Mambo matatu (3) ya kuzingatia kabla na wakati wa kumiliki nyumba au kiwanja cha kwanza kwa ajili ya kujenga utajiri

Mambo matatu (3) ya kuzingatia kabla na wakati wa kumiliki nyumba au kiwanja cha kwanza kwa ajili ya kujenga utajiri

Kwangu mimi, utajiri ni perception. Hapa nina maana kuwa ukiwa na malengo ya kutengeneza milioni moja kwa mwezi na ukaona kwako ni mafanikio makubwa ni jambo zuri sana.

Kila mtu apambanie malengo yake ya kimafanikio. Lakini kutokuwa na malengo na kuishi kama kuku wa kienyeji hapo ndipo inaanzia changamoto.

KUANZIA CHINI KABISA.

Nimependa sana ushauri wako wa vijana kutosubiri mitaji mikubwa ndipo waanze kujishughulisha.

Rafiki yako,

Aliko Musa.

Mbobezi wa ardhi na majengo.
Aısee umeongea point moja ya msingi, kuna mtu kwake akipata 10,000 kwa siku basi karidhika na anaamini yeye ni tajiri na kuna mtu anapata million 5 na bado anajiona maskini
 
Umenena Vizuri sana rafiki yangu,

Lakini binafsi ninaamini kuna mikopo mizuri na mikopo mibaya kama ambavyo nimetumia mlinganyo wa 30%.

Ni kweli vyanzo vingi vya maarifa ni ughaibuni.

Pia, kumbuka kuwa makundi mengi ya utaalamu tunategemea vyanzo vya maarifa kutoka ughaibuni kama Marekani, india, canada n.k.

Hii kwangu sio hoja. Hoja ya msingi sana uliyonena ni kuwa tuwe tunadigest maarifa ya kutoa kwa wengine kabla ya kuwashirikisha.

Muhimu; huwa siandiki kuhusu nyumba za kuishi. Nimelenga wawekezaji kwenye ardhi na majengo ambao wanahitaji kujenga utajiri mkubwa kupitia uwekezaji huu.

Na kutokopa kwenye uwekezaji wa ardhi na majengo ni kipengele cha mbinu ya B-R-R-R-R ya nyumba za kupangisha.

Mbinu hii inawafaa ambao wanaweza kuweka kiasi kikubwa cha akiba kwa ajili kumiliki nyumba ya kwanza.

Nashukuru sana kwa kuandika maoni yenye ushauri mzuri ndani.

Karibu sana rafiki.

Rafiki yako,

Aliko Musa.
Ndugu yangu 'Aliko Musa' ,ni mradi upi wa uendelezaji makazi unaoweza kufanya kwa pesa za kudunduliza?,hii mentality ya kuogopa mikopo siafikiani nayo kabisa,nakuomba urudi hapa kusema umelenga kundi la kipato gani Cha Juu au Cha kati?
 
Ndugu yangu 'Aliko Musa' ,ni mradi upi wa uendelezaji makazi unaoweza kufanya kwa pesa za kudunduliza?,hii mentality ya kuogopa mikopo siafikiani nayo kabisa,nakuomba urudi hapa kusema umelenga kundi la kipato gani Cha Juu au Cha kati?

Sijalenga kipato,

Nimelenga mbinu ya kuwekeza kwenye nyumba ya kupangisha iitwayo B-R-R-R-R.

Kwa mbinu hii, hutakiwi kutumia mkopo kumiliki nyumba ya kwanza.

Lakini sio kwamba nimeeleza mentality ya kuogopa mikopo.

Nadhani umesema makala zangu chache sana.

Naomba uwe unatembelea blogu ya UWEKEZAJI MAJENGO.

Ingie Google andika UWEKEZAJI MAJENGO BLOG.

Hapa utanielewa mengi kuhusu jinsi ninavyoamini na kuwaanisha wengine kuhusu mikopo.

Kuna makala ninawaandikia wasomaji wangu kuwa ni vigumu mno kujenga utajiri mkubwa sana kupitia ardhi na majengo bila kutumia fedha za wengine "MIKOPO".

Mikopo ya majengo ninaiita Nyenzo ya maajabu kati ya nyenzo tano anazotakiwa kutumia mwekezaji kwenye ardhi na majengo.

Naomba uwe unatembelea hiyo blogu ya UWEKEZAJI MAJENGO.

Huwezi kupata kila kitu kwenye makala moja rafiki yangu.

Ninashukuru sana sana kwa swali lako na mchango mzuri.

Karibu sana.
 
Back
Top Bottom