Mambo muhimu ambayo Mzee Mkapa hajaweka wazi katika kitabu chake ''My Life, My Purpose''

Mambo muhimu ambayo Mzee Mkapa hajaweka wazi katika kitabu chake ''My Life, My Purpose''

Kifo cha Marehem Dr Omar Ali Juma kilitatatiza sana nacho si familia wala yoyote alieweza kuuona mwili wa marehem Dr Omar Ali Juma. Alifariki baada ya mauaji ya Pemba kutokea.
Dr Omar Ali Juma alifariki akiwa amelala nyumbani kwake familia yake (Mkewe na Mwanae) ndio walimpigia daktari wake aje kumpima
 
Ikiwa tutaka andike tuhuma na propaganda za vijiweni, basi hivyo vitakuwa vitabu.

Pili mwanadamu anavyozidi kupanda cheo kikazi ama kutajirika, basi ndipo anavyozidi kutungiwa mauchafu ya uongo na wasiomoenda, na pia misifa ya uongo na wanaompenda.

Tumesikia Mbowe ni mtoto wa Nyerere, tuamini na wengi twajua sio ukweli.

Tumesikia Nyerere ni mnyaruanda tena mtusi?
Tumesikia Agustino Mrema ni Msomali?
Tumesikia Mh.Amani Karume ni mtoto wa marehemi Dirie?

Sasa vitabu kuhusu hawa viongozi, zinahitaji kuzungumzia mambo yasio ya ukweli wala ushadi na hayathibitishiki?

Tuwe na akili na busara, tuachane na hii tabia ya kupayuka payuka ovyo
 
Ndugu si unatujua tulivyo wajinga, lakini wenyewe tunajiona wajanja. Bila uthibitisho na kufikiria tunakariri kama tape recorder, TAPE N PLAY
Cheni ya kilo Tano alikuwa anaovaa Shingoni? Au Mimi sijaelewa Mkuu
 
Dr Omar Ali Juma alifariki akiwa amelala nyumbani kwake familia yake (Mkewe na Mwanae) ndio walimpigia daktari wake aje kumpima
Alifanyiwa post-moterm examination na majibu yalikuaje? Alizikwa pemba fasta na familia hawakuruhusiwa kumuona.
 
JWTZ hawakuwa na tatizo na Salim. Salim alikataliwa na Zanzibar, ambao siku zote walimwona yuko upande wa Waarabu waliopinduliwa mwaka 1964 kwenye Mapinduzi ya Zanzibar. Tatizo ni pale ambapo Kikwete alitoa shinikizo kwamba asipopitishwa na CCM ataenda Chadema na akamwambia Mkapa nikienda Chadema nitashinda na historia itaandikwa CCM ilifia mikononi mwa Mkapa. Nasikia Mkapa akakubali, lakini kwa kuwa hakumwamini Prof. Mwandosya kuwa asingechukua hatua dhidi ya mambo ya "kifisadi" aliyofanya akiwa Raisi, wakakubaliana na Kikwete kwamba atashinikiza jina lake lipitishwe kwa masharti kwamba akistaafu mambo yake aliyofanya akiwa raisi yasiguswe, kutia ndani Kiwira, nyumba za serikali nk. Wakati huo Mkapa alikuwa na tuhuma nyingi sana za ufisadi, kutia ndani tetesi kwamba ABSA walimpa hoteli huko Afrika Kusini kama zawadi ya ubinafsishaji wa NBC. Na Mkapa zawadi kutoka makampuni binafsi alikuwa hazionei aibu kuzipokea!
inaonekana ulikuwepo kwenye ha yo makubaliano ya Mkapa na Kikwete. Anyway tunaojua kutazama nyuma ya Pazia tumeshakusoma kuwa hayo ni mambo yako ya kutunga tu na ukachanganya na story za kijiweni. LENGO LAKO LIKIWA NI UZANDIKI. Tatizo umesahau kuwa Humu ndani wengi ni GREAT THINKERS.
 
Nimekuelewa sana nahodha, bado inabaki ni utashi wake kwa kuzingatia dhumuni la kitabu chake.

Na mie bado naungana nawewe kwenye kilio cha hii tabia ya kusema unaandika maisha yako huku ukiacha mambo muhimu.
Mambo muhimu unayapima kwa mzani upi? Muhimu kwako ? Kwake? Ama kwa taifa? Ulitaka hadi aandike alivokua anatumwa nyanya sokoni? Demu wake wa kwanza and so forth!????? Ninini wewe unataka
 
Iringa Native,


Swali la Msingi1: Unafikiri kwanini EL alimuunga mkono JK, kwani yeye alikuwa hautaki Urais?
Swali la Msingi2: Unafikiri kwanini wanamtandao walimsimamisha JK na sio EL mwenye nguvu?
Swali la Msingi3: Unajua muasisi wa kundi la Wanamtandao?
Swali la Msingi4: Unajua nafasi ya JK kwenye kundi la wanamtandao ilikuwa nini?
Swali la Msingi5: Unajua kwanini Kundi la wanamtandao limekufa?
Swali la Msingi6: Unafahamu JK aligombea Urais 1995 na ukawepo mchuano na BWM (Chaguo la JKN).
Swali la Msingi7: Unafahamu sintofahamu iliyotokea chimwaga mbele ya JKN 1995 na BWM akawa mgombea wa CCM.

1.EL alishakuwa blacklisted na Nyerere alimuona ni fisadi so ilikuwa ngumu kutaka uraisi Nyerere akiwepo so walikubaliana aanze JK akimaliza miaka 10 atamuachia EL na estimation ni kuwa Nyerere asingekuwepo

2.JK ndio member aliyekuwa anakubalika kwenye makundi yote kuanzia TISS,JWTZ,Media,Viongozi wa dini,Chama (NEC,CC,UVCCM,UWT )tayari alikuwa na network kubwa ndio mgombea aliyekuwa anauzika.

3.JK aliutaka sana Uraisi lakini hakuwa na fedha so aliwatafuta wenzake akawapa idea wakakubaliana nae (EL,JK,RA,Makamba,Komba,Nchimbi,Salva,Kinana,Kingunge,Kamala,Kigoda,Membe,Makala) na wengine kibao

4.Again JK alikuwa ni playmaker ile charisma yake alikuwa anaweza kusikilizwa na pande zote even wapinzani wake tofauti na wenzake.Hakuwa na fedha kama wenzake bali fitina na mipango aiijua sana kuliko wenzake.Baada ya Nyerere kum-block mara ya kwanza ilikuwa impossible kumzuia hasa Nyerere alikuwa ameshafariki

5.Walichokubaliana wakati wanaanzisha mtandao hakikutimia baadae JK aliona EL anamzunguka na aligundua waliokuwa wanamtandao ndio walimuangusha kwenye utawala wake (walimhujumu)
 
Alifanyiwa post-moterm examination na majibu yalikuaje? Alizikwa pemba fasta na familia hawakuruhusiwa kumuona.
As i told you Dr Omary alifia nyumbani kwake akiwa amelala,mtu wa kwanza kumuona anakata roho alikuwa mkewe waliokuwa wamelala nae then alimuita mwanae wa pili ndio wakampigia mlinzi wake akamuita daktari wake ndio aka-comfirm kuwa amefariki.Dr Omar kwao ni Pemba ulitaka azikwe Kinondoni ?
Its obvious kwa waislamu kuzikwa mapema baada ya kufariki

For more info unaweza kuangalia hii documentary :Mkewe na wanae wanaeleza zaidi
 
Vp yale maisha yawatu kule zanzibar? Mkewe kujihusisha na bank ya kitapeli?
aliridhia tule majani yeye anunuliwe ndege? Alilazimika kukaa na mke kisa uikulu?...
 
Mkapa Ndiye aliyesababisba ushenzi wote unaoendelea mpaka leo!

Ilo la idala ya usalama wa taifa kukataa ni kweli ila kikwete alikuwa akiungwa mkono na JWTZ na Salim alikataliwa na jeshi na ndiye alikuwa apewe nchi so ndio ugumu ulipoanzia apo kwa Mkapa.
wewe unalijua vizuri hili swala. Nakumbuka Jwtz walimchukulia kikwete kama mtu wao ndio maana hata kipind cha kikwete kijana nyota mbili alikuwa na Prado na mjengo mbweni wakati wengine mbweni kipind cha kikwete ilikuwa haikamatiki
 
yes ilikuwa kubwa sana kiongozi, Mzee alikuwa anaivaa kama kikoi yaani inapita shingoni begani hadi kifuani chini ya mkono.... kuna kuda akiwa na press ilikuwa inaonekana kwa nadra nadra ....pembeni pembeni kwa suti.
Kwa chai hujambo kijana wangu
 
yes ilikuwa kubwa sana kiongozi, Mzee alikuwa anaivaa kama kikoi yaani inapita shingoni begani hadi kifuani chini ya mkono.... kuna kuda akiwa na press ilikuwa inaonekana kwa nadra nadra ....pembeni pembeni kwa suti.
Mkuu tumekukosea nini?
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]we mkuu
yes ilikuwa kubwa sana kiongozi, Mzee alikuwa anaivaa kama kikoi yaani inapita shingoni begani hadi kifuani chini ya mkono.... kuna kuda akiwa na press ilikuwa inaonekana kwa nadra nadra ....pembeni pembeni kwa suti.
 
Back
Top Bottom