Mambo muhimu ambayo Mzee Mkapa hajaweka wazi katika kitabu chake ''My Life, My Purpose''

Mambo muhimu ambayo Mzee Mkapa hajaweka wazi katika kitabu chake ''My Life, My Purpose''

Mambo sita ambayo ameyaeleza kama udhaifu in:
1. Mauaji ya Pemba
2.Ubinafsishaji was mashirika ya umma
3.Ufanyaji was biashara ikulu
4. EPA
 
Fuatilia uteuzi wa Kikwete ulivyokuwa utapata habari kamili, wakati ambapo majina ya mwisho yalikuwa Kikwete, Salim Ahmed Salim na Prof. Mwandosya. Kikwete alikuwa na taarifa chafu ambayo Mkapa aliamua "kuipuuza", lakini kuipuuza huku kulikuwa na walakini.
mkuu hii taarifa tunaifuatilia wapi? mwaga nondo hapa tujue maana wengine hatuna uwezo wa kupata taarifa kama hizi
 
Kitabu hujasoma unaanza kuuliza kwa kukosoa.

Dah! Hizi shule za kusomea ujinga zina matatizo sana.
 
Kilo Tano? Anavaa shingoni? Kweli?
Kuhusu suala ma maisha yake pale pale kwenye ndoa sijui kama kaandika kwamba walikuwa wameshaachana na Mama Mkapa ila Mwalimu akawaunganisha tena kabla ya kumpa Urais. Na pia sidhani amegusia watoto wake, maana kuna ndogo ndogo zinasema Mzee hajawahi kuwa na mtoto yoyote yule ila hao wanaodaiwa ni wa kwake aliwakuta kwa mkewe.. hilo nalo linahitaji ufafanuzi yakinifu. Na kuna habari kwamba miaka 5 ya mwisho alipata shinikizo kutoka kwa mkewe kwamba akwapue mali ili waishi vizuri....Eti mzee ndiyo akaanza na Kiwira, NET Group solutions nk...
Afu kuna tuhuma kwamba alipewa cheni ya dhahabu ya kilo 5 huko buli sasa badala ya kuikabidhi IKULU yeye akawa anaivaa shindoni akaifanya yake kumbe ni ya Taifa.

Hizi nazo kama angezifafanua ingekuwa vizuri sana ili kusafisha jina lake.
 
inaonekana ulikuwepo kwenye ha yo makubaliano ya Mkapa na Kikwete. Anyway tunaojua kutazama nyuma ya Pazia tumeshakusoma kuwa hayo ni mambo yako ya kutunga tu na ukachanganya na story za kijiweni. LENGO LAKO LIKIWA NI UZANDIKI. Tatizo umesahau kuwa Humu ndani wengi ni GREAT THINKERS.
I say kama Great thinkers wanaandika kama wewe sitaki kabisa kuwa mmoja wao!

HIvi umejiuliza naweza kuwa karibu kisi gani na hawa watu, au umekurupuka tu?

Ngoja nikupe story nyingine, sasa kama unaweza kumfuata Kikwete au Mwandosya akakuthibitishie fanya hivyo, lakini inakusaidia kuelewa kwamba sio kila mtu humu JF anakitungia hadithi. Sasa hii ni virgin story, hutaikuta popote pale!

Basi Raisi Kikwete alipochaguliwa kuwa raisi, akatuita. Akasema unajua mie nina ugomvi na Prof. wa siku nyingi, nadhani ili tufanye kazi vizuri pamoja ni vema tukasuluhiswah, hivyo nawaomba muende mkamwone Prof. Mwandosya ili tukutanishwe na kusuluhishwa. Tukaenda kumwona Mwandosaya na kumweleza ujumbe toka kwa Kikwete. Prof akatulia kidogo, akatuangalia halafu akatuuliza, "mimi nashangaa, kwa kuwa sijui kama nina ugomvi na Kikwete wa kutaka tusuluhishwe. Kwani Kikwete alivyosema tukatanishwe tusuluhishwe, aliwaambia kuna ugomvi gani kati yetu? Maana mimi sina tatizo na Kikwete ambalo naona linahitaji tusuluhishwe". Tukamwambia hajatuambia tatizo kati yenu. Basi Mwandosya akaonekana kushangaa na kukerwa kidogo, akatuuliza, "yaani nyie mlikubalije kuwa wasuluhishaji wa tatizo ambalo hamlijui na wala hamkumuuliza? Basi mie ningewashauri mrudi kwa Kikwete, mumwambie tumekutana nae, lakini amesema yeye hana tatizo na wewe, na kama kuna tatizo basi awaambie ni tatizo gani ili mnaposuluhisha mnakuwa mnajua mnasuluhisha juu ya tatizo gani. Sasa mnataka mie nikasuluhishwe na Kikwete bila kujua tunasuluhishwa kuhusu tatizo gani? Mtasema nini wakati wa kutusuluhisha? Na nyie mtakubalije kuwa wasuluhishaji bila kutaka kujua mtasuluhisha tatizo gani, mambo gani haya jamani?"

...nimabie nimekurupuka. Usione watu tuko JF ukadhani wote ni watu wa vijiweni tunakurupuka kama wewe. JF is a rich source of inside information. NIkikuambia naweza kuandika kitabu juu ya Mkapa usibishe, eboo. 😀😀😀
 
Synthesizer,
Wewe ukiambiwa uandike autobiography yako utaandika upuuzi wote uliokwisha fanya maishani ama utachagua tu yale ambayo yana staha na ambayo jamii ingependa kusikia? Ni vyema kama utaona inafaa kuandaa biography yake kama unaijua yeye autobiography aliyojiandikia ni sahihi!
Mkuu kama uppuzi niliofanya uko hadharani tayari, basi ni bora watu wakajua version yangu ya ukweli. Hivi kwa mfano, Mkapa hana maeleozo ya kuridhisha kuhusu kujiuzia Mradi wa Kiwira? Anapenda tubaki na version kwamba alifanya ufisadi na kaponea suala la kwamba raisi mstaafu hashitakiwi?
 
Kitabu kingetafsiriwa kwa kiswahili ili wengi wakisome, na kama wana kitu cha kukosoa wakosowe baada ya kufuatilia vyote alivyoandika na kuelewa.
Lakini pia, siku za karibuni kumekuwa na msukumo mkubwa ktk matumizi ya kiswahili, hadi ktk mikutano na wageni, sasa mbona tunarudishwa nyuma?
Angalia, Reginald Mengi, B. Mkapa, na huko nyuma Edwin Mtei. Kwani ni hadhira gani walikusudia kuigusa? Wazungu?Wasomi wa uni?Au?
 
Wabongo bana

Mtu anaanza kuchambua kitabu kabla hajakisoma
Hahaha


Wana historia yao wanayoijua, sasa wanaoanisha kama kaandika vyote vilivyotokea na wanavyohisi vina uzito. Pengine kitabu kilitakiwa kiwe na page 800 badala ya 320...
 
Hivi ktk hiki kitabu amegusia kuhusu maziwa makuu, yale maviwanda ya samaki ,na zile scandal

Maana kipindi chake ndio maziwa makuu vurugu zimepamba moto
 
Hajaeleza kuhusu alivyoua watu msikiti wa mwembechai na alivyoshiriki kumuuangamiza baba wa taifa.
 
Hawezi andika yote mkuu.noma nomaa

Waandishi mahiri wa Vitabu kwenye Utangulizi wao huwa wanaweka wakfu(dedication) ya kitabu kwa Mkewe, watoto au wazazi wao, Kuna habari za kuaminika kuwa mpaka Mkapa anateuliwa kuwa Mgombea Urahisi 1995 alikuwa akiishi kama Kapera(Bachela) yaani mtu asiye na mke...ilibidi Mwalimu amwite na kumlazimisha kurudiana na Mama Mkapa...!!! !!Haijulikani Mkapa ana watoto wangapi wa kike au wa kiume.....!!

Kuna kipindi Mama Anna Mkapa alionekana akiwa na muhogo(POP) kwene media kukawa na uvumi kuwa walitwangana Makonde kiasi cha kuumizana. Hata Mkapa alipokwenda kwa matibabu ya nyonga nje ya nchi nasikia alitenguliwa kiuono bada ya sekeseke...!!! Lakini pia kuna scandals nyingi sana za Mkapa kuhusu Ubinafsishaji hazijaguswa kabisa kwenye Kitabu chake cha His Life, His Purpose...!!!Mkapa pia ana sifa ya kukata maji kama mamba sina hakika kama atakuwa ameweka huo uhalisia wake...! Kama hakuweka basi kitabu hichi itakuwa ni ubabaishaji na kujimwambafai yeye na na askari wake wa Mwavuli numero one!!
 
Back
Top Bottom