mama na mtoto wameuwawa baada ya kukutwa wakijamiiana wilayani meatu mkoani Simiyu, Tukio hilo lilitokea saa saba ya usiku juzi na mme wa marehemu kuchukua jukumu la kuwachinja chinja na kisha kutembea umbali wa kilomita 18kwenda kutoa taarifa kuwa amemchinja mke wake na mtoto wake baada ya kuwakuta wakibanjuana na kisha kusalimisha silaha alizotumia kuchinjia...binafsi nauona mwisho wa dunia hauko mbali.[/QUOTE]
Ndugu yangu Cash Wise;
Tukio hili kama umelisikia kama ambavyo nimelisikia mimi; Mzee ana miaka 69, mtoto miaka 27 na mama miaka 40. Hivyo obvious mama huyu si mama mzazi wa mtoto aliyekuwa anafanya naye mapenzi sababu ukiangalia tofauti ya umri kati yao inasema hivyo. Tatizo liko kwa mzee kwamba una miaka 69 unaoa mwanamake miaka 40 ambayo ni sawa na kusema una miaka 39 unaoa mtoto wa miaka 10! Huu ni upumbavu kwa sababu huyu ni mtoto ambaye damu yake bado inachemka, na baba kishakuwa mzee, obvoius alikuwa hamtimizii. Halafu hawa wazee wa namna hii wanakuwaga na tendency ya kuoa wake zaidi ya mmoja wakati nguvu za kufanya kazi kitandani hamna, ili mradi tu ana ng'ombe wa kwenda kutoa mahali. Ningekuwa hakimu ningehakkisha nafanya lobbying kuipata kesi hii au ku-influence hukumu yake, na ningetoa fundisho ambalo wazee wa namna hii wanotumia kiburi cha utajiri wa ng'ombe halafu baadaye wanakuja kufanya madude, kutoa adhabu ambayo wangelikubali Tanzania nzima kuwa mahakimu wapo duniani. Yaani kweli tuseme ningekuwa hakimu halafu najaliwa kumuweka kati mwenye kesi ya namna hii, watu wote wangesikia hata pale ambapo hawana masikio.
Unaamua kuchinja watu sababu ya ujinga na kiburi cha ng'ombe? Halafu wazee wa namna hii mimi nawajua, wanakuwaga na tabia ya kuthamini sana NG"OMBE KULIKO BINADAMU. Huyu anastahili kunyongwa!