Mambo Haya Kumi (10) Usiyojua Kuhusu Fedha Ndiyo Yanakufanya Uendelee Kuwa Masikini.

Mambo Haya Kumi (10) Usiyojua Kuhusu Fedha Ndiyo Yanakufanya Uendelee Kuwa Masikini.

Hongera sana ndugu! kwa hatua uliyoifikia,
Nakupa pongezi kubwa sana, ila pia nina ushauri kwako,

Kwa ambao huwa wanasoma vitabu kwa hayo uliyoyaandika hapo juu nikwamba tumesoma tayari kitabu kizima,
Bado hatujakutana na wazo jipya, hata kama hakuna mawazo mapya basi sijapata ushawishi sababu naona mbona sina kipya cha kujifunza?
Ushauri wangu tumia lugha zaidi ya uandishi kuliko lugha ya maelezo,
Hata kama nikiwa na majibu yakwamba yai litachemsha ila bado nahitaji kujiuliza litachemshwaje? hii ndio point yangu

Zingatia lugha ya uandishi zaidi ongeza na sanaa yako basi utafanya makubwa zaidi, ila hongera sana kwa ulilolifanya
 
Hongera sana ndugu! kwa hatua uliyoifikia,
Nakupa pongezi kubwa sana, ila pia nina ushauri kwako,

Kwa ambao huwa wanasoma vitabu kwa hayo uliyoyaandika hapo juu nikwamba tumesoma tayari kitabu kizima,
Bado hatujakutana na wazo jipya, hata kama hakuna mawazo mapya basi sijapata ushawishi sababu naona mbona sina kipya cha kujifunza?
Ushauri wangu tumia lugha zaidi ya uandishi kuliko lugha ya maelezo,
Hata kama nikiwa na majibu yakwamba yai litachemsha ila bado nahitaji kujiuliza litachemshwaje? hii ndio point yangu

Zingatia lugha ya uandishi zaidi ongeza na sanaa yako basi utafanya makubwa zaidi, ila hongera sana kwa ulilolifanya
Asante kwa ushauri,
Kitu kikubwa ambacho naamini ni kwamba kila mtu ana kitu cha kujifunza kwenye kila kitu.
Hivyo kama umesoma maelezo hayo na ukaona hakuna cha kipya cha kujifunza, maana yake wewe siyo mtu wa kujifunza na hilo linaweza kuwa kikwazo kwako kupiga hatua zaidi ya pale ulipo sasa.
Mimi binafsi huwa nasoma vitabu nilivyoandika mwenyewe, na kila ninaposoma kuna kitu kipya najifunza, kuna mawazo mapya yanaunganika na siwezi kumaliza kusoma na nikabaki kama nilivyokuwa.
Na pia kuna baadhi ya vitabu ambavyo huwa nimechagua kusoma kwa kuvirudia rudia, vingine nimeshasoma zaidi ya mara kumi, lakini kila nikirudia kusoma kuna kitu kipya naondoka nacho, ambacho awali sikukipata au kukielewa vizuri.
Hivyo nikukaribishe ujipatie kitabu na ujifunze na kwa hakika kuna mapya utaondoka nayo, ambayo kama utakwend akuyafanyia kazi basi hutabaki pale ulipo sasa.
Karibu sana.
 
Uncle Sam system
Rafiki yangu mpendwa,

Tangu tunazaliwa mpaka tunakuwa watu wazima, kuna vitu vingi sana ambavyo tunafundishwa kwenye familia, kwenye jamii, shuleni na hata kwenye kazi au biashara.

Tunafundishwa jinsi ya kwenda vizuri na watu wengine, jinsi ya kufanya kazi au biashara zetu na umuhimu wa kufuata sheria mbalimbali. Yote haya yanalenga kutufanya kuwa watu wazuri kwenye jamii na kufanya shughuli zetu vizuri.

Lakini ipo elimu moja muhimu sana ambayo tunaikosa, elimu hii ambayo ndiyo inashika eneo kubwa la maisha yetu, hatuipati kwenye familia, hatuipati kwenye jamii, wala shuleni au kwenye kazi na biashara.

Elimu hii muhimu ambayo tumekuwa tunaikosa ni kuhusu fedha. Tumekuwa tunafundishwa mambo mengine yote, lakini inapokuja kwenye fedha, hakuna anayechukua muda wake kutufundisha. Na ni kwa sababu hata hao waliotutangulia hawakupata nafasi ya kufundishwa.

Hivyo chochote tunachojua kuhusu fedha imekuwa ni kwa kuiga. Tunaangalia wengine wanafanya kwa upande wa fedha na sisi tunafanya hivyo. Na haishangazi kwa nini watu wengi wana matatizo ya kifedha.

Nenda eneo lolote la kazi, na utakuta karibu wafanyakazi zote, moja mishahara yao haikutani, mbili, wana madeni. Hapo ni eneo la kazi ambapo watu wana mishahara tofauti, wapo wenye mshahara kidogo na wengine wenye mshahara mkubwa. Kinachoshangaza, wote wanaishia kuwa na matokeo sawa kifedha.

Rafiki yangu mpendwa, kwa kuona ukosefu mkubwa wa elimu hii muhimu ya fedha, na kwa kuona jinsi ambavyo watu wengi wanateseka inapokuja kwenye swala la fedha, nimetafiti kwa kina eneo hili na kuandika kitabu kinachoitwa ELIMU YA MSINGI YA FEDHA (BASIC FINANCIAL EDUCATION).

elimu fedha 2


Hii ni elimu ya msingi kabisa ya kifedha ambayo ukipaswa upewe kwenye familia, kwenye jamii, shuleni na hata kwenye kazi au biashara. Lakini hakuna anayekupa elimu hiyo. Mimi kocha wako, kwa sababu najali sana kuhusu wewe, na kwa sababu kazi yangu kubwa ni wewe, nimekuandalia elimu hii kwa njia rahisi sana kuelewa kupitia kitabu.

Kwenye kitabu hiki cha ELIMU YA MSINGI YA FEDHA, kuna mambo kumi muhimu sana niliyoyajadili kwa kina ambayo yamewafanya wengi kubaki kwenye umasikini kwa sababu hawajui.

Leo nakugusia mambo haya hapa kwa kifupi, na ili kujifunza kwa kina na hatua za kuchukua, nitakupa utaratibu wa kupata kitabu hiki kizuri sana.

Moja; FEDHA SIYO MAKARATASI.

Watu wengi wamekuwa wanafikiria fedha ni yale makaratasi au sarafu ambazo tunazishika. Na hapa ndipo wengi wanapokwama, kwa sababu wanakosa ule msingi muhimu kuhusu fedha. Kwa kukosa msingi muhimu kuhusu fedha, watu wanashindwa kuzipata kwa wingi na hata kuzitumia vizuri.

Fedha ni wazo ambalo lina thamani. Fedha ni matokeo ya mtu kuwa na wazo ambalo linaongeza thamani kwa wengine. Bila ya thamani hakuna fedha. Hivyo kama unataka fedha zaidi, lazima ujue thamani gani unatoa kwa wengine.

Kwenye sura ya kwanza ya kitabu cha ELIMU YA MSINGI YA FEDHA, nimekufafanulia kwa kina kuhusu maana halisi ya fedha, utajiri na uhuru wa kifedha. Bila kujua hii, huwezi kuondoka kwenye umasikini.

Mbili; KIPATO KIMOJA NI UTUMWA.

Kuwa na chanzo kimoja cha kipato pekee ni utumwa. Huwezi kuondoka kwenye umasikini kama unategemea kipato chako kitoke sehemu moja pekee. Kama umeajiriwa pekee, hata kama unalipwa kiasi kikubwa cha fedha, bado unabaki kwenye umasikini. Kama unafanya biashara na unategemea wateja wachache nayo pia inakuweka kwenye umasikini.

Utaondoka kwenye umasikini kwa kuwa na vyanzo vingi vya kipato. Bahari huwa haikauki kwa sababu mito mingi inaishia kwenye bahari. Hiyo kama unataka usikaukiwe na fedha, kuwa na vyanzo vingi vya kipato.

Kwenye sura ya pili ya kitabu cha ELIMU YA MSINGI YA FEDHA nimekufundisha kwa kina kuhusu kipato, umuhimu wa kuwa na vyanzo vingi vya kipato na jinsi ya kuongeza kipato chako pale ulipo sasa.

Tatu; MATUMIZI NI BOMU.

Watu wengi wamekuwa wanaanza maisha na kipato kidogo, na yanaenda. Kipato kinaongezeka na matumizi yanaongezeka, kila kipato kinapoongezeka na matumizi pia yanaongezeka. Matumizi ni bomu kama hayatadhibitiwa. Matumizi yana tabia ya kuongezeka pale tu kipato kinapoongezeka.

Huwezi kuondoka kwenye umasikini kama huwezi kuyadhibiti matumizi yako. Haijalishi unatengeneza kipato kikubwa kiasi gani, matumizi ni bomu, usipolitegua litakulipua.

Kwenye sura ya tatu ya kitabu cha ELIMU YA MSINGI YA FEDHA utajifunza jinsi ya kudhibiti matumizi yako na hivyo kuruhusu kipato chako kukua na kuweza kuondoka kwenye umasikini.

Nne; MADENI NI UTUMWA.

Umesikia hapo, na najua huenda kimoyomoyo unakataa, unajiambia siyo kweli, kwa sababu huenda umeshalishwa sumu kwamba bila madeni maisha hayawezi kwenda. Unajua nini, wale wanaonufaika na madeni ndiyo wanasambaza propaganda za aina hiyo. Madeni ni utumwa, na huwezi kuondoka kwenye umasikini kama huwezi kuondokana na madeni.

Kuna madeni mazuri na mabaya, na masikini wote huwa wapo kwenye madeni mabaya. Madeni mabaya ndiyo yanawafanya watu kuwa watumwa, wanajikuta wanafanya kazi sana kulipa madeni, halafu wanakopa tena. Kwa hiyo maisha yao yote yanakuwa mzunguko wa kopa, lipa, kopa tena.

Kwenye sura ya nne ya kitabu cha ELIMU YA MSINGI YA FEDHA unakwenda kujifunza aina mbili za madeni, jinsi ya kuondoka kwenye madeni na mambo muhimu ya kuzingatia unapotaka kuingia kwenye madeni mazuri.

Tano; BIASHARA NI MKOMBOZI.

Zile zama za nenda shule, soma kwa bidii, faulu na utapata kazi nzuri na inayolipa zimeshapitwa na wakati. Kila mtu anaona wingi wa watu wenye sifa za kuajiriwa, lakini hakuna nafasi za ajira. Na hata walioajiriwa, mazingira ya kazi na hata kipato wanachoingiza hakiridhishi.

Kwa zama tunazoishi sasa, mkombozi pekee, kitu pekee kitakachokuwezesha kuwa na maisha mazuri ni kuwa na biashara yako. Hivyo ni muhimu sana uwe na biashara kama unataka kutoka kwenye umasikini.

Kwenye sura ya tano ya kitabu cha ELIMU YA MSINGI YA FEDHA, utajifunza kwa nini kila mtu anapaswa kuwa na biashara, jinsi ya kuanzia biashara chini kabisa na kuikuza na biashara unazoweza kuanza kufanya hapo ulipo sasa.

Sita; UWEKEZAJI NI KIJAKAZI WAKO.

Inapokuja kwenye fedha, kuna mambo mawili, kuna kuifanyia kazi fedha, pale ambapo inabidi ufanye kazi ndiyo fedha iingie. Halafu kuna fedha kukufanyia kazi wewe, ambapo fedha inaingia hata kama hufanyi kazi moja kwa moja.

Ili kuondoka kwenye umasikini na kufikia uhuru wa kifedha, ni lazima fedha ziwe zinakufanyia kazi wewe. Na hapa ndipo unapohitaji kuwa na uwekezaji, ambao unafanya kazi ya kuuzalishia fedha, hata kama wewe umelala.

Kwenye sura ya sita ya kitabu cha ELIMU YA MSINGI YA FEDHA, nimekuchambulia kwa makini sana kuhusu uwekezaji, aina kuu tano za uwekezaji, jinsi ya kuchagua uwekezaji sahihi kwako na uwekezaji unaoweza kuanza nao mara moja.

Saba; KODI NI UWEKEZAJI.

Kodi ni gharama unayolipa kwa kuishi kwenye jamii iliyostaarabika. Ni kodi tunazolipa ndiyo zinazoleta huduma mbalimbali tunazozitegemea kwenye jamii. Huduma za afya, huduma za elimu, ulinzi na usalama, miundombinu kama barabara na mengineyo ni matokeo ya kodi tunazolipa.

Hivyo kodi ni uwekezaji ambao kila mmoja wetu anapaswa kuufanya ili tuwe na jamii bora. Tunapaswa kuondokana na dhana potofu kwamba kodi ni kitu kibaya. Kwa sababu hebu pata picha, umekazana kutafuta fedha na ukawa tajiri, halafu unaishi sehemu isiyo salama, je utaweza kufurahia utajiri wako?

Kwenye sura ya saba ya kitabu cha ELIMU YA MSINGI YA FEDHA utajifunza umuhimu wa kodi kwenye jamii, kodi zinazokuhusu wewe moja kwa moja na jinsi ya kupata unafuu wa kodi.

Nane; BIMA NI MKOMBOZI.

Kuna hatari mbalimbali ambazo zinatuzunguka kwenye maisha, na kadiri unavyopiga hatua kifedha, ndivyo hatari zinakuwa kubwa zaidi. Hili limekuwa linazua hofu kwa wengi na wakati mwingine kuwazuia hata kufanikiwa.

Ili kuondokana na hatari zinazokuzunguka na kukuzuia kuanguka pale unapokutana na changamoto kubwa, unapaswa kuwa na bima. Kwa bima unachangia kiasi kidogo cha fedha, lakini unapopata tatizo, unalipwa kiasi kamili cha fedha au mali ulizopoteza.

Kwenye sura ya nane ya kitabu cha ELIMU YA MSINGI YA FEDHA unakwenda kujifunza umuhimu wa kuwa na bima, bima unazopaswa kuwa nazo kwenye maisha yako na mambo ya kuzingatia unapochagua bima.

Tisa; WATOTO WAKO HAWAHITAJI FEDHA ZAKO.

Wazazi wengi wamekuwa wanakazana kutafuta fedha na mali kwa wingi, ili kuwaachia watoto wao urithi na wasiwe na maisha magumu. Lakini wote tumekuwa tunaona nini kinatokea baada ya wazazi hao kufariki, utajiri na mali zote zinapotea, kwa kutumiwa vibaya na watoto walioachwa.

Watoto wako hawahitaji sana fedha wala mali zako, bali kikubwa wanachohitaji ni msingi muhimu wa kufuata na kusimamia inapokuja kwenye swala la fedha. Kuliko uwape watoto fedha bila ya misingi, ni bora uwape misingi bila ya fedha. Kwa sababu misingi itawawezesha kupata fedha zaidi wakati fedha pekee bila misingi zitapotea.

Kwenye sura ya tisa ya kitabu cha ELIMU YA MSINGI YA FEDHA, utakwenda kujifunza jinsi ya kuwajengea watoto wako msingi sahihi wa kifedha ambao utawahakikishia kutokusumbuliwa kabisa na umasikini. Na kadiri unavyoanza mapema, ndivyo wanayonufaika zaidi.

Kumi; KUTOA NI UWEKEZAJI.

Mmoja wa watu matajiri sana kuwahi kuwepo hapa duniani, John D. Rockefelar amewahi kunukuliwa akisema unatumia nusu ya kwanza ya maisha yako kukusanya fedha, halafu nusu ya pili unaitumia kuzigawa fedha hizo kwenda kwa wengine.

Moja ya vitu vinavyowafanya matajiri kuendelea kuwa matajiri ni utoaji. Matajiri wengi wamekuwa watoaji wa misaada mbalimbali ya kijamii na hilo limekuwa linawasukuma kufanikiwa zaidi kifedha. Hivyo kutoa ni uwekezaji ambao unamlipa sana mtu baadaye.

Kwenye sura ya kumi ya kitabu cha ELIMU YA MSINGI YA FEDHA, utajifunza umuhimu wa kutoa, njia bora za kutoa utajiri wako kwa wengine na pia sadaka na utoaji mwingine.

HITIMISHO; MAISHA YA KITAJIRI SIYO RAHISI.

Watu wengi kabla hawajapata fedha huwa wanafikiri wakishapata fedha basi maisha yao yatakuwa rahisi na hakutakuwa tena na changamoto. Wanachokuja kugundua baada ya kupata fedha ni kwamba fedha huwa zinakuja na matatizo na changamoto zake. Hivyo maisha ya kitajiri siyo rahisi kama yanavyoonekana kwa nje.

Kwenye hitimisho la kitabu cha ELIMU YA MSINGI YA FEDHA, nimekushirikisha mambo kumi ya kuumiza sana kuhusu maisha ya kitajiri, ambayo unapaswa kuyajua na kusimama imara ili yasikuangushe.

Rafiki yangu mpendwa, kitabu ELIMU YA MSINGI YA FEDHA ni kitabu ambacho hupaswi kukosa kukisoma, kwa sababu kina kila kitu unachopaswa kujua kuhusu fedha. Elimu iliyo ndani ya kitabu hiki itakuwezesha kuondoka kwenye umasikini na kukufikisha kwenye utajiri na uhuru wa kifedha.

JINSI YA KUPATA KITABU CHA ELIMU YA MSINGI YA FEDHA.

Kitabu cha elimu ya msingi ya fedha kinapatikana kwa nakala ngumu (hardcopy) yaani kimechapwa na kinatumwa popote pale ndani ya nchi ya Tanzania.

Kitabu hiki kinapatikana kwa gharama ya shilingi za Kitanzania Elfu Ishirini (20,000/=) kwa nakala moja ya kitabu.

Lakini ipo ofa kwako wewe rafiki yangu, ya kukipata kitabu hiki kwa tsh elfu kumi na tano, (15,000/=) kama utakilipia kabla ya tarehe 31/07/2019.

Kupata kitabu hiki, tuma ujumbe kwenye namba 0717396253 au 0755953887 na kisha utaletewa kitabu ulipo kama upo dar au kama upo mkoani utatumiwa.

UZINDUZI WA KITABU CHA ELIMU YA MSINGI YA FEDHA.

Rafiki yangu mpendwa, kutakuwa na uzinduzi rasmi wa kitabu hiki cha ELIMU YA MSINGI YA FEDHA ambao utafanyika jijini Dar es salaam siku ya jumamosi tarehe 03/08/2019.

Kwenye uzinduzi huu tutajifunza kwa kina mambo muhimu sana ya kifedha na jinsi ya kukitumia kitabu hiki kupiga hatua zaidi kwenye maisha yako.

Ada ya kushiriki uzinduzi wa kitabu ni tsh elfu kumi (10,000/=) na ili kupata nafasi ya kushiriki uzinduzi wa kitabu, tuma ujumbe sasa wenye majina yako kamili na namba ya simu ukisema utashiriki uzinduzi wa kitabu. Na uhakikishe umelipa ada ya kushiriki mpaka kufikia tarehe 31/07/2019.

Karibu sana rafiki yangu, usikose uzinduzi wala kitabu chenyewe.

Pia kuna kitabu kingine kimetoka, kinaitwa TANO ZA MAJUMA 50 YA MWAKA, ambapo kuna mambo matano ya kujifunza kwenye kila juma la mwaka, kuanzia siri za mafanikio, uchambuzi wa kitabu, makala za mafanikio, mafunzo ya kifedha na tafakari mbalimbali.

Kupata kitabu hiki tumia mawasiliano 0717396253 au 0755953887, karibu sana.

Vitabu vyote viwili vitazinduliwa siku moja, hivyo jipatie mapema na ushiriki uzinduzi ili uweze kujifunza na kuchukua hatua zitakazoyafanya maisha yako kuwa bora zaidi.

Makala Hii Imeandikwa Na Dr. Makirita Amani Ambaye Ni Daktari Wa Binadamu, Kocha Wa Mafanikio, Mwandishi Na Mjasiriamali.
uncle Sam system
 
Ukisikia kuna fursa unakaribishwa ujue wewe ndio fursa
Mkuu achana na mitazamo hasi, itakukwamisha wewe mwenyewe kufanikiwa.
Pata maarifa na yatumie kupiga hatua zaidi.
Maarifa ndiyo uwekezaji pekee ambao hakuna anayeweza kukuibia.
Karibu sana.
 
Hongera sana ndugu! kwa hatua uliyoifikia,
Nakupa pongezi kubwa sana, ila pia nina ushauri kwako,

Kwa ambao huwa wanasoma vitabu kwa hayo uliyoyaandika hapo juu nikwamba tumesoma tayari kitabu kizima,
Bado hatujakutana na wazo jipya, hata kama hakuna mawazo mapya basi sijapata ushawishi sababu naona mbona sina kipya cha kujifunza?
Ushauri wangu tumia lugha zaidi ya uandishi kuliko lugha ya maelezo,
Hata kama nikiwa na majibu yakwamba yai litachemsha ila bado nahitaji kujiuliza litachemshwaje? hii ndio point yangu

Zingatia lugha ya uandishi zaidi ongeza na sanaa yako basi utafanya makubwa zaidi, ila hongera sana kwa ulilolifanya
Uncle SAM SYSTEM
 
Karibu Kwenye Uzinduzi Wa Vitabu; Elimu Ya Msingi Ya Fedha Na Tano Za Juma.

Rafiki yangu mpendwa,

Nachukua nafasi hii kukukaribisha kwenye uzinduzi wa vitabu vipya ambavyo nimevitoa.

Vitabu hivyo ni ELIMU YA MSINGI YA FEDHA, ambapo ndani yake utajifunza mambo yote muhimu sana kuhusu fedha, ambayo hujawahi kupata nafasi ya kujifunza sehemu nyingine yoyote kwenye jamii.

Kitabu cha pili ni TANO ZA MAJUMA 5O YA MWAKA, hiki ni kitabu kikubwa ambacho utakisoma kwa mwaka mzima. Ndani yake kuna uchambuzi wa kina wa vitabu 50 vya mafanikio, siri 50 za mafanikio na mafunzo mengine mazuri kwako kuweza kuchukua hatua na kufanikiwa zaidi.

Uzinduzi wa vitabu hivi viwili utafanyika jumamosi ya tarehe 03/08/2019 kuanzia saa 8 kamili mchana mpaka saa 12 kamili jioni.

Uzinduzi utafanyika jijini dar es salaam, kwenye ukumbi wa hoteli ya GOLDEN PARK iliyopo Sinza Kumekucha, Dar es salaam.

Ada ya kushiriki uzinduzi huu ni tsh elfu 10 (10,000/=).

Ili kushiriki uzinduzi huu unapaswa kuweka nafasi yako mapema kwa sababu nafasi za ushiriki ni chache. Kuweka nafasi ya kushiriki semina, tuma ujumbe wenye majina yako kamili na namba ya simu, pamoja na maelezo kwamba nitashiriki uzinduzi wa vitabu kwenda namba 0717396253 au 0755953887.

Ada ya kushiriki uzinduzi huu unapaswa kulipa kabla ya tarehe 01/08/2019.

Karibu sana kwenye uzinduzi wa vitabu hivi viwili muhimu ambavyo vitakuwezesha kupiga hatua sana kwenye maisha yako.

Kwenye uzinduzi huu, pamoja na kupitia yale muhimu kutoka kwenye vitabu hivi viwili, utajifunza yafuatayo;

1. Kwa nini uwekezaji kwenye maarifa ndiyo uwekezaji pekee unaolipa sana.

2. Sababu 10 kwa nini unapaswa kusoma kitabu kila siku na kutembea na kitabu popote unapokuwa.

3. Jinsi ya kupata muda wa kusoma kila siku hata kama umebanwa na majukumu yako mengine.

4. Jinsi unavyoweza kusoma kitabu kimoja kila mwezi.

5. Jinsi ya kutoa kitabu kilichopo ndani yako na ukaacha alama hapa duniani.

Uzinduzi huu wa vitabu siyo wa kukosa, karibu tujifunze kwa pamoja na uweze kupata maarifa sahihi pamoja na hamasa ya kuchukua hatua ili kufanikiwa zaidi.

Tuma sasa majina yako na namba ya simu na maelezo kwamba utashiriki uzinduzi kwenda namba 0717396253 au 0755953887 na nafasi yako itahifadhiwa.

Rafiki na kocha wako,

Dr. Makirita Amani.
 
Hongera sana doctor nitanunua nakala yangu! Nimehisi nasoma "the richest man in Babylon" na akina Kiyosaki

Hii itafungua watu akili

Kudos doctor.......
 
Kwingine kote tumeenda sawa. ..hapo kwenye Maisha ya kitajiri siyo rahisi umenichanganya kabisa.
 
Kwingine kote tumeenda sawa. ..hapo kwenye Maisha ya kitajiri siyo rahisi umenichanganya kabisa.
Jipatie kitabu usome, utaelewa kwa kina na kama kuna mahali utakwama au kutokuelewa tunaweza kuwasiliana nikakupa ufafanuzi.
Karibu sana.
 
Hakika nimeipenda sana makala yako naiona wazi ina funzo kubwa sana ndani yake! Ngoja nikomae nipate kitabu hicho naona kina kitu cha kujikwamua! Hongera sana mkuu kwa kazi nzuri
 
Ili kurahisisha na kuondoa hofu ya watu kuhisi kutapeliwa ungetafuta mawakala kila mkoa ili mtu akihitaji anaenda moja kwa moja analipa anaondoka na kitabu. Ni mawazo yangu lakini mkuu.
 
Ili kurahisisha na kuondoa hofu ya watu kuhisi kutapeliwa ungetafuta mawakala kila mkoa ili mtu akihitaji anaenda moja kwa moja analipa anaondoka na kitabu. Ni mawazo yangu lakini mkuu.
Asante kwa mawazo mazuri,
Hii inayofanyika sasa ni pre order ndiyo maana unaona kinauzwa kwa ofa.
Baada ya kuzinduliwa kitauzwa kwa bei kamili na kitapatikana kupitia mawakala mbalimbali nchi nzima.
 
Mara ya kwanza nilipokisoma kitabu Rich daddy poor daddy nilihisi utajiri na financial freedom vikimiminika ndani ya roho yangu, nikaona kabisa nguvu ya maandishi kwenye maisha yangu, but in the long run ndipo nilikuja kuujua upande wa pili wa kile nilichokiona kuwa ukweli wa kimuujiza, sasa nipo huru, na hata sikumbuki nilichokisoma huko miaka hiyo, thanks for sharing
 
Back
Top Bottom