Uchaguzi 2020 Mambo ya kujibizana kwenye kampeni ya nini wakati mnaweza kumaliza kila kitu kwenye mdahalo?

Uchaguzi 2020 Mambo ya kujibizana kwenye kampeni ya nini wakati mnaweza kumaliza kila kitu kwenye mdahalo?

L
Kama Magufuli na Lowassa wangeshiriki mdahalo na wagombea wengine wananchi wangegundua udhaifu wa hao wawili na hata kama wangechaguliwa wasingeshinda kwa kishindo na wananchi wangekuwa wanajilaumu wenyewe. Magufuli ndo Rais pekee toka Uhuru ambaye wananchi walitambua udhaifu wake kwa matendo na maneno yake miezi michache tu baada ya kushika madaraka. Wananchi walinunua mbuzi kwenye kiroba bila kujiridhisha kuwa wamenunua mbuzi kumbe wameuziwa mtoto wa fisi bahati nzuri wamegundua kosa lao itabidi wammalize kabla hajawa mkubwa awamalize. Fisi ni fisi huwezi kumbadili kuwa mbuzi hata ujaribu kwa nguvu zako zote!
Sasa mtu kama Lowassa ambaye hakuwa vizuri kiafya bado tu mtu huyo ilihitaji afanye mdahalo ndio mjue kama kuna shida? Alihojiwa na Zuhur Yunus akaanza kusema anamuonea.
Pamoja na yote hayo ila bado watu wakampigia kura kutaka awe rais.

Lissu kama kweli ana nia ya kufanya mdahalo basi sio lazima hadi afanye mdahalo na Magufuli,wote tunajua kuwa Magufuli hawezi mdahalo na ndio maana hata 2015 hakufanya ila bado mdahalo unaweza kufanyika na tukaona huo uwezo wa Lissu kama tulivyoonaga uwezo wa Mama Anna Mghwila.
 
Lisu kama haeleweki kwenye mkutano wa kampeni wa maelfu akitegemea aeleweke kwenye mdahahalo na mtu mmoja basi uwezo wa kujieleza na kuekeweka mdogo mno Mdahalo ni kupotezea muda watu tu ni sawa na mwalimu anafundisha darasa la watoto 40 hawaelewi halafu anasema nipeni mwanafunzi mmoja nifundihe muone!! Mmm Lisu Hawezi kueleza sera za chadema zikaeleweka kwenye mikutano ya kampeni period
Nani kakwambia haeleweki..... Watu haeaelewi kuhusu ndege na madaraja na ujenzi wa chato int airport.....

Hakuna mwanaccm mwenye akili za kufanya mdahalo na Mh Tundu Antipas Mugway LISSU......
 
Nchi zote walizopigana wa kwa wao yaani civil war ndio wana huo mfumo kuanzia hapo Kenya marekani India Afrika ya kusini Nigeria nk wote hao walitwangana civil war wakaamua kugawana nchi kwa majimbo .Kenya tu hapo utawala wa majimbo ulianza baada ya wakikuyu na wajaluo kutwangana barabara Kikwete akaenda kuwasaidia

Ndio majimbo yakaibuka baada ya kutembezeana marungu na mapanga wao kwa wao
Sasa huoni na sisi Tanzania ni bora tuanzishe utawala wa majimbo kabla ya kufikia huko kwenye kutwangana, na inawezekana tukafika maana haiingii akilini watu walime korosho kwa nguvu na jasho lao wewe upore pesa ukajengee uwanja wa ndege kijijini kwenu,

Kama mmeshindwa kuigawa keki ya taifa kwa usawa ni bora utawala wa majimbo ili rasilimali za eneo husika zianze kuwaneemesha wakazi wa eneo mahalia
 
Leo nimemskia Rais Magufuli akijibu hoja ya Lissu kuhusu CHADEMA kutengeneza Majimbo wakipata madaraka.

Dkt. Magufuli ameeleza kwamba mfumo wa majimbo utakua mwanzo wa mfarakano, japo sielewi mfarakano utatokana na nini maana sioni mifarakano USA, Nigeria, India na nchi zingine.

Sisi kama wapiga kura hatupendi kuona mnajibishana kwenye majukwaa. Tunamuomba baba yetu kipenzi Amri Jeshi Mkuu, Mwenyekiti wa CCM, Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akubali mdahalo kati yake yeye na Tundu Lissu ili kumaliza sekeseke lililopo.
Jiwe hana uwezo kiakili hata kifikra kufanya mdahalo na Lissu juu ya jambo lolote sembuse Sera ya majimbo! Ufafanuzu wake Jana kuhusu Sera hii umezua mjadala zaidi ya ufinyu wa uelewa wake. Ni heri angekaa kimya. Sera ya majimbo ndiyo mwendo wa dunia sasa hivi.
 
Back
Top Bottom