Nafaka
JF-Expert Member
- Feb 17, 2015
- 12,154
- 31,246
Kuna siku nilikuwa nachat na mdada flani mwenye pesa zake, lakini ana ndoto za kuolewa na mzungu. Hivyo anatumia muda mwingi kwenye online dating platforms akitafuta bwana wa kizungu. Katika kuzungumza akawa amenitajia mtandao flani ambapo kila msg unayotuma inalipiwa. Akaniambia kuanzia mwaka jana mpaka mwaka huu mwezi wa saba ameshatumia $7000 kulipia hiyo huduma. Nilishtushwa sana inawezekanaje mtu kutumia pesa hiyo yote. Na mbaya zaidi pesa nyingi kazitumia kwa mtu mmoja tu ambaye anaonyesha interest ya kama wako karibu
Nikamuuliza kama washakuwa karibu kwanini wasipeane njia nyingine za kuwasiliana kama email, au whatsapp number ili wawe wanawasiliana bila kutumia pesa. Akasema yeye alimpa namba yake, na email ila jamaa hajawahi kumtumia any msg whatsapp wala kwenye email hivyo akitaka kuwasiliana naye mpaka aende kwenye huo mtandao. Nilianza kuhisi kuna jambo haliko sawa na nikahisi huenda jamaa hamtaki huyo dada huwa anachat naye tu.
Juzi juzi hapa ndipo nilikuja kupata jibu la swali langu. Mimi muda mwingi nakuwa online nafanya shughuli za freelancing as my full time job, sasa juzi juzi nikaona kuwa jamaa anatafuta watu wa kumanage customer support online services. Kumcheki, akaniambia nimchek whatsapp akanipa namba nikamcheck whatsapp akanipa link ya skype, kuiclick ikanipeleka kwenye group flani la skype. Kufika mle nikakutana watu kibao na halikuanza leo yani kuna members wengi sana na shared documents nyingi sana na wanajadili kuhusu seminars ambazo washapata.
Mimi nikatumiwa document moja ili niisome. Nilipoisoma ndipo nikajua nini kinaendelea. Kwanza, kumbe ni kazi ya kuchat na watu wanaotafuta wapenzi, yani mtu akiingia kwenye ule mtandao ataona profile ambayo itakuwa na picha fake na kila kitu fake atakuchagua mtaanza chat, na ni kwamba leo anaweza chat na mimi kesho akachat na mwingine akidhani ni same person. Na kwa wakati mmoja mtu anaweza kuwa anachat na watu zaidi ya watu wakiwa wao wanadhani wana chat na mtu mmoja au watu tofauti.
Kuna jinsi ya kuhandle unafundishwa, lugha utakayotumia na huruhisiwi kuwa unatuma sentence zinazofanana iwapo unachat na watu tofauti kwa wakati mmoja. Kitu kingine huruhusiwi kumfanya mtu aone kama umekubali kuwa mpenzi wake, au kupanga miadi ya kukutana, au kubadilishana namba au mawasiliano ya aina yoyote. Ikitokea akakupeleka huko au akakutumia mawasiliano we ignore anzisha topic nyingine.
Jambo lingine hakikisha mtu unamuuliza maswali ili umfanye asiondoke yani umfanye aendelee kuchat kwasababu kila msg anayotuma anakatwa pesa na wewe unalipwa kutokana umechatisha watu msg ngapi.
Kuna mengi hata document sikufika mwisho nikamwambia jamaa mimi siwezi kufanya kazi hiyo nikajitoa. Ila nikajua kumbe yule mdada alikutana na kitu cha namna hii. Ndiyo maana jamaa alikuwa hampi mawasiliano na alipompa ya kwake alikuwa ana ignore wala hata hashukuru kusema ameyaona.
Nikamuuliza kama washakuwa karibu kwanini wasipeane njia nyingine za kuwasiliana kama email, au whatsapp number ili wawe wanawasiliana bila kutumia pesa. Akasema yeye alimpa namba yake, na email ila jamaa hajawahi kumtumia any msg whatsapp wala kwenye email hivyo akitaka kuwasiliana naye mpaka aende kwenye huo mtandao. Nilianza kuhisi kuna jambo haliko sawa na nikahisi huenda jamaa hamtaki huyo dada huwa anachat naye tu.
Juzi juzi hapa ndipo nilikuja kupata jibu la swali langu. Mimi muda mwingi nakuwa online nafanya shughuli za freelancing as my full time job, sasa juzi juzi nikaona kuwa jamaa anatafuta watu wa kumanage customer support online services. Kumcheki, akaniambia nimchek whatsapp akanipa namba nikamcheck whatsapp akanipa link ya skype, kuiclick ikanipeleka kwenye group flani la skype. Kufika mle nikakutana watu kibao na halikuanza leo yani kuna members wengi sana na shared documents nyingi sana na wanajadili kuhusu seminars ambazo washapata.
Mimi nikatumiwa document moja ili niisome. Nilipoisoma ndipo nikajua nini kinaendelea. Kwanza, kumbe ni kazi ya kuchat na watu wanaotafuta wapenzi, yani mtu akiingia kwenye ule mtandao ataona profile ambayo itakuwa na picha fake na kila kitu fake atakuchagua mtaanza chat, na ni kwamba leo anaweza chat na mimi kesho akachat na mwingine akidhani ni same person. Na kwa wakati mmoja mtu anaweza kuwa anachat na watu zaidi ya watu wakiwa wao wanadhani wana chat na mtu mmoja au watu tofauti.
Kuna jinsi ya kuhandle unafundishwa, lugha utakayotumia na huruhisiwi kuwa unatuma sentence zinazofanana iwapo unachat na watu tofauti kwa wakati mmoja. Kitu kingine huruhusiwi kumfanya mtu aone kama umekubali kuwa mpenzi wake, au kupanga miadi ya kukutana, au kubadilishana namba au mawasiliano ya aina yoyote. Ikitokea akakupeleka huko au akakutumia mawasiliano we ignore anzisha topic nyingine.
Jambo lingine hakikisha mtu unamuuliza maswali ili umfanye asiondoke yani umfanye aendelee kuchat kwasababu kila msg anayotuma anakatwa pesa na wewe unalipwa kutokana umechatisha watu msg ngapi.
Kuna mengi hata document sikufika mwisho nikamwambia jamaa mimi siwezi kufanya kazi hiyo nikajitoa. Ila nikajua kumbe yule mdada alikutana na kitu cha namna hii. Ndiyo maana jamaa alikuwa hampi mawasiliano na alipompa ya kwake alikuwa ana ignore wala hata hashukuru kusema ameyaona.