wahifadhiwe ndani, hata kwa mwaka mmoja tu..!
 
yeye ni kutoka katika chungu kile kile kwa hiyo kwa wanaomjua hawashangai sana
 
".......wizi , undugunazation, ufisadi mpaka kwenye nchi za watu ? Mwataka kwenda kula jasho la waafrika wengine pia, Hamjatosheka na jasho la watanzania tu ?

Huyu mama alitakiwa akitua tu bongo moja kwa moja na hao aliowashirikisha kwenye ulaji wahifadhiwe ndani, hata kwa mwaka mmoja tu..!"

__________________________________


John74e:

Nanii amhifadhi nani katika Bongo hii ya JK? Unazungumza kitu gani ndugu yangu? Ingekuwa hayo unayosema yapo akina RA, Mzee Vijisenti na wengine saa hizi wangekuwa wanakula dona.

Ndiyo maana hawa wanatamba na kuzidi kutukana Watanzania kwa kuwaamrisha baadhi ya mawaziri kuwatetea hadharani. Watanzania tunaklishwauchafu tu -- na mkuu wa kaya anaangalia, akichoka aenda majuu kuongelea masuala ya Basketball! huku mafisadi wanafanya wanavyotaka.

kikubwa tunachoona ni kesi za kisanii tu kule mahakamani -- hakuna lolote litakalopatikana.



 
Back
Top Bottom