Kigi Makasi
JF-Expert Member
- Oct 4, 2022
- 1,259
- 2,483
Naweka kambi
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Brother you're life story is so much appreciated 🙏EPISODE 16: Mthamini sana mtu anayeona una kitu ambacho wewe mwenyewe hukioni
Katika maisha yetu ya kawaida iwe kwenye ajira, mtaani au shuleni kuna wale watu ambao wanaweza wakakushauri au kukulazimisha ufanye mambo ambayo wewe jukuwa na wazo nalo au hukujua kama unauwezo wa kulifanya jambo husika. I want to talk about the importance of appreciating and valuing individuals who recognize qualities, potential, or aspects of yourself that you might be unaware of or underestimate, in supporting one's life.
Baada ya kumaliza kile kikao Dodoma tulirudi ofisini kuendelea na majukumu kama kama kawaida. Namshukuru Mungu nilimaliza probation period salama na officially nikawa full employed pale. Kwa ambao mnategemewa kuwa waajiriwa wapya msishangae nakazia kazia sana swala la kumaliza probation period salama, labda niwaambie tuu hiki ni kipindi muhimu sana kwa mfanyakazi mpya kwenye kazi yako au ajira yako mpya. Ni kipindi ambacho mwajiri wako anakupima kama kweli unaweza kuleta tija kwenye kampuni au ni mzigo. Hii inaenda sambamba na kukupima kwenye uwezo wa kutekeleza majukumu yako, uwezo wa kujifunza au kumasta mazingira ya kazi kwa haraka, namna unavyoshirikiana na wenzako pale kazini, maadili ya kazi na swala la nidhamu kwa ujumla, just to mention the few. Makampuni au mashirika mengi mara ntyngi wanatoa kati ya miezi mitatu mpaka sita kulingana na utaratibu wa ofisi husika. Na katika kipindi hiki mara nyingi unakuwa hupewi kwanza stahiki zako zote muhimu mfano bonus kazini na wengine wanakupa kwanza nusu mshahara. Ukifanikiwa kumshawishi mwajiri basi unakuwa unapewa barua yako kwamba you have been successfully completed your probation period and you are endorsed as full employee. So kwa mfanyakazi mpya hicho ni kipindi cha kuwa makini sana ili usiwape sababu ya kukupiga chini au kukuongezea muda wa probation (Probation extension period).
Basi bhana nikawa napiga mzigo pale kutekeleza majukumu yangu kama kawaida. Sasa kwenye ile program mimi nilikuwa na-lead social deparment. Lakini kulikuwa na department nyingine kama medical na M&E. Sasa kwenye kufanya fanya kazi pale karibia tunamaliza mwaka mmoja tangu ile program ianze, ikatokea msala wa mambo ya safeguarding issues pale ofisini. Kwa wasiofahamu, safeguarding issues are the actions or behaviors by employees that may harm or compromise the well-being, safety, dignity, or rights of the individuals the project aims to assist. Inaweza kuwa maswala ya upendeleao, kuomba ngono kwa wanufaika wa progamu, any form of harassment, fraud nk. Ili kupambana na maswala ya safeguarding issues mara nyingi mashirika au makampuni yanakuwa na sera au miongozo ya kuwalinda wafanyakazi na wanufaika wa miradi by providing regular training to employees, establish reporting mechanisms, and conduct thorough investigations when concerns are raised.
Baada ya investigation ule msala uliondoka na watu wengi tu pale ofisini akiwemo jamaa aliyekuwa ana-lead department ya medical. Ile ishu ilichafua hali ya hew asana pale ofsini na kulitokea kuwa na magepu mengi ya kazi. Wazungu wapo seriazi sana na mswala ya safeguarding yaani wanayachukulia kwa uzito mno. Sikuwahi kuexperience hasira za wazungu kwenye kazi lakini kwenye ile ishu walikasirika mno, ilitumwa timu ya investigators kutoka makao makuu Europe pamoja na Nairobi kuja kufanya uchunguzi pale. Nakumbuka shughuli za ofisi zilisimama kama mwezi kupisha uchunguzi na kila mmoja aliwekwa kitimoto hadi CD mwenyewe.
Watu matumbo yaliwaka moto, yaani moja haikai mbili haisimami. Unajua kwenye haya mambo yanayohusisha uchunguzi usiwe unajiamini moja kwa moja hata kama hujafanya maana anaweza akaibuka mtu mwenye visa na wewe akakupigilia kitu kizito ukajikuta na wewe upo kwenye victims. To survive in such issues ni Mungu aingilie kati. Hata baadhi ya watu waliopigwa benchi akiwemo yule leaders wa medical department binafsi ilinguwa ngumu sana kuamini ila ndio hivyo majibu ya uchunguzi yaliomdaka na yeye. Wakati wote wa uchunguzi watu tulikuwa tunaogopana kama ukoma pale ofsini kifupi ilikuwa uwe umehusika au hujahusika kujiamini kulipungua kama sio kutoweka kabisa. Ni kama unapokuwa unasubiria majibu ya ukimwi hata kama ni bikra wa kiume au kike kale kamoment ka kusubiria kanakuletea kahofu flani ka kutokujiamini amini hahaaa.
Basi siku ya siku majibu yakakamilika, kikaitishwa kikao cha staff wote pale ofsini, tukaunganishwa na management ya Nairobi na makuu then report ikasomwa. Kisha maamuzi yakatolewa kwa waliokutwa na ule msala wanaachishwa kazi mara moja kwa mujibu wa sera ya safeguarding. Victims wakaaambiwa kama hawajaridhika na maamuzi wanaweza kwenda kwenye vyombo vya sheria ndani ya mwezi mmoja na kwa muda huo walitakiwa wakabidhi kila kitu cha ofisi. Kwa sisi survivors tulipigwa mkwara mzito kwamba ofisi haitakuwa na mswalie mtume kwa yoyote itakapothibitika kwamba mfanyakazi amejihusisha na violation of safeguarding policy.
Kwa kuwa maamuzi yalikuwa yameshatolewa mara paap wakaingia polisi pale, nafikiri waliandaliwa mapema ili kusimamia zoezi la kukabidhiana ofisi. Nadhani walijihami maana huwezi jua mtu atalipokeaje swala la kufukuzwa kazi tena gafla unaweza ukadundwa au kuuliwa hivi hivi. Basi zoezi la kukabidhi ofisi lilifanikiwa na kwa wale waliokuwa na madeni wanaodaiwa na ofisi wazungu waliamua kuwasemehe, yaani kama walikuwa wanaona kero hata kuendelea kuwadai. Nakumbuka kuna mshikaji mmoja ndio alikuwa ametoka kuchukua advance salalry ya miezi minne na alikuwa hajaanza hata kulipa/kukatwa akawa ametimuliwa na ofisi haikujali.
Nakumbuka baada ya wenzetu kuondoka na wale investigators kurudi kwao maisha yalikuwa magumu sana pale ofisi watu ni kama morale ilishuka sana. Hata shughuli nying zilikuwa haziendi kwa sababu nafasi nyingi zilikuwa wazi. Ikabidi makao makuu wafikiria kurestructure ofisi ya Tanzania ili kuangalia ni namna gani ya kurudisha ufanisi wa ofisi na kujaribu kudhibiti swala kama lile lisijirudie tena. Ikabidi CD na Head of Programs wasafiri kwenda makao makuu kwa ajili ya kulishughulikia hilo. Maana hao ndio walikuwa ndio mabosi wenyewe wa pale ofsini. Iko hivi pale ofisini kulikuwa na nanagement team na baadhi ya wafanyakazi tunaweza kusema ni kudumu kwamaana ya kwamba hawakuwa wanaajiriwa na miradi. Yaani ni hivi hapa tuwekane sawa kidogo, mfano mimi na wenzangu wengine tuliajiriwa na mradi ambao tulikuwa tunautekeleza kwa miaka minne. Kulikuwa pia na miradi mingine tofauti tofauti ambayo nayo pia ilikuwa inaajiri project team yake. Sasa project staff mnaajiriwa na mradi na mnaondoka mradi ukiisha, labda kama kuna mradi mwingine unaweza ukaomba endapo mradi wenu utakuwa umeisha. Lakini kulikuwa na wale ambao tunaweza sema ni wakudumu yaani wao wanaajiriwa pale bila kutegemea miradi ndio akiwemo huyo CD na huyo Head of Programs. Ndio ilivokuwa sijui kama nimeeleweka.
Kule ulaya kwenye kikao chao walikuja na strategies mbalimbali na mabadiliko kidogo ili kuendana na kasi ya utekelezaji wa mradi wetu. Baada ya two weeks walikuwa wamesharudi ofisini na wakaitisha kikao cha staff wote. One hour before the meeting CD akaniita niende ofsini kwake. Nilisthuka kidogo maana haikuwa kawaida CD kukuita ofsini. Mara nyingi kama kulikuwa na jambo anataka mjadiliane alikuwa anakuja mwenyewe kwenye ofisi yako. Ishu ya kuitwa ofsini wafanyakazi wa pale tuliichukulia kwa uzito kidogo. Kihoro kikanishika sana nikajisemea isije ikawa wale investigaors walilisahau jina langu na sasa ndio naenda kuhukumiwa. Usicheke ile situation ilikuwa ni ngumu mno kwa siku ile. Nikasema huyu labda anataka kuniandaa kisaikolojia ili kwenye kikao nikipigwa na kitu kizito isiwe cha kunishtukiza.
Basi nikaingia akanikaribisha pale na straight forward akanimbia “Taidume, the management has entrusted you with leading the medical department, and now you will serve as our medical-social coordinator”. Nikashtuka sana nikamtumbulia macho pale huku nikiwa nina maswali mengi sijui hata nianze kuuliza lipi lifate lipi. Maana nikawa nakiuliza mimi mtu wa massosholoji huko wapi na wapi leo kulead mambo ya madakatari? Alipoona nashangaa akagongomelea kwa kuniambia najua unashangaa hususani kwa kuwa wewe sio daktari na tunakutaka uchukue nafasi ya dakta ………… (akamtaja yule daktari aliyetimuliwa), lakini nikuhakikishie tuu sisi kama menejimenttumekujiridhisha kwamba utaweza.
Binafsi sikukubaliana naye kabisa nakumbuka kile kikao cha mimi na yeye kilichukua kama nusu saa nzima. Mimi nilikuwa nampa hoja zangu za kukataa ile nafasi lakini yeye anazipangua kwa kuniaminisha kwamba naiweza ile nafasi. Sasa, mimi sio kwamba nilikuwa tu siitaki ile nafasi lakini nilikuwa naona napwaya na italeta shida kwenye ufanisi wangu. Maana kwanza nilikuwa nawaza kwa harakaharaka pale namna yule dakatari alikuwa anafanya kazi zake. Yeye shughuli zake kubwa alikuwa anafanya na madakatari wenzake mikoani na wizarani, maswala ya kusimamia upimaji, utoaji dawa na ufuatiliajo wa maendeleo ya walengwa wetu. Kwanza nilikuwa namsikia tu hayo mabombastic ya kidaktari anaovoongea na madaktari wenzie basi mimi nikawa navurugwa tuu nikaona huyu CD vipi huyu naona ananitafutia tuu sababu ya kunitimua kazi maana performance ikiwa ndogo nayo ni ishu sana kufanya kazi na wazungu.
Nakumbuka tulivutana sana kwenye hilo. Mwisho wa siku CD akanipa job description ya ile position akasema tuzijadili moja moja. Yeye akawa anasoma kipengere kimoja kisha ananiuliza nimekiewlewaje? Nikawa naelezea kile kipengele nilivokielewa. Kwa ufuoi inaonekana aliridhika na jinsi nilivovielewa vile vipengere vya job description. Mwisho wa siku akaniuliza hapo sasa ni ni kigumu kwako? Kiukweli nilivyovipitia ile vipengere vya majukumu, asilimia zaidi ya 70 ilikuwa ni kuoragnize na kucoordinate the project implementation partners watekeleze majukumu yao within time and budget, baasi. Sikuhitajika kuwapima walengwa, wala kutoa dawa, wala kutoa ushauri wa kidaktari, hizi zote walikuwa wanatakiwa kufanya madakari wa mikoa husika huko tunakofanya kazi. Kwahiyo sikuhitajika kuvaa koti jeupe na Stethoscope kama madaktari wanavofanya. Yale mambombastic ya kidaktari zilikuwa ni mbwembwe za kututisha wengine hahaaa. Maana nakukumbuka kwenye zile reflection meetings au weekly feedback meeting na kupeana updates za mradi yule bwana daktari alikuwa anashusha vigongo sana mpaka wengine tukawa tunajisemea kumbe udaktari ni mgumu hivi na inaonekana wanaakili sana madaktari (jokes).
Basi nakumbuka CD akanikumbusha ile ishu niliyoorganize meeting na watu watu wa wizara ya afya wakati tunaenda kuutambulisha mradi, ile ambayo nilipata msala wa kusekwa sello. Akaniambia, that was an excellent entry point that the management team built trust in my coordination abilities. Nikajisemea laiti mngejua nililazwa selo sijui ingekuwaje hahaha. CD akaniambia “Taidume wewe una kitu kikubwa sana sema tuu hujijui. Naweza nikakuambia ilikuwa rahisi sana mimi kushawishi menejimenti kukubaliana tukuongezee hiyo idara kwa sababu naamini una skills na uwezo wa kudili na complex issues katika kudeliver project results”. Mimi nikamwambia kama vipi anipe muda nikafikirie, akanikatalia na kuniambia that was like an order to me and he is going to officially announce that to all staff in the meeting. Akaniambia tukimaliza mkutano atanipa my new contract.
Kwa upande mmoja nilikuwa na hofu lakini kwa upande mwingine nilikuwa nilikuwa na furaha. Hofu ilikuwa vipi je nitaweza kuhandle yale majukumu maana ilikuwa ni kama nafasi mbili kwa moja. Lakini pia niliassess the situation nikasema hapa lazima vijimaneno vitazuka maana wakati wa investigation kama ilivokawaida kunakuchomana sana, sasa nikawa nahofu kwamba lazima kuna watakaofikiria kwamba niliwachoma watu na asante yake ndio hiyo nafasi. Maswala ya uchawa hayo. Kwaupande mwingine nilifurahi kwa sababu hakuna kitu kizuri kama kuaminiwa tena wakati wewe mwenyewe ukiwa haujui kama una huo uwezo. Inakupa faraja sana, nilishawahi kuaminiwa katika maswala mbali mbali lakini haikuwa kwenye levp ya surprise kama ile. Nikajisemea mwenyewe let me take it, mambo mengine yatajiset juu kwa juu.
Basi tulikubalina hivyo. Muda wa kikao ulipofika staff wote tulikuwepo. Basi CD pamoja na mabo mengine akatoa mrejesho wa safari yao ya makao makuu. Akatoa feedback ya mikakati mbali mbali waliyokubalina na management team namna bora ya kuendesha ofisi ili swala lile lisijirudie tena. Watu wakauliza maswali na yakajibiwa na kusisitizana kuhusu hiyo mikakati mipya, mwisho wa siku CD akatangizia kwamba kuna baadhi ya nafasi zitatafutiwa watu wengine lakini kawaambia kuhusu ishu ya mimi kuwa appointed to lead also the medical unit of our project. Watu wengi hawakutegemea na walipigwa na mshangao, lakini ilibidi wakubaliane na ukweli huo maana ilikuwa tayari imeshaamuliwa na management tena kwa kupewa Baraka zote kutoka makao makuu. Basi walinipongeza pongeza pale na ndio ikawa stori kubwa ya siku.
Tulipomaliza mkutano, nikaenda ofisini kwa CD nikamkuta wakiwa na HR. basi nikakabidhiwa contarct yangu nikatakiwa niisaini by kesho yake maana ile position ilitakiwa ianze immediately. Nikaingia ofsini kwangu nikawa naipitia mdogo mdogo. Najua wengi mtataka kujua kama kulikuwa na nyongeza ya mshahara. Ofcourse kambuzi kaliongezeka kidogo japo kalikuwa bado hakajanona kiviile. Mimi nikausaini hapo hapo na kurudisha nakala moja kwa HR, officially nikaanza majukumu mapya. CD aliandika barua kuwasiliana na partners wetu hususani wale wapya kwangu (madaktari) kuhusiana na mabadiliko ya ile nafasi, huku akiwaomba ushirikiano.
Nikapanga mkakati wa kwenda kutembelea maeneo yote ya mradi ili kufahamiana na partners ili kwa pamoja tuweze kuweka mikakati mipya. Kwakweli nashukuru walinipa ushirikiano wa kutosha sana na tulifanya kazi kwa ushirikiano mkubwa sana. Changamoto ndogondogo ni kitu cha kawaida na tulifanikiwa kuzimaliza na kusonga mbele.
Kiufupi na kwa ile ofisi ya wazungu nilifanikiwa kujiimarisha au kuongeza ujuzi katika maeneo yafuatayo
Experience in designing and implementing projects. Skills in project planning, budgeting, and resource management. Understanding of project lifecycle from inception to evaluation. Knowledge of fundraising strategies and techniques. Leadership skills in supervising personnel and resources. Ability to coordinate with implementing partners including government officials Skills in monitoring program effectiveness and impact. Relationship-building with community leaders, government, and local organizations. Identifying and addressing training needs for staff, partners, volunteers, and local organizations. Presentation skills for sharing program reports and findings with management, donors, and stakeholders.Nilifanya ile kwa muda wa miaka minne na tukafanikiwa kuhitimisha na kuumaliza ule mradi salama salmini. Mradi uliisha tangu Disemba 2022 lakini mimi niliombwa kubakia pale ofsini kwa miezi mingine mitatu kusaidia kukamilisha baadhi ya mambo hususani mfadhili wa mradi alikuwa anayahitaji. So officialy nilirudi uraiani mwezi wa tatu na kuanza harakati mpya za kusaka ajira nyingine.
MWISHO:
Wadau wangu yapo mengi sana ambayo ningeweza kushea nanyi naomba mniwie radhi kama haya machache hayakuwatosha. However, as I reflect on the chapters of my professional journey, each episode has been a lesson with the vibrant sort of experience. Your time invested in reading my story is sincerely appreciated. In sharing these moments of growth, challenge, and achievement, my hope is that you have found inspiration and some thing to takehome as an assignment.
Nimesoma na nitaendelea kuzisoma koments zenu kwa umakini mkubwa na binafsi nimefarijika kwa maoni, maonyo, mafunzo na mijadala ambayo imekuwa ikiibuka katikati ya stori, hahaa hii ni kawaida. Kwa pale nilipoweza nilitoa na nitaendelea kutoa ufafanuzi na kwa wale wanaonifata PM for more detals, I respect and salute you guys.
Kwa kipindi hiki ambacho nahangaika huku na huko kusaka sehemu nyingine nafanya kazi za kujitolea kwenye maeneo mbalimbali hususani vile viNGO vidogo ambavyo ndio vinaanza. Pia kuna watu hata humu JF wapo tunasaidiana kudizaini concept notes na kuandika full project proposals. Huwa najitolea kwa wale ambao nimehakikisha hawana uwezo, maana hata mimi nikiangalia nilikopita pita mpaka hapa nilipo sijawahi kutoa hata sh10 ili kusaidiwa.
Nipo hapa pia kuendelea kutoa uzoefu wangu kwa yeyote ambaye anaona nitafaa kushea naye ninachokifahamu muda na wakati wowote. Na pia ninawaahidi kama nitafanikiwa kupata sehemu nyingine ya kupiga mzigo basi niatwashirikisha hapa hapa. Kwa sasa bado natafuta kazi.
Thank you guys niwatakie maandalizi mema ya sikuku za mwisho wa mwaka na heri sana ya mwaka mpya 2024 kwenu woote. Na kama kuna mtu kwa namna moja ama nyingine nimemkwaza naomba anisamehe, Mungu awabariki sana.
MIALIKO YA SIKUU INAKARIBISHWA PIA
TaiDume 0748 586 059
Nimesoma andiko lako lote.Kwa kweli nimependa uhandishi wako. Watu wengi wanakwazika mwandishi anapoamua kuchanganya Kiswahili na Kiingereza ila mimi ninapenda sana kwani ni Swaga nzuri,ila kingine kuna maneno au situation ukiiwasilisha kwa Kiingereza inaleta mvuto mzuri sana.UTANGULIZI
Wakuu habari.
Naandika hii story yangu ikiwa ni mwaka sasa nipo mtaani nikiendelea na harakati za kusaka ajira mpya toka mkataba wangu wa ajira ulipoisha mnamo Desemba 2022. Nimeamua kushea uzoefu wangu kwa mtindo wa Masimulizi (katika episodes) kwa kuamini pengine inaweza kuwa na mafunzo kwa waajiri, waajiriwa au wanaotegemewa kuajiriwa. Naomba moderatoes wa JF wauache huu uzi wangu hapa hapa kwenye Jukwa la Ajira kwani muktadha wa simulizi hii maswala ya kubadilishana uzoefu katika swala la ajira na sio mambo ya entertainment. Twende kazi.
Episode 1: Sikuogopa kujidhalilisha ili kupata reliable connection
Mwaka 2011 nilipomaliza my 1st degree kama ilivo kwa wanachuo wengine, nilikuwa na expectation kubwa sana ya kupata ajira nzuri ndani ya muda mfupi. Hii ilijengwa na kiburi kwamba mwaka mmoja before sijamaliza niliwaaproach ndugu na wadau kwenye network yangu kwamba mwakani namaliza. Kila mmoja alinipromise kunisaidia kupata job au kuniconnect na waajiri mbali mbali. Swala likawa ni kwamba wewe maliza tu chuo then utuambie ili tukafanyie mipango.
Kimbebe kilikuja baada ya kumaliza. Nilitulia kwanza mwezi mmoja then nikaanza kucheki walionipromise job kwamba I am available. Asee nilipigwa dana dana za kutisha na mwishowe wengine wakawa hata hawapokei simu zangu. Nikiwaibukia nyumbani au maeneo yao ya kazi wanaishia kunipa nauli ya kurudia na kuniambia ajira ngumu cha muhimu wewe endelea kumuomba Mungu. It was very disappointing situation at that time na nikafikia hatua ya kuanza kuwachukia bila sababu as if wao ndio wanaonisababishia ugumu wa kuajiriwa, hahahaaa.
Basi nikaanza kuumiza kichwa how to go about finding the job. Nikaaply sana kazi kupitia job adverts za mtandaoni lakini mimi mwenyewe nikaona as a fresh graduate I didn’t have the skills and required experiences. Nikaanza kuona hata elimu yenyewe may be course niliyosoma haina maana bora lile boom ningelitumia kwa kuanzisha hata kimradi cha kuchoma popcorn mtaani.
Hali ilikuwa mbaya to most of the graduates maana kila nikiwacheki wana nao wanalalamika kama mimi tuu isipokuwa wachache sana wenye connection tena za familia zao za kuzaliwa. Hapo nikakumbuka wakati naenda kuanza form 5 way back bro wangu aliwahi kuniambia “dogo huko shule nenda kawe na marafiki wa aina mbili, either wenye akili sana darasani au wale wanaotoka kwenye familia bora”. Nilikuja kumwelewa kipindi hiki ni nini bro alichomaanisha. Kwamba wale wenye akili sana darasani watakuinfluence kufauru na wale wanaotoka maisha bora ni future asset katika connection za ajira.
Sasa mimi kutoka na usela wangu mavi wa teenager sikuwa na hata mmoja kati ya hao. Roho ilikuja kuniuma zaidi nilipogundua nilipokuwa advance niligombana na jamaa mmoja ambaye kwao walikuwa wapo poa sana wa kutokea mkoa wa Iringa, nilipooulizia habari zake nikasikia kwa kipindi kile natafuta ajira alikuwa ni msimamizi wa kampuni ya usafirishaji mizigo(malori) na walikuwa na ofisi zao bandarini (clearing and forwarding). Laiti yule jamaa ningemfanya best friend ukute ingekuwa rahisi kwa yeye kunipa mchongo. Anyway, les forget about him.
Nakumbuka siku moja nikiendelea kusaga visigino katika harakati zangu za kutembeza bahasha, kwenye foleni nikamwona lecturer wangu mmoja hivi, tumuite Dr KJ (PhD ya kihaya hiyo) kwenye shangingi lake akiendeshwa na dereva wake kama kawaida. Huyu lecturer nilimkumbuka kwa sababu alikuwa na sifa sana kwenye vipindi vyake na alikuwa anafundisha somo la project Management.
Yaani huyu Muhaya alikuwa anatumia nusu ya muda wake kwenye lecture kujisifia. Ataanza kuwananga maprof kwamba japo yeye ana PhD ila hakuna prof anaemzidi akili na pesa chuo kizima, kwanza yeye anaendeshwa na mshahara anamlipa dereva wake ni sawa na wa tutorial assistant wa pale chuo. Alikuwa mdhalilishaji sana kwa wanafunzi hususani watoto wa kike au wanaofeli somo lake.
Ila watu walichompendea jamaa alikuwa sometimes anagawa sana maokoto akiwakuta wanafunzi njiani ila ndio mjue mtadhalilishwa. Jamaa alikuwa anatembea na dola au Euro akidai pesa za madafu ni nzito, hatukujua anapata wapi zile dola dola. Nakumbuka kuna semester alimlipia ada jamaa mmoja alikuwa anasoma kwa shida sana alikuwa hana boom. Alimlipia ada ya semester ya mwisho ila yule jamaa cha moto alikiona maana Dr KJ kwenye kila kipindi alichofundisha kwenye madarasa yake lazima amtolee mfano yule jamaa mpaka mlipiwa ada akawa famous chuo hahahaaa.
Basi bhana nilipomwona kwenye foleni Dr KJ vitu vingi vingi vikapita kama mshale kwenye mawazo yangu. Kwamba huyu jamaa anaweza akawa asset lakini anaweza akanidhalilisha vibaya sana na nitamuanzaje yupo kwenye gari. Je atanikumbuka maana wanafunzi tulikuwa wengi sana. Lakini nikifikiria pale geto nadaiwa kodi mwenye nyumba keshanivumilia kama two months (niliamua kukomaa mjini sikutaka kwenda mkoani).
Wakati naendelea kuwaza foleni ikaanza kutembea, asee sijui ni nini kilinikuta nikajikuta naikimbilia ile gari na kwenda kuisimamia kwa mbele nikiizuia isiende huku nikimwonyeshea ishara dereva apaki pembeni. Dereva alipoona anaweka foleni akamuuliza bosi wake wafanyeje hahaaa maana nacheka kama ni mazuri. Basi Dr KJ kwa wasiwasi akamwambia aweke pembeni.
Basi nikasogea upande wa Dr KJ akawa hataki kushusha kioo, akanielekeza niende upande upande wa dereva. Nikajua tuu boss anaogopa labda nitamdhuru so he decided to sacrifice his driver- hahahaa. Basi nikaenda upande wa dereva aliposhusha kioo nikamsalimia.
Mimi: shikamoo Dr KJ
Yeye: Unanifahamu?
Mimi: Ndio wewe ni mwalimu wangu wa somo flani nimemaliza mwaka jana.
Yeye: (Bado akiwa na wasiwasi) Nitaamini vipi na kwanini unanisimamisha kama jambazi?
Mimi: (Bila kujiuma uma) Naomba unisamehe sana Dr, ni kuvurugwa na hapa nimeona kama bahati
kukuona. Dr mimi nipo katika harakati za kutafuta kazi, nimekusimamisha ili nikuachie CV yangu maana naamini wewe network yako ni kubwa pengine unaweza ukaniconnect na wadau wako.
Yeye: (Akacheka sana huku akiniita niende upande wake). Kwa hiyo unatafuta kazi gani?
Mimi: Kwa sasa nahitaji sehemu yoyote ya kujishikiza ili nipate uzoefu, lakini uzuri wewe ni mwalimu wangu wa PM so unaweza ukaona ni wapi zile theory wapi naweza kuziapply.
Akaniangalia sana kisha akaniuliza unajua nini kuhusu project management na principles for effective project management? Nikamshushia madude kwa style ambayo nadhani ilimkamata kisawa sawa. nIkamsisitizia kwamba mimi sijawahi kushikwa kwenye somo lake. Baada ya kumjibu pale akaniambia. Mbona unaonekana una njaa sana? Shika hii nenda kale mimi nina mambo mengi sana na hapa unanichelewesha tuu. Sikupokea kwanza ile pesa ila nikamwambia Sir please just take my CV may you can see how you can help.
Akaniuliza, sasa CV yako umeandika nini wakati hujawahi kufanya kazi popote? Halafu sina muda wa kutembea na makaratazi kwa gari yangu. Akawa anafunga kioo, asee nikaking’anga’ania. Akaniambia unataka nini sasa pesa nimekupa umekataa. Nikamwambia, kama huwezi kutembea na makaratasi basi naomba email address yako ili nikutumie. Akaniangaliaa, kisha akatoa business card akanipa. Mimi nikaicheki nikaona ile biz card sio yake ni ya mdada. Nikamwambia mbona sio yako. Akaniambia “vizuri sana upo makini, mpigie huyo dada simu kesho muda kama huu”. Hiyo ilikuwa ni kama saa tisa hivi. Kisha akanipa ile pesa, akasepa zake.
Mwendelezo=>
Sehemu ya 2
Sehemu ya 3
late vyoombo mwan'nguWaswahili wengi hawajui kiswahili, neno kujishusha na kujidhalilisha zina maana tofauti kabisa sema tu watu vichwa vigumu wanaforce.