Mambo haya hutafunzwa shuleni katu........

Mambo haya hutafunzwa shuleni katu........

boniuso

JF-Expert Member
Joined
Mar 13, 2013
Posts
786
Reaction score
1,043
VITU 4 AMBAVYO HUFUNDISHWI SHULENI LAKINI NI MUHIMU MAISHANI MWAKO

Shuleni watu hufundishwa kufanikiwa tu ila hakuna somo la kumuelekeza mtu afanye nini anapokuwa katika nyakati ngumu sana

Kila mtu amekaririshwa kuwa soma sana,faulu utapata kazi nzuri kisha utakuwa na maisha mazuri

Hivyo kila mtu husoma na kufanya kazi kwa bidii sana ili afanikiwe kuwa na maisha mazuri

Endapo hatapata maisha mazuri ataona hakuna thamani ya kwenda shule hivyo kwake shule haina maana

Unatakiwa utambue kuwa kama hutojifunza kwenye historia unakwenda kurudia makosa ya watangulizi wako

Unaweza kukumbuka mwaka ambao maisha yalikuwa mazuri nchi nzima kwamba kila mtu ni mwenye afya,hana kesi,hana madeni,kila mtu maisha mazuri sherehe kila nyumba ?

Haijawahi kutokea na haiwezi kutokea hivyo tuache kujidanganya bali tuangalie maisha katika uhalisia sio kuwapa watu matumaini ya uongo

Ukweli ni kuwa maisha bila matatizo hayana maana hivyo kwa sababu watu wengi hawataki matatizo hivyo huteseka kwa kila tatizo

Madaktari wasome ili iweje kama hakuna wagonjwa ?

Watu waende jeshini ili iweje kama upo usalama kila kona

Watu watafute walinzi wa mageti ili iweje kama hakuna uhalifu?

Maana yake ujiandae na matatizo au usijiandae lazima utapata matatizo tu

Matatizo ni kama mvua hivyo itanyesha kwa watu wote ila kila mmoja ataona uzuri wa mvua au ubaya wa mvua ila mvua ipo palepale

Ndiyo sawa na matatizo kwako utaona sio tatizo kwa mwengine ataona ni tatizo maana yake maisha hayawezi kuwa fair kwa kila mtu.

Mambo 4 shule huwezi kufundishwa ni

1.KUKABILIANA NA NYAKATI NGUMU
Watu wengi hufanya vizuri shuleni lakini hawana elimu ya kuibuka baada ya kuanguka

Wengi wanajua fanya kazi kwa bidii kisha utapanda vyeo na kuwa na mshahara mzuri hivyo utakuwa na maisha mazuri sana

Tatizo ni kwamba hakuna anaewafundisha kuwa ukifanya kazi kwa bidii sana na usipopanda vyeo ufanye nini?

Wengi huambiwa wakiwa na bidii kazini ndio watadumu kazini lakini hakuna mwenye kuwaambia kuwa kampuni inaweza kupunguza wafanyakazi wake kama haipati faida bila kujali juhudi za wafanyakazi

Endapo utapata matatizo na hukujiandaa kuyapokea lazima utapata msongo wa mawazo

Wafanyakazi wengi maofisini huwezi kuwaona wanatabasamu muda wote wamenuna mpaka unaogopa kuwauliza chochote wengi huona ni jambo la kawaida

Hakuna mtu ambaye yupo kawaida muda wote amenuna

Ukiona mtu amenuna kuna kitu hakipo sawa

2.KUKATALIWA NI KAWAIDA
Haijalishi umesoma kwa kiwango gani lazima utakataliwa tu

Hakuna mtu mzuri kwa 100% au mbaya kwaa 100%

Wapo hujiua tu kisa marafiki zao wamepata kazi yeye amekosa

Wapo huamua kuwa walevi kisa tu wamekosa ajira

Wapo huamua kuishi kwa kulalamika kisa ajira hamna

Wapo hujidhuri kisa talaka
Wapo husomesha wachumba zao kisha wakiambiwa hakuna ndoa huamua kuwaua wachumba zao kisa kukataliwa

Lazima utambue kuwa utakataliwa sana labda usiombe chochote kwa mtu yeyote

Kwenye kukataliwa hakuna msomi,tajiri, maskini, Handsome, beautiful,mzuri wa sura au mbaya
Mwenye muonekano mzuri au mbaya

Hakuna cha rangi,urefu,ucheshi,upole wala kipaji bila kujali upoje lazima utakataliwa sana katika maisha yako kuliko kukubaliwa

Sehemu kubwa ya maisha ni maumivu na sehemu ndogo tu ndio sherehe

Ndio maana unasoma miaka 4 sekondari lakini graduation ni siku moja tu

Kama hukujiandaa kupokea taarifa mbaya lazima utateseka sana

3.NAMNA YA KUPOKEA TAARIFA MBAYA
Hakuna somo la kukuelewesha namna ya kupokea taarifa mbaya kama kifo,ajali,talaka,ugomvi,namna ya kuishi na watu wenye tabia tofauti na zako

Hakuna mwenye kukufahamisha kuwa maishani mwako utapata matatizo bali utaambiwa ukisoma sana ndio unakuwa na maisha mazuri

Ukweli ni kuwa huwezi kuepuka matatizo na endapo huwezi kutatua matatizo katika maisha yako ni wewe tu unaekwenda kuteseka

4.NAMNA YA KUBADILIKA KUENDANA NA MAZINGIRA
Shuleni mnaweza kusoma somo moja baba na mtoto notes zilezile na nyote mkapewa vyeti lakini katika maisha hakuna kitu kama hicho

Mnaweza kuwa na tatizo moja lakini kila mmoja akatumia njia tofauti
Shule ulijibu swali tofauti na mwalimu alivyokuelekeza unakosa hata kama umekesha unasoma

Katika maisha ni kuwa hakuna maelekezo ya namna ya kuishi bali unaishi kuendana na wakati uliopo

Huku unakosea kwanza ndio unajifunza ila shule unajifunza kwanza kisha unapewa mtihani na mtihani lazima uwe katika silabasi

Matatizo ya kwenye maisha hayana silabasi

Huku unaweza kuzaliwa katika familia ya kitajiri baba yako akafa na ndugu wakachukua mali zote ukaishi maisha ya kimaskini

Unaweza zaliwa katika maisha mazuri lakini ukapoteza kila kitu na usijue pa kuanzia

Huku hakuna kuanza shule ni miaka 7 huku unaweza kuwa na miaka 23 ukapata matatizo ambayo alitakiwa kupata mzee wa miaka 60 lakini bado unatakiwa uyatatue

Lazima ujue kuwa ahadi kuvunjwa ni kawaida,unaowaamini kukugeuka ni kawaida

Unaowadai kukunyima pesa kawaida

Unaowasaidia kukuacha mpweke wakati mgumu ni kawaida

4.MAISHA SIYO VILE UNAPANGA WEWE
Kukosolewa ni kawaida
Watu kukuchukia ni kawaida
Watu kukushangilia leo na kesho kukuzomea ni kawaida

Kanuni mbili za kukusaidia ukiwa na matatizo

1. Accept Whatever comes to your life
Pokea chochote kinachotokea katika maisha yako bila kukasirika kwa sababu kukasirika sio suluhisho la matatizo yako

"Train your mind to accept disappointment because they will come from people you trusted most"
2.Change what you can and let go what you can't change
Kubali kuwa kile huwezi kukibadilisha sio jukumu lako kujitesa juu yake

Huwezi kupanga fursa gani zije kwako ila unapanga ufanye nini kwa fursa zinazokuja kwako

Huwezi kufuta historia yako bali unaweza kuandika historia mpya

Kujitesa kwa makosa ya zamani ni kupoteza muda

Huwezi kuifanya jana irejee na fursa za jana zirejee bali unaweza kuwekeza nguvu zako kwa fursa mpya

Kupata kitabu cha
1.FIKRA ZAKO FURAHA YAKO (softcopy)
2TIBA YA MSONGO WA MAWAZO (hardcopy & softcopy)
3.BADILI FIKRA ZAKO BADILI MAISHA YAKO (hardcopy & Softcopy)
4.MALEZI YA UBONGO KISAYANSI( hardcopy & softcopy)
5.TABIA ZA WATU WALIOFANIKIWA (Hardcopy & softcopy)

6 MISINGI 10 YA FURAHA SIKU ZOTE (hardcopy &softcopy)

+255766862579
+255622414991

Imeandikwa na Psychologist
Said Kasege
Temeke,Dar es salaam
 
Maisha Kama trekta hata ulijengee lami LAZIMA lirukeruke,

Niliamini maisha hayatulii kwa kiumbe hai baada ya kufunga ndoa ambayo kwa Sasa ni mfu. na baada ya kununua Gari kwa Mara ya kwanza, hapo kabla nilijua nitapata furaha ya kudumu nikitimiza hizo ndoto zangu, kumbeee wapi.

Now Ibelive life is unpredictable, More money More problem.
 
Maisha Kama trekta hata ulijengee lami LAZIMA lirukeruke,

Niliamini maisha hayatulii kwa kiumbe hai baada ya kufunga ndoa ambayo kwa Sasa ni mfu. na baada ya kununua Gari kwa Mara ya kwanza, hapo kabla nilijua nitapata furaha ya kudumu nikitimiza hizo ndoto zangu, kumbeee wapi.

Now Ibelive life is unpredictable, More money More problem.
Ndiomana kuna watu wanaamin sio sisi tunachagua maisha, yanatuchagua yenyewe kwanza. Ndiomana hata wazaza hukuwachagua wew. Happiness is not a station you arrive but a manner of travelling.
 
Back
Top Bottom