Mambo muhimu ambayo Mzee Mkapa hajaweka wazi katika kitabu chake ''My Life, My Purpose''

Mambo muhimu ambayo Mzee Mkapa hajaweka wazi katika kitabu chake ''My Life, My Purpose''

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
NI watu wachache sana ambao wakiandika vitabu kuhusu maisha yao, huwa wanaweka mambo yote makuu yaliyotokea katika maisha yao, kwa kuwa labda wanahofia yatawachafua au yatawapotezea umaarufu. Hivyo basi mara nyingi vitabu kuhusu maisha ya watu ambavyo vimehaririwa na wao wenyewe, hutokea kuwa kama namna tu ya publicity stunts za namna ya kujisafisha mbele ya jamii.

Je, tunaweza kusema hivyo kuhusu kitabu cha Mkapa? Mimi binafsi sijakisoma bado, lakini bado nina shauku sana kujua kama Mkapa ameweka wazi mambo ambayo sisi kama jamii tunaona yameacha maswali mengi kuliko majibu. Kwa mfano, amegusia jinsi alivyopishana vikali na Mwalimu Nyerere kuhusu suala la ubinafsishaji? Na je, Mkapa ameeleza ukweli kuhusu suala la rada iliyoleta mgogoro kama vile EPA? Je, suala la uuzaji nyumba za serikali? Suala la Mradi wa Makaa ya Mawe Kiwira?

Mkapa amegusia kuhusu maisha ya familia na tuhuma za uchawi kwa wazee wake, lakini vipi suala lake la maisha ya ndoa ambalo tumekuwa tukisikia kila namna ya habari, ameliongelea ili kuiweka jamii sawa? Ni kweli Mkapa alioa mtu ambae alikuwa mke wa Basil Mramba au ni porojo tu? Vipi hisia zake pale ambapo hadi watoto walimzomea "fisadi fisadi", ameeleza alijisikiaje kuona hadi watoto wakimtuhumu ufisadi?

Na vipi tuhuma zilizomkabili kuhusu uuzwaji wa NBC ambazo zilifanya karibu uasi wa Bunge utokee, amezigusia? Na vipi tuhuma na mkanganyiko kulelekea mwishoni mwa maisha ya Nyerere, akituhumiwa kumsusa Nyerere akiwa mgonjwa, je ametoa ufafanuzi juu ya hilo? Na vipi mgogoro wa Bulyanhulu watu kufukiwa na yeye kupewa kilo ya dhahabu, na pia kukubali asilimia 5% ya hisa kwa ajili ya Tanzania wakati Nyerere alikataa asilimia 49%, ametoa sababu zinazofanya watu waone kweli hakuwa muuza nchi? Vipi suala la kwamba katika uteuzi wa Kikwete kuwa mgombea wa uraisi wa CCM alikubali japo TISS walimpa taarifa iliyomuondolea sifa Kikwete kuwa mgombea wa wa uraisi? Je ni kweli alimpitisha Kikwete kwa nguvu kwa kuwa Kikwete alitishia kujiunga na Chadema, na wakakubaliana Kikwete amlinde atakapokuwa raisi?

Sasa haya ni baadhi ya mambo ambayo wengine tukisikia Mkapa kaamua kuandika kitabu, tunategemea ayagusie. Vinginevyo inakuwa ni kitabu cha kujikosha na kujisafisha mbele ya jamii. Na kama hajayaweka, basi mie binafsi labda niandike kitabu "Benjamini Mkapa: Your Life, Tanzania's Purpose".

Pengine wewe unajua mengine ya muhimu ambayo unahisi Mkapa alipaswa kuzungumzia katika hiki kitabu alichaoandika, "My Life, My Purpose".
 
Ni taarifa gani hiyo ya kikwete ambayo mkapa alipewa na TISS. ?
Ni vizuri mleta mada ukiisema
Fuatilia uteuzi wa Kikwete ulivyokuwa utapata habari kamili, wakati ambapo majina ya mwisho yalikuwa Kikwete, Salim Ahmed Salim na Prof. Mwandosya. Kikwete alikuwa na taarifa chafu ambayo Mkapa aliamua "kuipuuza", lakini kuipuuza huku kulikuwa na walakini.
 
Mkapa Ndiye aliyesababisba ushenzi wote unaoendelea mpaka leo!

Ilo la idala ya usalama wa taifa kukataa ni kweli ila kikwete alikuwa akiungwa mkono na JWTZ na Salim alikataliwa na jeshi na ndiye alikuwa apewe nchi so ndio ugumu ulipoanzia apo kwa Mkapa.
 
Kuhusu suala ma maisha yake pale pale kwenye ndoa sijui kama kaandika kwamba walikuwa wameshaachana na Mama Mkapa ila Mwalimu akawaunganisha tena kabla ya kumpa Urais. Na pia sidhani amegusia watoto wake, maana kuna ndogo ndogo zinasema Mzee hajawahi kuwa na mtoto yoyote yule ila hao wanaodaiwa ni wa kwake aliwakuta kwa mkewe.. hilo nalo linahitaji ufafanuzi yakinifu. Na kuna habari kwamba miaka 5 ya mwisho alipata shinikizo kutoka kwa mkewe kwamba akwapue mali ili waishi vizuri....Eti mzee ndiyo akaanza na Kiwira, NET Group solutions nk...
Afu kuna tuhuma kwamba alipewa cheni ya dhahabu ya kilo 5 huko buli sasa badala ya kuikabidhi IKULU yeye akawa anaivaa shindoni akaifanya yake kumbe ni ya Taifa.

Hizi nazo kama angezifafanua ingekuwa vizuri sana ili kusafisha jina lake.
 
Sifikirii anaweza kuandika kila kitu kitabu kimoja kikatosha. Dhumuni au lengo la mwandishi linaamua kitu gani kiwepo au kisiwepo kwenye kitabu. Shida ni pale unaposema unaandika kitabu kuhusu maisha yako huku unaweka baadhi ya mambo na kuandika machache, Title ingebadilika.

Mfano naweza kuamua kuandika kitabu kuwatia moyo wanaopitia changamoto wanaotaka kufanya biashara, sitaandika mambo yangu mengi yasiyohusu hilo eneo.

Naweza kutaka kuelezea safari yangu ya maisha ya kiroho, ntajikita zaidi kwenye hayo maudhui.

Mie huyohuyo naweza kuamua kutoa maelezo yangu binafsi kuhusu mahusiano, ntaandika mambo mengi sana na mahusiano tofauti tofauti kadri nilivyojihusisha nayo na ntaangalia kipi kitaleta tija.

Ndio maana kwa sie wakristo imeandikwa endapo kila jambo alilolifanya Yesu lingeandikwa, kitabu kisingetosha.

Mwisho wa siku ukweli wa mtu anabaki nao mhusika, kosa ni pale unapojitutumua kuandika kitabu cha maisha yako huku ukichagua kipi kiandikwe na kipi kiachwe.
 
Mkapa Ndiye aliyesababisba ushenzi wote unaoendelea mpaka leo!

Ilo la idala ya usalama wa taifa kukataa ni kweli ila kikwete alikuwa akiungwa mkono na JWTZ na Salim alikataliwa na jeshi na ndiye alikuwa apewe nchi so ndio ugumu ulipoanzia apo kwa Mkapa.
Na bado anaendelea na kutusababishia ushenzi hadi leo,kwa kutuwekea jiwe mlangoni hadi tunashindwa kutoka,na bado amelikalia.Jiwe.
 
Kuna mifumo 5 ya uandishi nitaitaja; Poetry, Drama, prose, non fiction na media.
Kwa mfumo ambao BWM alioamua kuandika Kitabu chake ni "Non fiction".

Non-fiction can be creative, such as the personal essay, or factual, such as the scientific paper. Sometimes the purpose of non-fiction is to tell a story (hence the autobiography), but most of the time the purpose is to pass on information and educate the reader about certain facts, ideas, and/or issues.

Kwa hiyo mfumo huo hapo hauwezi kuchanganya gossip kama ambazo mtoa mada umeziweka kwenye uzi wako. Hayo unayotaka wewe yatapatikana kwenye vitabu vya Eric Shigongo.
 
Chain ya kilo 5!!!!! Are you serious??????
yes ilikuwa kubwa sana kiongozi, Mzee alikuwa anaivaa kama kikoi yaani inapita shingoni begani hadi kifuani chini ya mkono.... kuna kuda akiwa na press ilikuwa inaonekana kwa nadra nadra ....pembeni pembeni kwa suti.
 
Mkapa Ndiye aliyesababisba ushenzi wote unaoendelea mpaka leo!

Ilo la idala ya usalama wa taifa kukataa ni kweli ila kikwete alikuwa akiungwa mkono na JWTZ na Salim alikataliwa na jeshi na ndiye alikuwa apewe nchi so ndio ugumu ulipoanzia apo kwa Mkapa.
JWTZ hawakuwa na tatizo na Salim. Salim alikataliwa na Zanzibar, ambao siku zote walimwona yuko upande wa Waarabu waliopinduliwa mwaka 1964 kwenye Mapinduzi ya Zanzibar. Tatizo ni pale ambapo Kikwete alitoa shinikizo kwamba asipopitishwa na CCM ataenda Chadema na akamwambia Mkapa nikienda Chadema nitashinda na historia itaandikwa CCM ilifia mikononi mwa Mkapa. Nasikia Mkapa akakubali, lakini kwa kuwa hakumwamini Prof. Mwandosya kuwa asingechukua hatua dhidi ya mambo ya "kifisadi" aliyofanya akiwa Raisi, wakakubaliana na Kikwete kwamba atashinikiza jina lake lipitishwe kwa masharti kwamba akistaafu mambo yake aliyofanya akiwa raisi yasiguswe, kutia ndani Kiwira, nyumba za serikali nk. Wakati huo Mkapa alikuwa na tuhuma nyingi sana za ufisadi, kutia ndani tetesi kwamba ABSA walimpa hoteli huko Afrika Kusini kama zawadi ya ubinafsishaji wa NBC. Na Mkapa zawadi kutoka makampuni binafsi alikuwa hazionei aibu kuzipokea!
 
yes ilikuwa kubwa sana kiongozi, Mzee alikuwa anaivaa kama kikoi yaani inapita shingoni begani hadi kifuani chini ya mkono.... kuna kuda akiwa na press ilikuwa inaonekana kwa nadra nadra ....pembeni pembeni kwa suti.
Hehehe! Kuna wakati aliuwa anavaa bullet proof vest. Sasa nafikiria bullet proof vest na hiyo chain ya kilo tano, du, kama kweli jamaa nguvu anazo!
 
Back
Top Bottom