Habari zenu wanajamii, siku hizi kuna makanisa mengi sana yanaibuka yenye wachungaji, manabii, mitume, walimu, n.k. Jambo linalopelekea upotoshwaji mwingi kufanyika kwa kutumia jina la Mungu na mwanae wa pekee Yesu Kristu.
Haya ni mambo matatu unayoweza kutumia kujua kanisa au mtumishi gani ni wa kweli na yupi ni tapeli wa imani.
1. Maudhui ya mahubiri yake.
Jambo la kwanza unaloweza kutumia kujua kama mchungaji huyu au kanisa hili ni la kweli sikiliza mahubiri yanayohubiriwa hapo. Jukumu la msingi la kanisa na watumishi wake ni kuwasaidia waumini wao. kuboresha mahusiano mazuri na Mungu wao. Njia kuu ya kuboresha mahusiano na Mungu ni kuwa na imani thabiti nae kwa kuzishika amri zake na kutenda matendo mema. Haya ndo yanatakiwa yawe maudhui makuu ya kanisa pamoja na watumishi wake.
Ukiona kanisa au mtumishi hahubiri kuhusu hayo basi huyo sio mchungaji wa kweli wa Mungu. Ukiona anahubiri zaidi kuhusu mafanikio ya kidunia kama vile kupata utajiri, kutopata shida, kupona magonjwa, uchawi, na mambo mengine kama maudhui yake makuu basi ujue kuna ulakini. Haimaanishi kuwa haya hayatakiwi kuhubiriwa makanisani, lakini lisiwe ndo madhumuni makuu ya mahubiri.
2. Maisha ya gharama na anasa ya wachungaji.
Ukiona mchungaji, mtume, nabii au pastor anayeishi maisha ya kifahari na anasa kwa kutumia sadaka za waumini wake ujue kabisa hapo unapigwa. Maisha ya kifahari na gharama ni kama vile kumiliki gari la mil. 200, nyumba ya milioni zaidi ya 100, na mambo mengine kama hayo basi ujue huyo sio mtumishi wa kweli wa Mungu bali ni mfanyabiashara anayetapeli wananchi maskini kwa kutumia jina la Yesu Kristu wa Nazareth.
3. Miujiza ya kila siku.
Kuna makanisa ambayo kila siku au kila wiki kuna msururu wa watu wanafanyiwa au kutoa ushuhuda wa miujiza. Makanisa ya aina hii hayafanyi kazi ya Mungu.
Hapa kuna mawili kwenye hayo miujiza. Aidha wanafanya usanii kwa kuwalipa watu waigize kutendewa miujiza au wanatumia nguvu zisizohusiana na Bwana Yesu Kristu (nguvu za giza au mazingaombwe).
Hapa sisemi kuwa makanisa na wachungaji hawatakiwi kufanya miujiza, la hasha, maana hata Yesu mwenyewe na mitume wake wa mwanzoni walifanya miujiza mara kadhaa. Lakini hawakufanya miujiza kila siku. Walifanya miujiza pale palipohitajika. Lakini kuna makanisa kadhaa ya sasa wana kipengele kabisa cha miujiza na ushuhuda kila siku au kila wiki ambapo watu hupanga mistari mirefu kupokea hiyo miujiza. Hapo lazima uwe na mashaka rafiki.
Kwahiyi ndugu zanguni, kuweni makini.
Mtume Paulo ameongelea kuhusu manabii wa uwongo katika baadhi ya barua zake. Mojawapo ya sehemu inayoelezea hili ni katika 2 Wakorintho 11:13-15, ambapo anasema:
Vilevile, Bwana wetu Yesu Kristu kwenye injili ya Mathayo 7:15-20, ametuonya aliposema:
Hivyo, Bwana wetu Yesu Kristu na mtume Paulo wote wanasisitiza kuwa matendo ya watu ndiyo yanaonyesha ukweli wa wao kuwa ni wa Mungu au la.
Haya ni mambo matatu unayoweza kutumia kujua kanisa au mtumishi gani ni wa kweli na yupi ni tapeli wa imani.
1. Maudhui ya mahubiri yake.
Jambo la kwanza unaloweza kutumia kujua kama mchungaji huyu au kanisa hili ni la kweli sikiliza mahubiri yanayohubiriwa hapo. Jukumu la msingi la kanisa na watumishi wake ni kuwasaidia waumini wao. kuboresha mahusiano mazuri na Mungu wao. Njia kuu ya kuboresha mahusiano na Mungu ni kuwa na imani thabiti nae kwa kuzishika amri zake na kutenda matendo mema. Haya ndo yanatakiwa yawe maudhui makuu ya kanisa pamoja na watumishi wake.
Ukiona kanisa au mtumishi hahubiri kuhusu hayo basi huyo sio mchungaji wa kweli wa Mungu. Ukiona anahubiri zaidi kuhusu mafanikio ya kidunia kama vile kupata utajiri, kutopata shida, kupona magonjwa, uchawi, na mambo mengine kama maudhui yake makuu basi ujue kuna ulakini. Haimaanishi kuwa haya hayatakiwi kuhubiriwa makanisani, lakini lisiwe ndo madhumuni makuu ya mahubiri.
2. Maisha ya gharama na anasa ya wachungaji.
Ukiona mchungaji, mtume, nabii au pastor anayeishi maisha ya kifahari na anasa kwa kutumia sadaka za waumini wake ujue kabisa hapo unapigwa. Maisha ya kifahari na gharama ni kama vile kumiliki gari la mil. 200, nyumba ya milioni zaidi ya 100, na mambo mengine kama hayo basi ujue huyo sio mtumishi wa kweli wa Mungu bali ni mfanyabiashara anayetapeli wananchi maskini kwa kutumia jina la Yesu Kristu wa Nazareth.
3. Miujiza ya kila siku.
Kuna makanisa ambayo kila siku au kila wiki kuna msururu wa watu wanafanyiwa au kutoa ushuhuda wa miujiza. Makanisa ya aina hii hayafanyi kazi ya Mungu.
Hapa kuna mawili kwenye hayo miujiza. Aidha wanafanya usanii kwa kuwalipa watu waigize kutendewa miujiza au wanatumia nguvu zisizohusiana na Bwana Yesu Kristu (nguvu za giza au mazingaombwe).
Hapa sisemi kuwa makanisa na wachungaji hawatakiwi kufanya miujiza, la hasha, maana hata Yesu mwenyewe na mitume wake wa mwanzoni walifanya miujiza mara kadhaa. Lakini hawakufanya miujiza kila siku. Walifanya miujiza pale palipohitajika. Lakini kuna makanisa kadhaa ya sasa wana kipengele kabisa cha miujiza na ushuhuda kila siku au kila wiki ambapo watu hupanga mistari mirefu kupokea hiyo miujiza. Hapo lazima uwe na mashaka rafiki.
Kwahiyi ndugu zanguni, kuweni makini.
Mtume Paulo ameongelea kuhusu manabii wa uwongo katika baadhi ya barua zake. Mojawapo ya sehemu inayoelezea hili ni katika 2 Wakorintho 11:13-15, ambapo anasema:
Katika kifungu hiki, Paulo anasisitiza kuwa manabii wa uwongo wanaweza kujifanya kuwa wa haki, lakini utambuzi wao unaweza kupatikana kwa kuangalia matendo yao, ambayo hayakuwa ya haki au ya kweli."Kwa maana manabii wa uwongo ni kama mitume wa uwongo, wanajifanya kuwa mitume wa Kristo. Na hilo si jambo la ajabu, kwa maana Shetani mwenyewe anajifanya kuwa malaika wa nuru. Hivyo, si ajabu ikiwa watumishi wake nao wanajifanya kuwa watumishi wa haki. Mwishowe yao yatakuwa kulingana na matendo yao."
Vilevile, Bwana wetu Yesu Kristu kwenye injili ya Mathayo 7:15-20, ametuonya aliposema:
Hii pia inaonyesha kwamba tunapaswa kutambua manabii wa uwongo kupitia matendo yao, kwani matunda yao hayaendani na mafundisho ya kweli."Jihadharini na manabii wa uwongo, ambao wanakuja kwenu kwa mavazi ya kondoo, lakini kwa ndani ni mbwa mwitu wauaji. Mta wajua kwa matunda yao."
Hivyo, Bwana wetu Yesu Kristu na mtume Paulo wote wanasisitiza kuwa matendo ya watu ndiyo yanaonyesha ukweli wa wao kuwa ni wa Mungu au la.