Mambo gani umeyafanya au kuyapitia maishani mwako ambayo hutamani mwanao/mtu mwingine kuyapitia?

Mambo gani umeyafanya au kuyapitia maishani mwako ambayo hutamani mwanao/mtu mwingine kuyapitia?

Sitapenda Mtu yoyote wa kizazi changu akatae Shule.
Avute sigara au Bangi.
Anywe Pombe.
Akose utiifu kwa Wazazi,hasa Mama yake.
Alale na Wanawake watu wazima.

Nimechora mstari mwekundu kwa hayo.
Sitaki Wanangu warudie makosa yangu.
Mkuu hebu fafanua hapo kwenye kulala na wanawake watu wazima
 
Kubeti na pombe.
Pombe nakunywa hadharani ila kubeti najificha na huwa nawasema vibaya sana wanaobeti kukiwa na hiyo mada.
Sema kuna siku nabahatisha nambutua kanjibai lakini na kipigo hakiepukiki.
Sitaki kabisa mwanangu aige au ajue kuwa mimi baba yake nabeti.
Kamari ni ulevi wa siri sana, yaani hata mkeo hawezi kujua kama unabeti.Huwezi amini hadi mapadri na masheikh wanabeti. Ni ulevi uliorahisishwa kiganjani.

Zamani ilikuwa ukitaka kucheza kamari ni lazima uende kwenye vijumba vya wahuni wa korokoro (dice games) au zile za karata.Ulikuwa ukionekana ni mchezo mahususi kwa vibaka, wahuni,walevi na watu waliokata tamaa na maisha.

Ila kuanzia hii miaka ya 2008 huu ulevi umerasimishwa na kuwa accessible kwa kila mtu ,kila rika. Yaani hadi wazee unakuta wanabeti.

Majuzi nimeingia katika betting shop ya throne bet kucheki mechi ,nikamkuta mlemavu ambae anaomba omba njiani nae yumo humo anasuka mikeka ili abeti.

Hili ni janga kwa kweli
 
Sitaki mwanangu awe polisi kwani walishanifanyia vitendo vibaya tena mbele ya watoto wangu,nilipigwa vibao mbele yao wakawa wanalia,nilijikakamua na kuleta noma ambayo hao PT hawatasahau maishani mwao kwani si mwenye jicho, jino,uso kilichotoka salama,ilinigharamu sana baada ya hapo but nilirudisha heshima kwa wanangu.Toka siku hiyo niliwaambia siku niko hai au nimekufa nikisikia mmojawenu amekuwa polisi namlaani.Sumu ambayo nimewalisha sidhan kuna mwanangu anaweza kuwa PT
NYINGINE :Sitaki wanangu wanywe pombe hata kwa kuonja hili ni somo ambalo nawambia kila nikiwa nao,mie bado nakunywa na wameshuhudia madhara ya pombe kupitia kwangu,sidhani km wanaweza kunywa maishani mwao,pombe imenipotezea kazi za maana kama mara 3 nikawa takakata,nina kazi sasa naitunza km yai wanangu wameona ni jinsi kipindi cha pombe kupita kiasi kilivokuwa na kipindi cha sasa pombe za wastani kilivo
Kuwausia watoto ni jambo jema sana
 
Sitampangia mwanangu cha kufanya, atafanya anachopenda mradi havunji sheria. Ninaposema cha kufanya namaanisha shughuli ya kumuingizia kipato
Hatuzungumzii kuhusu kumpangia bali kumuhusia mambo ambayo yamekugharimu wewe katika maisha yako hivyo hutaki kuona mwanao nae anayapitia
 
Yani kuna watu wanabeti hadi wanakonda
Acha tu mzee.....hili ni janga. Hakuna ulevi mzuri, kubeti ni ugonjwa wa akili ambapo mbetiji hujawa na false hopes daily kuwa atafanikiwa kupitia kamari.
 
Hatuzungumzii kuhusu kumpangia bali kumuhusia mambo ambayo yamekugharimu wewe katika maisha yako hivyo hutaki kuona mwanao nae anayapitia
Ndio sitampangia kwa sababu sitaki apitie niliyopitia mimi kwa sababu ya kupangiwa
 
Now nimekuelewa...yeah wengi wameharibikiwa maishani kutokana na kupangiwa/ kushurutishwa kufanya mambo fulani (ndoa,elimu, kazi n.k) baadae wamejikuta wakiishi maisha yasiyo na furaha
Ndio sitampangia kwa sababu sitaki apitie niliyopitia mimi kwa sababu ya kupangiwa
 
Growing up without a Mom. I always pray that nitawalea watoto wangu wakue na kupata akili za kujisimamia wenyewe. I dont know how to put that better.

I am a doting Mom, I miss my own Mom and I hope am half the woman she was.
 
Mkuu hebu fafanua hapo kwenye kulala na wanawake watu wazima

Ni kwamba hakuna faida yoyote anayoipata kijana mdogo kulala na mwanamke anayeweza kumzaa.

Kwa kipindi kifupi unaweza kufurahia lakini majuto yake hayaishi.

Mbaya zaidi ni Uraibu mkubwa.

Hii tabia ni ngumu kuacha.

Kuna mambo unaweza kuyafanya ukiwa kijana mdogo na ukajiona uko sahihi sana,lakini unapopevuka unagundua kuwa ulifanya makosa makubwa.

Na inakuwa too late to correct,hayo majuto ndio mimi siyataki.
 
Back
Top Bottom