Mama unayefungua nchi muandikie Barua Rais huyu atutembelee anamashabiki wengi Tanzania na jina tumempa

mtwa mkulu

JF-Expert Member
Joined
Sep 11, 2013
Posts
8,586
Reaction score
11,227

Tanzania ni taifa rafiki na babu yake mzee Kim il sun na kumbukumbu zake nyingi sana za utawala wa Juche zipo maktaba ya kibaha. Karibu Tanzania Kim jong kiduku un
 
Hayati Kim il sung, alikuwa ni rafiki mkubwa wa mwl. Jkn, vitabu vya North Korea vilijaa kweli Tanzania, hasa vikionyesha harakati za kilimo, hawa jamaa walijibidisha na kilimo toka zamani mno, nakumbuka mzee wangu kwenye shelf za vitabu vyake almost nusu ya shelf ilijazwa vitabu vya Kim il sung.
 
Kuwa na marafiki wa ajabu ajabu ni mojawapo ya mambo yaliyochangia umaskini wa taifa letu.
 
Sema vinachosha kusoma asikwambie mtu
 
Aje kufanya nini hamna hata Dira kama Taifa, na kibaya zaidi hana mpango wa kuiba rasirimali za nchi masikini kama yale Ma ubwa USA
 
View attachment 2900658
Tanzania ni taifa rafiki na babu yake mzee Kim il sun na kumbukumbu zake nyingi sana za utawala wa Juche zipo maktaba ya kibaha. Karibu Tanzania Kim jong kiduku un

Huwa nachoka nikisikia Tanzania ni rafiki sijui wa Korea ama China. Viongozi wakikutana na kusalimiana kwa tabasamu ndio mnasema hizo nchi ni marafiki! Hebu nenda North Korea kisha jitambulishe kuwa ww ni mtanzania, uone hata kama wanaijua Tanzania, au watakufagilia kama rafiki. Acheni story za kulazimisha urafiki usiokuwepo.
 
Tunavyo kwambia ni marafiki tunamaanishaa... nikupe tu mfano ujamaa wa Tanzania uliitwa ujamaa na kujitegemea wakati wa korea uliitwa Juche means kujitegemea!
 
Ndio maana hata ww unasujudu siasa za kiduwanzi, kumbe una asili nazo!
 
Tunavyo kwambia ni marafiki tunamaanishaa... nikupe tu mfano ujamaa wa Tanzania uliitwa ujamaa na kujitegemea wakati wa korea uliitwa Juche means kujitegemea!
Tanzania Kuna ujamaa boss?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…