TANZIA Mama mzazi wa Mwandishi Erick Kabendera, Verdiana Mjwahuzi amefariki dunia leo Jumanne Desemba 31, 2019

TANZIA Mama mzazi wa Mwandishi Erick Kabendera, Verdiana Mjwahuzi amefariki dunia leo Jumanne Desemba 31, 2019

Shocked!.
Kama ni kweli Eric Kabendera anashikiliwa kwa sababu ya kalamu yake hivyo hayo mengine yote ni kisingizio tuu, na yeye ndiye alikuwa tegemeo la mama yake na mama yake amefariki baada ya kukosa huduma na usongo wa mawazo wa kukamatwa kwa mwanaye, then karma ya kifo cha huyu mama itakuwa ni kubwa na haina mfano!.
Karma is real na haina mswalie Mtume.
Pole sana Eric Kabendera
Mungu akufariji na Mungu akupiganie.
P
Acha unafki basi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Aisee...R.I.P; Mungu awape nguvu familia ya marehemu. Hivi kwanini tunalazimishwa kuishi kwa huzuni na kikundi cha wachache?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kabendera nayo atakufa kwa simanzi ya mama yake..
Shocked!.
Kama ni kweli Eric Kabendera anashikiliwa kwa sababu ya kalamu yake hivyo hayo mengine yote ni kisingizio tuu, na yeye ndiye alikuwa tegemeo la mama yake na mama yake amefariki baada ya kukosa huduma na usongo wa mawazo wa kukamatwa kwa mwanaye, then karma ya kifo cha huyu mama itakuwa ni kubwa na haina mfano!.
Karma is real na haina mswalie Mtume.
Pole sana Eric Kabendera
Mungu akufariji na Mungu akupiganie.
P

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wasalam ndugu wana JF, kwa kweli nimeshtushwa sana na kifo cha huyu mama ambaye yapata mwezi tu alionekana kwenye social media akiiomba serikali kumsamehe mwanae kwani ndiye anayemtegemea kwenye matibabu yake.

Nimewaza sana juu ya mahali tulipo.
Nimewaza sana juu ya maana ya msamaha.
Nimewaza sana juu ya laana.
Nimewaza sana juu ya mateso ya kifo cha Mama Kabendera, najua hakufa kwa amani, amekufa na maumivu mazito.
Nawaza alitamka nini akilini mwake, na picha ya nani ilimjia juu ya hali aliyokuwa akiipitia mpaka kifo chake.

Mwisho katika tafakari yangu nimekuja kujikuta nimo katika maisha ya Uchina ya Mwenyekiti Mao na Korea ya Kusini yaMmwenyekiti Kim.

Nimeamka kumbe kumekucha. RIP Mama Kabendera

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakati nasoma nilihamisha mawazo yangu kwa Jezebel mkewe mfalme Ahabu alivyompiga mkwara nabii Eliya na kumkimbia mwanamke ali aokoke, hii ni jinsi waovu wanavyowakandamiza wenye haki ambao wanamtegemea Mungu
Inasikitisha sana.

Shetani anapotamalaki juu ya nchi, haki hupotea, majuto na huzuni huenea, uonevu huwa furaha ya watawala, ibilisi hufurahia uwezo wa kutwaa uhuru wa watu, machozi ya wenye haki hudondokea mavumbini, Bwana wa mbingu huruhusu ubaya udhihirike ili shetani apate kuonekana kwa uwazi. Mioyo ya wenye hekima hutiwa upofu na woga. Ibilisi hujisifia kwa mateso ya wana wa Mungu.

Naam, lakini nyakati zaja, ibilisi atakapokanyagwa na nguvu ya Mungu. Ndipo watu wote, walio wa Mungu na mawakala wa shetani, watauchukia uovu na yule bwana wa uovu, yaani shetani. Watazilaani nafsi zao maana hawakutenda lolote lililowapasa kutenda kwaajili ya utukufu wa Mungu wa kweli. Waliwaabudu wanadamu, na walijisogeza kwa ibilisi ili wajipatie mvinyo wenye ladha nzuri bila ya kujali kama mvinyo ule ulikuwa na matone ya damu na machozi ya waliodhulumiwa haki.

Pole sana wafiwa, pole sana Kabendera. Kabendera na wafiwa wote, mkumbuke kuwa katika maisha yetu wanadamu, kila litokealo, limeandikwa katika akaunti zetu za safari yetu ya maisha. Shukuruni katika kila jambo maana Mungu wetu hakuwahi kupungukiwa hekima wala ukuu wake, wala maombi ya wenye haki hayakuwahi kulikosa sikio la Mungu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haki ya kweli itapatikana Mbinguni kwa wale wanaoamini. Pumzika kwa amani Mama
 
RIP Mama.
Kiukweli muwe na akili kidogo tu, kila mama ya mtu akilia so mtuhumiwa aachiwe?
Acheni ufala nyinyi kabendera aenjoy tu makosa yake huko alipo.mahakama ndo itaamua kama kaonewa au kafanya makosa kweli
Itawezaamua bila maagizo?
 
Halafu haya majitu yanajiita viongozi wa dini badala ya kukemea haya maonevu yanakenua meno. Hasa hili li Pengo na Salum, yalaaniwe mashetani ya uwakala wa shetani eti ni viongozi wa dini!
RIP mama! Nenda kawashitaki kwa Mungu awapatilize na adhabu hapa duniani!
 
RIP Mama.
Kiukweli muwe na akili kidogo tu, kila mama ya mtu akilia so mtuhumiwa aachiwe?
Acheni ufala nyinyi kabendera aenjoy tu makosa yake huko alipo.mahakama ndo itaamua kama kaonewa au kafanya makosa kweli
Kwahiyo na wewe unaamini Erick alitakatisha pesa na kuhujumu uchumi, na upelelezi wa kesi yake ni mgumu sana kukamilika, na kwamba wako sawa wanavyoipiga danadana kesi yake? Ubarikiwe mkuu kwa mawazo yako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom