Mambo ya kuzingatia ukiwa katika nchi za bara la Asia, Ulaya na Marekani

Mambo ya kuzingatia ukiwa katika nchi za bara la Asia, Ulaya na Marekani

*Bado tupo South Korea tukitoka South tunaenda North kwa Kiduku

Ukiwa South Korea Usitarajie Wakorea kuzungumza nawe. Watakukwepa na Wala usihisi kubaguliwa, Wengi wao ni wenye haya na wanajaribu kuwaepuka wageni ili kuepuka aibu ya kuongea Kingereza kibovu

*Katika mazungumzo Wanawake hufunika midomo yao wakati wa kucheka.

Hapo awali, wasichana walifundishwa kwamba kucheka sio tabia ya kike. Na ikitokea kitu kitakacho wafanya wacheke, basi watacheka huku wakitazama kando au kujaribu kuficha tabasamu zao (kwasasa, wanafunika midomo). Ukiona mwanamke wa Kikorea amefunika mdomo wake, usije kudhani anapiga miayo Bali anacheka
43f2db557ab9be623b3206a9ca.jpg
 
Naongezea ukifika Saudia ama Kuwait chonde chonde kama wewe ni Mkristo hakikisha usivae rozali wala usiweke Biblia kwenye begi wala picha ya yule Yesu wa kwenye snema na hakikisha simu yako haina password na huna hata picha ya mkeo kwenye simu na pia usiwke miziki yoyote ya kimagharibi kwenye simu na ikitokea umeingia kipindi cha mfungo wa Ramadhani usipige mihayo hadharani ukiwa umeacha mdomo wazi na mfano umeenda sokoni ukanunua ndizi ukiimenya unavyo taka kula ishike kwa mkono wa kushoto then wa kulia ndio umenye kisha ikate kwa mkono ndio ule usije ukala ndizi kwa ule mtindo wa kama unanyonya icecream aisee umeondoka maana hayo mataifa wanafuata shariya na tena zinafanya kazi kwa wageni tu.

Kufanya hivyo itakusaidia sana kuishi kwa amani usije ukadhani umejificha maana kila baada ya hatua kwenye maeneo ya public na roads zote ni mwendo wa cctv.Utashangaa tu polisi mwenye kanzu akaja kukuzoa hapo ndio utaelewa.
Umenifanya nicheke sana eti polisi mwenye kanzu teh teh... teh [emoji23]
 
Naongezea ukifika Saudia ama Kuwait chonde chonde kama wewe ni Mkristo hakikisha usivae rozali wala usiweke Biblia kwenye begi wala picha ya yule Yesu wa kwenye snema na hakikisha simu yako haina password na huna hata picha ya mkeo kwenye simu na pia usiwke miziki yoyote ya kimagharibi kwenye simu na ikitokea umeingia kipindi cha mfungo wa Ramadhani usipige mihayo hadharani ukiwa umeacha mdomo wazi na mfano umeenda sokoni ukanunua ndizi ukiimenya unavyo taka kula ishike kwa mkono wa kushoto then wa kulia ndio umenye kisha ikate kwa mkono ndio ule usije ukala ndizi kwa ule mtindo wa kama unanyonya icecream aisee umeondoka maana hayo mataifa wanafuata shariya na tena zinafanya kazi kwa wageni tu.

Kufanya hivyo itakusaidia sana kuishi kwa amani usije ukadhani umejificha maana kila baada ya hatua kwenye maeneo ya public na roads zote ni mwendo wa cctv.Utashangaa tu polisi mwenye kanzu akaja kukuzoa hapo ndio utaelewa.
Safi, Kuna mengine hata mm nilikuwa siyajua hapa. Itabidi nijitahidi nifike nchi za kiarabu
 
msaada wa nchi za ukanda wa Scandinavia counties…utaratubu wa maisha upo upoje (lifestyle) na kipi na kipi kinatakiwa na kipi hakitakiwi, natanguliza shukrani ..
 
Kuna yule inshomile alitaka kuleta ujuaji wa mambo ya kuwaiga black america yakamkuta. Don't mess up with american police be cooperative.
Kuna mtza simu ilimponza alisimamishwa na police mara simu ikaita mfukoni alifanya kosa kubwa Sana kuingiza mkono mfukoni Ili achukue simu apokee ikawa ndo mwisho wa maisha yake palepale askari walidhani anatoa bastola, hadi uchunguzi upite ijulikane ni simu ushapotea. Police wa USA au Ulaya ukiwapa ushirikiano unajiongezea maksi ni rahisi kukusikiliza.
 
Nchi yeyeto ukienda achana na mambo ya feki, shortcut, illegal hasa ukiwa mgeni. Kuishi vyema fanya KILA kitu halali, ubaguzi wao usikuathiri, wabaguzi wengi ni watu wasio na exposure, kuwa Mzungu hakumaanishi mtu ana exposure, wapo wazungu wengi tu primitives, hawana exposure washamba awajatembea. Ukifanyiwa dhihaka yeyeto usionyeshe hisia ya kuchukia wataendelea kukuumiza Ili wafurahi, wakiinuka kwenye siti lala kabisa siti zote kwa raha zako hadi mwisho wa safari au kuwa bize na simu
 
Yapi ya kuzingatia ukiwa Uingereza?

Nikisikia story kama hizi ndio naona bora kufia hapahapa kwa Nyerere.
 
Yapi ya kuzingatia ukiwa Uingereza?

Nikisikia story kama hizi ndio naona bora kufia hapahapa kwa Nyerere.
Story nyingi ni over exaggerated, jambo muhimu kwa watu wa nchi yoyote ni 'mean your own business' hutapata mshikira wowote.
 
Story nyingi ni over exaggerated, jambo muhimu kwa watu wa nchi yoyote ni 'mean your own business' hutapata mshikira wowote.
Haziko over exaggerated ndugu, Acha nikuambie kitu kimoja unachoshindwa kuelewa, Sheria zote unazozisikia kwenye hayo ma nchi baadhi huvunjwa kila wakati na wenyeji, ila ukivunja wewe mgeni ndio utajua kama ni over exaggerated au sio, Yani watakufanya kama wewe ndiye mtu pekee kuvunja hizo Sheria, kwa hivyo ni bora kuwa mpole
 
Ndugu Watanganyika Mungu ni Mwema, sifa kwake kwa kutujalia Uhai

Ikiwa una Mpango wa kwenda nchi yeyote Ile Duniani hasa Nje ya bara la Afrika jitahidi kuijua nchi hiyo japo kwa machache mambo ya kuzingatia ukiwa huko pamoja na tamaduni zao, kufanya hivyo itakusaidia sana kuishi kwa amani na kuepuka matatizo ambayo siyo ya lazima.

Naenda kuelezea mambo ya kuzingatia na ambayo hutakiwi kufanya pindi unapokua MAREKANI. nitakuelezea baadhi ya nchi nyingine pia kwa uchache

MAREKANI
Ndugu Mtanzania ukiwa marekani peana mikono (handshake [emoji1666]) kama salamu ya kawaida, japokuwa hii kwangu sio lazima sana kwasababu tu ya ngozi yangu nyeusi, nikiwa Marekani Mimi Binafsi kwenye hili swala la handshake mm Nina principal zangu huwa siwi wa kwanza kutoa mkono nasubiri mwenzangu aanze lakini pia hii nai apply sana hapa Bongo, maana mswahili hakawii kusema nataka kumuibia nyota

Ukisalimiwa "How are you" take it as if they are saying ā€œYou good?ā€ na ujibu "Good" au "Good thank" jibu hivyo hata kama unahisi kufa sekunde zijazo, Marekani salamu haimaanishi kumjulia mtu hali, ni changamsha genge tu. Sasa wewe salimiwa halafu jichanganye kwa kutoa maelezo marefu.

Pia usisahau kuonesha katabasamu kwa mbali unaposalimia au unapojibu salamu. Marekani tabasamu ni ishara ya ukarimu, ndugu Mtanganyika usije ukafika Marekani watoto wa kizungu wakawa wanakutabasamia ukazani wanakutaka na wewe ukajimix kuwatongoza, utaharibu kila kitu, chonde chonde hizo hisia ziache Bongo.

Ndugu Mtanzania ukifika Marekani usifanye mazungumzo moja kwa moja na watoto usiowajua. Watoto wa Marekani wanafundishwa tangu wakiwa wadogo kuogopa wageni, na ukianza kuzungumza na mtoto asiyekujua utamtia kiwewe mtoto wa watu, na kama kuna mtu aliye karibu atafikia hitimisho lisilo sahihi kuhusu nia yako. Ikiwa una kitu cha kumwambia mtoto, mwambie mtu mzima aliye naye.

Ndugu Mtanzania ukifika Marekani usitoe maoni ya kudhalilisha kuhusu serikali au jeshi lao. Wamarekani wanathamini uhuru wao wenyewe wa kukosoa serikali na jeshi lao, lakini hawataki kusikia wageni wakikosoa nchi yao.

Ndugu Mtanzania hii point ninayoenda kueleza ni Muhimu sana, haswa ikiwa wewe sio Mzungu: Unaposimamishwa na polisi, USITOKE NDANI YA GARI LAKO NA KUMFUATA ASKARI. Kaa ndani ya gari lako na askari anapokaribia gari lako, weka mikono yako mahali ambapo askari anaweza kuiona.

Tatizo ni kwamba katika nchi nyingine au hapa Tanzania inachukuliwa kuwa ni adabu kumfuata police pale alipo, Kwa Marekani ni kosa kubwa sana[emoji777] askari anaweza kuwa na wasiwasi haraka sana ukifa hivyo, na hiyo inaweza kusababisha madhara makubwa, shuka kwenye gari pale tu atakapokuamlisha

VITU VYA KUFANYA UTAKAPOSHIKWA NA POLICE MAREKANI

(1) Zima injini ya gari lako
(2) Washa taa za ndani ikiwa nje ni giza (usiku)
(3) Teremsha kioo Cha mlango wa gari lako kama kipo juu
(4) Weka mikono yako kwenye usukani ambapo afisa wa polisi anaweza kuiona kwa urahisi
(5) Ukifuatisha hayo yote hapo juu then fuata kwa upole maagizo ya polisi (isipokuwa kwa maagizo ambayo hayafai, kama vile ombi la kupekua gari bila hati au sababu inayowezekana)

Ndugu Mtanzania narudia tena, Usitoke kwenye gari hadi uamliwe kufanya hivyo. Sasa jichanganye utoke kwenye gari utafurahia show.

Vivyo hivyo, usiguse pochi yako au kitambulisho hadi uulize. Ukianza kujigusagusa Police atadhani una bastora unataka kumdhuru, kwasababu Marekani kuwa na Bastola ni kitu cha kawaida na Sheria inawaruhusu yani ni kama wewe tu kuwa na namba za NIDA.

Inatosha kwa Marekani Wacha nikupe hints fupi fupi kwa nchi tofauti tofauti

ITALY
Italy: usivae nguo za Kiitaliano.

JAPAN
Japani: Ukifurahia huduma Nzuri iwe hotelini au mahala popote pale ndani japani usijidai Mshua saana ukatoa tip (Usitoe tip) ni ishara mbaya kwao, hawatachukulia kama wewe unavyoichukulia

UTURUKI
Ndugu Mtanzania ukifika Uturuki ukipewa chai usikatae kubali na inywe kwa amani ya moyo

INDIA
Ndugu Mtanzania ukifika India na Ukiona madume mawili wameshikana mikono huku wanatembea ni sawa kwao, inakubalika kijamii, usidhani kuwa wao ni mashoga. Nyingine kwa India ni kwamba usikanyage pesa, pesa inachukuliwa kuwa toleo la mungu wa kike katika dini ya Kihindu.

Hayo ni mambo baadhi kwa nchi ya Marekani na baadhi ya nchi nyingine kwa uchache pia unaweza nitajia nchi ambayo unataka kwenda au unataka kujua vitu gani havitakiwi kufanywa huko au ni mambo gani ya kuzingatia unapokuwa katika nchi ngeni na nitakujibu nikishindwa Watanganyika wenzangu watanisaidia

Huu uzi ni wa kila mtu, kuwa huru kueleza chochote kile unachokijua ili kutusaidia sisi Watanganyika wenzako

NB: Swala la kwamba utafikaje huko hilo ni juu yako Sina msaada wowote katika jambo hilo we niambie ushafika au unatarajia kwenda kwa namna unayoijua wewe then Mimi nitakupa hits.

MUNGU NI MWEMA

View attachment 2266318
Kwanini unasema tusivae nguo za kitaliano ? Na hizo nguo zipoje ?
 
This is free education. Asante mkuu.
Ahsante sana! Ni material haswaa.
Nasikia pia japan mkiwa kwenye usafiri wa umma na jirani yako akasinzia na kukuegemea huruhusiwi kumsukuma (kumuamsha); ni ishara kuwa amefanya kazi vya kutosha katika kujenga taifa lao.....hii imekaaje?
 
Back
Top Bottom