Mambo 10 yaliyofanywa na Rais Samia yanayowagusa Walimu na Jamii kwa ujumla

Mambo 10 yaliyofanywa na Rais Samia yanayowagusa Walimu na Jamii kwa ujumla

Nyabukika

JF-Expert Member
Joined
Jun 15, 2022
Posts
1,440
Reaction score
1,046
Siku ya jana katika kuadhimisha siku ya walimu Duniani, nimekutana na jumbe nyingi zinazoonyesha uelewa wa Watanzania juu ya kazi ya utekelezaji wa miradi katika Elimu inayofanywa kwa weledi chini ya Uongozi wa serikali ya awamu ya sita, tuangazie baadhi ya mambo;

1.Ujenzi wa Shule mpya za sekondari na shule ya msingi zipatazo 266.

2. Ujenzi wa vyumba vipya vya madarasa ya shule za msingi, vituo shikizi, na shule za sekondari vipatavyo 18,219.

3. Ukamilishaji wa ujenzi wa vyumba vya madarasa shule za msingi na sekondari vipatavyo 4,525.

4. Ukamilishaji ujenzi wa vyumba vya maabara vipatavyo 1,399.

5. Ujenzi wa matundu ya vyoo kwa shule za msingi na sekondari yapatayo 568.

6. Ujenzi wa mabweni kwa shule za msingi na sekondari yapatayo 170.

7. Ujenzi wa nyumba za walimu wa shule za msingi na sekondari zipatazo 42.

8. Kutolewa ajira za walimu wapatao 9800 wa kada tofauti tofauti.

9. Watumishi katika wizara ya Elimu kwa maana ya walimu, waratibu wa Elimu na Maafisa Elimu kulipwa malimbikizo na madai yao yote yaliyohakikiwa.

10. Kutolewa fedha za Mikopo ya Elimu ya juu na kuondolewa kwa tozo ya VRF kiasi cha asilimia 6 kwa wanufaika wa Bodi ya Mikopo.

Rais Samia Suluhu anachapa kazi na anastahili pongezi za dhati, kama mwananchi mwenye kujitambua nitaendelea kushiriki ujenzi wa Taifa langu kwa vitendo.
 
Siku ya jana katika kuadhimisha siku ya walimu Duniani, nimekutana na jumbe nyingi zinazoonyesha uelewa wa Watanzania juu ya kazi ya utekelezaji wa miradi katika Elimu inayofanywa kwa weledi chini ya Uongozi wa serikali ya awamu ya sita, tuangazie baadhi ya mambo;

1.Ujenzi wa Shule mpya za sekondari na shule ya msingi zipatazo 266.

2. Ujenzi wa vyumba vipya vya madarasa ya shule za msingi, vituo shikizi, na shule za sekondari vipatavyo 18,219.

3. Ukamilishaji wa ujenzi wa vyumba vya madarasa shule za msingi na sekondari vipatavyo 4,525.

4. Ukamilishaji ujenzi wa vyumba vya maabara vipatavyo 1,399.

5. Ujenzi wa matundu ya vyoo kwa shule za msingi na sekondari yapatayo 568.

6. Ujenzi wa mabweni kwa shule za msingi na sekondari yapatayo 170.

7. Ujenzi wa nyumba za walimu wa shule za msingi na sekondari zipatazo 42.

8. Kutolewa ajira za walimu wapatao 9800 wa kada tofauti tofauti.

9. Watumishi katika wizara ya Elimu kwa maana ya walimu, waratibu wa Elimu na Maafisa Elimu kulipwa malimbikizo na madai yao yote yaliyohakikiwa.

10. Kutolewa fedha za Mikopo ya Elimu ya juu na kuondolewa kwa tozo ya VRF kiasi cha asilimia 6 kwa wanufaika wa Bodi ya Mikopo.

Rais Samia Suluhu anachapa kazi na anastahili pongezi za dhati, kama mwananchi mwenye kujitambua nitaendelea kushiriki ujenzi wa Taifa langu kwa vitendo.
11.Nimefaidika kupandishwa daraja
na hiyo VRF ya Heslb.
Ameteleza kwenye ile 23% ....but anaweza kurekebisha bado.Muda upo kama ana nia.
 
Ukiona wadau wapo kimya kwa hili, jua kuna la kujifunza!!!??
 
11.Nimefaidika kupandishwa daraja
na hiyo VRF ya Heslb.
Ameteleza kwenye ile 23% ....but anaweza kurekebisha bado.Muda upo kama ana nia.
Lengo la Rais Samia Suluhu ni kutoa elimu bure na iliyo bora ndio maana unaona ameipa sekta ya elimu kipaumbele na anaendelea na utakelezaji
 
Siku ya jana katika kuadhimisha siku ya walimu Duniani, nimekutana na jumbe nyingi zinazoonyesha uelewa wa Watanzania juu ya kazi ya utekelezaji wa miradi katika Elimu inayofanywa kwa weledi chini ya Uongozi wa serikali ya awamu ya sita, tuangazie baadhi ya mambo;

1.Ujenzi wa Shule mpya za sekondari na shule ya msingi zipatazo 266.

2. Ujenzi wa vyumba vipya vya madarasa ya shule za msingi, vituo shikizi, na shule za sekondari vipatavyo 18,219.

3. Ukamilishaji wa ujenzi wa vyumba vya madarasa shule za msingi na sekondari vipatavyo 4,525.

4. Ukamilishaji ujenzi wa vyumba vya maabara vipatavyo 1,399.

5. Ujenzi wa matundu ya vyoo kwa shule za msingi na sekondari yapatayo 568.

6. Ujenzi wa mabweni kwa shule za msingi na sekondari yapatayo 170.

7. Ujenzi wa nyumba za walimu wa shule za msingi na sekondari zipatazo 42.

8. Kutolewa ajira za walimu wapatao 9800 wa kada tofauti tofauti.

9. Watumishi katika wizara ya Elimu kwa maana ya walimu, waratibu wa Elimu na Maafisa Elimu kulipwa malimbikizo na madai yao yote yaliyohakikiwa.

10. Kutolewa fedha za Mikopo ya Elimu ya juu na kuondolewa kwa tozo ya VRF kiasi cha asilimia 6 kwa wanufaika wa Bodi ya Mikopo.

Rais Samia Suluhu anachapa kazi na anastahili pongezi za dhati, kama mwananchi mwenye kujitambua nitaendelea kushiriki ujenzi wa Taifa langu kwa vitendo.
Wewe jamaa unachekesha sana! Yaani kujengwa kwa vyumba vya madarasa ndiyo kunamsaidia mwalimu!

Zimejengwa nyumba 42 katika shule ngapi nchini? Hizo nyumba 42 zimetatua changamoto ya ukosefu wa nyumba za walimu kwa asilimia ngapi? Eti ujenzi wa matundu ya vyoo! Umewaona hao walimu wanapenda sana kukata gogo siyo!!!

Mkubali tu serikali yenu ya ccm kwa sasa inatembelea tu mbeleko ya policcm na tumeccm wenu! Kinyume na hapo mngebakia kuwa historia. Chama chenu kimewekeza nguvu kubwa kwenye ufisadi, rushwa, na kulindana nyinyi kwa nyinyi.
 
Wewe jamaa unachekesha sana! Yaani kujengwa kwa vyumba vya madarasa ndiyo kunamsaidia mwalimu!

Zimejengwa nyumba 42 katika shule ngapi nchini? Hizo nyumba 42 zimetatua changamoto ya ukosefu wa nyumba za walimu kwa asilimia ngapi? Eti ujenzi wa matundu ya vyoo! Umewaona hao walimu wanapenda sana kukata gogo siyo!!!

Mkubali tu serikali yenu ya ccm kwa sasa inatembelea tu mbeleko ya policcm na tumeccm wenu! Kinyume na hapo mngebakia kuwa historia. Chama chenu kimewekeza nguvu kubwa kwenye ufisadi, rushwa, na kulindana nyinyi kwa nyinyi.
Acha makasiliko ndugu walimu wameboreshewa mazingira ya utendaji kazi sio kama zamani na utekelezaji unaendelea kwaiyo acha makasiliko angalia maendeleo yanayofanya na serikali yako
 
Acha makasiliko ndugu walimu wameboreshewa mazingira ya utendaji kazi sio kama zamani na utekelezaji unaendelea kwaiyo acha makasiliko angalia maendeleo yanayofanya na serikali yako
Huwezi kuboresha mazingira ya utendaji kazi kwa mwalimu kupitia ujenzi wa vyumba vya madarasa na kuongeza matundu ya vyoo. Hapo umeboresha mazingira ya watoto kutoka familia duni kusoma kwenye hizo shule zenu za kata mlizo zijenga kisiasa!

Mkitaka kuboresha mazingira bora ya utendaji kazi kwa walimu; waongezeeni mishahara, wajengeeni nyumba bora za kuishi, boresheni ofisi zao wanazo fanyia kazi! Walipeni posho za mazingira magumu ya kazi (kwa walimu wa vijijini), wapandisheni madaraja yao kwa wakati!

Toeni ajira kwa maelfu ya wahitimu wa fani ya ualimu wanao hangaika mitaani kwa miaka nenda sasa, ili kuwepo na uwiano sahihi kati ya mwalimu ma mwanafunzi! Wapeni walimu mafunzo ya mara kwa mara kwa masomo yote ili kuongeza tija ya ufundishaji, wapeni motisha wanapofanya vizuri! Nk. Ila siyo kujenga vyumba vya madarasa na matundu ya choo, halafu mnajipongeza kuboresha maisha ya walimu!
 
Huwezi kuboresha mazingira ya utendaji kazi kwa mwalimu kupitia ujenzi wa vyumba vya madarasa na kuongeza matundu ya vyoo. Hapo umeboresha mazingira ya watoto kutoka familia duni kusoma kwenye hizo shule zenu za kata mlizo zijenga kisiasa!

Mkitaka kuboresha mazingira bora ya utendaji kazi kwa walimu; waongezeeni mishahara, wajengeeni nyumba bora za kuishi, boresheni ofisi zao wanazo fanyia kazi! Walipeni posho za mazingira magumu ya kazi (kwa walimu wa vijijini), wapandisheni madaraja yao kwa wakati!

Toeni ajira kwa maelfu ya wahitimu wa fani ya ualimu wanao hangaika mitaani kwa miaka nenda sasa, ili kuwepo na uwiano sahihi kati ya mwalimu ma mwanafunzi! Wapeni walimu mafunzo ya mara kwa mara kwa masomo yote ili kuongeza tija ya ufundishaji, wapeni motisha wanapofanya vizuri! Nk. Ila siyo kujenga vyumba vya madarasa na matundu ya choo, halafu mnajipongeza kuboresha maisha ya walimu!
Inaonekana una uhaba wa taarifa mzee kuna ajira za walimu zaidi ya elfu 42 zimepitishwa pia utendaji kazi wa walimu umeboreshwa kwa kujengewa nyumba pia posho za walimu zinatolewa kwa wakati na bado mama anaendelea na uboreshaji
 
Inaonekana una uhaba wa taarifa mzee kuna ajira za walimu zaidi ya elfu 42 zimepitishwa pia utendaji kazi wa walimu umeboreshwa kwa kujengewa nyumba pia posho za walimu zinatolewa kwa wakati na bado mama anaendelea na uboreshaji
Hamna uwezo wa kuajiri walimu elfu 42! Aliyethubutu kufanya hivyo ni JK peke yake.
 
Hakuna cha uchawa hapa zaidi ni kua mzalendo na kufatilia maendeleo makubwa yanayofanywa na serikali ya awamu ya sita
Working class asiyejua on the ground kuko vipi, kama utasoma hii muda huu fungulia TV,UTV uone na kusikia kutoka kwa aliyekua Rais wa Chama cha waalimu, facts kuhusu waalimu ikiwa ni pamoja na ulinganishi na waalimu wa nchi jirani, unafikiri why SA imechukua waalimu wa kenya kwenda kufundisha kiswahili kule?,why Rwanda iende Zimbabwe kubeba waalim wa kufundisha kiingereza kwao?,after all ualimu kwangu ni wanafiki tu
 
Ukweli mimi nimeona madarasa ya covid19 tu. Hayo mengine yapo mkoa gani?
 
Back
Top Bottom