Etugrul Bey
JF-Expert Member
- Aug 6, 2020
- 6,514
- 15,247
Sura hii kama inavyojulikana inahusu vijana wa pangoni....lakini kuna matukio mengine ambayo ni mafunzo tosha katika Maisha yetu ya kila siku,na ndio maana imesisitizwa tuisome kila siku ya ijumaa.
Funzo la Kwanza - siku zote tusitetereke katika kumwabudu Mwenyezi Mungu ambaye ndie WA kweli,tuilinde Imani yetu thabiti na tusiichanganye na ushirikina,,,,kama tulivyoona vijana hawa WA pangoni walikuwa katika jamii ambayo ni watu wachache Sana ndio walimwamini Mungu wa kweli na jamii kubwa ilikuwa inaabudu miungu ya uongo,,,,wakaona ili wasalimike na Imani Yao wakaona Bora waende wakajifiche pangoni kuliko kuiharibu Imani Yao,,,,,na siku zote ukimwamini Mwenyezi Mungu hakika atakulinda,basi Mola wao akawajaalia usingizi ndani ya pango lile na walikaa mule pangoni takribani miaka 309,na baadae akaja kuwaamsha na kukuta jamii ya pale imebadilika na watu wote Wanamwamini Mungu Mmoja,,,,na katika tukio Hilo la kukaa Miaka yote usingizini na kuja kuamshwa, Allah anasema hiyo ni ishara Kwa wale ambao hawaamini hiyo siku ya kiama kuwa hakika IPO na itakuja bilashaka.
Funzo la pili - fitina ya Mali, kuna bwana mmoja alijaaliwa mabustani mawili ambayo katikati yake kuna mito,kulikuwa na mizabibu na mitende na matunda mbali mbali,hakika bustani ilibarikiwa na kusheheni mazao,,,akiwa na mwenzake katika bustani yake,alijigamba kuwa yeye ana Mali nyingi na watoto wengi kuliko huyo mwenzake,na akasema kuwa hadhani kama kiama kitatokea na akaenda mbele zaidi Kwa kusema kuwa hata kikitokea basi atapewa Mali nyingi zaidi ya hizo.Hakika Mali zilimfanya akufuru na kusahau hiyo yote ni neema ya Mola wake,na mwenzake akamwambia Lau kuwa baada ya kuona Mimi Nina Mali kidogo kuliko wewe,basi ungesema hakuna hila wala nguvu isipokuwa Kwa Mwenyezi Mungu na alitakalo huwa,lakini huenda ukajitapa Kwa Mali nyingi na Mola wako akaja futilia mbali bustani yako! Na ndio Hicho kilicho tokea, Mola wake akaleta tufani na kulimalizia mbali shamba lake akabaki kujuta Kwa kauli zake.
Tukijaaliwa Utajiri na Mali basi inatakiwa tumshukuru Mwenyezi Mungu Kwa neema aliyotujaalia na wala tusikufuru Kwa kuona kuwa Ni ujanja wetu na tuitumie Mali hiyo katika njia yake inayompendeza ili tupate mwisho mwema.
Funzo la Tatu - Cheo au Uongozi,,, hivi vitu ni dhamana hivyo basi hatuna budi kuvitumia Kwa uadilifu Sana,,,hapa tunaonyeshwa Dhurqarnain alikuwa ni mfalme muadilifu Sana alikuwa anatembea maeneo mbali mbali kuwasaidia watu wenye uhitaji,na alitumia Cheo chake Kwa hekima na Busara,,,,alipofika katika vilima viwili aliwakuta watu ambao walitaka msaada dhidi ya yajuju na majuju,hawa walikuwa watu ambao walikuwa wanaleta uharibufu katika ardhi,hivyo Dhurqarnain akaombwa kuwadhibiti hawa watu,basi aliwajengea ukuta wa Chuma na kumimina Shaba juu yake,wale watu wabaya wakashindwa kuukwea ule ukuta,na utakuja kuvunjwa na Mwenyezi Mungu siku ya kiama. Na siku zote mfalme huyu hakumsahau Mola wake,,,,hivyo Kwa dhamana yoyote utakayo pewa basi hekima na Busara viwe sehemu ya Uongozi wako.
Funzo la nne - Ni fitna ya Elimu,,, hapa tunakutana na habari ya Nabii Musa na bwana Khizir. Nabii Musa kwakuwa alikuwa anaongea na Mwenyezi Mungu basi alijiona kuwa yeye ndio binadamu mwenye elimu kubwa zaidi,,,lakini Mola wake akamkutanisha na mja wake mmoja Anaitwa Khizir huyu amejaaliwa elimu zaidi kuliko ya Musa,na anajua mambo yajayo au ya ghaibu,IPO siku nitagusia mambo yake aliyomfundisha Musa,Ila hapa ni kuelezea Tu kuwa Kwa kila mjuzi kuna mjuzi zaidi. Na hata uwe na elimu kiasi gani basi Mwenyezi Mungu ndio mjuzi zaidi,,,kwahiyo tuitumie elimu zetu kuleta faida Kwa jamii zetu.
Ni hayo Tu!
Funzo la Kwanza - siku zote tusitetereke katika kumwabudu Mwenyezi Mungu ambaye ndie WA kweli,tuilinde Imani yetu thabiti na tusiichanganye na ushirikina,,,,kama tulivyoona vijana hawa WA pangoni walikuwa katika jamii ambayo ni watu wachache Sana ndio walimwamini Mungu wa kweli na jamii kubwa ilikuwa inaabudu miungu ya uongo,,,,wakaona ili wasalimike na Imani Yao wakaona Bora waende wakajifiche pangoni kuliko kuiharibu Imani Yao,,,,,na siku zote ukimwamini Mwenyezi Mungu hakika atakulinda,basi Mola wao akawajaalia usingizi ndani ya pango lile na walikaa mule pangoni takribani miaka 309,na baadae akaja kuwaamsha na kukuta jamii ya pale imebadilika na watu wote Wanamwamini Mungu Mmoja,,,,na katika tukio Hilo la kukaa Miaka yote usingizini na kuja kuamshwa, Allah anasema hiyo ni ishara Kwa wale ambao hawaamini hiyo siku ya kiama kuwa hakika IPO na itakuja bilashaka.
Funzo la pili - fitina ya Mali, kuna bwana mmoja alijaaliwa mabustani mawili ambayo katikati yake kuna mito,kulikuwa na mizabibu na mitende na matunda mbali mbali,hakika bustani ilibarikiwa na kusheheni mazao,,,akiwa na mwenzake katika bustani yake,alijigamba kuwa yeye ana Mali nyingi na watoto wengi kuliko huyo mwenzake,na akasema kuwa hadhani kama kiama kitatokea na akaenda mbele zaidi Kwa kusema kuwa hata kikitokea basi atapewa Mali nyingi zaidi ya hizo.Hakika Mali zilimfanya akufuru na kusahau hiyo yote ni neema ya Mola wake,na mwenzake akamwambia Lau kuwa baada ya kuona Mimi Nina Mali kidogo kuliko wewe,basi ungesema hakuna hila wala nguvu isipokuwa Kwa Mwenyezi Mungu na alitakalo huwa,lakini huenda ukajitapa Kwa Mali nyingi na Mola wako akaja futilia mbali bustani yako! Na ndio Hicho kilicho tokea, Mola wake akaleta tufani na kulimalizia mbali shamba lake akabaki kujuta Kwa kauli zake.
Tukijaaliwa Utajiri na Mali basi inatakiwa tumshukuru Mwenyezi Mungu Kwa neema aliyotujaalia na wala tusikufuru Kwa kuona kuwa Ni ujanja wetu na tuitumie Mali hiyo katika njia yake inayompendeza ili tupate mwisho mwema.
Funzo la Tatu - Cheo au Uongozi,,, hivi vitu ni dhamana hivyo basi hatuna budi kuvitumia Kwa uadilifu Sana,,,hapa tunaonyeshwa Dhurqarnain alikuwa ni mfalme muadilifu Sana alikuwa anatembea maeneo mbali mbali kuwasaidia watu wenye uhitaji,na alitumia Cheo chake Kwa hekima na Busara,,,,alipofika katika vilima viwili aliwakuta watu ambao walitaka msaada dhidi ya yajuju na majuju,hawa walikuwa watu ambao walikuwa wanaleta uharibufu katika ardhi,hivyo Dhurqarnain akaombwa kuwadhibiti hawa watu,basi aliwajengea ukuta wa Chuma na kumimina Shaba juu yake,wale watu wabaya wakashindwa kuukwea ule ukuta,na utakuja kuvunjwa na Mwenyezi Mungu siku ya kiama. Na siku zote mfalme huyu hakumsahau Mola wake,,,,hivyo Kwa dhamana yoyote utakayo pewa basi hekima na Busara viwe sehemu ya Uongozi wako.
Funzo la nne - Ni fitna ya Elimu,,, hapa tunakutana na habari ya Nabii Musa na bwana Khizir. Nabii Musa kwakuwa alikuwa anaongea na Mwenyezi Mungu basi alijiona kuwa yeye ndio binadamu mwenye elimu kubwa zaidi,,,lakini Mola wake akamkutanisha na mja wake mmoja Anaitwa Khizir huyu amejaaliwa elimu zaidi kuliko ya Musa,na anajua mambo yajayo au ya ghaibu,IPO siku nitagusia mambo yake aliyomfundisha Musa,Ila hapa ni kuelezea Tu kuwa Kwa kila mjuzi kuna mjuzi zaidi. Na hata uwe na elimu kiasi gani basi Mwenyezi Mungu ndio mjuzi zaidi,,,kwahiyo tuitumie elimu zetu kuleta faida Kwa jamii zetu.
Ni hayo Tu!