Tanganian
JF-Expert Member
- Jan 27, 2025
- 999
- 1,898
Sisi tumepishana sana na kila mtu ana maisha yake ,mimi kipindi niko form two dada zangu walikuwa wakubwa zaidi ya miaka 30 na wote wameshaolewa tena miji ya mbali huko.Wewe Kama unatoka familia bora na mmekuzwa katika Upendo unabidi kushukuru Mungu Sana .
Dada yangu wa kwanza hatujawasiliana almost miaka 4 wala sina namba yake ,ila hakuna bifu kwa sababu yeye anakaa mbali kwa sababu ya kazi na familia yake .
Ule undugu tu kuzaliwa pamoja unanifanya nijue hakuna bifu kati yetu , kumbuku kwetu ni waislamu : hatuwez ndugu kununiana zaidi ya siku 3 ,sina historia ya ugomvi na ndugu mpaka sasa.