Stephen Ngalya Chelu
JF-Expert Member
- Oct 31, 2017
- 8,252
- 18,335
Ni kweli Mama nyau hivi majuzi nilikuona uko na vitoto vyako vidogo viwili(vifaranga vya nyau) ulikuwa unavinyonyesha. Na baada ya muda ukaondoka ukaviacha pekeyake, mimi nikajua umevitelekeza hivyo nikavichukua na kuviweka ndani kwa sababu nawapenda nyau hasa tunyau tudogo kama huto tutoto twako.
Baada ya wewe kurudi ukavikosa vifaranga vyako ukaanza kulia unajigaragagaza chini na kuparamia maua yangu ukivililia. Nilikuonea huruma sana ila nikasema tu ngoja nikaze, nikakaza. Ukaondoka, juzi usiku ukaja ukalia usiku kucha sikulala unanisumbua unawataka wanao. Wanao wenyewe sijui ulikuwa unawanyanyasa! Kwa sababu pamoja na wewe mama nyau kuwalilia wenyewe walikuwa hawana hata mpango na wewe, walikuwa wanetulia tu kimya. Jana usiku ukaja tena kunisumbua nikaona isiwe tabu nikafungua mlango ukaingia sebuleni na vitoto vyako vikatoka chumbani kwangu vikakufuata na kwa macho yangu nilikuoneni mnatoka nje mkiwa mmeongozana na tunyau twako. Nikafunga mlango nikalala nikiwa najua kuwa tatizo limekwisha.
Nashangaa tena, alfajiri ya leo masaa machache tu baada ya wewe na vitoto vyako kuondoka umerudi ukiwa pekeyako unalia tena. Kwani nini tatizo, vitoto vyako si nilikupa ukaenda navyo? Kama vimekutoroka huko mlikokwenda basi ni uzembe wako na havijarudi kwangu tena. Naona unanitazama kwa jicho kali ila ukweli ndo huo mama nyau, mimi siko na wanao tena. Nimechoka na makelele yako ukiendelea kunisumbua nitakuonyesha kazi.
Cc: Mama nyau
Baada ya wewe kurudi ukavikosa vifaranga vyako ukaanza kulia unajigaragagaza chini na kuparamia maua yangu ukivililia. Nilikuonea huruma sana ila nikasema tu ngoja nikaze, nikakaza. Ukaondoka, juzi usiku ukaja ukalia usiku kucha sikulala unanisumbua unawataka wanao. Wanao wenyewe sijui ulikuwa unawanyanyasa! Kwa sababu pamoja na wewe mama nyau kuwalilia wenyewe walikuwa hawana hata mpango na wewe, walikuwa wanetulia tu kimya. Jana usiku ukaja tena kunisumbua nikaona isiwe tabu nikafungua mlango ukaingia sebuleni na vitoto vyako vikatoka chumbani kwangu vikakufuata na kwa macho yangu nilikuoneni mnatoka nje mkiwa mmeongozana na tunyau twako. Nikafunga mlango nikalala nikiwa najua kuwa tatizo limekwisha.
Nashangaa tena, alfajiri ya leo masaa machache tu baada ya wewe na vitoto vyako kuondoka umerudi ukiwa pekeyako unalia tena. Kwani nini tatizo, vitoto vyako si nilikupa ukaenda navyo? Kama vimekutoroka huko mlikokwenda basi ni uzembe wako na havijarudi kwangu tena. Naona unanitazama kwa jicho kali ila ukweli ndo huo mama nyau, mimi siko na wanao tena. Nimechoka na makelele yako ukiendelea kunisumbua nitakuonyesha kazi.
Cc: Mama nyau